Thursday 26 November 2020

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi Novemba 26



Share:

TPB BENKI YATOA MSAADA VITENDEA KAZI OFISI YA ARDHI MKOA WA TANGA


Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kulia akipokea msaada wa komputa mbili na printa moja zilizotolewa na Benki ya Posta (TPB)  wenye thamani ya milioni 3.5 kutoka kwa Mkurugenzi wa Fedha wa Benki hiyo Regina Semakafu kwa ajili ya ofisi ya Ardhi Mkoa wa Tanga
Mkuu WA Mkoa wa Tanga Martine Shigella kulia akipokea msaada wa komputa mbili na printa moja zilizotolewa na Benki ya Posta (TPB)  wenye thamani ya milioni 3.5 kutoka kwa Mkurugenzi wa Fedha wa Benki hiyo Regina Semakafu kwa ajili ya ofisi ya Ardhi Mkoa wa Tanga
Mkuu WA Mkoa wa Tanga Martine Shigella kulia akipokea msaada wa komputa mbili na printa moja zilizotolewa na Benki ya Posta (TPB)  wenye thamani ya milioni 3.5 kutoka kwa Mkurugenzi wa Fedha wa Benki hiyo Regina Semakafu kwa ajili ya ofisi ya Ardhi Mkoa wa Tanga

BENKI ya Posta imetoa msaada wa vitendea kazi kompyuta mbili na printa moja zenye thamani ya milioni 3.5 kwa ajili ya ofisi ya Ardhi mpya Mkoa wa Tanga ikiwa ni sehemu yao ya kuisaidia jamii katika kutatua changamoto mbalimbali.

Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo,Mkurugenzi wa Fedha wa Benki hiyo Regina Semakafu alisema msaada huo ni wajibu wao kama benki wakiwa wanaihudumia jamii hivyo wakaona umuhimu wa kuisaidia jamii katika kukutana na changamoto mbalimbali.

Alisema kwamba wanaamini hivyo vifaa ambavyo wamevitoa vitasaidia kuwahudumia wananchi na kupunguza changamoto za ofisi mpya ya ardhi mkoa wa Tanga .

“Hivyo tunaamini vifaa tulivyovitoa leo vitasaidia kuwahudumia wananchi na kupunguza changamoto za ofisi mpya ya ardhi mkoa wa Tanga “Alisema Mkurugenzi huyo wa Fedha.

Awali akizungumza mara baada ya kupokea hivyo,Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella aliishuku Benki hiyo kwa msaada huo ambao wameutoa kwa ajili ya ofisi ya ardhi mkoa huo.

Alisema kwamba kama wanavyofahamu serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt John Magufuli imejipambanua kwenye kufanya maboresho na kutatua changamoto za ardhi katika Taifa letu.

Mkuu huyo wa mkoa alisema ardhi inachangamoto nyingi sana na kwa mkoa huo hivyo anafarijika kuona kwamba ofisi imefunguliwa ikiwa inahitaji mahitaji mengi ikiwemo upatikanaji wa thamani na vifaa kama ambavyo vimekabidhiwa.

“Hivyo niwaambie kwamba mmekuja wakati muafaka kusawaidia na kuwapatia huduma watumishi wetu wa ofisi ya ardhina vifaa hii sio kwamba watavitumia kwa maslahi yao bali ni kwa maslahi ya wananchi wa mkoa wa Tanga “Alisema RC Shigella.

Hata hivyo aliwaishukuru benki hiyo kwa msaada huo huku akieleza kwamba ni matumaini yake kuona vifaa hivyo vinatunza na ili viweze kudumu na kupata thamani.

“Lakini niwaambie wananchi wa mkoa watembelea ofisi ya ardhi wapate hati na waweze kuzitumia kwa ajili ya kukopa na eneo pekee ni benki ya posta lakini wafungue akanti zao kwenye benki hiyo”Alisema RC Shigella.
Share:

Wednesday 25 November 2020

BABA ASAKWA KWA KUMUUA MTOTO WAKE


Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linamsaka baba mzazi, Adam Athuman (30-40) kwa tuhuma za kumuua mtoto wake mwenye umri wa miaka 10 Adam Athuman aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya msingi Nyamadoke Kata ya Buswelu Wilaya ya Ilemela. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, ACP Muliro Jumanne amesema  limetokea Novemba 22, 2020 majira ya saa 5:30 katika Kata ya Buswelu wilayani Ilemela ambapo mtoto huyo aliuawa kwa kushambuliwa na fimbo sehemu za mwili wake.

TAREHE 22.11.2020 MAJIRA YA 11:30HRS HUKO KATA YA BUSWELU, WILAYA YA ILEMELA, ATHUMAN ADAM,  MIAKA 10, MKEREWE, MWANAFUNZI WA DARASA LA TATU, SHULE YA MSINGI NYAMADOKE, BUSWELU, ALIUAWA KWA KILE KICHODAIWA KUSHAMBULIWA NA FIMBO SEHEMU ZA MWILI WAKE NA BABA YAKE MZAZI ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA ADAM ATHUMAN, MIAKA KATI YA 30-40, MKEREWE, FUNDI UJENZI, NYAMADOKE, MTUHUMIWA HUYO BAADA YA KUTEKELEZA UKATILI  HUO ALITOROKA, NA JESHI LA POLISI  LINAFANYA KILA JITIHADA KUHAKIKISHA ANATIWA  NGUVUNI  ILI AFIKISHWE KWENYE VYOMBO VYA SHERIA. MWILI WA MAREHEMU UMEFANYIWA UCHUNGUZI HOSPITALI YA BUGANDO NA KUKABIDIWA NDUGU KWA MAZISHI.

JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA LINAWAONYA NA KUTOA WITO KWA WAZAZI NA WALEZI WOTE KUWA MAKINI NA AINA YA ADHABU WANAZOTOA KWA WATOTO, KWANI WANAWEZA KUJIKUTA WAKITENDA MAKOSA YA KIJINAI NA HATIMAYE KUFIKISHWA MAHAKAMANI. 

IMETOLEWA NA;

Muliro JUMANNE MULIRO – ACP

KAMANDA WA POLISI (M) MWANZA

25, NOVEMBA 2020

Share:

SAVE THE CHILDREN YATOA MAFUNZO JUU YA BAJETI INAYOMHUSU MTOTO


Mratibu wa mradi wa mijadala jumuishi katika masuala ya uchumi na utawala wa kifedha Alex Enock kutoka Shirika la Save The Children mkoani Shinyanga, akizungumza kwenye mafunzo namna ya uaandaji wa bajeti inayomhusu mtoto.


Na Marco Maduhu -Shinyanga. 
Shirika la Save The Children linalotetea haki za watoto, limetoa mafunzo ya mchakato wa bajeti inayomhusu mtoto ngazi ya halmashauri, ili kuisaidia Serikali uaandaji wa bajeti nzuri ambayo itatoa haki za watoto na kukidhi mahitaji yao.

Mafunzo hayo ambayo yalianza jana na yamekoma leo, yamefanyika kwenye ukumbi wa mikutano katika hoteli ya Empire, yameshirikisha watendaji wa Kata, wataalamu kutoka halmashauri ya manispaa ya Shinyanga, waandishi wa habari, pamoja na wadau kutoka asasi za kiraia. 

Mratibu wa mradi wa mijadala jumuishi katika masuala ya uchumi na utawala wa kifedha Alex Enock kutoka Shirika la Save The Children mkoani Shinyanga, amesema lengo la mafunzo hayo ambayo yamedumu kwa siku mbili, ni kuwajengea uwezo wadau mbalimbali katika kushiriki kikamilifu kuandaa masuala ya bajeti, na kutambua wajibu wao katika kushiriki uundaji wa bajeti. 

Amesema katika mchakato mzima wa uaandaji wa bajeti za watoto, ni vyema bajeti hizo zikashirikisha watoto wenyewe katika utoaji wa mapendekezo yao ili kutambua nini wanakihitaji kutekelezewa, kuliko kuipitisha tu kwa mazoea na kuendelea kuwanyima haki zao za msingi. 

“Save the Children tunataka upangaji wa bajeti za watoto zishirikishe watoto wenyewe katika utoaji wa mapendekezo, ili kujua nini wanakihitaji, mfano katika masuala ya ukatili ambayo tunakumbana nayo moja ya sababu ni umbali wa shule, hivyo katika upangaji wa bajeti ya watoto ukiwashilikisha huenda wakatoa maoni ya kutaka kujengewa shule karibu,” amesema Enock. 

“Ukishirikisha watoto kwenye uaandaji wa bajeti yao, itatoa fursa kwa maendeleo ya mtoto bila ya ubaguzi, kutambua mahitaji maalumu ya watoto, pia kutambua mtiririko wa maamuzi katika matumizi ya rasilimali zinazolenga watoto,” ameongeza. 

Naye mwezeshaji wa mada ya uaandaji wa bajeti, Afisa mipango Mwandamizi Ofisi ya Rais tawala za mikoa Zanzibar Masika Baraka, amesema uaandaji wa bajeti nzuri ni ile ambayo inashirikisha walengwa husika, katika utoaji wa mapendekezo ili kujua nini wanakihitaji. 

Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo akiwamo mkurugenzi wa Shirika la Investing Childern and their Society mkoani Shinyanga (ICS) Kudely Sokoine, wameshukuru kupewa elimu hiyo, ambayo wamebainisha imewaongezea ufanisi katika utendaji wao kazi, hasa kwenye utekelezaji wa miradi ya watoto. 

TAZAMA PICHA HAPA CHINI 

Mratibu wa mradi wa mijadala jumuishi katika masuala ya uchumi na utawala wa kifedha Alex Enock kutoka Shirika la Save The Children mkoani Shinyanga, akizungumza kwenye mafunzo namna ya uaandaji wa bajeti inayomhusu mtoto.
Mratibu wa mradi wa mijadala jumuishi katika masuala ya uchumi na utawala wa kifedha Alex Enock kutoka Shirika la Save The Children mkoani Shinyanga, akizungumza kwenye mafunzo namna ya uaandaji wa bajeti inayomhusu mtoto.
Mwezeshaji wa mada ya uaandaji wa bajeti, Afisa mipango Mwandamizi Ofisi ya Rais tawala za mikoa Zanzibar Masika Baraka, akitoa elimu hiyo kwa washiriki.
Mwezeshaji wa mada kwenye mafunzo hayo mchumi kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga Allex Mpasa, akitoa elimu kwa washiriki.
Washiriki wakiwa kwenye mafunzo namna ya uaandaji wa bajeti inayomhusu mtoto.
Washiriki wakiwa kwenye mafunzo namna ya uaandaji wa bajeti inayomhusu mtoto.
Mafunzo yakiendelea.
Washiriki wakiendelea na mafunzo.
Washiriki wakiendelea na mafunzo.
Washiriki wakiendelea na mafunzo.
Washiriki wakiendelea na mafunzo.
Washiriki wakiendelea na mafunzo.
Washiriki wakiendelea na mafunzo.
John Shija kutoka Shirika la (PACESHI) Mkoani Shinyanga, akichangia mada kwenye mafunzo hayo.
Kudely Sokoine kutoka Shirika la (ICS) Mkoani Shinyanga akichangia mada kwenye mafunzo hayo.
John Eddy kutoka Shirika la (YWCA) akichangia mada kwenye mafunzo hayo.
Mwakilishi wa shirika la Women Fund Tanzania Mkoani Shinyanga Glory Mbia, akichangia mada kwenye mafunzo hayo.
Picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa mafunzo ya siku mbili yaliyojikita namna ya kuandaa bajeti inayokidhi mahitaji ya wananchi, wakiwamo watoto, yalioandaliwa na Shirika la Save The Children.


Na Marco Maduhu- Shinyanga.




Share:

MNYIKA : MDEE NA WENZAKE WALIOAPISHWA WAMEJITEUA ...TUMEWAITA KWENYE KIKAO CHA KAMATI KUU

 

 Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetoa siku mbili kwa wanachama wake 19, ambao jana walikula viapo Bungeni vya kuwa wabunge wa viti maalum bila ridhaa ya chama kwa ajili ya kuhudhuria kikao cha kamati kuu ya chama hicho kitakachofanyika Novemba 27, 2020.

 Mnyika amesema wanachama 19 wa chama hicho walioapishwa kuwa wabunge wa viti maalum hawakuteuliwa na chama hicho, “hawana baraka za chama wala uongozi. Kundi hilo la wabunge wa viti maalum limejiteua lenyewe.”

Kauli hiyo imetolewa leo Novemba 25, 2002, na Katibu Mkuu wa chama hicho John Mnyika, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, ambapo amesema kuwa kwa kuwa jambo hilo ni la dharura wameamua kufuata katiba yao inayosema kuwa, hatua zozote zisichukuliwe bila wahusika kuitwa kujieleza ili kujua ni nini kilichowapelekea wao kukisaliti chama.

"Kwa kuwa jambo hili ni la dharura natangaza wito (Public notice), kupitia vyombo vya habari kwa wanachama wetu 19 walioshiriki kwenda kula kiapo jana, kufika makao makuu ya chama bila kukosa siku ya Ijumaaa ya Novemba 27, 2020, saa 2:00 asubuhi, kutoka popote pale walipo kamati kuu inaweza kuchukua hatua za dharura kama itaona maslahi ya jumla ya chama yanaweza kuathiriwa", amesema John Mnyika.

Aidha Mnyika akizungumzia suala la wabunge hao kula kiapo hicho amesema kuwa, "Mimi kama Katibu Mkuu hakuna fomu yoyote ya mtu yeyote niliyowahi kuijaza popote kuthibitisha uteuzi wa yeyote, hii fomu pia ina sehemu ya kujazwa na kiapo cha hakimu kwa hiyo kwa tafsiri nyepesi ni kilichofanyika ni biashara haramu ya kughushi, wameenda kuapishwa bila baraka ya chama".

Wabunge 19 wanaotakiwa kuwasili siku ya ijumaa ni pamoja na Halima Mdee, Ester Bulaya, Esther Matiko na wengine walioapishwa kwa siku ya jana katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

CHANZO: EATV 

Share:

IPE USHINDI JAMBO... TUPIGIE KURA KATIKA TUZO ZA TANZANIA CONSUMER CHOICE AWARDS'

Jambo Food Products LTD Tumependekezwa katika Kipengele cha “Most Preferred Manufacturer Of The Year In Soft Drinks” Katika Tuzo za Tanzania Consumer Choice Awards.
.
Tupigie Kura Kwa Kubonyeza <HAPA>Link 
https://ift.tt/2V2w5Ko


Share:

Picha : AGPAHI YASHIRIKI KONGAMANO LA AFYA DODOMA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto  Profesa Mabula Nchembe akifungua Kongamano la Afya nchini  (Tanzania Health Summit) leo Novemba 25,2020 katika ukumbi wa St. Gaspar Jijini Dodoma.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Profesa Mabula Nchembe amefungua Kongamano la Afya nchini (Tanzania Health Summit) litakalojikita katika kujadili masuala mbalimbali ya afya hasa katika kipindi hiki ambacho nchi imeingia katika uchumi wa kati. 

Kongamano hilo litakalofanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia leo Jumatano Novemba 25,2020 hadi Novemba 26,2020 linafanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar jijini Dodoma limekutanisha pamoja wadau wa sekta ya Afya kutoka taasisi za umma,Mashirika ya dini na binafsi. 

Asasi ya kitaifa isiyo ya kiserikali ya Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) inayojihusisha na mapambano dhidi ya Virusi Vya Ukimwi na Ukimwi ni Miongoni mwa wadau wa afya wanaoshiriki katika Kongamano hilo linaloongozwa na Kauli Mbiu ya “Mafanikio ya Uchumi wa Kati Katika Kuweka Afya Bora kwa Watanzania – Transforming The Success of Middle – Income Economy Into a Healthier Nation)"

Akizungumza wakati wa kufungua Kongamano hilo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Profesa Mabula Nchembe amesema licha ya maendeleo makubwa yaliyofikiwa na serikali katika kuboresha huduma za afya kwa wananchi lakini bado kuna baadhi ya watu wanashindwa kuvifikia vituo vya afya na kupata huduma za afya. 

“Naomba mtumie kongamano hili kujadili ni namna gani tutoe huduma bora za afya,namna gani tuboreshe vifaa,miundo mbinu katika hospitali zetu.Namna gani tufanye ili kila mtu apate huduma za fya”,amesema Prof. Nchembe. 

“Kupitia kongamano hili tujadili na kutoa mapendekezo ya namna ya kuwasaidia kupata huduma za afya watu wa hali ya chini wakiwemo wakulima ambao hawawezi kufikia huduma za afya na hawana na bima za afya”,ameongeza Prof. Nchembe.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto  Profesa Mabula Nchembe akifungua Kongamano la Afya nchini  (Tanzania Health Summit) leo Novemba 25,2020 katika ukumbi wa St. Gaspar Jijini Dodoma. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto  Profesa Mabula Nchembe akifungua Kongamano la Afya nchini  (Tanzania Health Summit) leo Novemba 25,2020 katika ukumbi wa St. Gaspar Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto  Profesa Mabula Nchembe akifungua Kongamano la Afya nchini  (Tanzania Health Summit) leo Novemba 25,2020 katika ukumbi wa St. Gaspar Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto  Profesa Mabula Nchembe akifungua Kongamano la Afya nchini  (Tanzania Health Summit) leo Novemba 25,2020 katika ukumbi wa St. Gaspar Jijini Dodoma.
Wafanyakazi wa Asasi ya kitaifa isiyo ya kiserikali ya Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) inayojihusisha na mapambano dhidi ya Virusi Vya Ukimwi na Ukimwi wakiwa kwenye Kongamano la Afya jijini Dodoma leo Novemba 25,2020.
Wafanyakazi wa Asasi ya kitaifa isiyo ya kiserikali ya Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) inayojihusisha na mapambano dhidi ya Virusi Vya Ukimwi na Ukimwi wakiwa kwenye Kongamano la Afya jijini Dodoma leo Novemba 25,2020.
Wadau wa afya wakiwa kwenye Kongamano la Afya jijini Dodoma leo Novemba 25,2020.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto  Profesa Mabula Nchembe akifungua Kongamano la Afya nchini  (Tanzania Health Summit) leo Novemba 25,2020 katika ukumbi wa St. Gaspar Jijini Dodoma.
Wadau wa afya wakiwa kwenye kongamano.
Wadau wa afya wakiwa kwenye kongamano la afya.
Mkurugenzi wa Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Dk. Ntuli Kapologwe akizungumza kwenye Kongamano la Afya nchini linalofanyika jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Dk. Ntuli Kapologwe akizungumza kwenye Kongamano la Afya nchini linalofanyika jijini Dodoma.
Wadau wa afya wakiwa kwenye Kongamano la Afya.
Wadau wa afya wakiwa ukumbini.
Mkurugenzi wa Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii, Peter Maduki akizungumza kwenye Kongamano la Afya.
Mkurugenzi wa Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii, Peter Maduki akizungumza kwenye Kongamano la Afya.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Kongamano la afya.
Wa tatu kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Profesa Mabula Nchembe akijiandaa kukabidhi vyeti kwa washiriki wa Kongamano la afya.
Wa tatu kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Profesa Mabula Nchembe akimkabidhi  Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la AGPAHI, Alio Hussein ambaye ni Meneja Mradi AGPAHI mkoa wa Mara cheti cha Ushiriki wa Kongamano la Afya nchini (Tanzania Health Summit).
Wa tatu kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Profesa Mabula Nchembe akimkabidhi  Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la AGPAHI, Alio Hussein ambaye ni Meneja Mradi AGPAHI mkoa wa Mara cheti cha Ushiriki wa Kongamano la Afya nchini (Tanzania Health Summit).
Wa pili kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Profesa Mabula Nchembe akimkabidhi Mkurugenzi wa Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Dk. Ntuli Kapologwe cheti cha Ushiriki wa Kongamano la Afya nchini (Tanzania Health Summit).
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Profesa Mabula Nchembe akipiga picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano la Afya.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Profesa Mabula Nchembe akipiga picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano la Afya.
Wafanyakazi wa AGPAHI wakipiga picha ya kumbukumbu na Mkurugenzi wa Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Dk. Ntuli Kapologwe (wa tatu kulia).
Awali Meneja Mradi AGPAHI mkoa wa Mara (kushoto) , Alio Hussein akiwasili katika Kongamano la Afya.
Wafanyakazi wa AGPAHI wakiwa kwenye kongamano la afya.
Wafanyakazi wa AGPAHI wakiwa kwenye kongamano la afya.
Wadau wa afya wakiwa kwenye kongamano la afya.
Wadau wakiwa kwenye kongamano la afya

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger