Tuesday, 18 October 2016

MAGAZETI YA LEO JUMANNE OCTOBER 18 2016



Share:

Basi la Barcelona Lapata Ajali na Kuua Watu 10 Mkoani Lindi

Watu 10 wamefariki dunia na wengine 44 wamejeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Barcelona walilokuwa wakisafiria kutoka jijini Dar es Salaam kwenda mkoani Lindi  kupata ajali eneo na Miteja mkoani Lindi.

Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Renata Mzinga imesema kuwa chanzo cha ajali hiyo kimetokana na tairi ya gari ya upande wa kushoto kupasuka na kutokana na mwendo wa kasi wa basi hilo, dereva alipoteza uelekeo ndipo likapinduka.

Pia Kamanda Mzinga amesema kuwa wamechunguza na kugundua kua licha ya kuwa basi hilo lilikuwa na uwezo wa kubeba abiria 48, wakati basi hilo linapata ajali kulikuwa na abiria 54 kitu ambacho ni kosa kisheria.

Aidha, Kamanda Mzinga amesema kuwa bado wanaendelea na uchunguzi kuweza kubaini alipo dereva ili kuweza kufahamu ni kipi hasa kilichotokea. Hadi sasa wanamshikilia kondakta wa basi hilo lakini bado hajaweza kuelezea tukio halisi.
Share:

Monday, 17 October 2016

MPYA:TAARIFA KWA UMMA KUTOKA JESHI LA KUJENGA TAIFA JKT LEO TAREHE 17.10.2016

Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA AMUCTA TABORA,FIRST,SECOND AND THIRD BATCH 2016/2017

 Image result for AMUCTA.AC.TZ
Share:

Magazeti ya Tanzania Leo Jumatatu October 17, 2016


habar1
Share:

WAFANYAKAZI NEW HABARI CORPORATION HATARINI KUWA VIZIWI

Share:

Mfanyabiashara wa Mwanza ajishindia lori la Konyagi


kona1
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Devis Deogratius akiongea na  mawakala na wageni waalikwa
kona2
Mfanyabiashara  Julius  Masalu mkazi wa Mwanza (katikati) akipokea funguo za gari alilojishindia katika droo ya promosheni ya Nunua,Uza ,Shinda na Konyagi iliyohusisha mawakala wa kuuza bidhaa za kampuni ya Tanzania Distillers Ltd (TDL) kutoka kwa Meneja wa Chapa ya Konyagi,Martha Bangu (Kulia),anayeshuhudia kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TDL,Devis Deogratius.Droo ya pili ya promosheni hiyo ilifanyika  mwishoni mwa wiki katika viwanja vya hoteli ya Kili Home mjini Moshi mwishoni mwa wiki ikihusisha washiriki 31 kutoka mikoa ya kanda ya kaskazini na kanda ya ziwa
kona3
Baadhi ya maofisa wa TDL na mawakala katika picha ya pamoja
kona4
Mawakala wa Konyagi wakiserebuka wakati wa hafla hiyo
kona5
Meneja Masoko wa TDL,George Kavishe akiwashukuru mawakala walioshiriki kwenye promosheni hiyo
Mfanyabiashara  Julius  Masalu (58) mkazi wa Mwanza ameibuka mshidi wa gari aina ya Eicher lenye thamani ya shilingi milioni  56  katika mzunguko wa pili wa bahati nasibu ya Promosheni ya  Nunua,Uza ,Shinda na Konyagi iliyohusisha mawakala wa kuuza bidhaa za kampuni ya Tanzania Distillers Ltd (TDL).
Droo ya pili ya promosheni hiyo ilifanyika  katika viwanja vya hoteli ya Kili Home mjini Moshi mwihoni mwa wiki ikihusisha washiriki 31 kutoka mikoa ya kanda ya kaskazini na kanda ya ziwa na kusimamiwa na afisa wa Bodi ya Taifa ya michezo ya kubahatisha Humudi Abdul Hussein.
Akiongea kwa furaha baada ya kutangazwa kuwa mshindi, Masalu alisema ametoka Mwanza akiamini kuwa atajishindia gari hilo na kwamba bahati nasibu hiyo imeendeshwa kwa uwazi na hakuna upendeleo unaoweza kufanyika.
“Katika bahati nasibu hii hakuna  longo longo,shindano limeendeshwa kwa uwazi mkubwa sana na namshukuru Mungu kwa kuweza kupata zawadi hii ya gari itanisaidia sana katika kusambaza bidhaa zakampuni  ya konyagi kwa wateja wangu,” alisema Masalu.
Kaimu Meneja  Mkuu wa Konyagi, Devis  Deogratius alisema dhumuni ya promosheni hiyo ni  kukuza uhusiano wa kibiashara na wasambazaji wa bidhaa za TDL pamoja na kuwapatia kifaa kitakachosaidia katika kupanua masoko ,kusambaza na kuongeza ufanisi.
“Safari ilianza mwezi wa saba hadi mwezi wa tisa ,kumekuwa na usawa katika mchakato huu wa kumpata mshindi na hakuna upendeleo wowote ,wale ambao wamefikia malengo wamefika katika promosheni hii  na kuwepo hali ya usawa katika kushinda zawadi ya gari”alisema Deogratius.Alisema mbali na mshindi huyo wa gari  katika droo hii ya kwanza washiriki  watano walibahatika  kujishindia katoni 10 za Konyagi kila mmoja.
Baadhi ya washiriki katika droo hiyo, Mkamba Zephania na Joas Muganyizi  walisema wameridhishwa na mchakato mzima ulivyofanyika katika kuchezesha droo na wala hapakuwa na kasoro ama udanganyifu wowote.
“Kampuni ya TDL kupitia bidhaa yake ya Konyagi katika promosheni ya Nunua  Uza,Shinda na Konyagi imesaidia kuwakutanisha wafanyabiashara wa maeneo mengine ya kanda ya Kaskazini na kanda ya ziwa hali inayochangia kuongeza wigo katika kufanya biashara”.Alisema Muganyizi.
Washindi wengine waliojinyakulia katoni 10 kila mmoja za bidhaa ya Konyagi na maeneo wanayotoka kwenye mabano ni pamoja na Linus Mathew (Kagera) Msemo Enterprises (Arusha) ,Joace Muganyizi(Bukoba) Mkamba Zephania (Bariadi) na Yohana Masunga (Geita).
Huu ni mzunguko wa pili wa droo ya bahati nasibu ya Promosheni ya Nunua Uza,shinda na Konyagi ambapo katika droo ya kwanza mfanyabiashara Grace Oroki,  mkazi wa Jijini Dar es salaam, alijinyakulia gari kwa mawakala wa kuuza bidhaa za kampuni ya TDL wa mikoa ya Nyanda za juu Kusini na Pwani. 
Share:

WAZIRI MKUU AAGIZA MAPATO YA HOSPITALI YA NACHINGWEA YAKUSANYWE KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI


imgm9052
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa mwezi mmoja kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea, Bw. Bakari Mohammed kuhakikisha hospitali ya wilaya hiyo inakusanya mapato kwa kutumia mfumo wa kielektroniki.
Ametoa agizo hilo leo (Jumapili, Oktoba 16, 2016) wakati alipotembelea hospitali ya wilaya ya Nachingwea akiwa kwenye ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Lindi.
Waziri Mkuu amesema Serikali ilishaagiza taasisi zote za umma kutumia mfumo wa kielektroniki katika ukusanyaji wa mapato kwa lengo la kudhibiti mianya ya upotevu wa fedha za umma.
Amesema taasisi ambazo tayari ziameanza kutumia mfuko huo katika ukusanyaji wa mapato zimeweza kuongeza kiwango cha makusanyo kutoka sh. 300,000 hadi milioni nne kwa siku.
Pia aliwaagiza viongozi wa wilaya hiyo kuendelea kuwahamasisha wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ambao utawawezesha kupata huduma ya matibabu bure katika kipindi cha mwaka mzima.
Akizungumzia kuhusu matibabu kwa wazee, Waziri Mkuu amemuagiza Bw. Mohammed kuhakikisha anafungua dirisha la kuwahudumia wazee ili kuwarahisishia upatikanaji wa huduma wanapofika hospitalini hapo.
“Mkurugenzi hakikisha watendaji wako wa kata na vijiji wamebaini wazee wote katika maeneo yao na kuwatengenezea vitambulisho vitakavyowawezesha kupatibiwa bure,” amesema.
Naye Mganga Mkuu wa wilaya hiyo Dk. Samwel Laizer amesema muamko mdogo wa jamii kujiunga na CHF ni moja kati ya changamoto zinazowakabili katika utoaji wa huduma za afya.
Dk. Laizer amasema kati ya kaya 30,000 zilizoko wilayani Nachingwea ni kaya 7,133 tu ndizo zilizojiunga na mfuko wa CHF.
Awali Waziri Mkuu alizungumza na watumishi wa wilaya hiyo kwenye ukumbi wa Chuo Cha Walimu na kuwataka wabadilike ili waweze kuwatumikia wananchi kwa uadilifu bila ya kujali itikadi zao za kidini na kisiasa.
Amesema Serikali haitamvumilia mtumishi yeyote atakayeshindwa kutekeleza wajibu wake wa kuwatumikia wananchi. “Serikali haitaridhika kuona wananchi wakizagaa kwenye ofisi za halmashauri hiyo bila ya kusikilizwa,” amesema.
Share:

Grants Assistant at ACDI/VOCA


ACDI/VOCA, an International NGO with Headquarters based in Washington, D.C., is currently advertising for the position outlined below for the Cereals Market System Development (CMSD) Activity. CMSD is a four-year project funded by The United States Age, for International Development (USAID), which promotes economic growth by facilitating the competitiveness of the smallholder-based rice and maize value chains, especially in rural areas.

Position:Grants Assistant

Location:lringa

Job Summary:

The Grants Assistant is a member of the CMSD Grants team. The primary role of the Grants Assistant is to work with the Gran. Manager to ensure that grants are executed in an efficient and timely manner, in full compliance with ACD/VOCA grants policies and procedures, as well as USAID rules and regulations. The Grant& Assistant works with the Grants Manager on ensuring the integrity and transparency of the process of identifying grantees and the procedures used to award them. S/he ensures that processes and procedures are clear and clearly communicated to staff, applicants, grantees and subcontractors.

Key Responsibilities:

• Participate in improving/clarifying processes and procedures for awarding and administering grants, and propose corrective action when these are unclear or causing unnecessary delays

• Collect and safely store received prequalification applications and submit to Grants Manager for processing Distribute grant applications to evaluation committee and with collaboration with Grants Manager, perform Pre-Award Assessments

• Coordinate approval of milestones/deliverabies and payments to grantees

• Ensure that all grants files are well filed and property documented according to the grant documentation checklist requirement

• Ensure and Make proper filing and documentation of Grantees files with respect to the grant documentation check list

• In the absence of Grants Manager, serve as a non-voting member of the grant application evaluation committee

• Identify and document any problems or shortcomings of grantee performance, recommend corrective actions, and communicate these to the Grants Manager and appropriate personnel in timely fashion

• Review and analyze grantee budget estimates for allow ability and reasonableness, and consistency and routinely spot check visit grantees to ensure that funds allocated are used for specified purposes

• In close collaboration with Grants Manager, conduct internal training sessions on CMSD grants Processes including the preparation of grant applications, financial management and reporting requirements

• In close collaboration with Grants Manager, conduct mandatory training for all grantees regarding administration and technical reporting requirements

• Engage and facilitate interaction with our technical team to ensure that roles and responsibilities in the granting ()MGM are clear and clearly communicated

Qualifications and Experience:

• University Degree in Accounting, Finance, Business Administration, Economics or related field with at least 1.2 years of work experience in Grants Management, Accounting, or Finance

• Proven knowledge of USAID rules and regulations, preferred with International NGO experience.

• High level of English, both spoken and written English,strong communication and interpersonal skills 

Application Instructions:

To apply for this position, qualified candidates should submit an application letter describing why he/she is the best fit for this position, and a curriculum vitae detailing relevant work experience with three referees to hr@nafaka-tz.org.

Closing date for applications is 21st October 2016 (Only shortlisted candidates will be contacted)
======== ============
Are you disappointed by fruitless job applications and never get shortlisted? The problem is not you, its your CV. This comes to an end, Now for outstanding CV and Jobs professional advice, contact Bright Professionals Tanzania  and grab your dream job. We  also prepare social science business researches  and proposals.
Email cv.bptz@gmail.com
Phone +255 678 226 793
Share:

Sunday, 16 October 2016

New AUDIO | RAYVAN & NEY LEE - RUDI | Download


Share:

Diamond na Harmonize Washinda tuzo za AFRIMMA 2016,Orodha kamili ya washindi ipo hapa

Utoaji wa tuzo za AFRIMMA kwa mwaka 2016 umefanyika Dallas, Marekani huku watanzania watatu, Diamond Platnumz, Harmonize na DJ D Ommy wakiibuka na tuzo kila mmoja akipata tuzo moja.

Diamond ameshinda tuzo ya mwanamuziki bora wa kiume kwa Afrika Mashariki, Harmonize kashinda tuzo ya msanii anayechipukia Afrika na DJ D Ommy akishinda tuzo ya DJ bora Afrika.

Orodha kamili ya washindi waweza isoma hapa chini;

Best Male West Africa – Olamide (Nigeria)

Best Female West Africa – Efya

Best Male North Africa – Amr Diab

Best Female North Africa – Ibtissam

Best African DJ USA – Dj Dee Money

Best Male Central Africa – C4 Pedro

AFRIMMA Video of the year – Brother brother Bisa Kdei

Best Female Central Africa – Daphne

Music Producer of the year – Masterkraft

Best male South Africa – AKA

Best Female Southern Africa – Chikune

Best Rap Act – Phyno (Nigeria)

Best African Group – Sauti Sol (Kenya)

Best collaboration – Reggae blues ( Harrysong, Kcee) Nigeria

Crossing boundaries with Music – Wizkid (Nigeria)

Song of the year – Tecno Duro (Nigeria)

Best Gospel Act – Willy Paul (Kenya)

Best Male East Africa – Diamond Platnumz ( Tanzania)

Artist of the year – Flavour ( Nigeria)

Best Newcomer – Harmonize (Tanzania)

Best Dancehall Act – Shatta Wale

Best Video Director – Patrick Elis

Carribean Artist of the year – Machel Montano
Share:

Mwana Samatta Atajwa Tuzo ya Mchezaji Bora ya Shirikisho la Soka la Afrika (CAF).


Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayecheza soka la kulipwa katika klabu ya GENK ya nchini Ubelgiji ametajwa miongoni mwa wachezaji 30 wanaowani Tuzo ya Mchezaji Bora ya Shirikisho la Soka la Afrika (CAF).

Wachezaji wengine ni pamoja na Mkenya Victor Wanyama anayecheza ligi kuu ya Uingereza katika klabu ya Tottenham Hotspur, Denis Onyango kutoka Uganda anayekipiga katika klabu ya Mamelodi Sundowns.

Hapa chini ni orodha kamili.

1. Riyad Mahrez (Algeria & Leicester City)

2. El Arabi Hillel Soudani (Algeria & Dinamo Zagreb)

3. Islam Slimani (Algeria & Leicester City)

4. Samuel Eto’o (Cameroon & Antalyaspor)

5. Benjamin Mounkandjo (Cameroon & Lorient)

6. Serge Aurier (Cote d’Ivoire & PSG)

7. Eric Bailly (Cote d’Ivoire & Manchester City)

8. Yao Kouasi Gervais ‘Gervinho’ (Cote d’Ivoire & Hebei Fortune)

9. Mohamed Salah (Egypt & Roma)

10. Mohamed El Neny (Egypt & Arsenal)

11. Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon & Dortmund)

12. Andre Ayew (Ghana & West Ham)

13. Victor Wanyama (Kenya & Tottenham)

14. William Jebor (Liberia & Wydad Athletic Club)

15. Mehdi Benatia (Morocco & Juventus)

16. Hakim Ziyech (Morocco & Ajax)

17. John Mikel Obi (Nigeria & Chelsea)

18. Kelechi Iheanacho (Nigeria & Manchester City)

19. Ahmed Musa (Nigeria & Leicester City)

20. Cedric Bakambu (DR Congo & Villareal)

21. Yannick Bolasie (DR Congo & Everton)

22. Sadio Mane (Senegal & Liverpool)

23. Kalidou Koulibaly (Senegal & Napoli)

24. Keegan Dolly (South Africa & Mamelodi Sundowns)

25. Itumeleng Khune (South Africa & Kaizer Chiefs)

26. Mbwana Samatta (Tanzania & Genk)

27. Aymen Abdennour Tunisia & Valencia)

28. Wahbi Khazri (Tunisia & Sunderland)

29. Dennis Onyango (Uganda & Mamelodi Sundowns)

30. Khama Billiat (Zimbabwe & Mamelodi Sundowns)
Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO KIKUU MARIAN UNIVERSITY(THIRD ROUND) 2016/2017

KUONA MAJINA 

Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WA CHUO CHA MAJI UBUNGO WALIOPATA MKOPO 2016/2017

 

Names of WTF Loan Beneficiaries 2016-17

ATTENTION TO THE WTF LOAN APPLICANTS
The Board of The Registered Trustees of Water Technicians Fund (RTWTF) hereby wishes to inform all loan applicants that by applying and meeting the loan allocation criteria, eighty eight (88) applicants have qualified to be beneficiaries of the loan
Share:

VIDEO[Singeli] | MSAGA SUMU - IGA TENA [Teaser]


Share:

New AUDIO | Salamu TMK - Dada | Download

Share:

Upepo Mkali Waezua Nyumba 44 Musoma

Upepo mkali ukiambatana na mvua umeezua nyumba 44 katika Kijiji cha Kiemba Kata ya Ifulifu, Wilaya ya Musoma mkoani Mara. 
Kati ya nyumba hizo, tano ziliathirika vibaya kiasi cha kusababisha wamiliki wake kulala nje. Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alikagua baadhi ya nyumba zilizoathirika ili kuona athari za uharibifu huo. 
Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dk Vicent Naano na viongozi wa halmashauri, walitembelea eneo hilo baada ya kupata taarifa za athari za kuezuliwa paa na kuagiza tathmini ifanyike ili Serikali iweze kutoa msaada kwa wananchi hao. 
Profesa Muhongo aliwaambia waathirika hao kuwa Serikali ya Rais John Magufuli ipo pamoja nao na ametumwa kuwapa pole kutoka kwa viongozi wa juu wa Serikali. 
“Ndugu wananchi, nimetumwa na Rais wetu Dk John Magufuli niwape pole sana kwa kukutwa na kadhia hii ya kuezuliwa na upepo kwa paa za nyumba zenu. Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wanawapa pole pia na wanawatakia heri wale wote walioathirika,” alisema. 
Profesa Muhongo aliwaelekeza viongozi wa kijiji hicho wahakikishe wanafanya tathmini ya kweli kwa kupita kila nyumba iliyoathirika na yoyote atakayegundulika amedanganya ili Serikali imlipe, zoezi zima litaahirishwa na kurudiwa upya, pia wahusika watachukuliwa hatua za kinidhamu. 
Aliwaahidi wananchi hao kuanza kupewa misaada baada ya kikao cha halmashauri kupitia taarifa ya tathmini kesho, na kuwaelekeza viongozi kufanya kazi hiyo kwa haraka. 
Profesa Muhongo alikuwa mkoani Mara kwa ziara ya kikazi ya kukagua umeme na kushiriki maadhimisho ya kumbukumbu ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere iliyofanyika nyumbani kwake Butiama juzi.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger