Thursday 21 October 2021

TANZANIA INA WATU MILIONI 2.4 WENYE TATIZO LA KUTOKUONA



WAZIRI wa Afya,Mandeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt.Dorothy Gwajima,akizungumza kwenye hafla ya kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani,pamoja na uzinduzi wa mwongozo wa kufundishia afya msingi na upokeaji wa taarifa ya Dunia kuhusu Uoni iliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia magonjwa yasiyoyakuambukiza kutoka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.James Kihologwe,akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani,yaliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Shirika la Christian Blind Mission Tanzania (CBM) Bi Nesia Mahenge,akisoma risala fupi kwa niaba ya wadau wa huduma za afya ya macho nchni wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani,yaliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


WAZIRI wa Afya,Mandeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt.Dorothy Gwajima,akipokea risala kutoka kwa Mkurugenzi wa Shirika la Christian Blind Mission Tanzania (CBM) Bi Nesia Mahenge,aliyesoma risala hiyo kwa niaba ya wadau wa huduma za afya ya macho nchni wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani,yaliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Shirika la Sightsavers,Godwin Kabalika,akisoma taarifa ya hali ya uoni Duniani wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani,yaliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


Meneja Mpango wa Taifa wa Huduma za Macho kutoka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Bernadetha Shilio,akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani,yaliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


Baadhi ya washiriki wakifatilia hotuba mbalimbali wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani,yaliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


WAZIRI wa Afya,Mandeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt.Dorothy Gwajima,akizindua mwongozo wa kufundishia afya Msingi wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani yaliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


WAZIRI wa Afya,Mandeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt.Dorothy Gwajima,akimkabidhi Meneja Mpango wa Taifa wa Huduma za Macho kutoka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Bernadetha Shilio Mwongozo wa kufundishia afya Msingi wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani yaliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


WAZIRI wa Afya,Mandeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt.Dorothy Gwajima,akimkabidhi Mkurugenzi wa Shirika la Brien Holden Vision Institute Bw.Eden Mashayo Mwongozo wa kufundishia afya Msingi wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani yaliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


WAZIRI wa Afya,Mandeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt.Dorothy Gwajima,akimkabidhi Mkurugenzi wa Shirika la Christian Blind Mission Tanzania (CBM) Bi Nesia Mahenge, Mwongozo wa kufundishia afya Msingi wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani yaliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


WAZIRI wa Afya,Mandeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt.Dorothy Gwajima,akimkabidhi Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Kalidushi Charles Mwongozo wa kufundishia afya Msingi wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani yaliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


WAZIRI wa Afya,Mandeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt.Dorothy Gwajima,akiwa katika picha ya pamoja na wadau mara baada ya kuzindua Mwongozo wa kufundishia afya msingi na upokeaji wa taarifa ya Dunia kuhusu Uoni wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani yaliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufunga kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani,pamoja na uzinduzi wa mwongozo wa kufundishia afya msingi na upokeaji wa taarifa ya Dunia kuhusu Uoni iliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Kalidushi Charles,akitoa neno la shukrani kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani,pamoja na uzinduzi wa mwongozo wa kufundishia afya msingi na upokeaji wa taarifa ya Dunia kuhusu Uoni iliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Shirika la Brien Holden Vision Institute Bw.Eden Mashayo,akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wadau kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy G Gwajima,(hayupo pichani) wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani,pamoja na uzinduzi wa mwongozo wa kufundishia afya msingi na upokeaji wa taarifa ya Dunia kuhusu Uoni iliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.


WAZIRI wa Afya,Mandeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt.Dorothy Gwajima,akiwaaga washiriki mara baada ya kufunga kilele cha maadhimisho ya siku ya afya ya Macho Duniani,pamoja na uzinduzi wa mwongozo wa kufundishia afya msingi na upokeaji wa taarifa ya Dunia kuhusu Uoni iliyofanyika leo Oktoba 21,2021 jijini Dodoma.

.......................................................................................................

Na.Alex Sonna,Dodoma

WAZIRI wa Afya,Mandeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt.Dorothy Gwajima,ameeleza kuwa Tanzania ina watu zaidi ya milioni 2.4 wenye matatizo ya kutokuona huku asilimia 55 ya matatizo haya yanawaathiri wanawake.

Pia amesema visababishi vikubwa vya ulemavu wa kutokuona na upungufu wa kuona unaoweza kuzuilika kama vile upeo mdogo wa macho kuona na uoni hafifu vinavyorekebishika kwa miwani, mtoto wa jicho na shinikizo la jicho.

Kauli hiyo ameitoa leo Oktoba 21,2021,Jijini Dodoma wakati akizungumza kwenye kilele cha siku ya afya ya macho Duniani Waziri Gwajima amesema taarifa ya Shirika la Afya Duniani imeonyesha kuwa idadi kubwa ya watu wenye matatizo ya kutokuona asilimia 89 wanaishi katika nchi za uchumi wa kati na wa chini, Tanzania ikiwa miongoni mwa hizo.

Amesema pamoja na kuwa kiwango cha matatizo ya kuona yanayoepukika kwa ujumla kimepungua duniani, Tanzania inakadiriwa kuwa na watu 640,000 wasioona.

Aidha, watu wenye matatizo ya kutokuona kwa viwango cha kati na cha juu wanakadiriwa kuwa ni mara tatu ya watu wasioona ambao ni takriban watu milioni 1.8.

“Kwa ujumla Tanzania ina watu zaidi ya milioni 2.4 wenye matatizo ya kutokuona. Asilimia 55 ya matatizo haya yanawaathiri wanawake. Visababishi vikubwa vya ulemavu wa kutokuona na upungufu wa kuona unaoweza kuzuilika kama vile Upeo mdogo wa Macho kuona na uoni hafifu vinavyorekebishika kwa miwani, mtoto wa jicho na Shinikizo la jicho,”amesema.

Dkt.Gwajima amesema Takwimu za hapa Tanzania zinaonyesha watu milioni 1.2 tu kwa mwaka 2020 ndio walifikiwa na huduma za macho katika vituo vyetu vya kutolea huduma za afya ikilinganishwa na uhitaji wa takribani watu milioni 12,000,000.

“Na kati yao, asilimia 32% wanakuwa tayari wana upungufu wa kuona ikijumuisha ulemavu wa kutokuona. Upasuaji wa mtoto wa jicho kwa mwaka jana ulifanyika kwa wastani wa macho 200 tu kwa kila watu milioni 1, ikilinganishwa na macho 2,000 kwa kila watu milioni 1 kama inavyoshauriwa na Shirika la Afya Duniani,”amesema.

Amesema asilimia 38 tu ya watu wenye uhitaji wa miwani ya kurekebisha uoni ndiyo waliweza kupata miwani hiyo kutoka kwenye vituo vya tiba.

Aidha,Dkt. Gwajima amesema kwa mwaka huu, Wizara ilipanga kuelimisha jamii na viongozi pia kuhimiza watu kupima macho kupitia vituo mbalimbali.

“Maadhimisho ya siku ya kuona duniani ya mwaka huu yamekuwa tofauti sana kwa sababu ni mwaka mwingine tangu kuisha kwa utekelezaji wa Mkakati wa Kimataifa wa Dira ya mwaka 2020. Mkakati mpya umeandaliwa uliojikita kwenye Mapendekezo Taarifa ya Dunia ya Uoni iliyoandaliwa na ya Shirika la Afya Duniani,”amesema.

Waziri Gwajima amewaasa wananchi kujizuia kupata matatizo ya macho,kuepuka kuweka kwenye macho dawa ambazo hujaandikiwa na wataalamu kutoka kwenye Hospitali na vituo vya tiba au dawa zisizo rasmi.

Hata hivyo amesema kuwa kuhifadhi hali ya uoni ikiwa ni pamoja na kupanga angalao siku moja kwa mwaka kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa kina wa afya ya macho yako yaani kupimwa uwezo wa kuona, upeo wa macho kuona na pia kipimo cha ndani ya jicho.

“Ifanye Afya ya Macho kuwa kipaumbele, hakikisha kuwa swala la upimani wa macho ni sehemu ya huduma ya Afya inayotolewa kwenye eneo lako.Penda Macho yak ni Utume wa Maisha,”amesema

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Christian Blind Mission Tanzania (CBM) Bi Nesia Mahenge amesema tatizo la uoni hafifu na upofu linapelekea jamii kushindwa kushiriki kikamilifu katika shughuli mbali mbali za kiuchumi na maendeleo ya jamii na kuzidi kuongeza tatizo la umaskini Tanzania.

Pia,amesema Tanzania kuna changamoto ya upungufu wa rasilimali watu wa kutoa huduma ya afya ya machoa ambapo amedai Takwimu zinaonyesha kuwa zaidi ya asilimia 75 ya matatizo ya uoni hafifu na upofu Tanzania yanazuilika.

“Tunaiomba Serikali kwenye sera ya Afya na miongozo ya kuandaa bajeti na mahitaji ya Afya ya Macho iainishe vema kipengele cha Afya ya Macho na kukipa uzito unaostahili. Wadau tunaiomba Serikali ihakikishe kuna uwepo wa rasilimali watu kwenye ngazi zote za Taifa ili kurahisisha wadau kufika maeneo,”amesema.

Akisoma taarifa ya hali ya uoni duniani,Mkurugenzi wa Shirika la Sightsavers,Godwin Kabalika amesema uoni unabaki kuwa mlango mkubwa wa fahamu katika kila hatua ya maisha ya mwanadamu.

“Mtoto anayezaliwa anategemea uoni kutambua na kuweka mahusiano karibu na mama mtoto anaeanza kutembea pia anahitaji uoni ili aweze kujifunza na hatua zake hali kadhalika mtoto wa shule anapoenda shule na vijana wanahitaji uoni ili kujitegemea hata watu wazima wanahitaji uoni,”amesema.

Amesema matatizo ya macho bado yapo na kwa kiasi kikubwa kila mmoja hupata tatizo la macho amedai kwa miaka ijayo idadi ya tatizo litaendelea kukua kutokana na uongezeko la watu mabadiliko ya tabia Nchi.

Amesema Mifumo ya afya inakabiliwa na changamoto ya kufikia uhitaji wa sasa na unaotarajiwa duniani

Amesema ili kukabiliana na ongezeko hilo kunahitajika kuongezeka kasi za afua kukabiliana na changamoto hizo

“Mapendekezo ya taarifa hiyo ni pamoja na afya macho iwe sehemu afya kwa wote,kujumuisha afya ya macho kwenye huduma za afya kwa kumlenga mhitaji ,kuhamasisha tafiti ya utekelezaji wa viwango vya juu na kuongeza uelewa,kufanya ufuatiliati na tathimini ya maendeleo,kuongeza uelewa na kushirikishwa watu na jamii,”amesema.
Share:

MWENDESHA BODABODA AOKOTA SHILINGI MILIONI 115 NA KUZIRUDISHA KWA MWENYEWE... AITWA IKULU



Siku chache zilizopita, tukio lisilo la kawaida lilitokea nchini Liberia na kuzua gumzo kubwa kwenye mitandao ya kijamii.

Lilikuwa ni tukio la kijana mdogo, Emmanuel Tuloe ambaye ni dereva wa bodaboda katika Mji wa Nimba nchini Liberia, kuokota kitita cha dola za Kimarekani 50,000, sawa na takribani shilingi milioni 115 za Kitanzania zilizokuwa zimeangushwa kando ya barabara.

Katika hali ya kushangaza, kijana huyo alirudisha fedha hizo kwa mwenyewe na kusababisha watu wengi wamcheke na kumuona hana akili timamu, yaani uokote shilingi milioni 115 halafu umrudishie mwenyewe, hakika kijana huyo alionekana kuwa kilaza kupitiliza.

Tukio hilo lilivyokuwa, ni kwamba kijana huyo akiwa katika shughuli zake za bodaboda, akitokea katika eneo la Tappita kurejea nyumbani kwake alishtuka baada ya kuona maburungutu ya fedha yaliyokuwa yamefungwa kwenye mfuko wa plastiki, yakiwa kando ya barabara.

Alichokifanya, ilikuwa ni kuchukua fedha hizo na kwenda kuzihifadhi kwa shangazi yake na kumueleza kila kitu, akamwambia shangazi yake huyo kwamba anasubiri kusikia kama mtu yeyote atalalamika kupoteza kiasi hicho cha fedha, basi atamrudishia.

Muda mfupi baadaye, mwanamama mfanyabiashara, Musu Yancy alisikika katika kituo kimoja cha redio, akiwa analia na kueleza kuwa amepoteza kiasi hicho cha fedha na kuomba kama kuna yeyote aliyeokota, basi anaomba amrudishie!

Ni hapo ndipo kijana huyo alipochukua mawasiliano yake na hatimaye, akamrudishia mzigo wake wote, bila kupunguza hata senti tano!

Wema wake ulimsababishia matatizo makubwa kwani alianza kudhihakiwa na kutukanwa mno kwenye mitandao ya kijamii.

Sasa habari mpya ni kwamba, kufuatia kitendo hicho cha uungwana uliopitiliza kilichofanywa na kijana huyo, Rais wa nchi hiyo, George Weah ameguswa mno na moyo wa kipekee wa kijana huyo na kuamua kumuita ikulu jijini Monrovia.

Akiwa ikulu, Rais Weah kwanza alitaka kujua historia yake ambapo kijana huyo alimueleza kwamba alikuwa bado mwanafunzi lakini kutokana na ukosefu wa ada, aliamua kusimama masomo na badala yake, akawa anaazima bodaboda kutoka kwa moja ya marafiki zake na kufanya kazi ili akusanye fedha ambazo atazitumia kwa ajili ya ada.

Maelezo hayo yakamgusa mno Rais Weah ambaye baadaye alimtunuku kijana huyo medali ya heshima kutoka ikulu, Liberia’s Highest Orders of Distinction, akampa zawadi ya dola elfu 10, sawa na takribani shilingi milioni 23, akamnunulia bodaboda mpya mbili na kubwa zaidi, akamuahidi kwamba Rais atamgharamia ada ya masomo mpaka atakapofika chuo kikuu, ngazi ya digrii ya pili, masters.

Kama hiyo haitoshi, mwanamke aliyeokotewa fedha zake, yeye ametoa kiasi cha dola 2500, sawa na takribani shilingi milioni tano, huku Baraza la Maaskofu nchini humo Liberia Council of Churches (LCC) kupitia kwa kiongozi wake, Bishop Kortu K. Brown nalo likitoa kiasi cha dola efu 10, sawa na shilingi milioni 23.

Pia Rais Weah ameamuahidi kijana huyo kwamba atakuwa balozi wa kupinga rushwa nchini humo na atakuwa akipewa mshahara kila mwezi.

Kwa kifupi ni kwamba jamaa amepewa takribani shilingi milioni 50 za Kitanzania, pikipiki mbili na ofa ya kusomeshwa mpaka chuo kikuu lakini pia akiingia kwenye rekodi ya watu waliowahi kupewa medali ya heshima kutoka kwa rais!

Vipi, bado huamini kama wema unalipa? Bado unamchukulia kijana huyo kama kilaza? Unaambiwa malipo ni hapahapa duniani, ukifanya wema utalipwa wema, ukifanya ubaya, vivyo hivyo utalipwa ubaya!

Imeandaliwa na Hashim Aziz
Share:

BINADAMU APANDIKIZWA FIGO YA NGURUWE



Timu ya upasuaji ya Afya ya NYU ikichunguza Figo ya Nguruwe
**

Wanasayansi kutoka Marekani wamefanikiwa majaribio ya kupandikiza Figo ya Nguruwe kwa Binadamu na kugundua kuwa kiungo hicho kinaweza fanya kazi kikamilifu.

Wataalamu hao kutoka N.Y.U. Langone Health Taasisi ya kupandikiza Figo huko Manhattan wanasema walitoa Figo inayofanya kazi kwa Nguruwe kisha ikabadilishiwa vinasaba na kuipandikiza kwa Mwanadamu.

Hatua hiyo ya mafanikio inaweza kuleta matumaini kwa wagonjwa na kuwa chanzo endelevu na mbadala kwenye upatikanaji wa viungo hivyo.
Share:

AHUKUMIWA KUNYONGWA BAADA YA KUUA ABIRIA MBEYA


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Mkoa wa Mbeya, imemhukumu kunyongwa hadi kufa, Emmanuel Msomba (30) baada ya kupatikana na kosa la mauaji ya abiria mmoja aliyekuwa akitoka Tunduma kwenda Sumbawanga mkoani Rukwa baada ya kumpiga na mti na kumpora fedha na simu ndogo aina ya Itel.

Uamuzi wa hukumu hiyo ulitolewa juzi na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mkoa wa Mbeya, Zawadi Laizer, baada ya kusikiliza mashahidi zaidi ya wanane wa upande wa Jamhuri na kuridhika.

Hakimu Laizer alisema ushahidi huo ulieleza kwa kina kwamba mshtakiwa Msomba akiwa na wenzake wawili huko Kijiji cha Chiwanda, wilayani Momba, walimuua Isack Kazuka wakati akiendesha pikipiki kutoka Tunduma kwenda nyumbani kwao Kalambo, mkoani Rukwa.

Alifafanua kuwa marehemu Kazuka aliombwa lifti na mshtakiwa ambaye alishirikiana na wenzake kutekeleza mauaji hayo na kisha kumpora fedha na simu ndogo aina ya Itel baada ya pikipiki ya marehemu kudaiwa kuharibika.

Kwenye utetezi wake mshtakiwa Msomba alikana kutenda mauaji hayo badala yake alidai kuomba lifti ya pikipiki kwa Kazuka na aliachana naye kwa fundi wa pikipiki alikokuwa akitengeneza pikipiki yake hadi aliposikia mtu huyo amekutwa na umauti na kuiomba mahakama kumwachia huru kwa madai hakuhusika na mauaji hayo.

Licha ya upande wa utetezi kuomba kupunguziwa adhabu kwa mteja wake Jamhuri kupitia wakili Davice Msanga, kwenye utolewaji hukumu hiyo iliisihi mahakama kutoa adhabu kama sheria inavyoelekeza kwa kuwa bado watu wengi wanaendekeza uhalifu mbalimbali ikiwamo kukatisha maisha ya wenzao kwa tamaa za fedha na mali nyingine badala ya kufanya kazi kwa bidii na kumtanguliza Mungu.

Hakimu Mkazi Mfawidhi mkoa wa Mbeya, Zawadi Laizer kwa mamlaka ya nyongeza kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya baada ya kusikiliza mashauri ya mauaji, alimhukumu mtu huyo kwenda kunyongwa hadi kufa baada ya mahakama yake kuthibitishiwa mshtakiwa kumuua msamaria huyo aliyekatishwa maisha kijijini Chiwanda Momba wakati akielekea mkoani Rukwa.
Share:

Kabwoba Secondary School

About Kabwoba Secondary School Kabwoba Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S4764 – Known as Shule ya Sekondari Kabwoba Secondary School Kabwoba Secondary School Facilities The Kabwoba Secondary School, features a number of facilities designed to meet specific requirements. The School Facilities includes: […]

This post Kabwoba Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

New Life Olosiva Secondary School

About New Life Olosiva Secondary School New Life Olosiva Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S5352 – Known as Shule ya Sekondari New Life Olosiva Secondary School New Life Olosiva Secondary School Facilities The New Life Olosiva Secondary School, features a number of […]

This post New Life Olosiva Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 03

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Lumesule Secondary School

About Lumesule Secondary School Lumesule Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S4763 – Known as Shule ya Sekondari Lumesule Secondary School Lumesule Secondary School is a public secondary school. This school is flagged as “Operational”, this institution is government owned Lumesule Secondary School […]

This post Lumesule Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Likokona Secondary School

About Likokona Secondary School Likokona Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S4762 – Known as Shule ya Sekondari Likokona Secondary School Likokona is a public secondary school, this institution is government owned. Likokona Secondary School Facilities The Likokona Secondary School, features a number […]

This post Likokona Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Rift Valley Babati Secondary School

About Rift Valley Babati Secondary School Rift Valley Babati Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S4761 – Known as Shule ya Sekondari Rift Valley Babati Secondary School Rift Valley Babati Secondary School Facilities The Rift Valley Babati Secondary School, features a number of […]

This post Rift Valley Babati Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Majembwe Secondary School

About Majembwe Secondary School Majembwe Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S5476 – Known as Shule ya Sekondari Majembwe Secondary School. Majembwe is a public secondary school, this institution is government owned. Majembwe Secondary School Facilities The Majembwe Secondary School, features a number […]

This post Majembwe Secondary School has been posted by Udahiliportal_01

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Ntonzo Secondary School

About Ntonzo Secondary School Ntonzo Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S5477 – Known as Shule ya Sekondari Ntonzo Secondary School. Ntonzo Secondary School is a independent secondary school, this institution is non government owned. This school is flagged as “Operational”. Ntonzo Secondary […]

This post Ntonzo Secondary School has been posted by Udahiliportal_01

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Kitwechenkura Secondary School

About Kitwechenkura Secondary School Kitwechenkura Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S4753 – Known as Shule ya Sekondari Kitwechenkura Secondary School Kitwechenkura Secondary School is located at Kagera. Kitwechenkura Secondary School is boys and girls school and it is doing well in English […]

This post Kitwechenkura Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Chanyangabwa Secondary School

About Chanyangabwa Secondary School Chanyangabwa Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S4752 – Known as Shule ya Sekondari Chanyangabwa Secondary School Chanyangabwa Secondary School is located at Kagera. Chanyangabwa Secondary School is boys and girls school and it is doing well in Kiswahili, […]

This post Chanyangabwa Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Sakura Girl’s Secondary School

About Sakura Girl’s Secondary School Sakura Girl’s Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S5478 – Known as Shule ya Sekondari Sakura Girl’s Secondary School. This school is flagged as “Operational”, this institution is non government owned. Sakura Girl’s Secondary School is a girls […]

This post Sakura Girl’s Secondary School has been posted by Udahiliportal_01

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Loiborsiret Secondary School

About Loiborsiret Secondary School Loiborsiret Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S4743 – Known as Shule ya Sekondari Loiborsiret Secondary School Loiborsiret is a public secondary school, this institution is government owned. Loiborsiret Secondary School Facilities The Loiborsiret Secondary School, features a number […]

This post Loiborsiret Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Luana Secondary School

About Luana Secondary School Luana Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S4742 – Known as Shule ya Sekondari Luana Secondary School Luana Secondary School is located at Njombe. Luana Secondary School is boys and girls school and it is doing well in Kiswahili, […]

This post Luana Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Emergency Response Officers 4 Job Opportunities at Geita Gold Mining Ltd

Emergency Response Officers   ABOUT GEITA GOLD MINING LTD Geita Gold Mining Ltd (GGML) is Tanzania’s leading gold producer with a single operation in Geita Region. The  company is a subsidiary of AngloGold Ashanti, an international gold producer headquartered in South Africa,  with operations in more than ten countries, in four continents. The mine is situated […]

This post Emergency Response Officers 4 Job Opportunities at Geita Gold Mining Ltd has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger