Friday 3 May 2024

JKT YAZALISHA MICHE 300,000 NA KUIGAWA BURE KWA WAKULIMA MKOANI KIGOMA

Mwenyekiti wa Kamati ya Kimkakati ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Brigedia Jenerali Hassan Mabena,akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua mradi wa kilimo cha mchikichi katika Kikosi cha 821 KJ Bulombora mkoani Kigoma.

Na.Alex Sonna-KIGOMA

JESHI la Kujenga Taifa (JKT) katika Kikosi cha 821 Bulombora wamezalisha miche takribani 300,000 na kuigawa bure kwa wakulima wakubwa, wa kati na mtu mmoja mmoja na kupitia vyama vya ushirika kwa halmashauri zote za Mkoa wa Kigoma.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kimkakati ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Brigedia Jenerali Hassan Mabena,wakati wa ziara yake ya kukagua mradi wa kilimo cha mchikichi katika Kikosi cha 821 KJ Bulombora mkoani Kigoma.


Amesema baada ya maagizo kutoka Serikalini walishirikiana na taasisi ya tari katika kuandaa vitalu ambavyo viliwasaidia kuandaa miche iliyokwenda kutumika katika kwa wakulima mbalimbali.

"Zoezi hili limekwenda vyema na miche zaidi ya 300,000 imegawiwa kwa wakulima bure na maofisa ugani katika kata walisimamia kuhakikisha kuwa inapandwa kitaalamu kwenye mashamba ya wakulima,"amesema Brigedia Jenerali Mabena

Brigedia Jenerali Mabena ambaye Mkuu wa Tawi la Utawala la JKT, amesema wamejiwekea malengo ya kuhakikisha kuwa wanafikia ekari 2000 hadi kufikia mwaka 2024/25 na kwamba hadi sasa wameandaa na kupanda ekari 1100.

“Wenzetu wa TARI (Taasisi ya Utafiti wa Kilimo) Mkoa wa Kigoma wapo hapa kuhakikisha kuwa wanashirikiana na kikosi kuhakikisha kuwa miche hii inakua na kama kuna changamoto zozote zile basi tuweze kuchukua hatua ili kufikia malengo tuliojipangia,”amesema.

Akizungumza kuhusu unufaika wa vijana wakujitolea na wale wa kwa mujibu wa sheria , Brigedia Jenerali Mabena amesema vijana wanaolelewa na JKT, mbali ya kufundishwa mafunzo ya uzalendo, ukakamavu wanafundishwa shughuli za kilimo, stadi za maisha pamoja na ujasiriamali.

Amesema katika mafunzo ya kilimo, vijana hao wamehusika katika hatua zote za kilimo cha chikichi ikiwemo kuandaa miche hadi kupanda.

Akielezea kuongeza thamani kwa mazao yanayozalishwa, Brigedia Jenerali Mabena amesema kupitia shamba darasa na mashine ndogo zilizopo katika kikosi hicho, vijana hao wameelekezwa namna ya kuchakata mafuta ya kula.

Amesema pia wameongezewa maarifa na kufundishwa jinsi ya kuongeza thamani mbegu pia zinazobakia kwa kutengeneza sabuni ambazo hutumika katika shughuli mbalimbali za usafi.

Aidha, Brigedia Jenerali Mabena amesema mpango wa kuongeza thamani kwa mazao yanayozalishwa kwenye vikosi na baadhi yake vimeshafungua viwanda vidogo vya kuchakata mafuta ya alizeti kwa ajili ya matumizi ya vikosi na majirani wanaowazunguka.


“Lakini pia mashudu kwa maana ya mabaki yanayotokana na alizeti yamekuwa yakichanganywa na virutubisho vingine kwa ajili ya kupata chakula cha mifugo. Sote tunafahamu mbali na kilimo Jeshi la Kujenga Taifa linajishughulisha na ufugaji wa ng’ombe, mbuzi, kondoo, kuku,”amesema.

Amesema tathimini imeshafanyika na maeneo yameshafanyiwa tathimini ( survey) kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vikubwa vya kuongeza thamani na kuwa wakipata fedha watakwenda kujenga.

Ametoa mfano wa maeneo waliyokwenda kuyatazama kuwa ni Kikosi cha JKT Chita,mkoani Morogoro ambapo wanalima mpunga kwa kutumia teknolojia ya kisasa na kuwa wakiweza kulima ekari zote 12,000, watahitaji kuwa na viwanda.

“Eneo lile limeshatengwa pale na tiyari hata ule mchakato wa kufuatilia katika baadhi ya nchi kuona kuwa kiwanda amcaho wakiweza umeshafanyika na pia hata katika vikosi ambavyo vinalima mazao mbalimbali kuweza kuongeza thamani. Kwa mfano hapa kwenye mchikichi kuweza kuwa na kiwanda kikubwa kitakacvhoweza kuchakata mafuta na mabaki kwenda kutumika kuzalisha,”amesema.


Kuhusu gharama, amesema zinatofautiana kati ya kiwanda na kiwanda ambapo kiwanda wanachotarajia kukijenga Chita mkoani Morogoro kinatarajiwa kugharimu Sh3 bilioni.
Amesema kiwanda hicho kitakuwa na sehemu ya kutengeneza chakula cha kuku.

Kwa upande wake Kamanda Kikosi cha 821 KJ Bulombora, Luteni Kanali Juma Hongo,amesema wamekuwa wakipokea maombi ya miche ya michikichi kutoka maeneo mbalimbali na hadi kufikia jana walikuwa wamegawa miche zaidi 300,000.

“Kama SUA (Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine), kimechukua miche na wametueleza maendeleo ni mazuri sana lakini kuna mabalozi ambao wako nje ya nchi wametuletea mrejesho mambo ni mazuri, kumekuwa na mahitaji makubwa. Hii inaonyesha kuwa JKT imetekeleza vyema maagizo ya Serikali,”amesema.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kimkakati ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Brigedia Jenerali Hassan Mabena,akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua mradi wa kilimo cha mchikichi katika Kikosi cha 821 KJ Bulombora mkoani Kigoma.


Kamanda Kikosi cha 821 KJ Bulombora, Luteni Kanali Juma Hongo,akielezea jinsi walivyojipanga kuzalisha miche ya michikichi kwa ajili ya kuwagawia wananchi miche hiyo.



Mwenyekiti wa Kamati ya Kimkakati ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Brigedia Jenerali Hassan Mabena,akikagua mradi wa kilimo cha mchikichi katika Kikosi cha 821 KJ Bulombora mkoani Kigoma mara baada ya kufanya ziara yake ya kukagua mradi huo.


Muonekano wa mbegu za kisasa za mchikichi zinazozalishwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) katika Kikosi cha 821 Bulombora mkoani Kigoma.
Share:

Thursday 2 May 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 3, 2024

Magazeti

Share:

CDF MKUNDA AELEZA UMUHIMU WA JKT KATIKA ULINZI WA TAIFA





MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akikagua gwaride kabla ya kufunga mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba



MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akikagua gwaride kabla ya kufunga mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba



MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akizungumza wakati alipofunga mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba




Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi la Ulinzi Tanzania Brigedia Jenerali Abubakari Charo akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba


Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Elias Sikaponda akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba




MKUU wa Kikosi cha Jeshi 838 JKT Maramba Kanali Ashraf Hassan akizungumza wakati wa mafunzo hayo





Na Oscar Assenga,MKINGA.


MKUU wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Jacob Mkunda amesema mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba huku akieleza umuhimu wa vijana hao ni mkubwa kutokana na kwamba wanaingia kwenye Jeshi la akiba ambalo inapotokea hitajiko la ulinzi wa Taifa wanaitwa kwa mujibu wa sheria.

Jenerali Mkunda aliyasema hayo Jumanne Aprili 30 mwaka huu wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo ambapo aliwakilishwa na Brigedia Jenerali Abubakari Charo ambapo alisema kutokana na miongozo mbalimbali iliyopo kwa mafunzo hayo ya vijana hasa kwa kuzingatia kwamba vijana hao wanapohitimu mafunzo yao wanaingia kwenye jeshi la akiba.

Alisema kwamba linapotokea hitajiko la ulinzi wa Taifa na Rais na Amri Jeshi Mkuu akatangaza hali ya hatari vijana hao wanaitwa kwa mujibu wa sheria kwenda kuungana na Jeshi la Wananchi (JWTZ) kulinda ulinzi wa Taifa.

Aidha alisema kutokana na umuhimu wa vijana kwenye Jeshi hilo wanapenda kuona wanafikia viwango na malengo ya mafunzo hayo na amewaona wamefikia viwango vinavyotakiwa huku akieleza yanawajenga kwenye nidhamu, ukakamavu, uzalengo, uhodari wa kujiamini na kulipenda taifa lao.

“Nichukue fursa hii kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi kutoa shukrani kwa dhati kwa Serikali kwa juhudi zinazofanyika kuhakikisha mazingira ya mafunzo kwa vijana ndani ya JKT yanaboreshwa”Alisema

“Kwani katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetoa kiasi cha sh Milioni 950 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni kwa vijana wanaojiunga na JKT fedha hizo zimeweza kujenga mabweni 12 kila moja lenye uwezo wa kuchukua vijana 120 hivyo kusaidia kikosi kuongeza uwezo kuchukua vijana 1440 na hii ni ishara za wazi kwamba serikali inatambua na kuthamini mafunzo ya vijana wa JKT”Alisema

“Lakini pia ujenzi wa vyoo vitano ambapo kila choo kina matundu 22 vitatumika kwa vijana hilo sio suala dogo ni jambo kubwa ambalo serikali imefanya kwa mazingira hayo wanawaomba vijana ambao hawapati fursa kujiunga na JKT wasije kufikiria wametengwa na kunyimwa fursa bali lengo vijana wote wapite Jkt na wale vijana wanaomaliza kidato cha sita”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba Jeshi la Kujenga Taifa litakuwa likiendelea kuongozewa uwezo huku akieleza wanathamini juhudi za serikali katika kuboresha mazingira ya jeshi hilo ambapo mafunzo ambayo wameyapata yatawawezesha kuajiriwa kwenye vyombo vya ulinzi na usalama,sekta mbalimbali za serikali au makampuni mbalimbali .

Awali akizungumza wakati akifunga mafunzo hayo Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian alisema mafunzo hayo kwa vijana wa JKT ni muhimu sana kwa vijana kwa maana wao ndio tegemeo la Taifa.

Balozi Batilda alisema Rais Dkt Samia Suluhu kupitia falsafa yake ya 4R ameendelea kusimamia na ndio maana juzi chadema walikuwa na maandamano yao wakasimamiwa vizuri na jeshi la Polisi wakafanya mkutano wao wakatembea.

Alisema kwa hakika wakawa na matumaini watapata mambo ya msingi yatakayowasaidia kujenga nchi lakini wakasikia mambo tofauti kwanini wakuu wa mikoa hawapigiri kura, kama madiwani sasa akasema hata RC akipigiwa kura atachaguliwa Tanga na RC ni msaidizi wa Rais anaweza kuhamishwa kila eneo .


“Tulitegemea kwamba hivi sasa nchi ipo kwenye kipindi kigumu na mvua zinanyesha madhara maeneo mengi barabara nyingi zimepata changamoto na maeneo mengi lami zimepasuka changamoto ni nyingi vita vya israel vinaendelea duniani gharama zinapanda bei ya dola ipo kubwa kulingana na bei yetu sisi tukaona haja hoja zao za za kwamba hazikuwasaidia wakapata mawazo mbadala hazipo"Alisema

Hata hivyo Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Elias Sikaponda alisema kwamba alisema mafunzo hayo ni muhimu kwa sababu yanaleta tija kwa vijana katika shughuli za kujitegemea huku akiwataka kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya

Aliwataka pia vijana hao kutumia elimu waliyoipata wakaweze kutatua changamoto mbalimbali pasipo kuvunja sheria na taratibu zilizowekwa hapa nchini huku akisiistiza watumie nidhamu pekee kama silaha kwenye jambo lolote mbeleni.
Share:

Wednesday 1 May 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MEI 2, 2024



















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger