Saturday 22 February 2020

Serikali ya Mseto yaundwa Sudan Kusini

Viongozi hasimu nchini Sudan Kusini wameunda serikali mpya ya umoja wa kitaifa leo hii inayotarajiwa kudumu kufuatia vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Siku moja baada ya Rais Salva Kiir kulivunja baraza la mawaziri la serikali iliyopita, kiongozi wa upinzani Riek Machar ameapishwa kama makamu wa kwanza wa rais wa Sudan Kusini. 
Hatua sawa na hiyo iliwahi kushindikana mara mbili zilizopita na kuzua mapigano yaliyopelekea vifo vya watu 400,000.
Maelfu ya vikosi hasimu vya makabila tofauti vitalazimika kujumuishwa katika jeshi la serikali mpya. 
Umoja wa Mataifa umesema hatua hiyo bado haikutimizwa kulingana na ratiba ilivyopangwa. 
Kiir na Machar wamesema masuala mengine muhimu yatajadiliwa chini ya serikali mpya.



Share:

Miji mitatu ya Tanzania yatajwa kasi ya ongezeko la watu duniani

Idadi ya watu duniani inatarajia kukua kufikia watu bilioni 8.6 ifikapo mwaka 2030, ambapo miji kutoka nchi mbalimbali za Afrika ndiyo itakayoongoza kwa ukuaji huo.

Kwa mujibu wa taarifa ya Umoja wa Mataifa (UN) ya mwaka 2017 ukuaji huo utatokea katika nchi tisa, kati ya nchi hizo, tano zinatoka barani Afrika ambazo ni Tanzania, Congo, Uganda, Nigeria, na Ethiopia.

Kwa mujibu wa Jukwaa la Uchumi Duniani (WEF) ifikapo mwaka 2035 miji 15 ambayo idadi ya watu inakuwa kwa kasi zaidi, ambayo yote inatokea Afrika, inatarajiwa kuwa na wastani wa watu mara mbili zaidi ya waliopo sasa, ambapo katika miji hiyo, Tanzania imefanikiwa kuingiza miji mitatu.

Nchi za Afrika zinakadiriwa kuwa zitakuwa zaidi kutokana na kuwa na vijana wengi zaidi duniani. Zaidi ya 75% ya watu wote barani Afrika wana umri chini ya miaka 35, kwa mujibu wa UN.

Hapa chini ni orodha kamili ya miji 15 duniani ambayo ongezeko la watu litakuwa kwa kasi zaidi hadi ifikapo mwaka 2035:

15. Lilongwe, Malawi: Hadi mwaka 2020 ina watu 1,122,000, na idadi hiyo inakadiriwa itakuwa kwa 97% hadi 2,210,000.

14. Ouagadougou, Burkina Faso: Hadi sasa kuna watu 2,780,000,na idadi itaongezeka kwa 97% kufikia 5,481,000.

13. Uige, Angola: Jumla ya watu sasa ni 511,000, makadirio ya ukuaji ni kwa 98% hadi kufikia 1,013,000.

12. Bobo-Dioulasso, Burkina Faso: Idadi ya watu mwaka sasa ni 972,000 ambapo itakuwa kwa 100% kufikia.

11. Dar es Salaam, Tanzania: Mji huu una jumla ya watu 6,702,000, kasi ya ukuaji ni 100% ambapo itafikia watu 13,383,000.

10. Tete, Mozambique: Jumla ya watu katika mji huu ni 371,000, ongezeko litakua kwa kasi ya 101%hadi kufikia 744,000.

9. Niamey, Niger: Jumla ya watu 1,292,000, kasi ya ukuaji ni 101% ambapo itafikia watu 2,600,000.

8. Bunia, Congo: Mji huu una jumla ya watu 679,000, ambapo idai ya watu itaongezeka kwa kasi 101% kufikia 1,368,000.

7. Gwagwalada, Nigeria: Mji wa Gwagwalada una jumla ya watu 410,000, ambapo ukuaji watu unatarajiwa kukua kwa kasi ya 102% kufikia 827,000.

6. Mwanza, Tanzania: Mji wa Mwanza una watu 1,120,000, ukuaji wake utakuwa kwa kasi ya 102% kufikia 2,267,000.

5. Songea, Tanzania: Mji huu uliopo mkoani Ruvuma una watu 353,000 na unakadiriwa kuwa utakua kwa 110% kufikia watu 740,000.

4. Kabinda, Congo: Mji unakadiriwa kuwa na watu 466,000, na ukuaji wake utakua kwa 110% kufikia watu 979,000.

3. Kampala, Uganda: Kampala ina makadirio ya watu 3,928,000, na kasi ya ukuaji inatarajiwa kuwa kasi 112% kufikia 7,004,000.

2. Zinder, Niger: Mji huu unakadiriwa kuwa na watu 489,000, ukuaji wake unakadiriwa kuongezeka kwa 118% kufikia 1,065,000.

1.Bujumbura, Burundi: Mji huu unaongoza kwa kasi ya ukuaji wa watu ambapo hadi mwaka 2020 unakadiriwa kuwa na watu 1,013,000, idadi hiyo itakua kwa 123% kufikia 2,263,000.


Share:

Serikali Kudhibiti Wahamiaji Haramu Wanaotumia Njia Za Treni

Na Mwandishi Wetu
Serikali imeapa kudhibiti wimbi la wahamiaji haramu wanaosafiri kwenda mikoa mbalimbali  nchini kwa kutumia usafiri wa treni huku ikiwataka wananchi kuacha tabia ya kuwahifadhi na kuwasafirisha wahamiaji hao kwani kufanya hivyo ni kinyume cha  sheria.

Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni, mkoani Tabora  wakati wa kikao na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani hapa baada ya kuwepo kwa taarifa za kiintelijinsia zinazohusisha baadhi ya wahamiaji haramu kutumia usafiri huo kuingia katika mikoa mbalimbali nchini

“Nchi yetu inaelekea kwenye uchaguzi mkuu mwishoni mwa mwaka huu,hivyo ni vyema kudhibiti watu wanaoingia nchini pasina kufuata utaratibu rasmi,na tuna taarifa juu ya wahamiaji haramu sasa kuanza kutumia njia ya treni kuingia nchini tena wengine wakisaidiwa na raia sasa natao onyo wenye tabia hiyo kuacha mara moja na vyombo vya ulinzi na usalama viimarishe ulinzi katika maeneo husika” alisema Masauni

Akizungumza katika Kikao hicho,Kaimu Afisa Uhamiaji Mkoa wa Tabora,Kamishna Msaidizi,Amiru Sadiki aliiomba serikali kuweka maafisa uhamiaji katika vituo vyote vya reli nchini ili kuweza kukagua wasafiri wanaoingia katika mikoa mbalimbali kama ilivyo katika viwanja vya ndege.

Awali akitoa taarifa ya hali ya ulinzi na usalama Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora,Kamishna Msaidizi wa Polisi,Barnabas Mwakalukwa alisema hali ni shwari huku kukiripotiwa matukio machache.

“Upungufu wa makosa ya mauaji ambayo hapo awali yalikuwa kero kubwa kwa wananchi umetokana na juhudi za polisi katika kufanya doria ya kukamata waganga wa kienyeji wanaojihusisha na ramli chonganishi na tayari jeshi tumeanza operesheni maalumu inayoendelea katika mikoa ya Shinyanga,Geita,Mwanza,Kagera,Simiyu na Tabora huku kukiwa na mafanikio makubwa na hali sasa inaendelea kutulia” alisema ACP Mwakalukwa.


Share:

YANGA YATOA MSAADA WODI YA AKINA MAMA KITUO CHA AFYA NGAMIANI JIJINI TANGA

  Afisa Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaz kulia akikabidhi msaada wa vitu mbalimbali kwa Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Ngamiani Jijini Tanga Anjelina Mahaka kushoto kwa ajili ya wakina mama wajawazito wanaojifungua kwenye kituo hicho  katikati anayeshuhudia ni Mkurugenzi wa Mashindano wa Klabu ya Yanga Thabithy Kandoro
  Afisa Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaz kulia akikabidhi msaada wa vitu mbalimbali kwa Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Ngamiani Jijini Tanga Anjelina Mahaka kushoto kwa ajili ya wakina mama wajawazito wanaojifungua kwenye kituo hicho leo katikati anayeshuhudia ni Mkurugenzi wa Mashindano wa Klabu ya Yanga Thabithy Kandoro
  Afisa Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaz kulia akikabidhi msaada wa vitu mbalimbali kwa Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Ngamiani Jijini Tanga Anjelina Mashaka kushoto kwa ajili ya wakina mama wajawazito wanaojifungua kwenye kituo hicho  katikati anayeshuhudia ni Mkurugenzi wa Mashindano wa Klabu ya Yanga Thabithy Kandoro

  Afisa Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaz kulia akikabidhi msaada wa vitu mzazi aliyemkuta kwenye wodi ya wakina mama wajazito kwenye Kituo cha Afya cha Ngamiani Jijini Tanga  kushoto ni kwa ajili ya wakina mama wajawazito wanaojifungua kwenye kituo hicho leo katikati anayeshuhudia ni Mkurugenzi wa Mashindano wa Klabu ya Yanga Thabithy Kandoro
 Afisa Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaz akizungumza mara baada ya kutoa msaada huo kulia ni Mkurugenzi wa Mashindano wa Klabu ya Yanga Thabithy Kandoro
 Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Ngamiani Jijini Tanga Anjelina Mashaka akizungumza huku akiishukuru Klabu ya Yanga kwa msaada huo
 Mkurugenzi wa Mashindano wa Klabu ya Yanga Thabithy Kandoro akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo kushoto ni Afisa Mhamasishaji wa klabu hiyo Antonio Nugaz
Afisa Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaza kushoto akiwaongoza wanachama na wapenzi wa klabu hiyo kuingia kwenye kituo cha Afya Ngamiani Jijini Tanga kwa ajili ya kutoa msaada .

KLABU ya Yanga imetoa msaada wa vitu mbalimbali kwenye wodi ya wakina mama wajawazito kwenye kituo cha Afya Ngamiani Jijini Tanga ikiwa ni mkakati wao kusaidia makundi mbalimbali kila wanapo kwenda kucheza mechi zao za ligi kuu ikiwa ni mpango wao wa kurudisha kwa jamii.

Msaada huo umekabidhiwa leo na Afisa Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaz kwa Mganga Mfawidhi wa kituo hicho Anjelina Mashaka katika halfa iliyohudhuriwa mashabiki na wanachama wa timu hiyo mkoani Tanga.

Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo Nugaz alisema wana mshukuru Mwenyezi Mungu amewawezesha kuwqa sehemu ambazo wazazi wao ambao walizaliwa kwenye vituo mbalimbali vya afy na wao wamefika kwenye kituo hicho kwa kile walichobarikiwa wakiotoe wodi ya wakina mama.

Alisema msaada ambao wameutoa pamoja na vitu vyengine lakini neti za kujikinga na mbu ambazo wamezikabidhi zitakuwa msaada mkubwa kwao ili kuepukana na kuumwa ugonjwa wa malaria.

“Wazazi ambao wamebahatika kupata watoto wanapaswa kujikinga na mbu ambao wanaeneza malaria hivyo katika kurudisha kwa jamii timu ya wananchi tumeona tuwasaidia neti na vitu vyengine ikiwemo sabuni na vifaa kwa ajili wa watoto wadogo”Alisema Mhamasishaji huyo.

Aidha alisema kwamba amefurahishwa na namna wanachama wa Yanga na mashabiki waliovyoonyesha mshikamano wa pamoja kwenye jambo hilo hivyo kwa niaba ya kamati ya utendaji chini ya Mwenyekiti wao Dkt Mshindo Msola na timu nzima.wanakwenda kuchukua pointi tatu ingawa mechi itakuwa ni ngumu.

Awali akizungumza katika halfa hiyo Mganga Mfawidhi wa kituo hicho Anjelina Mashaka aliishukuru klabu hiyo kwa kuona umuhimu wa kuwasaidia msaada huo ambao umefika wakati muafaka.

“Nashukuru kupokea neema ambazo mmezileta Yanga kwa niana ya Jiji la Tanga natoa shukrani zangu za dhati kwa ajili ya zawadi na wagonjwa wetu ambao wanajiandaa kupata watoto”Alisema Mganga huyo

Alisema kwamba pia wanathamini mchango wao wa kutoa sadaka kwap ambao utawasaidia kutokana na hapo awali kuwa na uhitaji wa neti ambazo zitasaidia kwenye kituo hicho.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Mashindano wa timu ya Yanga Thabithy Kandoro alisema kwamba timu halisi ya Yanga lazima iende kwa vitendo ni jambo la msingi wao.

Alisema wao kama timu ya wananchi wana sababu ya kuijenga timu yao na kuwa wazalendo na kuhakikisha wananchi wanafaidi na kupata afadhali watu wengine wajitokeze kuwasaidia watu wenye mahitaji mbalimbali.
Share:

Picha : MFANYABIASHARA MAARUFU GEORGIA BUYAMBA AFUNGUA DUKA JIPYA LA VINYWAJI ‘UNIQUE LIQUOR STORE’ SHINYANGA MJINI

Share:

WIZARA YABARIKI MSAFARA WA KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA


Kaimu Katibu Mkuu Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara Bw. Leornard Mchau akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa Msafara wa wa kitaifa wa wa kijinsia wenye lengo la kutokomeza ukatili wa kijinsia leo jijini Dodoma utakoanzia Mpanda mkoano Latavi tarehe 24/02/2020. Picha Zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW
Kaimu Katibu Mkuu Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara Bw. Leornard Mchau akizungumza na wawakilishi wa msafara wa wa kitaifa wa wa kijinsia wenye lengo la kutokomeza ukatili wa kijinsia leo jijini Dodoma utakoanzia Mpanda mkoano Latavi tarehe 24/02/2020.
Msanii wa  Muziki wa kizazi kipya Nurdin Bilal Shetta akielezea namna watakavyoupamba msafara wa wa kitaifa wa wa kijinsia wenye lengo la kutokomeza ukatili wa kijinsia wakati wa mamandalizi ya kuondoka kwa msafara huo leo jijini Dodoma utakoanzia Mpanda mkani Katavi tarehe 24/02/2020.
Kaimu Katibu Mkuu Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara Bw. Leornard Mchau akiagana na Msanii wa  Muziki wa kizazi kipya Nurdin Bilal Shetta mara baada ya kuzunumza na wawakilishi wa msafara wa wa kitaifa wa wa kijinsia wenye lengo la kutokomeza ukatili wa kijinsia leo jijini Dodoma utakoanzia Mpanda mkoano Latavi tarehe 24/02/2020.
**


Na Mwandishi Wetu Dodoma
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii imebariki kuanza kwa Msafara wa kitaifa wa wa kijinsia wenye lengo la kutokomeza ukatili wa kijinsia.

Akizungumza na wawakilishi wa Wizara, Wadau kutoka Legal Services Facility, Wildaf na wasanii wa muziki wa kizazi kipya leo jijini Dodoma Kaimu Katibu Mkuu Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Bw. Leonard Mchau amesema msafara huo umeandaliwa maalum kupeleka ujumbe wa kupambana na ukatili wa kijinsia kuelekea maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Wanawake Duniani.

Bw. Mchau amewaasa wawakilishi hao wa Msafara huo kupeleka ujumbe huo ambao utasaidia kuendeleza mapambano ya kutokomeza vitendi vya ukatili nchini ambavyo vimekuwa vikishamiri kila siku katika jamii.

Ameongeza kuwa Serikali imeweka mkazo katika kuhakikisha vitendo vya ukatili wa kijinsia vinatokomea kwa kasi ili watoto na wanawake wanaoathirika na vitendo hivyo kuoondokana na vitendo hivyo vinavyowanyima baadhi ya haki zao msingi.

Akizungumza kwa niaba ya Wadau Mwakilishi wa Shirika la LSF Bw. Joseph Magazi ameishukuru Serikali kwa kuwashirikisha waau katika kampeni ya kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia na wameahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika mapambano hayo.

Akizungumza kwa naiaba ya Wasanii Bw. Nurdil Bilal maarufu kama ‘Shetta’ amesema watatumia sanaa yao kufikisha ujumbe kwa jamii kwani wao ni mmoja ya wanajamii na wanapaswa kushirikiana nayo kusaidia kupambana kutokomeza vitendo vya kikatili katika jamii.

Msafara huu utaanzia katika mkoa wa Katavi wilaya ya Mpanda tarehe 24/02/2020 na kuendelea hadi tarehe 05/03/2020 katika vituo vifuatavyo, Sumbawanga, Rukwa tarehe 25/02/2020 Vwawa, Songwe tarehe 26/02/2020, Mbeya Mjini tarehe 27/02/2020 Makambako, Njombe tarehe 28/02/2020 Iringa Mjini, Iringa tarehe 29/02/2020 Tabora Mjini, Tabora Mjini tarehe 01/02/2020 Shinyanga mjini tarehe 03/03/2020 Maswa Simiyu tarehe 04/03/2020.
Share:

CHADEMA Yateua Makatibu Wa Kanda.




Share:

Waziri mkuu wa Lesotho anayekabiliwa na mashtaka ya kumuua mkewe wa zamani aondoka nchini

Waziri mkuu wa Lesotho Thomas Thabane anayekabiliwa na mashitaka ya kumuua mke wake wa kwanza Lipolelo Thabane hakufika mahakamani, wakati alitakiwa kufika mahakamani jana Ijumaa kusikiliza tuhuma zinazomkabili.

Mkewe wa kwanza bwana Thabane,58. alipigwa risasi katika mji mkuu wa Maseru, siku mbili kabla ya bwana Thabane kuwa waziri mkuu 2017.

"Hakufika mahakamani, alienda Afrika kusini kwa matibabu , na vipimo hivyo ni vya mara kwa mara" , katibu wake Thabo Thakalekoala ameliambia shirika lahabari la AFP.

Wakati huo huo naibu kamishna wa polisi Paseka Mokete amewaambia waandishi wa habari kwamba watasubiri ili kuendelea na kesi hiyo hadi atakaporudi nchini.

“Hatuwezi kwa sasa kusema kwamba alikiuka agizo la mahakama, ” Paseka Mokete ameongeza.

Mapema mwezi Februari 2020, mke mpya wa Waziri Mkuu, Maesaiah, alishtakiwa rasmi kwa mauaji ya mke mwenza na sasa yuko nje kwa dhamana ya dola 67.

Pia ameshtakiwa na jaribio la mauaji ya rafikiye Thato Sibolla ambaye alikuwa na Lipoleo wakati wa tukio hilo la mauaji na anatarajiwa kuwa shahidi mkuu katika mauaji hayo.


Share:

Bukoba DC Job opportunities, February 2020

Bukoba DC Job opportunities, February 2020  

The post Bukoba DC Job opportunities, February 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Walimu Mkoani Tabora Watakiwa Kuwafundisha Wanafunzi Umuhimu Wa Uzalendo

NA TIGANYA VINCENT
WALIMU Mkoani Tabora wametakiwa kuwalea kimaadili wanafunzi na wanavyuo ili waweze kukua katika uadilifu na uzalendo ambao utakaowawezesha kushiriki ujenzi wa Tanzania mpya msingi mkuu ni viwanda.

Kauli hiyo imetolewa leo  na katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora Msalika Makungu wakati wa ufunguzi wa mafunzo na maelekezo  kuhusiana na uendeshaji wa klabu za maadili kwa walimu wa shule za msingi ,sekondari na vyuo.

Alisema kuwa katika kukuza uchumi Tanzania mpya ipo haja ya kuwa na vijana ambao wamekuzwa katika msingi ya uadilifu na uzalendo ambao utaweka mbele maslahi ya Taifa na sio masalahi binafisi.

“Maslahi ya Taifa yatadumu daima …lakini maslahi ya mtu binafsi ni ya muda baada ya kufa basi nayo yamekwisha” alisema.

Makungu alisema mafunzo hayo ni muhimu sana katika kujenga jamii yenye maadili mema ambayo yatasaidia kuzalisha Viongozi wazalenda na waadilifu.

Aidha Katibu Tawala huyo wa Mkoa aliwapongeza  walimu kwa kazi kubwa na nzuri mnayoifanya ya kukuza maadili mkoani Tabora na kuongeza kuwa uanzishwaji wa Klabu  za Maadili utaleta mabadiliko chanya na  kuongeza ufaulu kwa vijana mashuleni na vyuoni.

Kwa upande wa Kaimu Mkuu wa Kanda ya Magharibi, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Gerald Mwaitebele alisema Ofisi hiyo imeamua kuanzishia Klabu hizo ili kuwajenga vijana tangu awali ili kuwajenga kukua kimaadili na uzalendo wakiwa wadogo.

Alisema ni kazi kubwa kufundisha umuhimu wa maadili kwa mtu mzima kuliko kufundisha akiwa mdogo kwa kuwa atajengeka katika hali ya uadilifu na kuipenda nchi yake.

 Mafunzo hayo ya siku moja yameshirikisha walimu wa shule za Msingi, sekondari na Vyuo vya Elimu vilivyopo Manispaa ya Tabora na yalikuwa na mada za Sheria  ya Maadili ya Viongozi wa Umma na Mgongano wa Masilahi na Mwongozo wa Uanzishwaji na Uendeshaji wa Klabu za Maadili

mwisho


Share:

Waziri Mkuu: Uzalishaji Mbegu Za Michikichi Unaridhisha

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema ameridhishwa na hatua iliyofikiwa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) katika uzalishaji wa mbegu bora za zao la michikichiki katika kituo cha Tari Kihinga mkoani Kigoma.

Aliyasema hayo jana jioni (Ijumaa, Frbruari 21, 2020) alipotembelea kituo cha utafiti wa zao la michikichi cha Tari Kihinga kilichopo wilayani Kigoma alipokuwa katika ziara yake ya siku moja mkoani Kigoma.

Akiwa kituoni hapo, Waziri Mkuu alipokea taarifa ya utafiti juu ya uendelezaji wa zao la michikichi uliliyofanywa na TARI kuanzia mwaka 2018, ambapo hadi kufikia Februari 15, 2020 taasisi hiyo ilikuwa imezalisha mbegu 1,525,017 ambazo zinaweza kupandwa katika shamba lenye ukubwa wa ekari 30,500.

Waziri Mkuu alisema Serikali imeamua kulipa kipaumbele zao la michikichi kwa lengo la kumaliza tatizo la upatikanaji wa mafuta ya kula nchini, hivyo ufufuaji zao hilo utaliwezesha Taifa kuzalisha mafuta ya kutosha kwa ajili ya mahitaji ya ndani na ziada itakayobakia itauzwa nje ya nchi.

Kufuatia hatua hiyo, Waziri Mkuu amewataka wananchi hasa vijana kuchangamkia fursa ya kulima zao hilo kwa wingi kwa kuwa upo uhakika wa kupata mbegu bora na pia zao hilo litawakwamua kiuchumi na kuwaondolea umasikini wa kipato.

Pia, amewaagiza Maofisa Ugani kuwafuata wakulima katika maeneo yao na kuwaelekeza namna ya kulima zao hilo kuanzia hatua za awali za utayarishaji mashamba, matumizi bora ya pembejeo ili waweze kulima kisasa na kujiongezea tija.

Baada kutembelea kituo hicho Waziri Mkuu alizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Mwanga Community Centre uliopo Manispaa ya Kigoma Ujiji, ambapo pamoja na mambo mengine aliwataka watumishi wa umma watenge muda ya kusikiliza kero za wananchi.

“Watumishi mnatakiwa kwenda kwa wananchi na kusikiliza kero zinazowakabili na kushirikiana nao katika kuzipatia ufumbuzi. …hamuendi na kama mngekuwa mnaenda kusingekuwepo na mabango kwani kitendo cha kuwepo mabango ni ishara tosha kwamba hamuendi.”

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema Serikali imepeleka fedha nyingi mkoani Kigoma za kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo zikiwemo sh bilioni 4.6 kwa ajili ya ununuzi wa dawa, ambapo Manispaa ya Kigoma Ujiji inapata sh milioni 50 kila mwezi hivyo hakuna sababu ya wananchi kukosa dawa.

Alisema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kuboresha na kusogeza huduma za afya kwa kujenga vituo vya afya karibu na makazi ya wananchi zikiwemo za afya ili kuwapunguzia kutembea umbali mrefu hadi hospitali za wilaya au mkoa.

Waziri Mkuu ameuagiza uongozi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji kupitia Baraza lake la Madiwani wahakikishe wanasimamia vizuri matumizi ya fedha mbalimbali zinazotolewa na Serikali kwa lengo la kugharamia miradi ya maendeleo.

 Waziri Mkuu alikemea tabia ya baadhi ya wananchi katika maeneo mengi ya mkoa wa Kigoma kudai fidia kwenye maeneo  hata ya mapori na kukwamisha baadhi ya miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa hospitali ya kanda, aliwataka wabadilike.

Awali, Waziri Mkuu alishiriki swala ya Ijumaa katika msikiti wa Mujahidina uliopo eneo la Buzebazeba mijini Kigoma, ambapo alitumia fursa hiyo kuwaasa waumini wa dini ya kiislam na wananchi kwa ujumla kuendelea kushikama na kulinda amani.

Pia, Waziri Mkuu aliwahamasisha walime zao la michikichi kwani Serikali imeamua kulifufua zao hilo ili waweze kuondokana na umasikini. Wanaotamani kulima michikichi wajiandae wakati utakapofika watasambaziwa miche.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi February 22
















Share:

Friday 21 February 2020

Picha : JAMBO YATOA MSAADA WA VINYWAJI KWA JESHI LA AKIBA SHINYANGA

Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ ya mkoani Shinyanga imetoa msaada wa katoni 50 za vinywaji kwa wanafunzi wa Jeshi la Akiba wilaya ya Shinyanga waliopo katika mafunzo yao.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo leo Ijumaa Februari 21,2020, Mkurugenzi wa Kampuni ya Jambo Food Products Ltd, Esme Salum amesema kampuni hiyo imeungana na wanafunzi wa Jeshi la akiba kwa kuchangia katika kufanikisha mahafali ya mafunzo yatakayofanyika Machi 4,2020.

“Jambo tumefurahi kuungana na wanafunzi wa jeshi la akiba kwa kuchangia katika kufanikisha mahafali yao ikiwa ni sehemu ya utamaduni wetu tuliojewekea kushirikiana na jamii inayotuzunguka. Tumetoa katoni 50 za vinywaji baridi kati ya katoni hizo 20 ni za maji na 30 ni za juisi mchanganyiko”,amesema Salum.

Akipokea katoni hizo za vinywaji baridi, Msaidizi Ofisi ya Jeshi la Akiba wilaya ya Shinyanga,Sajenti Geofrey Kamala ameishukuru Kampuni ya Jambo kwa kuwaunga mkono kufanikisha sherehe ya jeshi la akiba.

“Tuliwaandikia barua Jambo ya kuomba msaada watuchangie katika mahafali yetu ya jeshi la akiba.Kwa kweli tunawashukuru sana Jambo wamejitoa kwa moyo mmoja,wametupatia maji katoni 20 pamoja na juisi katoni 30.

Tunawashukuru sana kwa kutuunga mkono katika sherehe yetu ya jeshi la akiba Mungu awabariki sana,kazi yenu iendelee kubarikiwa”,amesema Kamala.

Jumla ya wanafunzi 143 wa Jeshi la akiba kutoka wilaya ya Shinyanga walioanza mafunzo yao Novemba 4,2019 wanatarajia kumaliza mafunzo yao Machi 4,2020.
Kushoto ni Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum akishikana mkono na Msaidizi Ofisi ya Jeshi la Akiba wilaya ya Shinyanga,Sajenti Geofrey Kamala wakati akimkabidhi katoni 50 za vinywaji baridi kuchangia mahafali ya wanafunzi wa Jeshi la Akiba yatakayofanyika Machi 4,2020. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum akishikana mkono na Msaidizi Ofisi ya Jeshi la Akiba wilaya ya Shinyanga,Sajenti Geofrey Kamala wakati akimkabidhi katoni 50 za vinywaji baridi kuchangia mahafali ya wanafunzi wa Jeshi la Akiba.
Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum (wa pili kushoto) akikabidhi vinywaji baridi kwa viongozi wa kamati ya sherehe mahafali ya Jeshi la akiba wilaya ya Shinyanga. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya sherehe Sarah Stephen,wa kwanza kulia ni Katibu wa sherehe Aderick Godfrey akifuatiwa na Mhasibu wa sherehe Martha Charles.
Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum akimwelezea Msaidizi Ofisi ya Jeshi la Akiba wilaya ya Shinyanga,Sajenti Geofrey Kamala na baadhi ya wanafunzi wa Jeshi la Akiba namna kiwanda cha Jambo kinavyoendesha shughuli za uzalishaji wa vinywaji baridi.
Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum akieelezea namna wanavyozalisha vinywaji baridi.
Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum akionesha muonekano wa chupa ya kuwekea vinywaji kabla ya kuingizwa kwenye mitambo.
Msaidizi Ofisi ya Jeshi la Akiba wilaya ya Shinyanga,Sajenti Geofrey Kamala na baadhi ya wanafunzi wa Jeshi la Akiba  wakiangalia namna uzalishaji wa vinywaji baridi unavyofanyika.
Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum akiendelea kuwatembeza kiwandani wageni wake.
Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum akiendelea kueleza namna kiwanda cha Jambo kinavyoendesha shughuli za uzalishaji wa vinywaji baridi.
Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum akiteta jambo na Msaidizi Ofisi ya Jeshi la Akiba wilaya ya Shinyanga,Sajenti Geofrey Kamala baada ya kutembelea kiwanda cha Jambo.
Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum.  akimkaribisha ofisini kwake Msaidizi Ofisi ya Jeshi la Akiba wilaya ya Shinyanga,Sajenti Geofrey Kamala (kulia).
 Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum. (wa pili kulia) akielezea namna Kampuni yao inavyoshirikiana na jamii kuchangia shughuli mbalimbali za maendeleo.
Msaidizi Ofisi ya Jeshi la Akiba wilaya ya Shinyanga,Sajenti Geofrey Kamala akiishukuru Kampuni ya Jambo Food Prouducts kwa kuchangia katoni 50 za vinywaji baridi ili kufanikisha mahafali ya Jeshi la Akiba.
Msaidizi Ofisi ya Jeshi la Akiba wilaya ya Shinyanga,Sajenti Geofrey Kamala  akiagana na Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum.
Msaidizi Ofisi ya Jeshi la Akiba wilaya ya Shinyanga,Sajenti Geofrey Kamala na wanafunzi wa Jeshi la Akiba wakipiga picha ya kumbukumbu na Mkurugenzi wa  Kampuni ya Utengenezaji na Usambazaji wa Vinywaji baridi ‘Jambo Food Products Limited’ Esme Salum.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger