Thursday 2 December 2021

Marketing Coordinator at CVPeople Tanzania

Marketing Coordinator   CVPeople Tanzania | Full time Job Description Main Purpose of the Job- (Job Summary) Brand officer oversee a wide array of business functions including branding, communication channels, product development, online and offline promotions, and market research. Also conduct various market research and survey for the company. Main Responsibilities   Responsible for brand […]

This post Marketing Coordinator at CVPeople Tanzania has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Human Resources Officer at CVPeople

Human Resources Officer   Dar es salaam , Tanzania Job summary Under the guidance and direct supervision of the supervisor (Finance and Administration), the HR Manager is responsible for transparent implementation of HR strategies, effective delivery of HR services and management of the HR Department. He/she analyses, interprets and applies HR policies, rules and regulations, […]

This post Human Resources Officer at CVPeople has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Supply Clerk (Welcome Kit & Loanable Property Supply Clerk)at U.S. Embassy Dar es Salaam

Supply Clerk (Welcome Kit & Loanable Property Supply Clerk)   Announcement Number: Dar es Salaam-2021-052 Hiring Agency: Embassy Dar Es Salaam Open Period: 12/01/2021 – 12/15/2021 This vacancy is limited to a certain number of applicants and may close before the close date listed here if that limit is reached. Vacancy Time Zone: GMT+3 Series/Grade:LE […]

This post Supply Clerk (Welcome Kit & Loanable Property Supply Clerk)at U.S. Embassy Dar es Salaam has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Warehouse Worker (Truck Driver) at U.S. Embassy Dar es Salaam

Warehouse Worker (Truck Driver)     Announcement Number: Dar es Salaam 2021-049 Hiring Agency: Embassy Dar Es Salaam Open Period: 12/01/2021 – 12/15/2021 This vacancy is limited to a certain number of applicants and may close before the close date listed here if that limit is reached. Vacancy Time Zone:GMT+3 Series/Grade:LE – 0805 3 Salary:Not Specified […]

This post Warehouse Worker (Truck Driver) at U.S. Embassy Dar es Salaam has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Warehouse Worker (Foreman) at U.S. Embassy Dar es Salaam

Position Title: Warehouse Worker (Foreman)    About Announcement Number: Dar es Salaam-2021-048 Hiring Agency: Embassy Dar Es Salaam Open Period: 12/01/2021 – 12/15/2021 Format MM/DD/YYYY This vacancy is limited to a certain number of applicants and may close before the close date listed here if that limit is reached. Vacancy Time Zone: GMT+3 Series/Grade: LE – […]

This post Warehouse Worker (Foreman) at U.S. Embassy Dar es Salaam has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Supply Clerk (Property Clerk) at U.S. Embassy Dar es Salaam

Position Title: Supply Clerk (Property Clerk  About Announcement Number: Dar es Salaam-2021-051 Hiring Agency: Embassy Dar Es Salaam Position Title: Supply Clerk (Property Clerk) (All Interested Candidates) Open Period: 12/01/2021 – 12/15/2021 This vacancy is limited to a certain number of applicants and may close before the close date listed here if that limit is reached. […]

This post Supply Clerk (Property Clerk) at U.S. Embassy Dar es Salaam has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Storekeeper at U.S. Embassy Dar es Salaam

Storekeeper (All Interested Candidates)   Announcement Number: Dar es Salaam-2021-050 Hiring Agency: Embassy Dar Es Salaam Open Period: 12/01/2021 – 12/15/2021 This vacancy is limited to a certain number of applicants and may close before the close date listed here if that limit is reached. Vacancy Time Zone: GMT+3 Series/Grade: LE – 0805 5 Salary: Not […]

This post Storekeeper at U.S. Embassy Dar es Salaam has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Customs Expeditor at U.S. Embassy Dar es Salaam

Position Title: Customs Expeditor (All Interested Candidates)   Announcement Number: Dar es Salaam-2021-047 Hiring Agency: Embassy Dar Es Salaam Open Period: 12/01/2021 – 12/15/2021 This vacancy is limited to a certain number of applicants and may close before the close date listed here if that limit is reached. Vacancy Time Zone: GMT+3 Series/Grade: LE – 0905 6 Salary: […]

This post Customs Expeditor at U.S. Embassy Dar es Salaam has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Freeman Mbowe na Wenzake Wafunga Ushahidi....Uamuzi wa Kesi Ndogo ndani ya Kesi ya Msingi Kutolewa Disemba 14


Mahakama  Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, jijini Dar ea Salaam, imepanga kutoa uamuzi wa kesi ndogo ya kupinga maelezo ya onyo ya mshtakiwa wa tatu, Mohammed Abdillah Ling’wenya yapokelewe au la tarehe 14 Desemba 2021.

Ni baada ya upande wa utetezi katika kesi hiyo ndogo ndani ya kesi ya msingi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake, watatu.

    Tarehe hiyo imepangwa janaJumatano, tarehe 1 Desemba 2021 na mahakama hiyo mbele ya Jaji Joachim Tiganga, baada ya upande wa utetezi kuomba kufunga ushahidi wake katika kesi hiyo ndogo.

Katika kesi hiyo, upande wa utetezi ulipinga maelezo hayo ya onyo yasipokelewe kwa madai si halali kwa mujibu wa sheria kwani hayakutolewa na mshtakiwa huyo.

Jaji Tiganga ameelekeza mawakili wa pande zote mbili kuwasilisha mawasilisho yao kwa njia za maandishi tarehe 7 Desemba 2021, ili kuandaa uamuzi dhidi ya kesi hiyo kama mahakama hiyo iyapokee maelezo ya onyo au isiyapokee.

Wakili wa Ling’wenya ambaye ni mshtakiwa wa tatu, Fredrick Kihwelo, aliomba wafunge ushahidi baada ya shahidi wao wa tatu, Gabriel  Mhina, kumaliza kutoa ushahidi wake.

Mhina ambaye alikuwa ni Komandoo wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), alianza na kumaliza kutoa ushahidi wake jana, ambapo aliieleza mahakama hiyo namna alivyoingizwa kwenye kesi hiyo na kisha kuachwa huru kabla haijahamishiwa mahakani hapo ikitokea Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Alidai, aliachiwa huru  baada ya Mbowe kukamatwa na kwamba upande wa mashtaka ulidai hauna nia ya kuendelea naye katika kesi ya uhujumu uchumi namba 63/2020 iliyokuwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Pia, Mhina alidai baada ya kukamatwa mkoani Tabora tarehe 19 Desemba 2020, alipatiwa mateso kwa kupigwa na kufungwa pingu muda wote. Pia alidai askari polisi waliomkamata hawakumuonya juu ya kosa lililokuwa linamkabili na wala hawakuandika taarifa zake katika kitabu cha kumbukumbu za mahabusu, katika vituo vya polisi alivyofikishwa.

Mbali na Mhina, mashahidi wengine wa utetezi walikuwa ni Ling’wenya mwenyewe aliyedai kwamba maelezo ya onyo yaliyoletwa mahakamani hapo na upande wa jamhuri hakuyatoa bali alilazimishwa kuandika nyaraka iliyodaiwa kuwa na maelezo hayo.



Share:

Ufafanuzi Wa Kauli Ya Waziri Wa Afya Juu Ya Viongozi Ambao Hawajachanja Chanjo Dhidi Ya Uviko- 19



Share:

Jela Miaka 30 Kwa Kubaka, Kumpa Mwanafunzi Ujauzito


Na Amiri Kilagalila,Njombe
MAHAKAMA ya wilaya ya Njombe imemuhukumu Bright Peter Dismas (25) mkazi wa Kitisi halmashauri ya mji wa Makambako kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya kupatikana na hatia ya makosa mawili likiwemo la ubakaji na kumpa ujauzito mwanafunzi.

Hukumu hiyo imetolewa jana na hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Njombe Isack Mlowe ambapo amesema mshtakiwa huyo alimbaka mwanafunzi wa kidato cha tatu mwenye umri wa miaka 17 wa shule ya sekondari Mkilima iliyopo mjini Makambako.

Alisema tukio hilo la ubakaji lilitokea mwaka jana mwezi Februari katika mtaa wa Kitisi halmashauri ya mji Makambako.

Amesema mshtakiwa alianzisha mahusiano ya kimapenzi na mwanafunzi huyo ambapo siku ya tukio alikwenda nyumbani kwao akiwa peke yake.

Amesema baada ya kufika nyumbani hapo mshtakiwa huyo aliingia ndani na kuandaliwa chakula na mwanafunzi huyo kisha baadae wote wakaenda chumbani na kufanya mapenzi.

Amesema ilipofika mwezi oktoba mwaka jana mwanafunzi huyo aligundulika kuwa na ujauzito baada ya kufanyika vipimo shuleni kwa wanafunzi wote wa kike.

"Mwanafunzi huyo baada ya kugundulika kuwa na ujauzito alihojiwa ndipo akaeleza mahusiano yake na mshtakiwa" alisema Mlowe.

Amesema mshtakiwa huyo alihukumiwa kulipa fidia ya shilingi 1,000,000/= kama fidia kwa mwanafunzi huyo baada ya kutoka gerezani.

Wakili wa serikali Matiko Nyangero aliyekuwa akiendesha shauri hilo la jinai Namba 198/2020 aliieleza Mahakama kuwa mshtakiwa ni mkosaji wa mara ya kwanza na katika kutoa adhabu izingatie matakwa ya kifungu cha 130 (1) (2) (e) na 131 (1) cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 marejeo ya 2019, ambavyo mshtakiwa ameshtakiwa navyo.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Disemba 02



Share:

Majaliwa: Hatua Kali Zichukuliwe Kwa Wanaowanyanyapaa Waviu


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameziagiza mamlaka husika kuchukua hatua kali za kisheria kwa watakaobainika kuwanyanyapaa na kuwabagua Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU) kwa kuwa vitendo, kauli au mitazamo ya unyanyapaa na ubaguzi kwa kundi hilo havikubaliki.

“Kumekuwa na madai kuwa watumishi wa afya wana tabia za unyanyapaa na kuvujisha siri za WAVIU wanapotoa huduma katika vituo vyetu vya tiba na matunzo kwa WAVIU. Vitendo na tabia hizi ziripotiwe mara moja pindi vitakapotokea.”

Ametoa agizo hilo jana (Jumatano, Desemba Mosi, 2021) wakati alipomuwakilisha Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambayo Kitaifa yamefanyika katika Uwanja wa Ruanda-Nzovwe mkoani Mbeya. Kaulimbiu ya maadhimisho hayo ni “Zingatia Usawa. Tokomeza Ukimwi. Tokomeza Magonjwa ya Mlipuko.”

Mheshimiwa Majaliwa amesema nchi ina sheria ya UKIMWI ambayo imefanyiwa marekebisho kadhaa ili kuhakikisha kuwa huduma za VVU na UKIMWI zinamfikia kila mlengwa. “Ninaelewa kuwa unyanyapaa na ubaguzi kwa WAVIU bado ni changamoto kubwa katika jamii zetu.”

“Hii inatukwaza na kurudisha nyuma juhudi za mwitikio wa mapambano dhidi ya UKIMWI nchini. Mfano baadhi ya watu wanaoishi na VVU wanaona aibu kutumia huduma za VVU na UKIMWI zilizopo kwa sababu ya unyanyapaa na ubaguzi, hasa katika maeneo ya vijijini.”

Akizungumzia kuhusu kaulimbiu ya maadhimisho hayo, Mheshimiwa Majaliwa amesema kaulimbiu hiyo ni thabiti kwa sababu inatoa muelekeo bora wa jinsi ya kuondoa changamoto zilizopo ili kupata matokeo bora zaidi, ikimaanisha kwamba kila wanachokifanya kwenye miradi na afua za udhibiti UKIMWI nchini usawa lazima uzingatiwe.

“Usawa unahitajika kwenye mahitaji ya msingi ya makundi mbalimbali kwani UKIMWI hauchagui umri, jinsi wala rika. Hivyo kaulimbiu hii inatukumbusha wajibu wetu wa kuzingatia utoaji wa huduma kwa makundi yote ambayo ni pamoja na watoto, vijana, wanawake, wasichana, wanaume, wazee, watu wenye ulemavu na makundi yaliyo katika mazingira hatarishi zaidi.”

Hivyo, Waziri Mkuu amesema ili kutekeleza kwa vitendo kaulimbiu hiyo uwekezaji unatakiwa uzingatie mahitaji halisi kwa kila kundi, mazingira halisi na uhatarishi uliopo. “Licha ya hayo haki za binadamu pia zizingatiwe ili huduma zote zinazohusu masuala ya VVU na UKIMWI zitolewe kwa usawa unaohitajika.”

Kadhakika, Mheshimiwa Majaliwa ametumia fursa hiyo kuwahakikishia wadau wote kuwa Serikali inaendelea kushirikiana na Wadau wa Maendeleo kuhakikisha uendelevu wa afua za VVU na UKIMWI nchini kwa kuweka mikakati ya kukusanya rasilimali za ndani.

“Serikali yetu sikivu itaendelea kutenga bajeti na kutafuta vyanzo endelevu vya kutunisha mfuko Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI kadiri uchumi utakavyoruhusu. Natoa agizo kwa TACAIDS kwa kushirikiana na Wizara ya fedha na Mipango na Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kuangalia utaratibu mzuri na wa uhakika wa kutunisha mfuko huu.”

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama amesema huduma za ARV kwa watu wanaoishi na VVU zinaendelea kuimarishwa kwa kuhakikisha kuwa wanaogundulika wanaishi na VVU wanapaswa kuanza kutumia ARV mapema pamoja na kuzingatia ufuasi sahihi wa huduma hizo.

Amesema katika kudhibiti kuenea kwa maambukizo mapya ya VVU, Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo inaendelea kutekeleza mkakati wa nne wa Taifa wa kudhibiti UKIMWI kwa kushirikisha sekta zote nchini. Mkakati huo wa mwaka 2018/2019 hadi 2022/2023 umelenga kupunguza maambukizi mapya ya VVU na vifo vinavyohusiana na UKIMWI.

“Kwa upande mwingine mkakati wa nne wa Taifa unaelekeza utekelezaji wa program za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na VVU na upimaji wa hiari. Huduma hizi hutolewa chini ya usimamizi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto huku wadau wengine wakifanya uhamasishaji kwa wananchi kuziendea huduma zinazotolewa.”

Naye, Mwenyekiti wa Baraza la Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI Tanzania (NACOPHA), Bibi Leticia Maurice ametumia fursa hiyo kumpongeza Mheshimiwa Rais Samia kwa maono na jitihada zake za kutafuta rasilimali fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini ikiwemo ya afya.

Mwenyekiti huyo wa NACOPHA ameongeza kwa kusema kuwa Watu Waishio na Virusi vya UKIMWI wanamshukuru Mheshimiwa Rais Samia kwa kuhakikisha wanapata dawa zao za ARV bila malipo, hivyo kuwawezesha kuishi na kuendesha shughuli zao za kinaendeleao ipasavyo.


Share:

Wednesday 1 December 2021

Wauza Madini Feki Wanaswa Sikonge


 Na Lucas Raphael,Tabora
Mwanamke mmoja mkazi wa mkoani wa Arusha amekamatwa na Jeshi la Polisi katika stendi ya mabasi wilayani Sikonge Mkoani Tabora kwa tuhuma za kukutwa na madini feki aina ya Dhahabu  waliyokuwa wakiwauzia wananchi wa kishrikiana na dereva wake .

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari jana Kamanda wa Polisi Mkoani hapa ACP Richard Abwao alisema walimkamata Mariam Said, mkazi wa Arusha akiwa na dereva wake David George wakiwa na madini hayo waliyoyatumia kumtapeli mkazi wa kijiji cha Usunga wilayani humo aitwaye Edward.

Alibainisha kuwa watuhumiwa walikamatwa baada ya kumtapeli mkazi huyo kiasi cha sh 340,000 ambapo pia baada ya kukaguliwa walikutwa na kadi 5 za benki tofauti tofauti ambazo ni kadi za NMB 3, Posta 1na CRDB 1.

Vitu vinginevyo walivyokutwa navyo ni simu 4 aina ya iphone 6s plus, Tecno Spark 5 Air, Infinix hot 10 na Sam sung zinazodhaniwa kuwa za wizi.

Kamanda Abwao alibainisha kuwa madini hayo yamekamatwa kutokana na jitihada za Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na wananchi na vyombo vya ulinzi na usalama katika kuzuia, kutanzua na kupambana na uhalifu.

Aidha aliongeza kuwa katika kukabiliana na matukio ya uhalifu, mauaji, unyang’anyi wa kutumia silaha, ujambazi na uvunjaji Mkoani humo, Jeshi hilo limeendelea kufanya oparesheni mbalimbali katika wilaya zote.

Alitaja mafanikio ya oparesheni hiyo kwa mwezi huu kuwa ni kukamatwa watu 2 Khamis Baruti na Mohamed Shaban wakazi wa Izimbili wilayani Uyui kwa kukutwa na silaha aina ya gobore isiyo na namba za usajili iliyokuwa ikitumika kwenye uwindaji haramu.

Aidha walikamata silaha 2 aina gobore zilizosalimishwa na watu wasiojulikana katika kata za Kipanga na Mole ( Usanganya) wilayani Sikonge na silaha nyingine ilisalimishwa na mkazi wa Mibono John Matuzya katika Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Kiloleni akidai anatii sheria bila shuruti.

Kamanda alitoa wito kwa wananchi wanazomiliki silaha kinyume na utaratibu kuendelea kuzisalimisha ndani ya kipindi hiki cha msamaha wa Waziri wa Ulinzi vinginevyo watakamatwa, aliitaka jamii kuendelea kushirikiana na Jeshi hilo kwa kutoa taarifa za vitendo vya uhalifu na wahalifu.


Mwisho.


Share:

REA YATAMBULISHA WAKANDARASI NA KUKABIDHI MIKATABA YA MRADI WA KUSAMBAZA UMEME VIJIJI 216 SHINYANGA

Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Elineema Mkumbo (kushoto) akimkabidhi Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary Mikataba itakayotumiwa na Wakandarasi kutekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili unaotarajia kunufaisha vijiji 216 mkoani Shinyanga kwa gharama ya zaidi ya shilingi Bilioni 60.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Wakala wa Nishati Vijijini (Rural Energy Agency – REA) umetambulisha kwa uongozi wa Mkoa wa Shinyanga Wakandarasi wanaotekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili na kukabidhi Mikataba itakayotumiwa na Wakandarasi Kutekeleza Mradi huo unaotarajia kunufaisha vijiji 216 kwa gharama ya zaidi ya shilingi Bilioni 60.


Akizungumza leo Jumatano Desemba 1,2021 wakati wa kukabidhi Mikataba hiyo kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary , Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Elineema Mkumbo amewataja Wakandarasi watakaosimamia mradi wa usambazaji umeme wilayani Kahama, Shinyanga na Kishapu kuwa ni Suma JKT na Tontan Project Technology Co. Ltd.


Mhandisi Mkumbo amesema kutokana na maelekezo ya Serikali ni lazima vijiji vyote vinatakiwa kupatiwa huduma ya umeme ifikapo Mwezi Desemba mwaka 2022.


“Kwa niaba ya Bodi ya Nishati Vijijini, Menejimenti pamoja na Wafanyakazi wa REA tunakukabidhi Mikataba ya kupeleka umeme kwa uongozi wa Mkoa wa Shinyanga ili uendelee kutusaidia katika usimamizi wa mradi wa kupeleka umeme vijijini awamu ya tatu mzunguko wa pili katika mkoa wa Shinyanga. Kufuatia maelekezo ya Serikali ni lazima vijiji vyote vinapata umeme ifikapo Mwezi Desemba mwaka 2022”,amesema Mhandisi Mkumbo.


“Mradi huu tumeugawa katika mafungu mawili ili kuharakisha utekelezaji wake. Fungu la kwanza linaenda Wilaya ya Kahama ambapo gharama ya mradi ni shilingi Bilioni 39. Fungu la pili ni kwa ajili ya wilaya ya Kishapu na halmashauri ya Shinyanga ambapo gharama yake ni zaidi ya Bilioni 21. Hivyo kwa mkoa wa Shinyanga tuna zaidi ya Bilioni 60 ili kukamilisha upelekaji wa umeme katika vijiji”,ameongeza Mhandisi Mkumbo.


Amebainisha kuwa huwa kuna changamoto zinajitokeza wakati Wakandarasi wanapofika ‘Site’ kwa hiyo wameona wafanye maandalizi ya mapema kuziwahi hizo changamoto kabla hazijafika mbali hivyo wamekutana REA, TANESCO na Wakandarasi ili wajue changamoto ni zipi huku wakizingatia vipaumbele vya serikali.


“Pia ilikuwa ni lazima tuwatambulishe Wakandarasi wetu kwenye Uongozi wa Serikali ya Mkoa wa Shinyanga. Kwa hiyo tuna Kampuni ya Tontan Project Technology Co. Ltd ambayo itatekeleza mradi katika wilaya ya Kahama na SUMA JKT ambao watakuwa wilaya ya Kishapu na Shinyanga Vijijini”,amesema.


Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary ameelekeza kwamba Mkandarasi anapokwenda eneo lolote la mradi TANESCO lazima wawepo, uongozi wa eneo husika uwepo ili uweze kuainisha sehemu za kipaumbele na kuhakikisha REA inafuatilia.


“Wananchi wanasubiri sana huduma ya umeme kwa sababu umeme ni muhimu kwa maendeleo ya jamii kwani kila kila kazi inayofanyika inahitaji nishati ya umeme. Tunaamini kabisa kwamba umeme ukifika hata kasi ya maendeleo itakuwa kubwa. Serikali inasubiri umeme na tupo tayari kutoa ushirikiano utakaohitajika wakati Wakandarasi wakiwa ‘Site’ ,cha muhimu ni Mkandarasi awe mwepesi kutoa changamoto ambazo zitakazokuwepo kwenye maeneo ya mradi”,amesema Omary.


“Mara nyingi miradi ya umeme inapopita kunakuwa na changamoto ya mradi unapoelekea siyo kwenye mahitaji makubwa na ya lazima ya jamii, nendeni mkazichukue hizo changamoto na mzifanyie kazi,isitokee mradi unapelekwa maeneo ya mbali sana na kuacha vijiji vikubwa vyenye uhitaji mkubwa wa umeme, tuanze na hao wenye athari kubwa za kijamii na kimaendeleo”,amesema.

Amebainisha ili mradi huo ukamilike kwa wakati ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha anatimiza wajibu wake ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kuhusu changamoto zinazojitokeza.


“Nina hakika kabisa kila mmoja, Mkandarasi, TANESCO, REA, Serikali ya mkoa wote tunataka kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa wakati. Kinachotakiwa ni kila mmoja atimize wajibu wake,kila mmoja awe na wajibu wa kutoa taarifa kwa mwingine iwapo anahitaji msaada ‘Support’ wa changamoto anayokutana nayo”, amesema Mhe. Omary


Msimamizi wa Miradi ya REA - TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Anthony Tarimo amesema mradi huo unatarajia kunufaisha vijiji 216 vya Mkoa wa Shinyanga na sasa wapo kwenye hatua za awali za utekelezaji wa mradi huu ikiwa ni pamoja na kuangalia namna ya kuingiza kwenye mradi vijiji 30 vilivyokuwa vimesalia kupatiwa umeme kwenye mipango iliyopita kwani serikali ilishatoa maagizo vipatiwe umeme kupitia Mradi huu mpya.


Naye Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Ukandarasi ya Tontan Project Technology Co. Ltd, Nasra Mwampashe ambao ni Wakandarasi wa Mradi huo wa REA wilaya ya Kahama wenye thamani ya shilingi Bilioni 39 ameahidi kuwa watatekeleza mradi huo kwa ufanisi na weledi mkubwa na kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati uliopangwa.


“Tukiwa Wakandarasi tunaishukuru sana Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutuamini na kutupatia huu mradi. Tunaahidi kufanya kazi kwa ufanisi na weledi wa hali ya juu kwa sababu uwezo tunao, nguvu tunayo, vifaa tunavyo na tumejipanga vilivyo kuhakikisha mradi unakamilika ndani ya muda tuliopangiwa”,amesema Mwampashe.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Elineema Mkumbo (kushoto) akimkabidhi Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary Mikataba itakayotumiwa na Wakandarasi kutekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili unaotarajia kunufaisha vijiji 216 mkoani Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Elineema Mkumbo (kushoto) akimkabidhi Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary Mikataba itakayotumiwa na Wakandarasi kutekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili unaotarajia kunufaisha vijiji 216 mkoani Shinyanga.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary akionesha Mikataba itakayotumiwa na Wakandarasi kutekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili unaotarajia kunufaisha vijiji 216 mkoani Shinyanga kwa gharama ya zaidi ya shilingi Bilioni 60.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary akizungumza wakati Wakala wa Nishati Vijijini (Rural Energy Agency – REA) ukitambulisha kwa uongozi wa Mkoa wa Shinyanga Wakandarasi wanaotekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili na kukabidhi Mikataba itakayotumiwa na Wakandarasi Kutekeleza Mradi huo.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary akizungumza wakati Wakala wa Nishati Vijijini (Rural Energy Agency – REA) ukitambulisha kwa uongozi wa Mkoa wa Shinyanga Wakandarasi wanaotekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili na kukabidhi Mikataba itakayotumiwa na Wakandarasi Kutekeleza Mradi huo.
Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Elineema Mkumbo akizungumza wakati akitambulisha kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary Wakandarasi wanaotekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili na kukabidhi Mikataba itakayotumiwa na Wakandarasi Kutekeleza Mradi huo.
Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Elineema Mkumbo akizungumza wakati akitambulisha kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary Wakandarasi wanaotekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili na kukabidhi Mikataba itakayotumiwa na Wakandarasi Kutekeleza Mradi huo.
Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Elineema Mkumbo (katikati) akizungumza wakati akitambulisha kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary Wakandarasi wanaotekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili na kukabidhi Mikataba itakayotumiwa na Wakandarasi Kutekeleza Mradi huo.
Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Elineema Mkumbo akielezea namna walivyojipanga kutekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili  mkoani Shinyanga.
Msimamizi wa Miradi ya REA - TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Anthony Tarimo akielezea namna vijiji 216 mkoani Shinyanga vitakavyonufaika na Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili.
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Ukandarasi ya Tontan Project Technology Co. Ltd, Nasra Mwampashe akielezea namna walivyojipanga kutekeleza kwa ufanisi na weledi mkubwa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili wilayani Kahama.

 Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:

Tanzania Yanadi Vivutio Vyake Vya Utalii Kwenye Mkutano Mkuu Wa 24 Wa Utalii Duniani Nchini Hispania


NA MWANDISHI MAALUM, MADRID, HISPANIA
UJUMBE wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro upo nchini Hispania, katika Jiji la Madrid kushiriki mkutano mkuu wa 24 wa Kimataifa wa Utalii Duniani ulioandaliwa na Shirika la Kimataifa  linaloshughulikia masuala ya Utalii Duniani ( UNWTO)

Katika mkutano huo wa siku nne ulioanza jana, unaotarajiwa kufunguliwa  rasmi leo hii Desemba Mosi, ambapo Waziri Ndumbaro akiwa katika jiji hili la Madrid, ameweka bayana mambo mbalimbali ambayo Tanzania itanufaika na mkutano huo.
 
Akizungumzia mambo hayo, Dkt. Ndumbaro amesema  ''katika  kuhakikisha kwamba tunaongeza idadi ya watalii kuitembelea Tanzania pamoja na mapato yatokanayo na Utalii, suala la kutangaza utalii wa Tanzania katika nyanja za kidunia ni suala ambalo haliepukiki ''

Ametaja moja ya kati ya maeneo ya  kutangaza Utalii huo, ni kuhudhuria mikutano mikubwa duniani ambayo Inahusisha masuala ya Utalii  ikiwemo kuja nchini Hispania ambako ndiko makao makuu ya utalii Duniani  katika jiji la Madrid, kwa ajili ya  kuhudhuria mkutano mkuu huu wa 24.

Ikiwa ni siku ya kwanza ya mkutano huo Tanzania ilipata fursa kadhaa ikiwemo kutumia  mkutano huu kutangaza vivutio vilivyopo Tanzania, kuwaambia dunia nzima  kwamba Tanzania  ipo salama na kuwataka watalii kuja kujionea vivutio vya utalii ilivyonanvyo

''Waje Tanzania wauone Mlima Kilimanjaro, waje Tanzania waione Serengeti, waje Tanzania waione Ngorongoro, waje Tanzania waone fukwe nzuri zenye mchanga mweupe zilizopo Zanzibar, waje Tanzania waone vivutio mbalimbali ambavyo tupo navyo.’’ Alisema Dkt. Ndumbaro.

Dkt. Ndumbaro aliongeza kuwa, katika suala la pili katika mkutano huo, Tanzania itasaini mkataba na UNWTO wa kuweza kuwa mwenyeji wa mkutano wa 65 wa Utalii Barani Afrika ambao utafanyika kati ya tarehe 6-8 Oktoba 2022 katika jiji la Arusha.

‘’Mkutano huu tunauleta kwa sababu ni fursa nyingine kwa  Tanzania, Tulishapewa kuwa mwenyeji wa mkutano wa utalii wa kanda ya Afrika  kule nchini Cape verde, lakini sasa tumekuja kusaini makubaliano ya kuwa wenyeji wa  mkutano huo, baada ya kusaini sasa tutakuwa na uhakika asilimia 100 na tumetengeneza ‘Post card’ ambapo kila mshiriki aliyekuja hapa tunampa post kadi hizi ambayo inasaidia sana kutangaza utalii wa Tanzania.’’ Alisema Dkt. Ndumbaro.

Aidha, alisema kuwa suala la tatu kwenye mkutano huo, Tanzania imekuwa  katikak  mstari wa mbele kupigania haki za Watalii ambapo watashiriki katika kufanikisha sheria ya Kimataifa inapitishwa.

‘’Jambo lingine ambalo tunalifanya katika mkutano huu, ni kupitisha sheria ya kutetea haki za watalii duniani pale inapotokea matatizo.. tumejifunza kutokana na kadhia ya UVIKO 19 kwamba nchi zilifunga mipaka, na baada ya nchi kufunga mipaka , watalii walikuwa wapo  kwenye nchi zingine na hawaweza kurudi.

‘’Sasa haki zao zilikuwa haziwezi kutetewa na sheria za kimataifa. Kwa hiyo sasa tunapitisha sheria ya kimataifa ya kutetea watalii katika mazingira ya dharura kama hayo. Ni sheria ambayo itaongeza heshima ya baishara ya utalii duniani, kwa sababu unapolinda haki ya mtalii, mtalii anajiona yupo salama zaidi kuja na kushiriki katika  nchi yako, Tanzania tumekuwa mstai wa mbele kuhakikisha sheria hiyo inapita.’’ Alisema Dkt. Ndumbaro.

Dkt. Ndumbaro alisema kuwa, mkutano huo una faida nyingi sana kwa nchi Tanzania, katika kuhakikisha kwamba tunatimiza idadi ya watalii milioni tano na mapato zaidi ya  bilioni sita.

‘’Tunatumia mkutano huu kama fursa ya sisi kuweza kutangaza utalii, lakini kama fursa ya kuwavuta wenzetu waje pia, tumepongezwa kwa namna ambavyo tumeweza kufanya onesho la kwanza la utalii katika nchi za Afrika Mashariki. Sisi tuliona dogo, lakini wenzetu huku katika nyanja za kimataifa tumepongezwa na nimesema kwamba kumbe kweli watanzania wanaweza kufanya mikutano kwa kiwango kikubwa zaidi’’ alisema Dkt. Ndumbaro.

Mkutano huo wa 24 wa Kimataifa wa Utalii duniani, ni wa siku nne, kuanzia jana Novemba 30 hadi 3 Desemba, ukijumuisha ujumbe mbalimbali wakiwemo Mawaziri wa Utalii, viongozi wakuu wanchi, Mashirika ya Kimataifa ya Serikali, binafsi, wadau wa Utalii  na watu mbalimbali waalikwa.

Mwisho.


Share:

Tanzania yafuzu kombe la Dunia mchezo wa soka kwa wenye ulemavu.


Na. John Mapepele
Waziri mwenye dhamana ya Michezo nchini. Mhe, Innocent Bashungwa leo Disemba 1, 2021 amewaongoza watanzania kuishangilia Timu ya Tanzania (Tembo Warriors) ambayo imefuzu na kuwa  timu ya kwanza miongoni mwa timu nne zinazoingia nusu fainali ya Soka ya Bara la Afrika kwa   wenye ulemavu (CANAF 2021) na hivyo kupata tiketi ya kushiriki  Mashindano ya Dunia  ya mchezo huo yatakayofanyika nchini Uturuki 2022 baada ya kuichapa timu ya Cameroon  mabao 5-0.

Timu ya Tanzania ambayo katika kipindi chote cha maandalizi imesimamiwa na  Kamati Maalum ya Kitaifa  chini ya Katibu Mkuu wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassani Abbasi ilianza vizuri  kutokana hamasa  iliyotolewa  na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hasan.

Katika mechi zote za mashindano haya Tanzania imepoteza mechi moja tu ya Uganda mbayo ilifungwa goli 1-0, ambapo Tembo iliifunga timu ya Morocco 2-1 na Sierra Leone ambapo  tembo ilishinda  goli 1-0.


 Akizungumza na Waandishi wa Habari mara  baada ya mechi hii, Mhe. Bashungwa amewahakikishia kwamba Serikali itaendelea kuiisaidia  timu  hiyo ili iendelee  kufanya vizuri  maandalizi ya Kombe  la Dunia.

 Aidha, Dkt Abbasi amesema  kwa  kuwa  safari ya kuelekea  kombe la  dunia imekamilika kazi iliyobaki ni kuhakikisha kuwa  kombe  linabaki  Tanzania.

Magoli mawili ya Tanzania yamefungwa na  Alfan Kyanga dakika ya  2 na 15 , Ramadhan Chomole  dakika ya  18, na Frank Ngailo  dakika ya  36 na  44.

Mchezo huo pia umeshuhudiwa na  Rais wa Mashindano hayo duniani  Mateus Wildack.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger