Friday 22 January 2021

Tutegemee Makubwa Kutoka Kampuni Ya Simu ya Infinix.


Kampuni ya simu Infinix Mobile LTD inasema tukae mkao wa kula. Je ni nini tutegemee kutoka Infinix?


Na kama ni simu mpya je nisimu kutoka series gani na kama ni valentine campaign basi watujuze tuanze kujichanga mapema ...nimewazatu.


Nikiwa bado najiuliza ni nini hasa Infinix kutuletea mapema mwaka huu? lakini pia tufahamu Infinix imekuwa kampuni imara na iliweza kuthibitisha hilo mwaka jana ambapo COVID-19 iliweza kusimamisha biashara nyingi lakini kwa Infinix bado walisimama imara nakuendelea kutupa simu zilizo bora kama vile Infinix NOTE 8 inayoendelea kutamba sokoni kutokana na ubora wake wa MP16 za camera ya mbele na MP64 za camera ya nyuma.


Uimara wa kampuni hii kunazidi kunipasha shauku ya kutaka kujua ni nini kipo njiani,lakini kwa taarifa zilizopo chini ya pazia ni kwamba Infinix itakuja na moja ya simu kabambe na huenda ikawa tishio kwa simu zote zenye kupatikana sokoni kwa bei isiyozidi sh. 350,000 huku baadhi ya sifa zikitajwa kupitia tovuti mbalimbali kwa kuusifu zaidi uwezo wa battery yenye mAh6000 kudumu na chaji kwa muda mrefu pamoja na ubora wa resolution yenye kukifanya kioo cha HOT 10 play kioo6.82 HD kuwa ang’avu wakati wote. 


Tembelea https://www.infinixmobility.com/tz/ ili kufahamu mengi zaidi.




Share:

AMUUA MDOGO WAKE KISA KUKU KUINGIA KWENYE SHAMBA LAKE

Na Amiri Kilagalila, Njombe
RAINARY Lugome mkazi wa wilaya ya Ludewa mkoani Njombe ameuawa na ndugu yake aliyefahamika kwa jina la Claus Samweli Lugome (46) kwa tuhuma za kuku wake kuingia katika shamba la kaka yake.

Akizungumza na vyombo vya habari kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamis Issa amesema wanawashikilia wanafamilia wawili akiwemo baba wa watoto hao, Ado Samweli Lugome pamoja na kijana aliyehusika na mauaji kwa ajili ya upelelezi.

“Haya mauaji ni ya hovyo,yaani kaka kamuua mdogo wake kisa na mkasa kuku wa mdogo mtu wameenda kwenye shamba la kaka mtu.”Alisema Kamanda Issa

Hata hivyo ameongeza kuwa katika upelelezi uliokuwa unaendelea wamebaini familia hizo zimekuwa zikituhumiana na maswala ya ushirikina.

“Katika ufuatiliaji wa swala hili tumeona wanatuhumiana kuwa mmoja anatembea na mke wake na mwingine anamtuhumu mwenzie kuwa alikuwa anamloga.”Alisema kamanda Issa

Ametoa rai kwa jamii kuacha kuamini ushirikina badala yake kutoa taarifa sehemu husika ili kusaidiwa kuliko kuchukua hatua mkononi.

Share:

SIMBA YATANGAZA MICHUANO YAKE....KOCHA MPYA KUTANGAZWA KESHO


Simba Sport Club leo January 22, 2021 , imetangaza michuano ya Kimataifa ‘Simba Super CUP’ ikihusisha timu tatu Simba, TP Mazembe ya Congo na Al Hilal ya Sudan.


Pia, timu hiyo imesema, kesho Jumamosi, itamtangaza kocha mpya atakayechukua mikoba ya Sven Vanderbroeck aliyeondoka. Kocha mpya atasaidiwa na kocha msaidizi, Suleiman Matola.

Akitangaza michuano hiyo leo Ijumaa tarehe 22 Januari 2021, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba (CEO), Barbara Gonzalez amesema, michuano hiyo, itaanza Jumatano ijayo tarehe 27- 31 Januari 2021.

Amesema, mechi ya kwanza itakuwa Simba dhidi ya Al Hilal saa 11 jioni.

Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema, michuano hiyo “ni maalum kwa mabingwa wa nchi, kama timu yako siyo bingwa, huhusiki na michuano hii.”


Share:

WALIMU WAWILI MKOANI NJOMBE WATIWA MBARONI KWA KUMTOA MIMBA MWANAFUNZI


Na Amiri Kilagalila, Njombe
JESHI la Polisi mkoani Njombe linawashikilia walimu wawili wa shule ya sekondari Mang’oto wilayani Makete mkoani Njombe kwa tuhuma za kumsababishia ujauzito na kumtoa mwanafunzi wa shule hiyo mwenye umri wa miaka 17.

Akizungumza na vyombo vya habari, kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Njombe,  Hamis Issa amesema wanamshikilia mwalimu Ezekiel Thomas (36) maarufu kwa jina la Dokole kwa kuwa na mahusiano na mwananfunzi na kumsababishia ujauzito.

“Huyu mwalimu amekuwa na mahusiano na mtoto wa sekondari mwenye umri wa miaka 17 na binti huyo amepimwa amegundulika ni mjamzito.” Alisema kamanda Issa

Aidha amesema wanamshikilia mwalimu, Ben Liamdilo (35) kwa kushirikiana katika tukio la utoaji wa mimba na kumsababishia maumivu mwanafunzi huyo.

“Mwalimu Thomas alifanya juhudi akamtuma huyu mwalimu mwenzake akambeba na boda boda kwenda kumtoa mimba mpaka sasa hivi walimu wote wawili tunawashikilia na wanatuhumiwa na makosa haya.”Alisema kamanda Issa

Vile vile ameitaka jamii kushirikiana kwa kutoa taarifa kwa jeshi la Polisi ili kukabiliana na vitendo kama hivyo.


Share:

WAZIRI MKUU ACHANGISHA SH. MILIONI 18.9 KUMSAIDIA MTOTO MIRIAM


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee ya papo kwa papo na kuchangisha sh. milioni 18.9 ambapo kati ya hizo, sh. milioni 10 zimetolewa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

“Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli anafuatilia tukio hili na amesema anamchangia Miriam shilingi milioni 10 ili ziweze kumsaidia katika mtaji wa biashara na umaliziaji wa ujenzi wa vyumba vya kupangisha”

Fedha hiyo ilichangishwa kwa ajili ya Miriam Msagati, binti mwenye ulemavu wa mwili ili ziweze kumsaidia kama mtaji wa biashara na uendelezaji wa ujenzi wa vyumba vya kupangisha katika nyumba ambayo amekabidhiwa leo (Ijumaa, Januari 22, 2021) na Waziri Mkuu. Gharama ya ujenzi wa nyumba na samani zilizomo ndani ni sh. milioni 47.32.

Waziri Mkuu ameendesha harambee hiyo kwenye kitongoji cha Fune, kata ya Mombo wilayani Korogwe baada ya kumkabidhi binti huyo nyumba aliyojengewa na wadau mbalimbali kutokana na mchango ulioasisiwa na Waziri Mkuu Machi 5, 2020 alipomtembelea Miriam na kumpatia mchango wa sh. milioni 5 za kuanza ujenzi wa nyumba hiyo.

Waziri Mkuu alimsaidia Miriam baada ya kumsikia binti akimuomba amsaide kupata makazi yeye na bibi yake kupitia kipindi cha Wape Nafasi kinachoongozwa na Tuma Dandi, mtangazaji wa Shirika la Utangazi Tanzania (TBC1).

Baada ya Waziri Mkuu kukabidhi nyumba hiyo, aliwaomba wadau wamchangie Miriam fedha ili apate mtaji pamoja na umaliziaji wa vyumba vya kupangisha ili aweze kujitegemea.

Akiwa bado anaendesha harambee hiyo, Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan alizungumza na wananchi hao kupitia simu aliyompigia Waziri Mkuu, ambapo alimpongeza kwa kuhakikisha Miriam anapata makazi bora. “Nimeona kazi kubwa iliyofanyika hapo, hongereni sana Waziri Mkuu pamoja na uongozi wa mkoa wa Tanga nami namuongezea shilingi milioni tano afanye mtaji.”

Kwa upande wake, Miriam baada ya kukabidhiwa nyumba hiyo alimshukuru Rais Dkt. Magufuli, Makamu wa Rais Mama Samia, Waziri Mkuu kwa uongozi wao wenye kujali wanyonge.

Alisema Tanzania imepata kiongozi mzuri anayewajali wanyonge, hivyo ameahidi kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu awazidishie baraka ili wapate mafanikio mazuri zaidi.

“Siwezi kusahau kitu kama hiki, Mwenyezi Mungu ameniona, Mwenyezi Mungu awabariki watu wote walioshiki katika kufanikisha jambo hili kwani mmeweka hazina yenu kwa Mungu.”

Kwa upande wake, Muandaaji wa Kipindi cah Wape Nafasi, Tuma Dandi alitumia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa namna inavyoshughulikia masuala mbalimbali ya watu wenye mahitaji maalumu.

“Nimeishiwa maneno, leo ni siku nyingine ambayo itaingia katika historia ya maisha yangu. Ninamshukuru Mwenyezi Mungu na Serikali kwa kufanikisha jambo hili kwani watu wenye ulemavu ni sehemu ya Watanzania ambao wanapaswa kuishi kama wengine.”

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


 


Share:

Livelihood Enhancement Manager

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Livelihood Enhancement Manager     The United Republic of Tanzania President’s Office TANZANIA SOCIAL ACTION FUND Tanzania Social Action Fund (TASAF) is currently implementing Productive Social Safety Net Program which aims at protecting the vulnerable poor households from severest consequences of poverty by implementing interventions that will lead to increased household incomes and opportunities while increasing […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Head of Communication and Public Relations at Sawa Initiative

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Head of Communication and Public Relations   SAWA INITIATIVE ORGANIZATION announces volunteering opportunity in. Instructions:   The email subject must be the position you are applying for eg; “PROJECT COORDINATOR” These positions are for applicants with bachelor degree in related field. Masters degree will be an added advantage. We only accept CV and applications letters. […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Project Coordinator at Sawa Initiative

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Project Coordinator (Volunteering)   SAWA INITIATIVE ORGANIZATION announces volunteering opportunity in. Instructions:   The email subject must be the position you are applying for eg; “PROJECT COORDINATOR” These positions are for applicants with bachelor degree in related field. Masters degree will be an added advantage. We only accept CV and applications letters. CV should have maximum […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Project Head at Sawa Initiative

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Project Head (Volunteering)   SAWA INITIATIVE ORGANIZATION announces volunteering opportunity in. Women applicants will be priotized for this position. Instructions:   The email subject must be the position you are applying for eg; “PROJECT COORDINATOR” These positions are for applicants with bachelor degree in related field. Masters degree will be an added advantage. We only accept […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

34 Job Opportunities at Startimes

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

StarTimes Group was founded in 1988.  It is the most influential system integrator, technology provider, network operator, and content provider in China’s television broadcasting industry, and it is on its way to become a media group with global influence. With a global vision, StarTimes began to expand its business to Africa in 2002, and has […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Assistant Quality Assurance Officer at NHIF

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST: ASSISTANT QUALITY ASSURANCE OFFICER III – 1 POST POST CATEGORY(S) HEALTHCARE AND PHARMACEUTICAL EMPLOYER Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) APPLICATION TIMELINE: 2021-01-20 2021-02-03 DUTIES AND RESPONSIBILITIES   To conduct inspection and supportive supervisions of health facilities. To deal with verification and checking of prescriptions; To make researches or market surveys with a view […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Communication and Member’s Affairs Officer at LHRC

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Public Relations, Communication and Member’s Affairs Officer     The Legal and Human Rights Centre (LHRC) is a Tanzanian, non-governmental organization that is private, voluntary, non-partisan, and not-for-profit sharing organization. It is registered and incorporated under the Companies (Act), Cap. 212, R.E. 2002, as a company without shares limited by guarantee, it has been in operation […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Research Associate, E-Savings at Innovations for Poverty Action (IPA)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

 Research Associate, E-Savings     Innovations for Poverty Action (IPA) seeks a Research Associate (RA) to support IPA-Tanzania, on the project “E-Savings.” This project will rigorously evaluate the role of intra-household bargaining on the take-up, usage, and effects of e-savings accounts offered to women in Tanzania. The RA will support completion of a baseline survey and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Mechanical Engineer at Gas Entec Co Ltd

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Mechanical Engineer PROJECT TITLE: CONSTRUCTION OF 1200 PASSENGER FERRY SHIP DESIGNATION: MECHANICAL ENGINEER (1 POST) PLACE OF WORK: MWANZA DUTIES & RESPONSIBILITIES Read and interpret blueprints, technical drawings, schematics, or computer-generated reports. Research, design, evaluate, install, operate, or maintain mechanical products, equipment, systems or processes to meet requirements. Confer with engineers or other personnel to […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

UINGEREZA YAPIGA MARUFUKU ABIRIA KUTOKA TANZANIA, DRC


Serikali ya Uingereza imepiga marufuku abiria kutoka Tanzania na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kuzuia maambukizi ya aina mpya ya virusi vya corona.

"Ili kusaidia kuzuia kuenea kwa aina ya COVID-19 iliyogundulika Afrika Kusini, tunapiga marufuku abiria wote wanaoingia kutoka Tanzania na DRC kuanzia saa 10 alfajiri kesho (Ijumaa)," ameandika Bw Grant Shapps, waziri wa usafirishaji nchini Uingereza kupitia mtandao wake wa Twitter Alhamisi usiku.

"To help to stop the spread of the COVID-19 variant identified in South Africa, we are banning all arrivals from Tanzania and Democratic Republic of Congo from 4am tomorrow.— Rt Hon Grant Shapps MP (@grantshapps) January 21, 2021"

Zuio hilo linaanza kwa wasafiri wote waliotoka ama kupita nchini Tanzania na DRC ndani ya siku 10 zilizopita. Hata hivyo, raia wa Uingereza na Ireland na raia kutoka mataifa mengine ambao wenye vibali vya ukaazi wataruhusiwa kuingia ila watatakiwa kujitenga nyumbani pamoja na familia zao kwa siku 10 baada ya kuwasili.

Tanzana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo zimeongezwa kwenye orodha ya Uingereza ya nchi zilizopigiwa marufuku ya wasafiri wake kuingia nchini humo kama hatua yza kudhibiti maambukizo ya aina mpya ya virusi vya Corona vilivyogunduliwa nchini Afrika kusini.

Awali mwezi huu mataifa mengine 11 ya Afrika yalipigwa marufuku kama hiyo. Mataifa hayo ni; Namibia, Zimbabwe, Botswana, Eswatini, Zambia, Malawi, Lesotho, Msumbiji na Angola - visiwa vya Ushelisheli na Mauritius.

Uingereza ilipiga marufuku abiria kutoka Afrika Kusini Desemba 24.

Uingereza ni miongoni mwa mataifa ambayo yanakabiliana na janga la virusi vya corona kwa kiwango kikubwa na uchumi wake ukiwa umeyumba kutokana na wimbi la kwanza la virusi mambukizi ya corona.

CHANZO- BBC SWAHILI

Share:

HAYA NDIYO MATAIFA 10 BARANI AFRIKA YENYE PASIPOTI ZENYE UWEZO MKUBWA


Mwaka 2021 unapojiandaa kusafiri kwa kutumia pasi yako ya kusafiria ni vyema kujua ni wapi pasi ya nchi yako inaweza kukupeleka.

Jinsi pasi ya kusafiria ya taifa lako inavyoweza kukuingiza katika mataifa mengi bila kutumia visa ndivyo jinsi kibali hicho kilivyo na uwezo.

Kila miezi mitatu kulingana na mtandao wa BBC Pidgin, Shirika la Henley Passport Index linashirikiana na shirika la usafiri wa kimataifa IATA ili kuripoti kuhusu uwezo wa pasipoti ya kila taifa wakati wa usafiri bila kutumia visa.

Katika robo ya kwanza ya mwaka 2021 shirika hilo limetoa idadi ya mataifa 10 yalio na pasipoti zenye uwezo mkubwa barani Afrika.

Pasipoti zenye uwezo mkubwa barani Afrika
Katika orodha hiyo taifa la Sycheles ndilo lenye pasipoti yenye uwezo mkubwa barani Afrika ikiwa na uwezo wa kukuingiza katika mataifa 151 bila kutumia Visa.

Katika nafasi ya pili, ni nchi ya Mauritius ambayo kibali chake cha usafiri kinaweza kukusaidia kuingia katika mataifa 142 bila kutumia Visa.

Taifa la tatu ni lile la Afrika Kusini ambalo unapoitumia pasipoti yake inaweza kukupeleka katika mataifa 101 bila kutumia visa.

Nafasi ya nne katika orodha hiyo ni taifa la Botswana ambalo pasipoti yake inaweza kukuingiza mataifa 85 bila kutumia visa.

Mataifa mengine yenye pasipoti zinazokaribiana kwa uwezo ni pamoja na Namibia, Lesotho, Eswatini na Malawi.

Pasi ya taifa la Nigeria inaweza kukuingiza katika mataifa 46 bila kutumia visa duniani, huku ile ya Ghana ikiwa na uwezo wa kukupeleka katika mataifa 65 nayo ya Cameroon ikikusafirisha na kukuingiza katika mataifa 49 bila ya kutumia visa.

Habari za hivi karibuni kuhusu pasi kumi zenye uwezo mkubwa Afrika zinaonesha kwamba Kenya ilishuka katika orodha hiyo na kuwa nambari 11.

Afrika mashariki

Kenya
Kulingana na mtandao huo wa Henley Index ,uwezo wa pasi ya Kenya umepungua katika miaka ya hivi karibuni kutoka nafasi ya 52 mwaka 2006.Taifa hilo la Afrika mashariki kwa sasa lipo katika nafasi ya 73 duniani huku wale wanaotumia pasi yake wakiwa na uwezo wa kuingia mataifa 72 pekee duniani.


Tanzania
Tanzania ni taifa la Afrika mashariki lenye sifa ya vivutio vya kitalii kama vile mbuga ya Serengeti na mlima Kilimanjaro ambao ndio mlima mrefu barani Afrika. limeorodheshwa kuwa taifa la 74 katika mtandao huo wa Henley index huku wanaomiliki pasi yake wakiwa na uwezo wa kuzuru mataifa 71 duniani bila kutumia visa.

Pasipoti zenye uwezo mkubwa duniani
Katika miaka mitatu mfululizo pasipoti ya Japan inasalia nambari moja kama pasi yenye uwezo mkubwa dunia ikiwa na uwezo wa kukuingiza katika mataifa 191 kote duniani bila kutumia visa.

Miaka michache iliopita walikuwa wakishikilia uwezo huo sawa na Singapore.

Hata hivyo Singapore imeshuka nafasi moja chini na kuwa nambari mbili huku pasi yake ikiwa na uwezo wa kukuingiza katika mataifa 190 duniani bila kutumia visa.

Korea Kusini na Ujerumani zinashikilia nafasi ya tatu kwa pamoja.

Mataifa matatu ambayo pasipoti zao zina uwezo wa chini duniani ni Syria, Iraq na Aghanistan.

CHANZO - BBC SWAHILI

Share:

KUWA WA KWANZA KUPOKEA HABARI UKIWA NA APP YA MALUNDE 1 BLOG...PAKUA HAPA IMEBORESHWA 2021

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger