Friday 29 May 2020

Associate, GAIN Premix Facility / Food Fortification Jobs at The Global Alliance for Improved Nutrition (GAIN)

Associate, GAIN Premix Facility / Food Fortification Location Tanzania, Dar es Salaam, Ethopia, Addis Ababa or Nigeria, Abuja Salary Competitive depending on experience Job Advert The Global Alliance for Improved Nutrition (GAIN) is seeking a Supply Chain and Business development professional to join their GAIN Premix Facility team. The role will be based in one of the following GAIN… Read More »

The post Associate, GAIN Premix Facility / Food Fortification Jobs at The Global Alliance for Improved Nutrition (GAIN) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

DevelopmentAid Recruitment Solutions – International Team Leader

Job Title: International Team Leader – Water Infrastructure Location: Tanzania Contract Duration: maximum 5 years and in any case to be implemented before August 9, 2025 Indicative start date: October 2020 DevelopmentAid Recruitment Solutions is seeking, on behalf of its international client, an individual to act as the International Team Leader for the Simiyu Climate Resilience Project, financed by… Read More »

The post DevelopmentAid Recruitment Solutions – International Team Leader appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

International Water Infrastructure, Water Engineering Team Leader for a project in Tanzania

Location: Tanzania Contract Duration: maximum 5 years and in any case to be implemented before August 9, 2025 Indicative start date: further specified Deadline Date: Friday, 05 June 2020 Organization: European Management Solutions Country: United Republic of Tanzania EMS is seeking, on behalf of its international client, an individual to act as the International Team Leader for the Simiyu Climate Resilience Project, financed by… Read More »

The post International Water Infrastructure, Water Engineering Team Leader for a project in Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

WASSHA Inc Tanzania – Assistant Group Leader -MWANZA and DSM

Assistant Group Leader Job Summary Assistant Group Leader is responsible to manage and lead the WASSHA team of 10-20 members among the four zones of coastal, southern, central and lakes. JOB DESCRIPTION JOB TITLE: Assistant Group Leader REPORT TO: Chief Operation Officer Job Summary: WASSHA Incorporation; provides the rental device and charging service using clean energy. Our mission is… Read More »

The post WASSHA Inc Tanzania – Assistant Group Leader -MWANZA and DSM appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Education Technical Assistant – Construction at NRC Tanzania

Education Technical Assistant – Construction  NRC Tanzania is looking for Education Technical Assistant – Construction base at Nyarugusu ,Kigoma The purpose of the technical assistant position is to assist in the day-to-day implementation of the Education project. All NRC employees are expected to work in accordance with the organization’s core values: dedication, innovation, inclusivity and accountability. These attitudes… Read More »

The post Education Technical Assistant – Construction at NRC Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Re-Advertisement: Terms of Reference for an Impact Study: Scaling Investment for Resilience of East Africa Coffee Producers Project

Deadline Date: Sunday, 31 May 2020 Tags: finance Organization: Solidaridad Eas & Central Africa Country: United Republic of Tanzania Preamble Solidaridad strives to be an organization that understands the signs of modern times, seeking to be a Civil Society Organization (CSO) with its own place and role in society, while simultaneously interacting with Governments and markets. The organization… Read More »

The post Re-Advertisement: Terms of Reference for an Impact Study: Scaling Investment for Resilience of East Africa Coffee Producers Project appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

The Toa Nafasi Project is hiring a new Executive Director

ABOUT US As a volunteer nursery school teacher in Tanzania’s Kilimanjaro Region in 2007, Sarah Rosenbloom was troubled to see a number of students writing backward or upside-down, in both literacy and numeracy exercises. These students found it difficult to catch on and were hard to correct; their teachers were at a loss as to how to help… Read More »

The post The Toa Nafasi Project is hiring a new Executive Director appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

BREAKING: Zitto Kabwe Kaachiwa Huru Kwa Sharti La Kutotoa Maneno ya Uchochezi

Kiongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo Zitto Kabwe ameachiwa huru  na Mahakama ya Kisutu kwa sharti kwamba asitoe matamshi ya uchochezi katika kipindi cha mwaka mmoja.

Katika kesi hiyo   ya uchochezi,  Zitto Kabwe  alikuwa anatuhumiwa kutoa maneno ya uchochezi yenye kuleta hisia ya hofu na chuki  akiwa katika mkutano na waandishi wa habari, uliofanyika katika makao makuu ya ofisi ya Chama cha ACT –Wazalendo Oktoba 28, 2018


Share:

PICHA: Zitto Kabwe Kawasili Mahakamani Kusikiliza Hukumu Yake Huku Tayari Akiwa Ameshanyoa Kipara

Mbunge wa Kigoma ambaye ni Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amewasili Mahakamani pamoja na Mawakili wake, kusubiri hukumu dhidi ya kesi yake ya uchochezi huku akiwa tayari amesha nyoa kipara.

Hukumu hiyo ya kesi ya uchochezi, inayotarajiwa kuvuta hisia za watu mbalimbali wa ndani na nje ya Tanzania, itatolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

Kesi hiyo iliyofunguliwa tarehe 2 Novemba 2018 na Jamhuri, itahitimishwa leo kwa Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo, ama kutupwa gerezani, kupigwa faini, au kuachiwa huru

Katika kesi ya msingi, Zitto anadaiwa Oktoba 28, 2018 akiwa katika mkutano na waandishi wa habari, uliofanyika katika makao makuu ya ofisi ya Chama cha ACT –Wazalendo, alitoa maneno ya uchochezi yenye kuleta hisia ya hofu na chuki.


Share:

Waziri Kairuki “Changamkieni Fursa Za Uwekezaji Wa Mafuta Ya Alizeti”.

NA MWANDISHI WETU
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Uwekezaji nchini Mhe. Angellah Kairuki ametoa rai kwa Watanzania kuwekeza katika sekta ya mafuta ya kula kwa kuzingatia uhitaji na soko lililopo ndani na nje ya nchi.

Ametoa rai hiyo Mei 28, 2020 alipotembelea na kukagua kiwanda cha kuzalisha mafuta ya kula cha SUNSHINE kinachozalisha mafuta yanayotengenezwa kwa kutumia malighafi ya alizeti yanayoitwa Sunbelt kilichopo katika eneo la Zuzu Jijini Dodoma.

Akiwa katika ziara hiyo, yenye lengo la kukagua, kusikiliza na kutatua changamoto za wawekezaji nchini.Waziri Kairuki alipongeza uwekezaji katika kiwanda hicho chenye uwezo wa kuzalisha tani 25 kwa siku na kilichowekeza zaidi ya shilingiBilioni 230.

“Niwapongeze kwa uwekezaji mkubwa mlioufanya katika eneo hili tangu mwaka 2015 na hii inaleta chachu kwa wawekezaji wazawa kuona fursa na soko la malighafi wanazozalisha hasa zao la alizeti,”alisema Waziri Kairuki

Aliongezea kuwa, ni vyema watanzania wakaendelea kuchangamkia fursa ya kilimo cha zao la alizeti kwa kuzingatia uhitaji mkubwa wa mafuta ya kula nchini kwani nchi imekuwa ikipoteza zaidi ya shilingi bilioni 443 kwa mwaka kwa kuagiza mafuta nje ya nchi.

Aidha Waziri alibainisha kuwa  uwekezaji huo ni miongoni mwa fursa muhimu na kuwataka wenye uwezo kulima zao hilo kwa wingi kuchangamkia  fursa hiyo kwa vile zao hilo linastawi katika ukanda huo.

Alitumia fursa hiyo kuendelea kuwasihi wataalam wa masuala ya kilimo kutoa elimu kwa umma kuhusu kilimo bora cha zao hilo ili kuwa na utaalam wa kutosha kuhusu kilimo cha zao hilo  ili kutumia mbinu za kisasa na zenye kuzingatia viwango vinavyotakiwa.

Akitoa taarifa ya kiwanda hicho, Meneja Biashara na Maendeleo wa kiwanda hicho Bw. Krishna Urs alieleza changamoto wanayokabiliana nayo ni uhaba wa malighafi kwa ajili ya uzalishaji na kuendelea kutoa wito kwa wadau kuitumia fursa ya kilimo cha zao hilo ili kuendana na mahitaji halisi.

“Ni muhimu kuwekeza zaidi katika alizeti kwa sababu soko lake lipo na hii itatatua changamoto ya kuzalisha kwa uchache na kuwafikia wananchi  wengi na kuapata soko la nchi za nje”, alisema Krishna.

Naye Afisa Viwango wa kiwanda hicho, Upendo Mganda alipongeza uwekezaji huo kwa kuwa, umesaidia kutoa ajira  na vibarua  kwa wananchi walio wengi.

“Tunashukuru uwepo wa kiwanda umetusaidia kupata ajira na wazawa wameweza kuuza malighafi zao kiwandani hapa kwa bei yenye tija,” alisema Upendo

Aidha aliongezea kuwa, ni kiwanda chenye tija kwa kuzingatia uwezo wake wa uzalisha tani 24 hadi 25 kwa siku na kinafanya vizuri sokoni kwa kuzingatia kuwa mafuta yanayozalishwa hayana kemikali zenye athari kwa watumiaji.

“Uzalishaji ni wa kuridhisha japo kuna changamoto ya uchache wa malighafi unaochangia kusuasua kwa uzalishaji na kusababisha kuzalisha kwa msimu si ya mavuno pekee inayochangia kutolifikia mahitaji halisi nchini,”alisema Upendo.

=MWISHO=


Share:

Hukumu Ya Zitto Kabwe Kusomwa Leo Ambapo Ndipo Hatima Yake Itajulikana Kama ni Faini, Kifungo au Kuachiwa Huru

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, leo  Ijumaa, tarehe 29 Mei, inatarajia kusoma hukumu ya kesi inayomkabili Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe

Hukumu hiyo ya kesi namba 327/2018 ya uchochezi, inayotarajiwa kuvuta hisia za watu mbalimbali wa ndani na nje ya Tanzania, itatolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi. 

Kesi hiyo iliyofunguliwa tarehe 2 Novemba 2018 na Jamhuri, itahitimishwa leo kwa Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo, ama kutupwa gerezani, kupigwa faini, kufungwa au kuachiwa huru
 
Katika kesi ya msingi, Zitto anadaiwa Oktoba 28, 2018 akiwa katika mkutano na waandishi wa habari, uliofanyika katika makao makuu ya ofisi ya Chama cha ACT –Wazalendo, alitoa maneno ya uchochezi yenye kuleta hisia ya hofu na chuki.

Ilidaiwa kuwa mshtakiwa alinukuliwa “…watu ambao walikuwa ni majeruhi katika tukio la mapambano baina ya wananchi na polisi wakiwa wamekwenda hospitali kupata matibabu katika kituo cha afya Nguruka, polisi wakapata taarifa kuwa kuna watu wanne wamekwenda hospitali kituo cha afya Nguruka kupata matibabu wakawafuata kule wakawaua…”

Katika shitaka ya pili ilidaiwa Oktoba 28, 2019 eneo la Kijitonyama katika makao makuu ya chama hicho, jijini Dar es Salaam, alitoa maneno ya uchochezi dhidi ya Jeshi la Polisi akisema “…lakini tumefuatilia kwa kina jambo hili, taarifa ambazo tumezipata kutoka kijijini Mpeta-Nguruka, Uvinza ni mbaya, ni taarifa ambazo zinaonyesha wananchi wengi sana wameuawa na jeshi la Polisi pamoja na kwamba afande Sirro amekwenda kule, haijatoa taarifa yoyote kuhusu wananchi…kama hawa Wanyantuzu walivamia eneo la Ranchi kuna taratibu za kisheria za kuchukua na sio kuwauwa, wananchi wengi sana wamekufa…”

Ilidaiwa kuwa katika tarehe hiyo hiyo, Zitto alitoa maneno ya uchochezi dhidi ya Jeshi la Polisi akisema “… Tumekuwa tukifuatilia kwa kina yanayojiri yote huko Uvinza tunasikitika kusema kuwa taarifa tunazozipata kutoka Uvinza zinaogofya mno, kwani tunaambiwa kuwa wananchi zaidi ya 100 wa kabila la Wanyantuzu wamepoteza maisha kwa kupigwa risasi na polisi, wengine wakisema kuuawa hata wakiwa kwenye matibabu hospitalini baada ya kujeruhiwa kwenye purukushani na jeshi la polisi…’’

Katika shauri hilo, upande wa mashitaka uliwasilisha mashahidi 15, huku Zitto akiwasilisha mashahidi nane.

Upande wa mashtaka uliongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Tumaini Kweka akisaidiwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga; huku Zitto akitetewa na mawakili watatu wakiongozwa na Jebra Kambole.

Mawakili wengine waliomtetea Zitto, ni Frank Mwakibolwa na Bonifacia Mapunda.



Share:

Ufaransa Yaipongeza Tanzania Mapambano Dhidi Ya Virusi Vya Corona

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Pamalagamba John Kabudi (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Ufaransa nchini, Mhe. Frederic Clavier ambapo pamoja na mambo mengine, Balozi Clavier ameipongeza Tanzania kwa hatua ilizochukua kupambana na janga a virusi vya corona nchini.

Balozi Clavier pia amemhakikishia Mhe. Waziri kuwa Ufaransa inaiunga mkono Tanzania kwa asilimia 100 kwa hatua ilizochukua kupambana na janga la virusi vya corona na kusema Ufaransa itaipatia Tanzania Euro milioni 30 ikiwa ni mkopo wenye masharti nafuu na riba ndogo kwa ajili ya kupambana na janga la virusi vya Corona pamoja na kusaidia kuinua uchumi.

Katika mazungumzo yao, Mhe. Waziri Kabudi amemuelezea Balozi wa Ufaransa jitihada zinazochukuliwa na Serikali ya Tanzania katika kupambana na Janga la Corona nchini na kumhakikishia utayari wa Tanzania katika kupambana na janga hilo na kuongeza kuwa Serikali ya Tanzania ilichukua hatua hizo kulingana na hali halisi ya maisha ya watanzania.

Prof. Kabudi amesema hatua zilizochukuliwa na Tanzania zililenga kuwafanya watanzania kuendelea na maisha yao bila ya kuathiriwa kiuchumi huku wakijilinda na kuchukua tahadhari ambazo zilikuwa zikitolewa na wataalamu wa afya nchini na duniani.

Balozi Clavier amemuambia Mhe. Waziri Kabudi kuwa Ufaransa pia imetoa msaada wa Dola 500,000 ambazo watapewa wakulima wadogowadogo 6,000 nchini kwa ajili ya kuboresha na kuimarisha kilimo chao na maghala ya kuhifadhia mazao yao.

Ameongeza kuwa Rais wa Ufaransa ameziandikia nchi za G20 na Paris Club kuzishawishi kuahirisha ulipaji wa madeni na riba zake na pia kufuta kabisa madeni hayo ili kuimarisha uchumi ambao umeathiriwa na janga la corona katika nchi zinazoendelea.

Katika hatua nyingine Waziri Kabudi amekutana na kuagana na Balozi wa Uturuki nchini Mhe. Ali Davutaglu ambaye amemaliza muda wake wa utumishi na amemtakia maisha mema na kumwambia kuwa ni matarajio yake kuwa atakuwa Balozi wa hiari wa Tanzania nchini uturuki na kwingineko duniani.

Naye balozi Davotaglu ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano ambao imekuwa ikimpatia alipokuwa akitekeleza majukumu yake nchini na kuahidi kuwa ushirikiano uliopo utaendelezwa hasa ikizingatiwa kuwa. 


Share:

Wafungwa Vifungo Vya Nje Watakiwa Kufanya Kazi Zinazoonekana Na Wadau

Na Veronica Mwafisi, MOHA-Morogoro
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Chritopher Kadio, ameitaka Idara ya Huduma za Uangalizi kuhakikisha wafungwa wenye vifungo vya nje wanafanya kazi zinazoonekana kwa wadau.

Alisema kutekelezwa kwa agizo hilo, wadau wataona faida ya wahalifu kutumikia adhabu zao nje ya Magereza badala ya kufanya usafi kwenye maofisi.

Kadio aliyasema hayo Mjini Morogoro jana wakati akifungua mkutano wa siku mbili unaoshirikisha Maafisa Wafawidhi wa idara hiyo kutoka mikoa 23 nchini.

Alitoa wito kwa idara hiyo kuandaa mpango mkakati ambao utaiwezesha Serikali kupunguza mzigo wa kuwahudumia wahalifu waliopo gerezani.

Alisema baadhi ya wahalifu wanaweza kutumikia adhabu zao nje ya Magereza hivyo ni wakati muafaka kwa idara hiyo kuwa na suluhisho ili changamoto hiyo iweze kupatiwa ufumbuzi.

“Lipo tatizo kubwa ambalo linaukabili mpango huu hasa fikra za kizamani kuwa adhabu ya kila mhalifu ni kwenda jela, dhana ya adhabu mbadala bado haijakolea katika fikra za wengi.

“Fikra hizo zipo kwenye sekta zote za jamii yetu kuanzia katika mahakama, baadhi ya Mahakimu wana kigugumizi cha kutoa adhabu za kutumikia jamii nje ya jela,” alisema.

Alifafanua kuwa, pia kwenye jamii vijijini na mitaani bado hawajaona umuhimu wa kutekeleza jukumu la kuwarekebisha na kuwalea jamaa zao wnaojiingiza katika uharifu.

Kadio alisema viongozi wa kisasa nao hawajalichangamkia jambo hilo na kulipigia debe kwa nguvu zote.

“Ni imani yangu kuwa idara pamoja na Wizara tunalo jukumu la kuhamasisha na kutoa elimu kwa wadau tukianzia mikoani, kila kiongozi wa Mkoa awe na mpango kazi wa kuelimisha.

“Mbali ya kuhamasisha matumizi ya adhabu mbadala pia ni jukumu letu kuhamasisha jamii ijiepushe na vitendo vya uhalifu, kuheshimu utawala wa sheria unaozingatia haki,” aliongeza.

Alisema pamoja na changamoto nyingi zinazoikabili idara hiyo katika utendaji kazi wao, aliwataka wakuu wa idara watafute ufumbuzi wake badala ya kuitegemea serikali izitatue.

Kadio alisema Wizara hiyo itaendelea kuwawezesha kadri inavyoweza ndio maana kila mwaka inaboresha bajeti yao.

“Ni vema mkafahamu kuwa, dhamira na dira ya Wizara yetu ni kudumisha utulivu, usalama na amani kwa Watanzania na ili dhamira hii ikamilike, idara imepewa jukumu la kusimamia utekelezwaji wa adhabu mbadala ya kifungo gerezani.

“Mnalo jukumu la kuchangia mafanikio ya Wizara iweze kufikia dhamira yake kwa Taifa,” alifafanua.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara hiyo, Aloyce Musika, alisema lengo la mkutano huo ni kufanya tathmini ya shughuli zilizofanyika mwaka mzima, kupanga mipango ya mwaka ujao.

Alimshuruku Kadio kwa kufungua mkutano huo ambao unashirikisha Maafisa Wafawidhi kutoka mikoa 23 ambayo wameifikia nchini isipokuwa mikoa mitatu ya Katavi, Lindi pamoja na Ruvuma.

“Miaka yote tumekuwa tukifanya mkutano kama huu kwa mafanikio makubwa mbali ya ugumu wa bajeti lakini Wizara imekuwa karibu na sisi, kukaa pamoja,” alisema.

MWISHO.


Share:

HALMASHAURI YA JIJI YAMPONGEZA RAIS JPM KWA HATUA ALIZOCHUKUA KUKABILIANA NA COVID 19



 Kaimu Ofisa Afya wa Jiji la Tanga Hamza Maulidi akizungumza wakati akitoa elimu katika semina ya siku mbili
inayotolewa kwa Wasaidizi wa msaada wa kisheria (Paralegals) kutoka halmashauri 11 zilizopo mkoani Tanga,

 Kaimu Ofisa Afya wa Jiji la Tanga Hamza Maulidi akizungumza wakati akitoa elimu katika semina ya siku mbili
inayotolewa kwa Wasaidizi wa msaada wa kisheria (Paralegals) kutoka halmashauri 11 zilizopo mkoani Tanga

 Programu Meneja wa Shirika la TEWOREC Halima
Jabiri Saguti akisisitiza jambo jana wakati akitoa elimu ya msaada wa kisheria kwa wasaidizi wa kisheria Mkoani Tanga yaliyoendeshwa na Shirika hilo Jijini Tanga kwa kushirikisha wilaya zote za mkoa huo
 AFISA wa Tathimini na Ufuatiliaji wa Taasisi ya TEWOREC akisisitiza jambo wakati wa semina hiyo
 Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Majira Mashaka Mhando akitoa uzoefu wake wakati wa semina hiyo

 Mmoja wa washiriki wa semina hiyo akichangia


HALMASHAURI ya Jiji la Tanga, imempongeza Rais John Magufuli, kwa hatua alizochukua kukabiliana na ugonjwa wa Corona nchini.

Sambamba na pongezi hizo, ugonjwa huo katika Jiji la Tanga unapungua kwa kasi kutokana na wananchi wengi kuchukua tahadhari zinazotolewa na Serikali pamoja na wataalamu wa afya.

Akizungumza kwenye semina ya siku mbili inayotolewa kwa Wasaidizi wa msaada wa kisheria (Paralegals) kutoka halmashauri 11 zilizopo mkoani Tanga, Kaimu Ofisa Afya wa Jiji la Tanga Hamza Maulidi alisema wananchi hawana budi kumpongeza Rais kutoka na kututoa hofu tangu alipogundulika mgonjwa mmoja hapa nchini.

Alisema kweli ugonjwa huo bado upo nchini na wananchi waendelee kuchukua tahadhari zote pamoja na kwamba maambukizi yanashuka kwa kasi kubwa Jijini hapa, lakini pia wanampongeza Rais kwa hatua alizochukua hadi ugonjwa unaendelea kupungua.

"Ugonjwa upo na Tanga pia upo, tuchukue hatua tunazoelekezwa na wataalamu wetu wa afya, lakini kwa kweli tunampongeza mheshimiwa Rais kwa kututia faraja tangu ugonjwa huu umeanza," alisema Maulidi.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo walisema yametolewa wakati muafaka ambao shughuli za kiserikali nyingi zimeanza kufanyika baada ya mikusanyiko kuzuia hivyo itawasaidia kupata uelewa mkubwa wa ugonjwa huo na taadhari zake.

Awali akifungua mafunzo hayo Meneja wa Shirika la kutoa msaada wa kisheria mkoani Tanga (TAWOREC) Halima Saguti alisema lengo la kutoa mafunzo kwa Paralegal hao ni kutaka wanapotoa huduma kwa wananchi huko vijijini waweze kujiinga na maambukizi ya ugonjwa huo.

Alisema kazi za wasaidizi hao wa kisheria zimekuwa zikiendelea huko vijijini na hivyo kupewa elimu hiyo kutasaidia kupunguza kusambaa kwa ugonjwa huo kwa watu wengine.
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa May 29



















Share:

Thursday 28 May 2020

Nafasi Mpya Za Kazi Zilizotangazwa Wiki Hii...Bofya Hapa

Share:

Ugonjwa Wa Malaria Wazidi Kupungua Nchini

Na.WAMJW,Chunya
Takwimu za kitaifa za viashiria vya malaria kwa mwaka 2017 (Malaria Indicator Survey) inaonesha kuwa upatikanaji wa vyandarua (access) kwa wananchi kitaifa ni asilimia 63 na matumizi ya vyandarua kwa wanajamii kitaifa ni asilimia 52.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa ugawaji wa vyandarua kwa kila kaya uliofanyika wilayani Chunya.

Waziri Ummy amesema kuwa Mkoa wa Mbeya, upatikanaji wa vyandarua ni asilimia 62 na kiwango cha matumizi ya vyandarua kwa Mkoa ni asilimia 32 tu.

“Nchi yetu imepiga hatua kubwa na kupata mafanikio katika mapambano dhidi ya Malaria ambapo kiwango cha maambukizi kimepungua kwa karibu asilimia 50, kutoka asilimia 14.8 mwaka 2015 hadi asilimia 7.3 mwaka 2017. Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema hiyo ni kutokana na takwimu za matokeo ya utafiti wa viashiria vya Malaria katika jamii (MIS 2017) ambapo visa vipya vya Malaria vimepungua kwa asilimia 19 kutoka visa 150 kati ya watu 1000(2015) hadi visa 122 kati ya watu 1000(2019).

Ameongeza kuwa idadi ya vifo vitokanavyo na Malaria vimepungua kwa asilimia 67 kutoka vifo 6311 mwaka 2015 hadi vifo 2079 mwaka 2019.

“Kwa mkoa wa Mbeya pia maambukizi yapo kwa kiasi cha asilimia 4 kiwango hiki ni kidogo ukilinganisha na wastani wa kitaifa wa asilimia 7.3

Aidha, Waziri Ummy amesema kila mwanafamilia mwenye dalili za Malaria ahakikishe kuwa anawahi kwenye kituo cha kutolea huduma za afya ili kupimwa kabla ya kutumia dawa kwani sio kila homa ni Malaria na endapo atagundulika kuwa na vimelea vya malaria ahakikishe anatumia dawa kulingana na maelekezo ya mtoa huduma za afya na kumaliza dozi ili kuepuka usugu wa dawa mwilini.

Ugawaji wa vyandarua unafanyika kwa awamu tatu kupitia Bohari Kuu ya Dawa(MSD) ambapo awamu ya kwanza inajumuisha mikoa ya Mbeya,Songwe,Njombe na Rukwa

Awamu ya pili ni mikoa ya Iringa, Dodoma na Singida na awamu ya tatu na ya mwisho itahusisha mikoa ya Tanga,Kilimanjaro na Manyara.

Hata hivyo mikoa mingine iliyobaki itaendelea kupata vyandarua kupitia kliniki ya afya ya uzazi (wajawazito) na watoto chini ya mwaka mmoja na pia kupitia wanafunzi wa shule za msingi.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger