Thursday 20 January 2022

MABALOZI WA KODI WATEMBELEA MIKOA YA KASIKAZINI KUHAMASISHA ULIPAJI KODI

Afisa Afya kutoka Wizara ya Afya Bw. Mohamed Mtosa akitoa maelezo kwa Mabalozi wa Kodi walipotembelea Kituo cha Huduma kwa Pamoja cha Forodha Namanga mkoani Arusha. Kutoka kushoto ni Balozi Zulfa Omary, ambae ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kusini Pemba, Zanzibar, Balozi Bw. Edo Kumwembe na Balozi Subira Mgalu Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Pwani. Afisa Forodha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. James Mwasambili akitoa maelezo kwa Mabalozi wa Kodi waliotembelea Kituo cha Huduma kwa Pamoja cha Forodha Namanga mkoani Arusha. Kutoka kulia ni Meneja Msaidizi wa Forodha Kituo cha Namanga Bw. Paul Kamukulu, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi kutoka TRA Bw. Richard Kayombo, Balozi Zulfa Omary, ambae ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kusini Pemba, Zanzibar na Balozi Subira Mgalu Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Pwani.Mshauri wa Kodi Bw. Nikolaus Duhia (wa kwanza kulia) akitoa maoni yake wakati wa kikao kazi cha Mabalozi wa Kodi, baadhi ya Wafanyabiashara na Wadau wa Kodi wa Mkoa wa Arusha uliofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoani humo. Lengo la kikao kazi hicho ni kuwahamasisha wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiari na wakati.

Mkurugenzi wa kiwanda cha A to Z cha mkoani Arusha akiwaonesha Mabalozi wa Kodi bidhaa mbalimbali wakati Mabalozi hao walipofanya ziara kiwandani hapo. Lengo la ziara hiyo ni kuwahamasisha wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiari na wakati.

Baadhi ya Mabalozi wakiangalia bidhaa zilizotengenezwa na kiwanda cha A to Z cha mkoani Arusha wakati Mabalozi hao walipofanya ziara kiwandani hapo. Lengo la ziara hiyo ni kuwahamasisha wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiari na wakati.

(Picha na TRA)

*************************
Na Mwandishi wetu,Namanga

Mabalozi wa Kodi walioteuliwa na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) wako katika mikoa ya Kaskazini ambayo ni Arusha, Kilimanjaro na Tanga kwa ajili ya kuhamasisha wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiari ili kuongeza mapato ya Serikali.

Mabalozi hao wamepata fursa ya kutembelea Kituo cha Huduma kwa Pamoja cha mpakani Namanga mkoani Arusha na kukutana na baadhi ya wadau na walipakodi ambapo wamewahimiza kuendelea kulipa kodi kwa hiari na wakati.

Wakizungumza wakati wa ziara hiyo Mabalozi hao wa kodi, wameipongeza Serikali kwa kuwa na Vituo vya Huduma kwa Pamoja mipakani kwani vimeondoa kero zilizokuwepo kipindi cha nyuma na kusifu ushirikiano uliopo katika ya TRA na wafanyabiashara ambao umesaidia Mkoa wa Arusha kuvuka malengo ukusanyaji mapato.

“Katika kituo hiki cha Namanga, nimejifunza mambo mengi, moja wapo ni namna nchi hizi mbili za Tanzania na Kenya zilivyoondoa urasimu uliokuwepo kipindi cha nyuma.

Nikiwa kama Balozi, nitatumia elimu hii niliyoipata kutoka TRA kuwahamasisha wananchi kujenga tabia ya kulipa kodi kwa wakati kwa maendeleo ya nchi yetu,” alisema Bw. Edo Kumwembe mmoja wa mabalozi hao.

Kwa upande wake Balozi Zulfa Omari, ambae ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kusini Pemba, Zanzibar akizungumza wakati wa kikao kati ya wafanyabiashara wa Arusha na mabalozi hao, alisema kuwa ni nadra sana kukuta wafanyabiashara wakiizungumzia vizuri TRA lakini amefarijika kuona walipakodi wa Arusha wakiipongeza TRA kwa kuboresha huduma zao.

“Kabla ya kuteuliwa kuwa Balozi kulikuwa na mambo mengi niliyokuwa nikiyasikia kuhusu TRA na yalikuwa yakiniumiza sana lakini hapa Arusha nimesikia kitu cha faraja kwamba TRA inazungumzwa vizuri mbele yetu kitu ambacho si kitu cha kawaida maana wafanyabiashara mara nyingi huwa hawaizungumzii vizuri TRA,” alisema Balozi Zulfa.

Balozi mwingine ni Subira Khamis Mgalu Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Pwani ambae alisema kuwa kupitia ziara hii amejifunza taratibu mbalimbali zinazotumika wakati wa uingizaji wa mizigo kutoka ndani na nje ya nchi kupitia Kituo cha Namanga.

“Kama Balozi nimefahamu kwa kina jinsi mifumo inavyofanya kazi katika kituo hiki cha Namanga ambayo huisaidia Serikali kukusanya mapato stahiki kutoka vyanzo mbalimbali.

Kwa upande wa walipakodi na wadau ambao tumekutana nao Arusha Mjini, naweza kusema kuwa, usemi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan umedhihilika wazi kuwa, kodi inaweza kukusanywa bila kutumia mabavu kwa sababu Mkoa huu wa Arusha umevuka malengo bila kuwasumbua walipakodi wake.”

Balozi Mgalu amewasisitiza walipakodi hao kuongeza ushirikiano kwa TRA ili kuendelea kulipa kodi kwa hiari na kuwaahidi kwamba, changamoto zote walizozitoa wamezipokea na watazifanyia kazi.

Kazi wanazozifanya Mabalozi hao wa Kodi katika ziara yao ya kikazi kwenye mikoa hiyo ya Arusha, Kilimanjaro na Tanga ni pamoja na kutembelea viwanda, kutembelea vituo vya huduma kwa pamoja mipakani na kukutana na wafanyabiashara kwa ajili kuwahamasisha kulipa kodi kwa hiari na wakati.
Share:

5G YAHARIBU SAFARI ZA NDEGE MAREKANI


Mashirika makubwa ya ndege Emirates, Air India, Air Nippon na Japan Airlines yamesitisha safari zake za kwenda Marekani kutokana na huduma ya mtandao wa 5G.

Jana asubuhi huduma ya mtandao wa 5G ilianza kutumika nchini Marekani kwa kuwashwa minara 4500 ya 5G.

Mashirika hayo ya ndege yamesitisha huduma zake nchini Marekani kwa madai kwamba mtandao wa 5G unaingilia mawasiliano ya ndege. Ndege za Boeing 777 mawasiliano yake huathiriwa na huduma ya 5G na kufanya kampuni hizo zitumie ndege nyingine.
Share:

WANAFUNZI WALIONUSURIKA AJALI YA LUCKY VINCENT WAFANYA MAAJABU KIDATO CHA IV



WANAFUNZI watatu walionusurika kwenye ajali ya Shule ya Lucky Vincent, wamefanya maajabu katika mtihani wa kidato cha nne na kufaulu vizuri kwenye masomo ya sayansi.

Wanafunzi hao ni Doreen Elibariki ambaye amepata daraja la pili, Wilson Godfrey (daraja la kwanza) na Sadia Awadh (daraja la pili).

Akizungumza kwa furaha kwa njia ya simu ya kiganjani, mzazi wa Sadia, Zaituni Abdul, alisema katika matokeo hayo anamshukuru Mungu kuwapigania watoto wao.

“Hakika namshukuru sana Mungu maana kwa matatizo waliyopitia hawa watoto sikutegemea kama watapata matokeo haya, hakika furaha yangu kubwa sana,” alisema.

Alisema mwanawe ndoto yake kubwa ni kuwa daktari wa binadamu au rubani.

Mama mzazi wa Doreen, Neema Mshana, alisema alipopata matokeo hayo alimuona Mungu akimshika mkono mwanawe na wenzake.

“Hakika Mungu mwema anajua waja wake na hajawaacha, naamini ataendelea kutembea na watoto hawa mpaka watakapofikia ndoto zao,” alisema.

Mwalimu wa darasa wa wanafunzi hao, Pascal Safari, aliwapongeza watoto hao kupata ufaulu mzuri licha ya matatizo waliyopitia.

Alisema katika darasa lao walikuwa jumla ya wanafunzi 65 ambao kati yao 26 wamepata daraja la kwanza akiwamo Wilson, 30 walipata daraja la pili akiwamo Doreen na mwenzake Sadia. Pascal alisema wanafunzi wengine nane walipata daraja la tatu na mmoja daraja la nne.

Alisema watoto hao ambao manusura ya ajali wote walikuwa mkondo wa sayansi na wamefaulu vizuri. “Naamini watoto hawa wanaweza kurudi hapa shuleni kuendelea na masomo yao ya kidato cha tano na sita kwani mazingira yaliyoko mazuri yanawafaa kuendelea na masomo,” alisema.

Wanafunzi hao walipata ajali ya gari Mei 6, mwaka 2017, wakati wakielekea kwenye Shule ya Tumaini Junior iliyoko wilayani Karatu kwa ajili ya kufanya mtihani wa kujipima.

Katika ajali hiyo wanafunzi 32, walimu wawili na dereva walifariki papo hapo eneo la Rhotia wilayani Karatu, huku wanafunzi hao watatu wakinusurika.

Baada ya ajali hiyo Shirika lisilo la kiserikali la STEMM chini ya mratibu wa safari hiyo, Lazaro Nyalandu, liliwasiliana na Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo nchini Marekani, Steve Meyer, ambaye kwa ushirikiano na serikali waliwezesha kupatikana kwa hati ya kusafiria haraka kwenda nchini Marekani kwa matibabu zaidi baada ya kugundulika kuvunjika mara 36 mwilini mwao kila mmoja.

Doreen alilazimika kupelekwa kituo maarufu duniani cha Madona nchini Marekani, kutokana na tatizo la uti wa mgongo.

Agosti 18, mwaka 2017 walirejea nchini kwa msaada wa Shirika la Ndege la Mfuko wa Msamaria la Marekani linaloendeshwa na Frankline Graham, mtoto wa mwimbaji maarufu duniani, Bill Graham, wakiwa wameambatana na wazazi wao watatu na daktari bingwa wa mifupa wa Hospitali ya Mount Meru, Elias Mashalla na Dk. Siniphorosa Silalye.
Share:

KAMATA HADI BONUS YA SH. 300,000 KWENYE AKAUNTI YAKO IJUMAA HII

  

Pata bonus ya asilimia 100% ukiweka pesa kwenye account yako ya 22bet Ijumaa hii, hadi 300,000  kumbuka bonus hiyo itakuwa mara mbili ya pesa uliyoweka kwenye account yako. Ofa hii ni kwa kila mteja atakayeweka pesa kwenye account weeekend hii. Pia kwa wateja wapya watapata bonus ya kuweka fedha kwenye account yake ya 22bet kwa mara ya kwanza. 


KUJIUNGA NA 22BET BOFYA >>>HAPA>>
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 20,2022


Magazetini leo Alhamisi Januari 20 2022





























Share:

COASTER YAGONGA TRENI DAR, WATU WAWILI WAFARIKI, 11 WAJERUHIWA


UONGOZI wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) umethibitisha kutokea kwa tukio la ajali lililotokea Januari 19, 2022 maeneo ya Banana jijini Dar es Salaam katika kivuko cha reli na barabara, ambapo gari la abiria aina ya ‘Coaster’ lenye namba za usajili T701 CKD linalofanya safari kati ya Tandika na Mbezi limegonga treni.

"Ajali imetokea majira ya saa 11:10 jioni na imehusisha treni ya mjini inayotoa huduma ya usafiri wa abiria kati ya Kamata na Pugu jijini Dar es Salaam, katika ajali hii majeruhi ni abiria 6 waliokuwa wakisafiri na basi ambapo wanawake ni watatu na wanaume watatu na kuna vifo vya wanawake wawili, majeruhi wote wamepelekwa Hospitali ya Amana kupatiwa matibabu.


"Dereva wa basi alitahadharishwa kwa kupigiwa honi na dereva wa treni, hakuzingatia na hata aliposimamishwa na mshika bendera dereva wa basi aliamua kukatiza reli na kupelekea ajali.


"Uongozi wa Shirika la Reli Tanzania unaendelea kusisitiza Umma kuwa makini na kufuata Sheria na taratibu zinazoonesha alama zilizopo katika vivuko vya reli na barabara na dereva anapokaribia makutano anapaswa kupunguza mwendo na kusimama umbali wa mita 100 kuhakikisha endapo njia ni salama ili kuendelea na safari;
Share:

Wednesday 19 January 2022

COMORO YAICHAPA 3-2 GHANA NA KUITUPA NJE AFCON



TIMU ya taifa ya Comoro imeitupa Ghana nje ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kuichapa mabao 3-2 katika mchezo wa mwisho wa Kundi C usiku wa Jumanne Uwanja wa Roumdé Adjia Jijini Garoua, Cameroon.

Mabao ya Comoro yalifungwa na El Fardou Mohamed Ben Nabouhane dakika ya nne na Ahmed Mogni mawili, dakika ya 61 na 85, wakati ya Ghana iliyomaliza pungufu baada ya Nahodha wake, Andre Ayew kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 25, yalifungwa na Richmond Boakye dakika ya 64 na Alexander Djiku dakika ya 77.
Share:

CHELSEA YAZIDI KUPUNGUZWA KASI MBIO ZA UBINGWA EPL YATOKA SARE YA 1-1 NA BRIGHTON



TIMU ya Chelsea imetoa sare ya 1-1 na wenyeji, Brighton & Hove Albion katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa Jumanne Uwanja wa The AMEX, Falmer, East Sussex.

Hakim Ziyech alianza kuwafungia wageni dakika ya 28, kabla ya Adam Webster kuwasawazishia wenyeji dakika ya 60 na sare hiyo ya nane ya msimu inazidi kuiondolea Chelsea matumaini ya ubingwa sasa kikosi cha kocha Mjerumani, Thomas Tuchel kikiachwa pointi 12 na mabingwa watetezi, Manchester City.

Chelsea inafikisha pointi 44 katika mchezo wa 23 nafasi ya tatu, nyuma ya Liverpool pointi 45 za mechi 21 na Man City pointi 56 za mechi 22, wakati Brighton imefikisha pointi 29 katika mechi ya 21 nafasi ya tisa.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 19,2022












Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger