Friday 14 May 2021

Forensic investigations Intern at Absa

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Bring your possibility to life! Define your career with us With over 100 years of rich history and strongly positioned as a local bank with regional and international expertise, a career with our family offers the opportunity to be part of this exciting growth journey, to reset our future and shape our destiny as a […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Communications Coordinator at Rivertrees Country Inn

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Rivertrees Country Inn is looking for a dynamic and experienced person to take the role of Communications Coordinator, based in Arusha Tanzania. The Communications Coordinator mission is to oversee and execute the Company’s communications strategies to external parties including developing the brand image, monitoring press releases, company articles and other related materials for business promotion […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Picha : MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO AZURU KABURI LA HAYATI DKT. JOHN POMBE MAGUFULI



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, akizuru Kaburi la aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli wakati aliposili na mama kwa muda Wilayani Chato alipokuwa njiani akielekea Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma kwa ajili ya kufunga Kampeni za Chama cha Mapinduzi CCM za Jimbo la Muhambwe kwa ajili ya Uchaguzi Mdogo wa Kiti cha Ubunge unaotarajiwa kufanyika Jumapili tarehe 16 Mei 2021 kufuatia Kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Hayati Nditye.
Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais

Share:

Fundraising and Communications Manager at TATU Project

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Fundraising and Communications Manager TATU Project is a non-profit organization that facilitates equal and sustainable development for the rural community of Msitu wa Tembo and Londoto in Northern Tanzania. We address community needs and build effective solutions through active collaboration with members of the community and relevant stakeholders. The communication &department fundraising TATU Project is […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Zanzibar Director at D-tree International

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Reports to:        Global Program Director Location:              Zanzibar, Tanzania Start Date:          Immediate opening (June 2021 or earlier if possible) Who we are D-tree International is on a mission to radically improve health by strengthening health systems through innovations in digital technology. D-tree works through partnerships with Ministries of Health and NGOs to bring humancentered design approaches […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Deputy Director at D-tree International

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Who we are D-tree International is a global digital health organization committed to improving lives by ensuring that everyone has access to quality primary healthcare in underserved areas. We do this by supporting governments to build and deploy digital tools for frontline health workers to improve their ability to deliver high-quality, evidence-based care. D-tree collaborates […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Enrolment Manager at International School of Tanganyika

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Title. Enrolment Manager Category (cf Policy 5.101): Administrative Management and Technical Support Reports to: School Director Department: Admissions, Marketing and Communications Start date: 1 August 2021 IST Foundational DocumentsIST Mission Challenging, inspiring and supporting all our students to fulfil their potential and improve the world IST Vision IST will be a global leader in the […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

MAZISHI YA MKURUGENZI WA PRINCESS RECORDS 'CHIEF CHRISS' KUFANYIKA KESHO LALAGO MASWA

Chief Chriss enzi za uhai wake
***
Mazishi ya Mwili wa Mkurugenzi wa Studio ya Princess Records, Christopher Joseph Mayenga maarufu Chief Chriss aliyefariki dunia Mei 12,2021 yanatarajiwa kufanyika kesho Jumamosi Mei 15,2021 mchana katika makaburi ya Mwandete Lalago wilayani Maswa mkoani Simiyu.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 14,2021




















Share:

Thursday 13 May 2021

Taarifa Ya Chama Cha Mapinduzi Kuhusu Mwenendo Wa Kampeni Za CCM Majimbo Ya Buhigwe Na Muhambwe Kuelekea Uchaguzi Wa Marudio


Chama Cha Mapinduzi kilifanya uzinduzi wa kampeni za ubunge katika Jimbo la Muhambwe tarehe 4 Mei 2021 na Jimbo la Buhigwe tarehe 5 Mei 2021 ukiongozwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa Ndugu Kassim Majaliwa.

Chaguzi hizi ni kutokana na kufariki kwa Mbunge wa Jimbo la Muhambwe Ndg. Atashasta Nditye na Mbunge wa Buhigwe, Ndugu Philip Mpango aliyeteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ifuatayo ni tathimini fupi ya Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa marudio katika majimbo hayo ya Muhambwe na Buhigwe.

Lengo kubwa la kampeni za CCM ni kutekeleza majukumu yafuatayo;

i.    Kutangaza Sera na Ilani ya CCM, kuwaeleza wananchi jinsi tulivyojipanga kuwaletea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

ii.    Kuwanadi kwa wananchi (wapigakura) wagombea wetu Dkt Frolence George Samizi wa Jimbo la Muhambwe na Mwalimu Eliadory Felix Kavejuru wa jimbo la Buhigwe.

Majimbo ya Buhigwe na Muhambwe ni ya CCM. Tulipoteza Mbunge wa CCM kwa kifo kule Muhambwe, hivyo wananchi wanachokitaka ni kuifariji CCM. Kwa Jimbo la Buhigwe wananchi wenyewe wanataka kumpa ahsante Mhe Rais Samia kwa kumteua Makamu wa Rais aliyekuwa mbunge wao Dkt Philip Mpango.

CCM imedhihirisha kivitendo uwezo wake mkubwa wa kuwatumikia wananchi katika awamu zote za uongozi. Kazi kubwa ya kisera na utekelezaji wa miradi, kuondoa kero imefanyika  chini ya CCM kwenye majimbo ya Muhambwe na Buhigwe hivyo ushindi wa CCM ni jambo lisilo na shaka  wala wasiwasi.

Mfumo wa Kampeni kwa Wagombea wetu ulijielekeza katika kufanya zaidi mikutano midogo, kukutana na kuzungumza na makundi ya kijamii katika maeneo yao/makazi/vijiji vyao.

Dkt Florence George Samizi amefika katika Kata zote 19 na amefanya mikutano midogo ya Kampeni na kukutana na makundi maalum ya Vijana, Wanawake, Wazee, Wafanyabiashara na makundi mengine ya kijamii. Wakati wote wa kampeni wananchi wamejitokeza kwa wingi kuhudhuria katika mikutano yetu ya Kampeni jimboni humo na kuonyesha matarajio yao kwa mgombea wa CCM Dkt Samizi.

Ndg  Eliadory Felix Kavejuru amefanya kampeni katika Kata zote 20, na kukutana na wananchi katika Vijiji 44 sawa na asilimia 100 ya vijiji vyote na anaendelea kumalizia kampeni katika vitongoji vinane (8) vilivyobaki kati ya 192.

Mikutano mikubwa imefanywa kimkakati katika viwanja vya Shule ya Msingi Buhigwe, Munanila, na Muyama maeneo hayo yana wakazi wengi  waliojiandikisha katika kupiga  kura. Mikutano midogo 62 aliyoifanya Mgombea wa CCM Ndugu Kavejuru pamoja na mazungumzo mahsusi na makundi ya kijamii yamemkutanisha na kumpa uhakika zaidi wa kupata ushindi .

Chama kimezishirikisha Jumuiya  zake zote katika kampeni za majimbo ya Muhambwe na Buhigwe pamoja na kuwatumia makada wake mbali mbali ambao wote tulia na lengo moja la kupata ushindi.

Viongozo na Makada hao wamekuwa wakihutubia mikutano  ya hadhara kwa kutumia sera za chama Sera nzuri za CCM ambazo zimekuwa zikitekelezeka na kuleta manufaa kwa wananchi

Kampeni za CCM katika Majimbo yote mawili zitafungwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa Nd. Philip Isdor Mpango tarehe 14 na 15 Mei 2021 katika uwanja wa Taifa kwa jimbo la Muhambwe na uwanja wa shule ya Mayama kwa jimbo la Buhigwe.

Tathmini ya awali imeonesha katika majimbo hayo CCM itashinda si chini ya 80% na ikumbukwe ushindi huu hautakuwa mgeni kwetu kwani CCM ni kinara na baba wa mageuzi ya demokrasia ya nchini, Afrika Mashariki na Kati.

Nilisema Siku ya uzinduzi na ninaendelea kusisitiza CCM itashinda Buhingwe na Muhambwe  kwa haki, amani na utulivu mkubwa pamoja na yote lakini ya sababu kubwa za ushindi ni imani kubwa walionayo wananchi kwa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na Chama Cha Mapinduzi.

Chini ya Uenyekiti wa CCM wa ndugu Samia Suluhu Hassan tutaendelea kuvilea vyama vya siasa chini ili viendelee kufanya siasa safi na yenye tija kwa Taifa baada ya kufanya siasa za danadana. Sote tunajenga nyumba moja hakuna sababu kugombeana fito.

Ikumbukwe kuwa tokea siasa za nchi hii kuanzia TANU hatimae CCM Chama chetu hakijawahi kufanya makosa katika mambo ya msingi yanayohusu maslahi ya Taifa tunakumbusha kuwa uchaguzi wa Buhingwe na Muhambwe umebeba maslahi mapana ya Taifa kwa maana unakwenda kuzalisha wabunge wanakwenda kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan katika kuleta maendeleo endelevu ya kiuchumi, kijamii na kisiasa hivyo hatuwezi kufanya makosa.

Tumejipanga kuhakikisha Wanachama wetu waliojiandikisha wanajitokeza kwa wingi katika vituo vya kupigia kura na kuwachagua Wabunge wanaotokana na Chama chao pendwa.

Aidha tunatoa wito kwa vyama vingine na wananchi kwa ujumla kuendelea kudumisha  amani, usalama na utulivu ambao umekuwepo  wakati wote wa kampeni zetu.

Imetolewa na;

SHAKA HAMDU SHAKA
KATIBU WA H/KUU - ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI
13 MEI 2021


Share:

Waziri Mchengerwa Azitaka Taasisi Za Kifedha Kutoa Mikopo Kupitia Hatimiliki Zinazotolewa Na MKURABITA

 


Na. James K. Mwanamyoto-Zanzibar
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amezitaka taasisi za kifedha nchini kutoa mikopo kwa wananchi wenye hatimiliki za kimila zinazotolewa na Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) ili kuwawezesha wananchi hao kuendesha shughuli zao na kuinua kipato.

Akikabidhi hatimiliki hizo kwa baadhi ya wananchi wa Shehia ya Welezo, Zanzibar, Mhe. Mchengerwa amesema, hatimiliki hizo zinalenga kutoa fursa kwa wananchi kupata mikopo itayowawezesha kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo na biashara ili kuboresha maisha yao.

“Taasisi za kifedha zitambue hatimiliki hizi na kupunguza masharti ili kuwawezesha wafanyabiashara wadogo kukopa na kuongeza mtaji.” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.

Akiwa katika kituo Jumuishi cha Urasimishaji na Uendelezaji Biashara kilichoko katika Baraza la Biashara, eneo la Darajani Wilaya ya Mjini, Mhe. Mchengerwa amezitaka pia taasisi za kifedha kutoa mikopo kwa wajasiriamali waliorasimisha biashara zao na kuongeza kuwa, mikopo hiyo itawaongezea mitaji ya kuendesha shughuli zao za ujasiriamali.

Kutokana na uwepo wa kituo hicho, Mhe. Mchengerwa amehimiza zoezi la urasimishaji biashara lisichukue muda mrefu ili kutoa hamasa kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kurasimisha biashara zao.

Akieleza mchango wa ofisi yake katika zoezi la urasimishaji biashara, Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum amesema kituo hicho kimejengwa ili kuondoa changamoto za urasimishaji walizokuwa wakikutana nazo wafanyabiashara wadogo.

Dkt. Salum ameongeza kuwa kutokana na faida za uwepo wa kituo hiki, Serikali imedhamiria kujenga kituo kama hiki Pemba ili wananchi wa eneo hilo nao waweze kunufaika.

Naye Mratibu wa Mkurabita, Dkt. Seraphia Mgembe amesema utekelezaji wa MKURABITA Zanzibar umewanufaisha wananchi wa Zanzibar kwa kuwapatia mafunzo ya utunzaji wa kumbukumbu za biashara ambapo hivi sasa wanazo takwimu sahihi za maendeleo ya biashara zao.

Mhe. Mchengerwa amehitimisha ziara yake ya kikazi Zanzibar ya kukagua miradi inayotekelezwa na taasisi zilizo chini ya ofisi yake ikiwa ni pamoja na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa Sekretarieti ya Ajira ofisi ya Zanzibar.


Share:

Wizara ya Maliasili na Utalii Yafungua Milango Mipya Ya Uwekezaji Katika Maeneo Ya Uhifadhi Nchini


Wizara ya Maliasili na Utalii imefungua milango mipya katika Sekta ya Utalii nchini kwa kutia saini ya  Uwekezaji wa kimkakati katika  maeneo ya Uhifadhi nchini kwa Wawekezaji wenye mitaji mikubwa wa kutoka ndani na nje ya nchi.

Ameyasema hayo leo Jijini Dodoma, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro   wakati akitia saini  kanuni za Uwekezaji wa kimkakati katika maeneo ya Uhifadhi nchini.

Waziri wa Maliasili na Utalii amesema utiaji saini huo ni miongoni mwa  njia  zitakazochangia kuongeza idadi ya Watalii kufika milion 5  na mapato yapatayo bilion 6 ifikapo mwaka 2025 kupitia Sekta ya Utalii nchini.

Kwa mujibu wa Kanuni hizo Wawekezaji wataweza kuwekeza katika maeneo ya Mapori ya Akiba, Mapori Tengefu pamoja na Maeneo ya Wazi ya Wanyamapori kwa miaka isiyopungua 25.

Akizungumza kabla ya utiaji saini huo, Waziri Dkt.Ndumbaro amesema kanuni hizo zimelenga Wawekezaji wenye mitaji mikubwa ambao hata watalii watakaokuja katika maeneo hayo ni Watalii wenye fedha nyingi ikiwemo watu maarufu duniani.

Amesisitiza kuwa kanuni hizo zitawezesha Wawekezaji hao kujenga mahoteli katika maeneo ya Uhifadhi pamoja na kuweka miundombinu ya Utalii itakayosaidia kuwavutia Watalii wengi kutembelea katika maeneo hayo.

Awali amesema kanuni hizo ni mpya na uwekezaji huo katika maeneo hayo utakuwa wa aina yake kwa vile umelenga Wawekezaji wenye mitaji mikubwa watakaowavutia Watalii matajiri hali itakayopelekea pato la taifa kuongezeka maradufu kupitia sekta ya utalii nchini.

Awali Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania ( TAWA) Meja Jenerali ( Mstaafu)  Hamis Semfuko amesema utiaji saini wa kanuni  ni moja ya hatua muhimu ya kupanua fursa zitokanazo na sekta ya utalii nchini.

” Tuliamua kuja na wazo hili ili Wawekezaji wenye mitaji mikubwa waweze kuwekeza katika maeneo ya Uhifadhi ambapo awali uwekezaji wa namna hii ulikuwa hauwezekani” alisisitiza Mwenyekiti huyo Meja Jenerali ( Mst) Semfuko

Kwa upande wake , Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt.Allan Kijazi amesema atahakikisha Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, ( TFS ) nao wanasaini kanuni za namna hiyo nao waweze kuwavutia Wawekezaji kuwekeza katika maeneo yao kwa vile wa maeneo yenye sifa kawa yalivyo ya TAWA


Share:

Zaidi Ya Bilioni 7 Zatumika Kufikisha Umeme Kisiwa Kilichopo Ziwa Tanganyika


Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kupitia Nakuroi Investment Co. Ltd inayotekeleza Mradi wa awamu ya tatu mzunguko wa kwanza wanaendelea na zoezi la kulaza nyaya chini ya maji katika ziwa Tanganyika ili kufikisha umeme katika kisiwa cha Mandakerenge, kilichopo kata ya Kipili Wilayani Nkasi, Mkoani Rukwa.

Zoezi hilo litakalogharimu zaidi ya shilingi bilioni 7 ni la kipekee kufanyika katika ziwa Tanganyika, na mikoa ya kanda ya ziwa, hali iliyopelekea Meneja wa Tanesco Mkoa wa Mwanza na timu kutoka makao makuu ya Shirika la umeme nchini (TANESCO) kufika katika eneo hilo na kujifunza utandazaji wa nyaya hizo ili kuja kuutumia ujuzi huo kufikisha umeme kisiwani Ukerewe, Mkoani Mwanza.

Akiongea wakati wa kushiriki kulaza nyaya hizo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amesema kuwa tukio hilo linaonesha ni kwa namna gani serikali inavyowatahamini wananchi wake na kuzingatia haki zao za kupata huduma za kijamii saw ana watu wanaoishi katika mengine ya nchi.

Aidha amewapongeza wazamiaji wazawa wanaofanya kazi hiyo, TANESCO Mkoa Pamoja na Mkandarasi wa Mradi huo pamoja na kuwaomba wananchi wa kisiwa na Kijiji cha Mandakerenge kuutumia umeme huo vizuri ikiwa ni pamoja na kuanzisha viwanda vya kuchakata samaki pamoja na mashine za kusaga na kukoboa

“Serikali ya Tanzania inathamini wananchi popote pale walipo na umeme huu utakwenda kila mahali ndani ya vijiji vyetu vya mkoa wa Rukwa, baada ya kufikisha umeme katika kisiwa cha Mandakerenge itakuwa ni takriban vijiji 181 vitakuwa vimefikiwa na umeme na nimeambiwa huyu mkandarasi Nakuroi amebakiza kama vijiji viwili vitatu ili vitimie vijiji 184 ambavyo vitakuwa vinapata umeme na vijiji vinavyobaki kama 155, hivi vijiji vitapata umeme ndani ya kipindi cha mwaka mmoja na nusu,” Alisema.

Amesema kuwa katika ya vijiji hivyo 155 vilivyobaki, vijiji 125 vimeingizwa katika mradi wa awamu ya tatu mzunguko wa pili na vijiji 30 vimeingia kwa maombi maalum na hivyo kufanya jumla ya vijiji vya mzunguko wa kwanza na wapili kuwa 339 ambavyo ni idadi ya vijiji vilivyopo mkoani Rukwa.

Kwa upande wake Meneja wa TANESCO Mkoa wa Rukwa Mhandisi Yusuf Ismail alieleza kuwa zoezi hilo lilitakiwa kukamilika ndani ya wiki nne lakini kutokana ushiriki mzuri wa wanakijiji katika mradi, hali nzuri ya hewa ziwani Pamoja na kasi ya kazi hiyo huenda zoezi hilo likamalizika chini ya muda uliopangwa.

“Serikali imewashirikisha wananchi ili kwanza wajue thamani ya mradi ambayo imewekezwa hapa lakini pia iwe ni kutoa elimu kwa wavuvi wengine au kwa wananchi wengine ambao wako ng’ambo ambao wanaweza kukutana na kitu kama hiki wajue thamani yake, mheshimiwa mkuu wa mkoa naomba nikushuruku kwa kuja kutupa moyo katika kazi hii naamini wazamiaji na wafanyakazi wote wa TANESCO tumfurahia ujio wako,” Alimalizia.

Kwa upande wake mwakilishi wa mkandarasi wa mradi huo wa REA Mkoani Rukwa Mhandisi Pascal Ndunguli alisema kuwa kwa upande wao walikabdihiwa kukamilisha mradi huo katika vijiji 137 na kati yahi vyo vijiji 135 tayari vimewashwa umeme na hivyo kubakiwa na vijiji 2 kimojawapo kikiwa ni hicho cha kisiwa cha Mandakerenge ambacho wanatazamia kukimaliza kabla ya mwezi wa sita mwaka huu.

“Mpaka sasa tupo hatua ya kulaza nyaya na baada ya hapo, wazamiaji watakuwa hawana kazi watafuata watu wa kitengo cha umeme na hivyo wahandisi watakuja kwaajili ya kukamilisha zoezi na baada ya hapo tutawaalika TANESCO kuja kufanya majaribio na kuthibitisha kuwa umeme unapita na kisha tutafikisha umeme katika Kijiji hicho na umeme utaanza kufanya kazi,” Alisema.

Katika ziara hiyo alikuwepo mwakilishi wa wavuvi na wanakijiji cha Kijiji cha Mandakerenge Seif Seba ambaye naye alitoa shukurani kwa serikali ya Tanzania, “Tunatoa shukurani za dhati kwa serikali yetu kwa kutujali kwa suala la kutuletea umeme hapo kisiwani na tunaiahidi serikali kuwa tutaulinda huu way ana hakuttotokea athari ya namna yoyote,” Alimalizia.

Kisiwa cha Mandakerenge kipo umbali wa km 1.2 kutoka bara ambapo shughuli kubwa za wanakijiji wa kisiwa hicho ni uvuvi na TANESCO wametandaza waya wenye urefu wa km 1.7 kutoka bara kwenda kisiwani ili wanakijiji hao nao wafaidike na mradi huo.


Share:

Taarifa Ya Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mbeya


KUKAMATWA KWA WATUHUMIWA WA MATUKIO YA UVUNJAJI NA WIZI.


Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa wawili 1. KELVIN TOBIAS [32] fundi kuchomelea, mkazi wa Iyela na 2. JOSHUA AMBAKISYE [18] mkazi wa Mwanjelwa jijini Mbeya kwa tuhuma za kujihusisha na matukio mbalimbali ya uvunjaji na wizi katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Mbeya.

Watuhumiwa wamekamatwa katika misako inayoendelea katika maeneo mbalimbali ndani ya Jiji la Mbeya na wamekiri kujihusisha na matukio ya uvunjaji na wizi. Katika upekuzi uliofanywa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya katika maeneo ambayo watuhumiwa wamekiri kuuza mali za wizi, mali zifuatazo zimepatikana:-
  1.     Kompyuta 2 [Desk top] aina ya HP,
  2.     Laptop 2 aina ya HP na Dell.
  3.     CPU 2 aina ya Dell,
  4.     TV flat screen aina ya Hicence inchi 55,
  5.     TV flat screen aina ya LG inchi 32,
  6.     TV flat screen aina ya Singsung inchi 32,
  7.     TV flat screen aina ya Samsung inchi 32,
  8.     Mitungi miwili mikubwa ya gesi Oryx,
  9.     Mitungi mitatu midogo ya gesi Oryx,
  10.     Redio Sub-woofer 6 aina tofauti,
  11.     Jiko moja la Gesi aina ya Afrox,
  12.     Blanketi 13,
  13.     Saa 2 za ukutani na
  14.     Redio 2 mali ya wizi.

Upelelezi unaendelea ili kubaini mtandao mzima wa matukio ya uvunjaji na wizi wa mali mbalimbali. Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa wananchi walioibiwa mali zao kufika kituo kikuu cha Polisi Mbeya Mjini kwa ajili ya  utambuzi wa mali zao.

KUKAMATWA KWA MTUHUMIWA WA TUKIO LA MAUAJI.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa GODLOVE PIMBI [50] Mkazi wa Lusonjo – Kisyosyo kwa tuhuma za mauaji ya mke wake aitwaye ELIZABETH MWAIKE [22] Mkazi wa Lusonjo – Kisyosyo.

Tukio hili limetokea mnamo tarehe 11.05.2021 nyumbani kwa mtuhumiwa huko Kijiji cha Kisyosyo kilichopo Kata ya Matema, Tarafa ya Ntebela, Wilaya ya Kyela, Mkoa wa Mbeya.   

Chanzo cha tukio hili ni wivu wa kimapenzi. Mwili wa marehemu ulikutwa umbali wa mita 500 kutoka nyumbani kwake ukiwa na jeraha la kupigwa na kitu kizito kichwani. Upelelezi wa tukio hili unaendelea na mara baada ya kukamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi ULRICH MATEI anatoa rai kwa jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi dhidi ya migogoro ya kimapenzi na badala yake watafute suluhisho kwa kukaa meza moja ya mazungumzo ili kutatua migogoro hiyo.

ASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA MAUAJI.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia CHIKU ABOUBAKARI [41] Mkazi wa DDC – Mbalizi kwa tuhuma za mauaji ya ROSE MWANDANJE [45] Mfanyabiashara na Mkazi wa DDC – Mbalizi.

Tukio hilo limetokea tarehe 11.05.2021 majira ya saa 20:00 usiku huko Mtaa wa DDC – Mbalizi uliopo Kata ya Utengule – Usongwe, Tarafa ya Usongwe, Wilaya ya Mbeya Vijijini, Mkoa wa Mbeya ambapo marehemu ROSE MWANDANJE [45] Mkazi wa DDC – Mbalizi aliuawa kwa kukatwa panga sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo nyuma ya shingo na viganja vya mikono yote kutoka na mtu / watu wasiofahamika akiwa sebuleni katika nyumba anapoishi.

Chanzo cha tukio hilo kinachunguzwa. Jeshi la Polisi mkoani hapa linaendelea na msako mkali dhidi ya watuhumiwa wengine waliohusika katika tukio hilo la kinyama. Aidha Jeshi la Polisi linaendelea kutoa rai kwa wananchi na watendaji wa mitaa kutoa ushirikiano kwa kuwafichua wahalifu ili wakamatwe na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

MTU MMOJA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUANGUKIWA NA KIFUSI.

Mtu mmoja aitwaye MWASHALA NYUNDURU [32] Mkazi wa Kabwe Jijini Mbeya alifariki dunia baada ya kuangukiwa na kifusi cha mchanga akiwa anafanya shughuli za uchimbaji mchanga katika eneo la Shewa.

Tukio hili limetokea tarehe 11.05.2021 majira ya saa 17:33 jioni huko maeneo ya Mtaa wa Shewa, Kata ya Mwakibete, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya wakati marehemu akiendelea na shughuli za uchimbaji mchanga akiwa na wenzake. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi ULRICH MATEI anatoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari wakiwa katika shughuli za uchimbaji ili kuepuka madhara yanayoweza kuepukika hasa katika kipindi hiki ambacho mvua za mwishoni zinaendelea kunyesha.



Share:

SUPER – NHESHA: Dawa Bora Ya Kutibu Tatizo La Kisukari


SUPER – NHESHA
Ni dawa ya kutibu tatizo la sukari au jina la kitaalamu (Diabetes Mellitus) ni kundi la magonjwa yanayohusiana na ufanyaji kazi wa mwili ambapo Mtu anakuwa na kiwango kikubwa cha sukari aina ya Glucose katika mwili kutokana na mwili wake kukosa uwezo wa kutengeneza Insulin ya kutosha au seli za mwili wake kutumia insulin iliyopo au pengine mwili kuwa na matatizo yote kwa pamoja na kupelekea mgonjwa wa sukari kupata haja ndogo mara kwa mara (Polyuria) uhisi kiu kila wakati (Polydipsia) Na (Polyphagia).


AINA YA KISUKARI
Kuna aina chache tofauti za ugonjwa wa kisukari (1) ni ugonjwa wa Auto hii aina mgonjwa wa Auto hushambulia mfumo wa kinga na kuharibu seli katika kongosho ambako insulin huzalishwa asilimia 10% ya watu wenye ungonjwa wa kisukari wanayo aina hii (Auto).


AINA YA PILI
Hii hutokea wakati mwili wako unakuwa sugu kwa insulin na sukari hujenga katika damu yako hii husababishwa na kuwa na sukari nyingi kwenye damu yako kuliko kawaida.


CHANZO CHA UGONJWA SUKARI
Viko vyanzo vingi mbalimbali vya sukari
1.     Shinikizo la damu (B.P)
2.     Viwango vya juu vya triglyceride (mafuta)
3.     Lishe yenye mafuta mengi na wanga
4.     Utumiaji mkubwa wa pombe kupita kiasi
5.     Ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi
6.     Mtindo wa maisha usiofaa kiafya
7.     Uzito na unene uliozidi
8.     Kutofanya mazoezi
9.     Umri
10.     Kurith


UNAJUAJE KUWA UNADALILI ZA KISUKARI
1.     Kusikia njaa mara kwa mara
2.     Kusikia kiu mara kwa mara
3.     Kupungua uzito
4.     Maono machafu
5.     Uchovu mara kwa mara
6.     Ukipata kidonda hakiponi
7.     Kushuka kwa kinga mwili


DALILI ZA KISUKARI KWA MWANAUME
Mbali na dalili za jumla za ugonjwa wa sukari wanaume wenye tatizo hilo wanakuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kushindwa kufanya tendo la ndoa uume hushindwa kusimama misuri hulegea na kusinyaa, maumivu ya mgongo, kiuno, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kupata choo  kama cha mbuzi


DALILI ZA WANAWAKE
Wanawake wenye ugonjwa wa sukari wanaweza pia kuwa na dalili kama vile maambukizi kwa njia ya mkojo (U.T.I) maambukizi  ya gonzi kukakamaa


TIBA YA MAGONJWA YA SUKARI
Ugonjwa wa sukari unatibika bila kujali ni mda gani umepata hilo tatizo wengi wamekata tama na kuwa wabishi amini tatizo hili linatibika vizuri sana wengi wemepona.


Tumia dawa ya SUPER-NHESHAambayo ni dawa ya miti shamba yaani (asilia) ambayo humfanya mtu kupona na kuimalika kabisa.


Tutakuelekeza pia mfumo wa mtindo wa maisha utakao takiwa kutumia ili kutoluhusu tatizo hilo kurudi tena.


BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO/KANISANI NJIA PANDA YA KWENDA SINZA  SIMU: 0652 102 152/0788 330 105/ 0755 684 297 NYOTE MNAKARIBISHWA PIA TUNATUMA MIKOANI WHATAPPS NO 0652 102 152 



Share:

Watatu washikiliwa kwa tuhuma za mauaji Moshi


 Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro linawashikilia watuhumiwa watatu kwa madai ya kuhusika na tukio la mauaji ya kijana wa bodaboda, Rogers Kesy, mkazi wa Mnazi- Kiboroloni, Manispaa ya Moshi.


Akisimulia tukio hilo mbele ya waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Amon Kakwale amesema mmoja wa watuhumiwa, Sifael Sarun alimkodisha marehemu ampeleke nyumbani kwake lakini baada ya kufikishwa nyumbani alimuua kijana huyo kwa kumpiga na nyundo kichwani na kisha kumnyonga na waya shingoni.

Kamanda Kakwale amesema mara baada ya mtuhumiwa huyo kutekeleza mauaji hayo waliuweka mwili wa kijana huyo kwenye mfuko wa sandarusi na kuutupa pembeni mwa barabara kuu ya Moshi - Himo.

Amesema Sifael Sarun alishirikiana na wenzake wawili Emanuel Sarun na Elia Laizer ambao wote wako chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi na kuwa uchunguzi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani.

Aidha, amesema Jeshi la Polisi limefanikiwa kukamata pikipiki yenye namba MC 880 AYR ambayo ilitumika kubeba mwili wa marehemu na kwenda kuutupa barabarani.




Share:

Mwalimu atuhumiwa kufanya mapenz kitanda kimoja na wanafunzi wawili

Mkuu wa  Wilaya  ya Magu mkoani Mwanza, Salim Kali, ameagiza kuhamishwa  wilayani kwake mwalimu anayetuhumiwa  kufanya mapenzi na wanafunzi watatu wa kike wa shule ya msingi ya Ilungu  katika kitanda kimoja.

Mwalimu huyo aliyetajwa na Mkuu wa wilaya kwa jina la Martin  Mambosasa anadaiwa kufanya vitendo hivyo kwa nyakati tofauti kwa miaka saba.

Mkuu huyo wa wilaya, alisema mwalimu huyo aliwahi kukamatwa na vyombo vya  dola na kufikshwa mahakamani, lakini akahonga wazazi wa watoto hao wakaharibu ushahidi.

Alitoa agizo hilo juzi kwenye kongamano la kuweka mikakati ya kukabiliana na ongezeko la vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto, mimba katika umri  mdogo na utoro kwa wanafunzi.

Alisema  mikakati hiyo itasaidia  kuongeza ufaulu na kwamba  mwaka 2020, takwimu zinaonyesha matukio ya ukatili wa kijinsia yalikuwa 304.

Alimuagiza mratibu Elimu wa  kata na ofisa elimu wa wilaya kumhamishia mwalimu huyo  sehemu nyingine Ili asionekane wilayani kwake.

"Huyu mwalimu amekuwa akidhalilisha watoto wadogo kwa kipindi kirefu na naagiza ahamishwe sitaki kumsikia wala kumuona hapa wilayani kwangu," alisema

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa  Wilaya ya  Magu,  Amandus Mboya alisema  mambo yanayochangia ongezeko la vitendo vya ukatili wa kijinsia ni pamoja na wazazi kushindwa kuwapatia huduma muhimu.

Alitaja huduma zingine wanazokosa kuwa ni pamoja na kukosa taulo za kike, mafuta ya kupaka pamoja  na kukosa fedha za kunyoa nywele 

 

Credit:Nipashe




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger