Chama
Cha Mapinduzi (CCM) kimepokea kwa majonzi na simanzi kubwa taarifa za
kifo cha Mhe. Samuel John Sitta, Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kilichotokea usiku wa jana tarehe 6/11/2016 katika
hospitali ya Technical University of Munich nchini Ujerumani alipokuwa
akitibiwa.
Mhe.
Samuel John Sitta, amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za utumishi
katika Chama na Serikali. Alikuwa Katibu wa CCM na Mkuu wa Mkoa,
Mkurugenzi Mkuu wa kituo cha uwekezaji, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya
Taifa (NEC), Mjumbe wa Kamati Kuu, Mbunge, Waziri na Spika.
Mhe.
Sitta alikuwa ni Kiongozi mchapakazi, mwadilifu na aliyejitambulisha
kwa utendaji wenye kufuata falsafa yake ya “kasi na viwango”. Ametoa
mchango mkubwa katika ujenzi wa Chama na Serikali.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndg Abdulrahman Kinana amemtumia salamu za rambi rambi
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai,
familia ya Mhe. Sitta pamoja na Wananchi wa Jimbo la Urambo kufuatia
kifo cha Kiongozi huyu. Tunaungana nao katika msiba huu ambao pia ni
msiba wetu
Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi, Ameni
Tunasikitika kuwataarifu kuwa mzee wetu mpendwa Samwel Sitta
amefariki dunia katika Hospitali ya Technical University of Munich
nchini Ujerumani saa 7:30 kwa muda wa Ujerumani alikokuwa akitibiwa
ugonjwa wa Saratani ya Tezi Dume.
Historia yake:
Samuel John Sitta alizaliwa Desemba 18, 1942 huko wilayani Urambo
Mkoa wa Tabora. Sitta alisoma Shule ya Msingi Urambo kati ya mwaka 1950
– 1953, kisha alikwenda Wilaya ya Sikonge mwaka 1954 - 1957 na
kuendelea na masomo ya “Middle School” katika shule ya “Sikonge Middle
School”. Baadaye mwaka 1958 – 1963 alianza masomo ya sekondari Shule ya
Wavulana Tabora yaani “Tabora Boys” kidato cha I – IV na cha V – VI.
Mara tu baada ya kuhitimu masomo ya sekondari, Sitta alijiunga Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kusomea Shahada ya Sheria (L LB) mwaka
1964 na kuhitimu mwaka 1971.
Sitta amesoma shahada yake kwa miaka 7 kwa sababu mwaka 1966, wakati
yuko mwaka wa pili na akiwa kiongozi wa wanafunzi UDSM, wanafunzi
waligoma na kuandamana kupinga kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT)
na kukatwa mishahara yao baada ya JKT. Hoja ya wanafunzi ilikuwa na
mantiki kubwa, kwamba mbona vigogo wa serikali na wanasiasa wanalipwa
mishahara minono na marupurupu makubwa?
Baada ya shinikizo hilo la wanafunzi Mwalimu Julius Nyerere alikubali
kupunguza mshahara wake wa Sh4,000 bila kodi akaagiza pia mishahara ya
mawaziri ipunguzwe kwa asilimia mbili. Miezi miwili baadaye akatangaza
Azimio la Arusha (Februari 5, 1967) kuyapa uzito malalamiko ya wanafunzi
hao.
Watukutu wawili – Sitta na Wilfred Mwabulambo (Wote sasa marehemu) na
wengine kadhaa – waliojitia wazimu na kutetea kile walichokiita haki
zao, (haki za wakulima na wafanyakazi), walimshutumu Mwalimu Nyerere kwa
maneno makali wakidai “…ni heri wakati wa ukoloni kuliko utawala wa
Mwalimu”.
Mwalimu Nyerere alikasirika na kuwafukuza chuo wanafunzi wote 400 kwa
kile alichokiita “kwenda kufunzwa adabu majumbani mwao”. Miezi kumi
baadaye, baada ya Nyerere kushawishiwa na hasira kutulia akaamua
kuwarudisha chuoni wanafunzi 392. Viongozi wa mgomo; Sitta na wenzake 7
walitiliwa ngumu, hawakurejeshwa chuoni.
Busara za viongozi wa chuo zilifanya Mwalimu aliliwe zaidi na kuandikiwa
barua mbili maalumu na chuo zenye Kumb. Na. C3/Sa.13 ya 2/3/1967 na
C3/Ss.13 ya 9/07/1967. Mwalimu alikubali kilio hicho na kuwaruhusu
vijana hao wanane warudi kwa sharti kwamba wale watukutu wawili (Sitta
na Mwabulambo) watandikwe viboko na “Mwalimu Nyerere” mwenyewe. Hii
ndiyo ilikuwa pona ya Sitta ambaye alirejea UDSM na kuendelea na masomo
kwa miaka kadhaa hadi alipohitimu mwaka 1971.
Wakati Sitta anarudi chuoni tayari alikuwa mwajiriwa wa Kampuni ya
Mafuta ya “CALTEX OIL” kama Meneja wa Tawi (1967 – 1969) na mwaka 1969 –
1975 aliajiriwa na Shirika la Maendeleo la Taifa kama Katibu na
Mkurugenzi wa Utawala.
Baadaye mwaka 1976 Sitta aliamua kujiendeleza kielimu katika masuala ya
Usimamizi nchini Uswisi kwenye Chuo Kikuu cha IMEDE ambako alihitimu
Stashahada ya Juu ya Usimamizi mwaka huohuo 1976.
Chini ya mfumo wa chama kimoja, Sitta alikuwa kiongozi wa juu wa CCM na
serikali akiwa mbunge, mkuu wa mkoa na Waziri katika nyakati tofauti na
ameendelea kuwa mbunge na waziri katika mfumo wa vyama vingi.
Sitta alimuoa Margareth Simwanza Sitta
Mbio za ubunge
Enzi za chama kimoja 1975 - 1995 Sitta alikuwa mbunge wa Jimbo la Urambo
(kabla halijagawanywa na kuwa Urambo Magharibi na Mashariki) na pia
alifanikiwa kuwa waziri kwa nyakati tofauti. Kwa mfano wakati wa kipindi
cha mwisho cha Mzee Mwinyi, Sitta alikuwa Waziri za Katiba na Sheria.
Mwaka 1995 Sitta aliingia kwenye mapambano mapya ya siasa za vyama vingi
na kwa bahati mbaya akawa mmoja wa vigogo walioangushwa na wabunge wa
NCCR. Mshindani wake mkuu alikuwa Msina Jacob Abraham. Msina alishinda
kwa kura 10,788 dhidi ya 9,497 za Sitta.
Sitta alirudi tena kwenye jukwaa la siasa mwaka 2005 kwenye uchaguzi
mkuu na aliwashinda wapinzani wake wakuu Lumatiliza Yotamu Lubungila wa
NCCR na Wilson George Ntakamulenga wa CUF. Sitta alipata kura 28,660
(72.3%) na kurejesha heshima yake jimboni Urambo Mashariki. Kurudi kwa
nguvu kulimpa nafasi ya kuwania na kuteuliwa na CCM kugombea uspika wa
Bunge la Tanzania na akaliongoza Bunge la Tisa aliloliita bunge la
Viwango Na Kasi "Speed and Standards" kwa mafanikio na changamoto
nyingi.
Mwaka 2010 Sitta alishiriki tena uchaguzi Urambo Mashariki akawashinda
wapinzani wake wakuu Msafiri Abdulrahmani Mtemelwa (CHADEMA) na Zombwe
Lotto Edward (CUF) kwa kupata kura 19,947 (70.47%). Baada ya ushindi
huo, Sitta alijaribu tena kuwania uspika bila mafanikio; utendaji wake
wa kuiuma serikali na wakati mwingine kuipuliza kwenye Bunge la Tisa
ulimfanya achukiwe na serikali.
Ilipoonekana ana nguvu akatengenezewa “chui wa karatasi” (mshindani),
Andrew Chenge. Chenge naye akachukua fomu ya uspika ghafla,
likatengenezwa ‘zengwe’ kuwa wagombea wote wana nguvu, hapo CCM ikapata
mwanya wa kutamka kuwa haiwataki wote ili kuondoa mvutano. Sitta
akapoteza ndoto za uspika na ukahamia kwa mwanamama Anne Makinda.
Rais Jakaya Kikwete alipotangaza Baraza la Mawaziri mwaka 2010 alimpa
Sitta Wizara ya Afrika Mashariki kama Waziri,vilevile alihamishiwa
Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi.
Mbio za urais
Samuel John Sitta alianza mbio za urais “kimyakimya” tangu alipokuwa
Spika wa Bunge la Tisa (2005 – 2010). Kuna nyakati alikuwa akitoa kauli
zinazoashiria kuwa nchi inayumba na haina uongozi thabiti huku
akionyesha kuwa nchi ina viongozi thabiti na hawajapewa uongozi mkuu wa
nchi, akiwemo yeye.
Hata alipoliongoza Bunge la Katiba mwaka 2014, mara nyingi Sitta
alionekana kama mtu mwenye shauku kubwa na urais na alipohojiwa, mara
kwa mara, juu ya urais alionyesha ana ndoto hizo. Mara kadhaa,
alilalamika kuwa wala rushwa wakubwa wanampiga vita kwa sababu ni msafi.
Katika Uchaguzi wa 2015, Sitta alitangaza nia ya kuwania Urais na
alichukua fomu ya kugombea urais kupita chama cha Mapinduzi ambapo baada
ya uchaguzi wa ndani chama, John Magufuli ndo jina lililofanikiwa
kupenya na kuteuliwa na chama kugombea Urais wa Tanzania.
Mungu Ailaze Roho Ya Marehemu Mahali Pema Peponi Amen.
Muswada
wa Sheria ya Mabadiliko ya Sheria Mbalimbali Namba 3 wa Mwaka 2016
unatarajiwa kuwasilishwa bungeni leo, ukigusa sheria tisa ikiwemo ya
Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu ambapo sasa mnufaika wa mkopo
aliyejiajiri atalipa kiasi kisichopungua Sh 120,000 au asilimia 15 ya
kipato chake, huku taasisi za umma, bodi, wakala na tume zimebanwa
zisirekebishe au kuwianisha mishahara, posho na marupurupu kwa
watumishi.
Kwa
mujibu wa muswada huo, kwenye Sheria ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu
ya Juu, waajiri wanaoshindwa kuwasilisha marejesho ya mwezi baada ya
makato wataadhibiwa, ambapo mwajiri atawajibika kuitaarifu Bodi ya
Mikopo kuhusu ajira ya mtu yeyote ambaye ana shahada au stashahada na
kukata makato ya mwezi kutoka kwenye mshahara wa mnufaika wa mkopo.
Kifungu
hicho kinapendekeza kufanya marejesho ya mkopo kuwa ya kisheria na
kupewa nafasi ya awali katika orodha ya makato na kinapendekeza
kupunguzwa idadi ya wajumbe wa Bodi ya Mikopo na kufikia saba kwa lengo
la kupunguza gharama za uendeshaji.
Kwenye
marekebisho ya Sheria ya Utumishi wa Umma, Kifungu cha 8 kinapendekeza
kufanyiwa marekebisho ili kumpa mamlaka Katibu Mkuu (Utumishi)
kurekebisha na kuwianisha mishahara, posho na marupurupu mengine kwa
watumishi wa umma.
Inapendekezwa
kumuondolea Katibu mamlaka ya kuteua watumishi wa umma wanaounda baraza
la majadiliano ya pamoja ya watumishi wa umma na sasa waziri atateua
katibu kutoka wizara yenye dhamana na kada husika ya watumishi.
Pia
inapendekezwa kufuta kifungu cha 11 ili kuondoa masharti yanayokataza
Baraza la majadiliano ya pamoja ya watumishi na baraza la pamoja la
watumishi wa umma kutoa mapendekezo kuhusu ujira.
Kwa
upande wa marekebisho ya Sheria ya Leseni na Usafirishaji, Mamlaka ya
Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) kutaongezwa kifungu
ili kuweka masharti yanayoruhusu ulipwaji wa faini pale mkosaji
anapokiri kosa, badala ya kila kosa kufuata taratibu za kimahakama.
Muswada
huo una marekebisho kwenye Sheria ya Mazingira ambako kutawekwa
mwongozo wa namna ya kupima urefu wa mita 60 kwenye kingo za bahari,
ziwa, mto au bwawa la maji kinachozuiliwa kufanyia shughuli zozote za
binadamu. Upimaji utapimwa kuanzia kwenye kingo za maeneo hayo.
Sheria
nyingine zitakazofanyiwa marekebisho kwenye Mkutano wa Tano wa Bunge la
11 ni ya Usafiri wa Anga, Sheria ya Msajili wa Hazina na Sheria ya
Vipimo.
Spika
Job Ndugai wakati akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kuanza
kwa Mkutano wa Tano wa Bunge wiki iliyopita, alieleza kuwa kwa wiki hii
Bunge litapokea taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za
Serikali(CAG) ya mwaka 2014/2015 kisha kujadili na kuishauri serikali
kuhusu Mkataba wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Jumuiya ya Ulaya (EU)
na Afrika Mashariki (EPA-EU) na kisha taarifa ya kamati ndogo kuhusu
uchambuzi wa sheria ndogo.
The following applicants have been selected to join various
undergraduate programmes (Diploma & Certificate) at Mzumbe
University in the the 2016/2017 academic year. Candidates are advised to
observe all instructions.
ALL STUDENTS WHO WERE SELECTED TO
RESUME STUDIES IN SPECIAL DIPLOMA IN EDUCATION- SCIENCE, MATHEMATICS AND
ICT AT THE UNIVERSITY OF DODOMA, ARE INFORMED TO REPORT AS CONTINUING
STUDENTS TO THE COLLEGE OF EDUCATION (5-6TH NOVEMBER, 2016), READY TO RESUME STUDIES ON 7TH NOVEMBER 2016. ISSUED BY THE DIRECTORATE OF UNDERGRADUATE STUDIES