Saturday 29 March 2014

TANGAZO KWA CSEE 2014 KUTOKA NECTA





                       BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA

TANGAZO
Kaimu Katibu Mtendaji, Baraza la Mitihani la Tanzania anapenda kuwatangazia watu wote wanaotaka kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT)  mwezi Novemba,  2014  kama Watahiniwa wa Kujitegemea kwamba kipindi cha usajili kwa malipo ya  ada ya kawaida (Shilingi 50,000/=kwa wanaojisajili CSEE na Shilingi 30,000/= kwa wanaojisajili QT ) kimeongezwa kutoka tarehe 28 Februari, 2014 hadi tarehe   31 Machi, 2014. Watahiniwa watakaojisajili  kuanzia tarehe 1 Aprili, 2014 hadi tarehe 30 Aprili, 2014 watatakiwa kulipa ada ya kawaida pamoja na faini mpaka usajili utakapofungwa rasmi tarehe 30 Aprili, 2014.
Waombaji wote wanasisitizwa kuhakikisha wanajisajili mapema kwa njia ya mtandao kupitia tovuti ya Baraza la Mitihani ya www.necta.go.tz. Kabla ya kujisajili kwenye mtandao, waombaji wanapaswa kwenda kwenye vituo vya mitihani kuchukua namba rejea (reference number) zinazotolewa bure na kulipa ada ya mtihani kwa njia ya Posta au Mpesa.

Imetolewa na:
KAIMU KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA.
Share:

KANGA MOJA:WAFANYA KUFURU

TAZAMA VIDEO HII HAPA CHINI


Share:

RODGERS:NO PRESSURE ON US













The Anfield outfit have won their last seven games on the bounce, putting them in contention for the title

Liverpool head into Sunday's game on the back of Wednesday's 2-1 success over Sunderland, a result that left Rodgers' side just one point behind Premier League leaders Chelsea.







The Merseyside club have won their last seven league games and are unbeaten in the Premier League in 2014, but that run has not prevented Sherwood from questioning Liverpool's ability to keep pace with Chelsea and fellow title rivals Manchester City.

However, Rodgers has been quick to dismiss Sherwood's comments, insisting that his players are calm ahead of the final run-in.

"We're very relaxed," Rodgers told reporters. "We're focused. There was no expectation on us being where we are, so there's certainly no pressure."

Rodgers also hit back at Sherwood, indicating that Tottenham - who sit seven points adrift of the top four in sixth - have performed below expectations this season.

"I suppose the likes of Tottenham are a team who were maybe looking to be challenging for the league this season. You spend £100m-odd - it's a group that's set up to challenge," he added.

"There's certainly no pressure on ourselves, and I think we've shown that over the course of the season. We're playing with no fear.

"We're very hungry to succeed and that can give you a real advantage. We've proved that already this season. Experience isn't everything.

"We're looking to make sustainable success. That's our objective. We're looking to build something here."
Share:

VIDEO:BUNGE LA KATIBA KUHUSU MARIDHIANO YA KANUNI JANA


ANGALIA VIDEO :

Share:

CHAMPIONI JUMAMOSI, JIPATIE NAKALA YAKO LEO

Share:

NO PRESSURE ON US-RODGERS

The Anfield outfit have won their last seven games on the bounce, putting them in contention for the title

Betare feeling the pressure in the title race.


Liverpool head into Sunday's game on the back of Wednesday's 2-1 success over Sunderland, a result that left Rodgers' side just one point behind Premier League leaders Chelsea.







The Merseyside club have won their last seven league games and are unbeaten in the Premier League in 2014, but that run has not prevented Sherwood from questioning Liverpool's ability to keep pace with Chelsea and fellow title rivals Manchester City.

However, Rodgers has been quick to dismiss Sherwood's comments, insisting that his players are calm ahead of the final run-in.

"We're very relaxed," Rodgers told reporters. "We're focused. There was no expectation on us being where we are, so there's certainly no pressure."

Rodgers also hit back at Sherwood, indicating that Tottenham - who sit seven points adrift of the top four in sixth - have performed below expectations this season.

"I suppose the likes of Tottenham are a team who were maybe looking to be challenging for the league this season. You spend £100m-odd - it's a group that's set up to challenge," he added.

"There's certainly no pressure on ourselves, and I think we've shown that over the course of the season. We're playing with no fear.

"We're very hungry to succeed and that can give you a real advantage. We've proved that already this season. Experience isn't everything.

"We're looking to make sustainable success. That's our objective. We're looking to build something here."
Share:

Kura mchanganyiko Bunge la Katiba

Kura mchanganyiko Bunge la Katiba

Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Profesa Abdul Shariff (kulia) akipiga kura ya siri wakati Bunge hilo jana lilipokuwa likipitisha utaratibu wa kupiga kura za aina mbili (siri na wazi). . 
Kwa ufupi
Mjumbe Vuai Ali Vuai alisema, wamefikia maridhiano hayo, ili kuwezesha kuendelea na mchakato wa katiba mpya kwani kila upande uliendelea kutetea msimamo wake hata katika kikao cha maridhiano.


Dodoma.Wajumbe wa Kamati ya Maridhiano jana walinusuru Bunge Maalumu la Katiba kuvunjika, baada ya kukubaliana kutumika kwa utaratibu wa upigaji kura wa wazi na siri kama ilivyopendekezwa na Kamati ya Kanuni na Haki za Bunge.
Wajumbe hao walitangaza uamuzi huo bungeni kutokana na makubaliano yaliyofikiwa katika kamati ndogo ya maridhiano iliyofanyika jana asubuhi baada ya kushindwa kuafikiana katika kikao cha awali kilichofanyika juzi kuanzia saa 3:00 usiku hadi usiku wa manane ili kunusuru kukwama kwa Bunge hilo.
Kabla ya uamuzi huo, Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta alisema juzi usiku walikutana hadi usiku wa manane baada ya hapo, walikabidhi kamati ndogo yenye mchanganyiko wa wajumbe kutoka Kamati ya Kanuni na Kamati ya Maridhiano.
“Baada ya kukamilisha kazi, wajumbe wa kamati ndogo watatoa taarifa hapa ambao ni John Mnyika, Profesa Ibrahimu Lipumba, Vual Ali Vual na Askofu Donald Mtetemela,”alisema Sitta.
Akitoa taarifa ya maridhiano hayo, kwa niaba Freeman Mbowe, Mjumbe John Mnyika alisema, alianza kwa kunukuu kitabu kilichoandikwa na Mwalimu Nyerere, mwaka 1962 chenye ujumbe mahususi kwa Chama cha TANU akisema ujumbe huo kwa sasa ni sahihi kwa watu wengi na taasisi ikiwamo CCM.
Mnyika pia alisema Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) hawana nia yoyote ya kuvuruga mchakato wa katiba kama ambavyo imeelezwa katika siku za karibuni na viongozi, kwani wazo la kutaka Katiba Mpya imekuwa ni kilio chao cha muda mrefu.
Naye Profesa Lipumba alisema suala ambalo tumekuwa tukisimamia kwa muda mrefu suala ambalo lina utata, kati ambao wanapenda kura za uwazi na wale wa siri.
Alisema: “Tuliletewa mchanganyiko wa uwazi na siri, lakini maana yake ni kura ya uwazi, wenzetu wamekuwa na msimamo mkali hata hili la kufanya uamuzi ilikuwa tufanye kwa siri, lakini hata hivyo hawakukubali.”
“Tulifanya uamuzi ili tusonge mbele, basi tulipendekeza upigaji kura wa kuamua tupige kura kwa mfumo wa siri, lakini pia wenzetu walikataa,”alisema Profesa Lipumba.
Alisema kwa kuzingatia kutokwama kwa zoezi la kuanza kujadili rasimu, wameamua kukubali kutokubaliana.
“Ili kusonga mbele tunahitaji kusonga mbele tuanze kujadili Katiba, natoa wito kwa wenzangu wa chama tawala kwa kuwa mpo wengi mnadhamana kubwa, ni vyema mkawa na utaratibu wa kuwasikiliza wachache,” alisema.
Mjumbe Vuai Ali Vuai alisema, wamefikia maridhiano hayo, ili kuwezesha kuendelea na mchakato wa katiba mpya kwani kila upande uliendelea kutetea msimamo wake hata katika kikao cha maridhiano.
Share:

DUDE APATA AJALI LOLIONDO

DUDE APATA AJALI LOLIONDO


STAA wa sinema za Kibongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ amepata ajali ya gari wakati akielekea Loliondo, Arusha kupata dawa ya kikombe inayotolewa na mchungaji mstaafu, Ambilikile Mwaisapila.
Staa wa sinema za Kibongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’
Dude ameiambia Bongowood kuwa, hivi karibuni walikuwa na gari aina ya Toyota Prado wakimpeleka mama yake kupata tiba ya ganzi mwilini ndipo tairi lilipopasuka na gari kuangukia gema.
“Ilipoteza muelekeo, likayumba lakini nashukuru Mungu hatukuumia, tukasaidiwa kunyanyua, tukaenda kupata tiba ya babu,” alisema Dude.
Share:

Friday 28 March 2014

VIDEO: TAZAMA AJALI HII KUBWA YA NDEGE ILIVYOTOKEA


Share:

MAPIGANO MAKALI DHIDI YA M23


Share:

VIDEO:25TH MATCH BETWEEN MAN CITY AND MAN UNITED


Share:

VIDEO:KAMATI YA MARIDIANO YA KANUNI ZA BUNGE IKIJADILI KUHUSU KANUN HIZO


Share:

Siri ya CCM kung’ang’ania Serikali mbili kikatiba

Siri ya CCM kung’ang’ania Serikali mbili kikatiba

 

  • Msimamo huo ni kinyume na mapendekezo au matakwa ya wengi kama ilivyoainishwa kwenye Rasimu ya Pili ya Katiba iliyoandaliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba


Katika maisha ya kawaida, binadamu ana msimamo wake na hata uamuzi  asiopenda ubadilike.
Katika medani ya siasa nchini msimamo wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) kuhusu Muungano na muundo  unafahamika. Ni muundo wa kutaka  Serikali mbili ambao chama hicho unakipigania kwa udi na uvumba.
Hata hivyo, msimamo huo ni kinyume na mapendekezo au matakwa ya wengi kama ilivyoainishwa kwenye Rasimu ya Pili ya Katiba iliyoandaliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
 Tume hiyo iliyokuwa chini ya Jaji Joseph Warioba ilikusanya maoni ya wananchi na ilipendekeza muundo wa Muungano wa Serikali tatu.
Hivi karibuni akifungua Bunge Maalumu la Katiba, Rais Jakaya Kikwete akaunga mkono msimamo wa chama chake, jambo lililoibua mjadala unaoendelea hadi sasa.
Hoja ya Serikali mbili
Kwanini CCM wanataka Serikali mbili na siyo tatu au moja kama ilivyo maoni ya wananchi walio wengi kwa mujibu wa maelezo ya Tume ya Warioba? Makala haya yanachambua hoja hiyo.
 Profesa Bakar Mohammed ni Mhadhiri Mwandamizi na Mkuu wa Idara ya Siasa na Utawala ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, anayesema msimamo wa CCM wa kudai Serikali mbili unatokana na hofu ya uhafidhina wa kuogopa mabadiliko.
Anasema viongozi wengi wa CCM wanasumbuliwa na hofu na woga wa mabadiliko na kwamba wanakuwa wagumu kuyakubali  yanapotaka kutokea.
“Kama mtu unaangalia madaraka zaidi, lazima kunakuwa na woga, na hii ni hulka ya binadamu kuwa na woga wa kuacha kile ulichokizoea… Lakini ukiangalia masilahi ya nchi na kuacha yale yanayokusukuma kusingekuwa na wasiwasi huu unaoonekana sasa,” anasema.
Anasema CCM inachofanya ni kuhakikisha haking’oki madarakani, huku viongozi wake wakiamini kuwa wana sifa za kuongoza na siyo wengineo.
Profesa Bakari anailinganisha hofu ya sasa ya CCM na ile waliyokuwa nayo viongozi wa chama hicho miaka ya 1990 zilipoanza vuguvugu za mabadiliko ya siasa za vyama vingi. Anasema CCM kiliendesha propaganda kuwa mfumo wa vyama vingi haukuwa na tija na ungeleta vita.
Share:

VIDEO:SPKA AKIONYA VURUGU NDANI YA BUNGE LA KATIBA


Share:

Seif: Hatuko tayari kujadili serikali mbili


Zanzibar. Makamu wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amesema chama chake cha CUF hakiko tayari kujadili mfumo wa Muungano wa serikali mbili kama inavyotetewa na wabunge wa CCM na Rais Jakaya Kikwete.

Amesema tayari amewaandikia barua Rais Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kuwaeleza juu ya msimamo huo.
Maalim Seif alitoa msimamo huo jana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kibandamaiti mjini Unguja.
Isitoshe, alisema CUF imebaini kuwa kuna njama za kufuta kipengele katika Katiba ya Zanzibar kinachosema; “Zanzibar ni nchi” na kwamba hiyo ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu kwa kuwa Wazanzibari kamwe hawatakubali kufanya hivyo.
Maalim Seif alisema haikuwa mwafaka kwa Rais Kikwete kukosoa mapendekezo ya Rasimu ya Katiba yanayotaka mfumo wa Muungano kuwa wa serikali tatu.
Alisema Jaji Warioba aliweka kando itikadi yake ya CCM katika utendaji wake kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kuja na uamuzi huo kwa vile ndiyo tiba ya kero za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
“Mapendekezo yaliyowasilishwa na Jaji Warioba hayakuwa maoni yake, yale ni maoni ya wananchi, Tanganyika imevaa koti la Muungano, ametoa ushahidi wake ili kujenga mwafaka katika kuendeleza Muungano wenye mfumo wa serikali tatu,” alisema Maalim Seif.
Alisema Muungano wa serikali mbili hauvumiliki na kama kuna watu wanaendelea kuutetea mfumo huo, Zanzibar inaweza kutumia sheria yake ya kura ya maoni kuwauliza wananchi wanaotaka na wasiotaka jambo hilo.
“Nimemwandikia barua Rais Kikwete, nakala nimempelekea Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, Tanzania Bara wanataka Zanzibar iondoe kifungu cha Katiba kinachosema Zanzibar ni nchi, jambo hilo halitapita...tutafanya kampeni wananchi walikatae,” alieleza Katibu Mkuu huyo wa CUF.
Alisema ni jambo la kusikitisha katika hotuba yake alijisahau kama ni mkuu wa nchi na analihutubia Bunge Maalumu badala yake akaegemea kuwa mwenyekiti wa CCM.
Alisema haikuwa sahihi kutoa vitisho na kutaja ikiwa Serikali ya Muungano chini ya Serikali tatu italegalega, jeshi litachukua madaraka ya nchi.
“Rafiki na ndugu yangu Kikwete, usifikiri huu ni wakati ule wa Julius Nyerere, akisema yeye hakuna wa kumpinga. Mambo yamebadilika, usijifanye ni Nyerere mpya, hakuna atakayekusikiliza na kubabaika,” alisisitiza Maalim Seif.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger