Sunday 1 December 2019

Picha : AGPAHI YASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI...SERIKALI YAONYA USHAMIRI MAAMBUKIZI YA VVU SHINYANGA


Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog 
Shirika lisilo la kiserikali ya Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) linalojihusisha na mapambano dhidi ya Virusi Vya UKIMWI na UKIMWI imeungana na serikali ya mkoa wa Shinyanga kuadhimisha Siku ya UKIMWI duniani Desemba 1,2019 kwa kutoa huduma mbalimbali zinazolenga kupunguza maambukizi mapya ya VVU.

Maadhimisho hayo kwa mkoa wa Shinyanga yamefanyika katika kijiji cha Negezi kata ya Ukenyenge wilayani Kishapu ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack. 

AGPAHI imeshiriki katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani kwa kutoa elimu ya VVU na UKIMWI na maonesho ya shughuli zinazofanywa na AGPAHI ikiwemo ujasiriamali kwa vijana wanaolelewa na shirika hilo. 

Akizungumza kwa niaba ya wadau wanaoshirikiana na serikali katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI,Meneja wa Shirika la AGPAHI Kanda ya Ziwa, Dkt. Nkingwa Mabelele amesema wadau ikiwemo AGPAHI wanaendelea kushirikiana serikali ili kuhakikisha maambukizi mapya ya VVU yanapungua. 

“Tunaendelea kushirikiana na serikali bega kwa bega ili kufikia asilimia 90 ya huduma za VVU na UKIMWI (malengo ya 90-90-90)”,amesema Dkt. Mabelele. 

“Tunataka asilimia 90 ya wananchi wote wanatambua afya zao,90% ya wanaogundulika kuwa na maambukizi ya VVU wanaingia katika mpango wa matumizi sahihi na ufuasi mzuri wa dawa na 90% inayobaki ni wale wote wanaotumia dawa kuhakikisha wanakuwa na kiwango cha chini cha VVU”,ameongeza Dkt. Mabelele. 

Alisema Tanzania bila UKIMWI inawezekana hivyo kuwaomba wadau na jamii kwa ujumla kushikamana na kushirikiana na serikali ili kuhakikisha maambukizi mapya ya VVU yanapungua. 

Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya ya Kishapu, Mhe. Nyabanga Talaba alisema kutokana na utafiti uliofanyika hivi karibuni,mkoa wa Shinyanga hivi sasa una ushamiri wa maambukizi ya VVU ya asilimia 5.9 (THIS 2017) ambayo iko juu ya kiwango cha taifa cha sasa cha asilimia 4.7 (THIS 2017). 

“Tafsiri rahisi ya ushamiri wa asilimia 5.9 ina maanisha kuwa watu 5 hadi 6 kati ya 100 huambukizwa Virusi vya UKIMWI takribani kila saa moja inayopita kwa mkoa wetu wa Shinyanga”,alieleza Talaba kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga. 

Talaba aliwahamasisha wananchi kuendelea kujitokeza kupima ili wajue afya zao huku akiwakumbusha wanaume kufanyiwa tohara ili kupunguza hatari ya kupata maambukizi ya VVU sambamba na kuachana na mila potofu zinazochochea maambukizi mapya ya VVU. 

“Tuendelee kuchukua tahadhari kwani UKIMWI bado upo na hauna chanjo wala tiba, bali una kinga na dawa za kufubaza makali ya VVU. Kama umepata maambukizi tafadhali endelea kutumia dawa za kufubaza makali ya VVU na zingatia lishe kwani kuwa na maambukizi ya VVU haimaanisi kuwa ndiyo mwisho wa maisha yako”,alisema Talaba. 

Mkuu huyo wa wilaya ametumia fursa hiyo kuyapongeza mashirika yanayoshirikiana na serikali katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI na kuyaomba yaongeze nguvu zaidi ili kufikia malengo ya 90-90-90. 

Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani Desemba 1,2019 ni ‘Jamii ni chachu ya mabadiliko tuungane kupunguza maambukizi mapya ya VVU’.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI

Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  Desemba 1,2019 ambapo katika Mkoa wa Shinyanga yamefanyika katika Kijiji cha Negezi kata ya Ukenyenge wilayani Kishapu. Wa kwanza kulia ni Meneja wa Shirika la AGPAHI Kanda ya Ziwa, Dkt. Nkingwa Mabelele. Wa kwanza kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Rashid Mfaume akifuatiwa na Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga Joachim Otaru. Picha zote na Kadama Malunde 1 blog
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Rashid Mfaume akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  Desemba 1,2019 ambapo katika Mkoa wa Shinyanga yamefanyika katika Kijiji cha Negezi kata ya Ukenyenge wilayani Kishapu.
Mratibu wa Kudhibiti UKIMWI mkoa wa Shinyanga, Dkt. Peter Mllacha akisoma taarifa ya UKIMWI mkoa wa Shinyanga kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  Desemba 1,2019 ambapo katika Mkoa wa Shinyanga yamefanyika katika Kijiji cha Negezi kata ya Ukenyenge wilayani Kishapu. 
Meneja wa Shirika la AGPAHI Kanda ya Ziwa, Dkt. Nkingwa Mabelele akizungumza kwa niaba ya wadau wanaoshirikiana na serikali katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI.
Meneja wa Shirika la AGPAHI Kanda ya Ziwa, Dkt. Nkingwa Mabelele akizungumza kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  Desemba 1,2019 ambapo amesema wadau ikiwemo AGPAHI wanaendelea kushirikiana serikali ili kuhakikisha maambukizi mapya ya VVU yanapungua. 
Kushoto  ni Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba (mwenye nguo nyekundu) akitembelea Banda la AGPAHI kwenye maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani Desemba 1,2019. Katikati ni Meneja wa Shirika la AGPAHI Kanda ya Ziwa, Dkt. Nkingwa Mabelele (katikati) akimwelezea Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba kuhusu shughuli zinazofanywa na shirika la AGPAHI ikiwemo kuhudumia watu wanaoishi na maambukizi ya VVU.
Meneja wa Shirika la AGPAHI Kanda ya Ziwa, Dkt. Nkingwa Mabelele akiendelea kumweleza Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba kuhusu shughuli zinazofanywa na shirika la AGPAHI katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba akiuliza swali kuhusu VVU na UKIMWI kwenye banda la AGPAHI.
Afisa Miradi Huduma Unganishi kwa Jamii AGPAHI mkoa wa Shinyanga Selephina Soteli akifafanua jambo kwa Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba akiangalia sabuni ya maji iliyotengenezwa na vijana wanaolelewa na Shirika la AGPAHI ambao wameanzisha kikundi cha Ujasiriamali ili kujikwamua kiuchumi. Wa pili kushoto ni kijana Edson Jastine akieleza namna wanavyotengeneza sabuni na kumuomba Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba kuwatafutia soko la kuuzia sabuni zao.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba akiangalia sabuni zilizotengenezwa na vijana wanaolelewa na shirika la AGPAHI.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba akiwapongeza vijana wanaolelewa na shirika la AGPAHI kwa kuanzisha kikundi cha ujasiriamali kinachowasaidia kujipatia kipato. Nyabaganga alitumia fursa hiyo kuwakumbusha wananchi kujishughulisha na kazi zitakazowasaidia kupata pesa ili ziwasaidie katika maisha yao.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba na Wakurugenzi wa halmashauri za Kishapu (Stephen Ndaki) na Shinyanga (Hoja Mahiba) katikati wakiwaunga mkono vijana hao kwa kununua sabuni ambapo sabuni zote walizokuja nazo kwenye maonesho wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ziliisha baada ya Mhe. Talaba kuzipigia debe.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba akiendelea kuuza sabuni zilizotengenezwa na vijana wanaolelewa na AGPAHI.
Wadau na wafanyakazi wa AGPAHI wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye banda la AGPAHI wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  Desemba 1,2019 ambapo katika Mkoa wa Shinyanga yamefanyika katika Kijiji cha Negezi kata ya Ukenyenge wilayani Kishapu.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Talaba akicheza muziki na akina mama wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  Desemba 1,2019 ambapo katika Mkoa wa Shinyanga yamefanyika katika Kijiji cha Negezi kata ya Ukenyenge wilayani Kishapu.
Wanenguaji wa Kundi la Msanii wa Nyimbo za Asili Jibhela Ngelela kutoka kijiji cha Mayanji wilayani Kishapu wakitoa burudani wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  Desemba 1,2019 ambapo katika Mkoa wa Shinyanga yamefanyika katika Kijiji cha Negezi kata ya Ukenyenge wilayani Kishapu.
Burudani ya sarakasi ikiendelea wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  Desemba 1,2019.
Meza kuu wakifuatilia burudani.
Kijana akitoa burudani ya wimbo akielimisha kuhusu VVU na UKIMWI.
Wadau na wananchi wakiwa kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  Desemba 1,2019 ambapo katika Mkoa wa Shinyanga yamefanyika katika Kijiji cha Negezi kata ya Ukenyenge wilayani Kishapu.
Wanafunzi wakiwa kwenye maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  Desemba 1,2019.
Wananchi na wanafunzi wakiwa kwenye  kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  Desemba 1,2019.
Mwalimu Kassim Mwenda akitoa ushuhuda jinsi alivyopata maambukizi ya VVU mwaka 2008 na mpaka sasa anaendelea kuishi kutokana na kuzingatia lishe na matumizi sahihi za dawa za kufubaza makali ya VVU.
Wadau wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani Desemba 1,2019.
 Diwani wa kata ya Ukenyenge Mhe. Underson Mandia akizungumza wakati wa kufunga kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  Desemba 1,2019. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

Lazaro Nyalandu Achaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kati

Aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu ameshinda nafasi ya Mwenyekiti wa Chadema, Kanda ya Kati kwa kupata kura 60 kati ya 86 zilizopigwa na kumshinda aliyekuwa mwenyekiti wa kanda hiyo, Alphonce Mbasa.

Akitangaza matokeo hayo leo Jumapili Desemba Mosi, 2019, Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Patrick Sosopi akisaidiana na katibu mkuu wa baraza hilo, Julius Mwita. amesema waliopiga kura walikuwa 86, hakuna kura iliyoharibika.

Amesema aliyekuwa mwenyekiti wa Kanda hiyo, Alphonce Mbasa amepata kura 26, sawa na asilimia 33.2.

Katika nafasi ya mweka hazina, Mbunge wa Viti Maalum,  Devotha Minja ameibuka mshindi baada ya kupata kura 44 sawa na asilimia 51.2 huku mshindani wake, Tully Kiwanga akipata kura 42 sawa na asilimia 48.8.


Share:

Waziri wa Kilimo: Watakaoajiri Watoto Chini Ya Miaka 18 Kwenye Tumbaku Kukiona Cha Moto

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amesisitiza marufuku yake aliyoitoa hivi karibuni kuhusu ajira kwa watoto ambao wapo chini ya miaka 18.

Mhe Hasunga amepiga marufuku hiyo jana tarehe 30 Novemba 2019 wakati akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo Jijini Dar es salaam.

Alisema kuwa suala la ajira kwa watoto ni miongoni mwa mambo yanazuiliwa kwenye Sheria za kimataifa kupitia Shirika la Kazi Duniani (International Labour Organization) na Sheria za Ajira hapa nchini hivyo mdau yeyote atakayebainika kukiukwa maelekezo hayo atashtakiwa.

“Nawasihi wadau wote hususani wakulima wa Tumbaku tuendelee kupiga vita ajira kwa watoto kwa kuwa ni eneo ambalo limeendelea kulalamikiwa na wadau wengi” Alikaririwa Mhe Hasunga

Kadhalika, Mhe Hasunga alisema kuwa katika kuhakikisha zao la tumbaku linaendelea kutoa mchango mkubwa katika pato la mkulima na Taifa, Wizara imejiwekea malengo ya haraka yanayopaswa kutekelezwa ambayo ni pamoja na usajili wa wakulima wote wa tumbaku, kuwapatia vitambulisho na kuwaingiza kwenye kanzidata ili kupata takwimu za uhakika za maeneo wanayolima na kuiwezesha serikali kusimamia upatikanaji wa pembejeo kulingana na mahitaji yao.

Aidha, mipango mingine ni kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo kwa wakati kwa kuweka utaratibu wa kumwezesha mkulima kujitegemea kwa pembejeo ili aache kuwa tegemezi wa mikopo ya mabenki yenye riba kubwa.

Pamoja na malengo hayo ya haraka, Wizara ya Kilimo inasimamia utekelezaji wa malengo ya muda mrefu yakiwemo Upatikanaji wa wanunuzi wapya wa tumbaku kwa sasa na kwa miaka ijayo kabla ya Juni, 2020, Kuongeza ubora wa zao la tumbaku kutoka asilimia 87 ya sasa hadi asilimia 92 ifikapo Juni 2022 na Kuongeza mbegu mpya na bora za tumbaku ili tuweze kupata masoko katika nchi nyingine kama vile China.

Alisema ili kufikia malengo hayo wadau wote wa tasnia ya tumbaku wanapaswa kushirikiana ili kufikia malengo hayo na wakulima kunufaika na jasho lao.

Tumbaku ni miongoni mwa mazao makuu ya kimkakati ya yaliyopewa kipaumbele na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Mhe Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mazao mengine ni pamoja na Tumbaku,  Kahawa, Pamba, Korosho, Chai, michikichi na alizeti. 

Mhe Hasunga alisema kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa malengo ya uzalishaji yanafikiwa kwa kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa pembejeo kwa wakati, kuboresha huduma za ugani na kutafuta masoko mapya ya tumbaku.

Waziri Hasunga amesema kuwa katika msimu wa kilimo 2019/2020 ambao masoko yake yataanza mwezi Mei 2020, kampuni za ununuzi zilizopo nchini ambazo ni Alliance One Tanzania, Premium Active Tanzania na Japan Tobacco International zimetoa mikataba ya kilo 42,225,985 na tayari wakulima wapatao 33,000 wameomba kusajiliwa na Bodi ya Tumbaku kutokana na uzalishaji huo. Uzalishaji huo ni mdogo na hivyo unaacha wakulima takribani 16,000 bila kulima tumbaku msimu huu.

Kutokana na hali hiyo, Wizara ya Kilimo kupitia Bodi ya Tumbaku ilianzisha jitihada za kutafuta masoko mengine ili kuziba pengo la kampuni ya Tanzania Leaf Tobacco – TLTC ambayo haijatoa makisio ya uzalishaji msimu huu.

Jihada hizo zimepelekea kupata kampuni nne (4) mpya ambazo zimeonesha nia ya kununua tumbaku ya Tanzania msimu ujao . Kampuni hizo Kampuni za Zambia kupitia kampuni ya kizawa ya MAGEFA GROWERS Ltd itanunua kilo 5,500,000, Kampuni ya TRANSAFRICQUE kupitia kampuni ya kizawa ya GRAND TOBACCO GROWERS Co. Ltd imeomba kununua kilo 9,000,000, Kampuni ya PETROBENA itanunua kilo 300,000, na Kampuni ya PACHTEC  Limited imeomba kununua kilo 500,000

Takwimu zinaonesha kwamba kwa kipindi cha zaidi ya miaka 10 hadi kufikia mwaka 2016 tumbaku imekuwa na mchango mkubwa wa kuliingizia Taifa fedha za kigeni.  Kwa mfano katika mwaka 2017, tumbaku iliingiza fedha za kigeni kiasi cha Dola za Kimarekani Milioni 195.8 ikishika nafasi ya pili baada ya zao la korosho. Licha ya faida kwa taifa, pia, uzalishaji wa tumbaku unawanufaisha wakulima, wanunuzi, viwanda vya kusindika tumbaku, mabenki, wasambazaji wa pembejeo, Halmashauri za wilaya na wadau wengine katika mnyororo wa thamani.

MWISHO


Share:

Halmashauri Ya Jiji La Dodoma Yaanza Kutekeleza Agizo La Rais La Kuwalipa Fidia Wananchi Waliopisha Eneo La Jeshi.

Na.Faustine Gimu Galafoni ,Dodoma
Halmashauri ya jiji la Dodoma imeshaanza kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli alilotoa Nov.25 mwaka huu la kulipa fidia kwa wananchi  1526 wanaopisha eneo la Jeshi la Wananchi Jijini Dodoma.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jana  Nov.30,2019  jijini Dodoma  mkurugenzi wa jiji la Dodoma Godwin Kunambi amesema kiasi kinachotakiwa kulipwa kwa wananchi hao ni Tsh.Bil.3.399  na ukubwa wa eneo zima  ni ekari elfu tano  na eneo linalopaswa kulipwa fidia ni ekari  elfu 3 mia 4 na 31 na kinachotakiwa kwa wanufaika  ni kufungua akaunti za benki huku uhakiki ukiendelea.

Aidha,Bw.Kunambi amesema ofisi ya mkurugenzi  jiji la Dodoma imeshaanza kuwasaidia wananchi kusaidia kufungua akaunti za benki na kuanzia wiki ijayo wananchi wataanza kulipwa fedha zao.

Ikumbukwe kuwa Nov.25,2019 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli wakati akiweka jiwe la Msingi eneo la Jeshi la Ulinzi alitoa agizo kwa  halmashauri ya jiji la Dodoma kuwalipa fidia wananchi  1526 wanaopisha mradi wa eneo la jeshi la Ulinzi.


Share:

Sekta Ya Ardhi yatakiwa Kupewa Kipaumbele Katika Mipango Ya Maendeleo Nchini

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Eng. Stellah Manyanya amezitaka idara mbalimbali za Serikali kuipa kipaumbele sekta ya ardhi katika mipango ya maendeleo inayofanyika nchini.

Eng. Stellah Manyanya ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano mkuu wa sita wa Mwaka wa Wataalaamu wa Mipangomiji ulioanza tarehe 27 hadi 29 Novemba 2019 jijini Dodoma.

Eng. Stellah Manyanya amesema, kumekuwepo na miradi mingi nchini inaanzishwa na Serikali inatumia gharama kubwa katika kuikamilisha matokeo yake imekuwa haitumiki na wakati mwingine inaingiliana na shughuri nyingine za kijamii hali inayopelekea kuzuka kwa migogoro katika jamii.

Akitolea mfano Jengo la Machinga Complex  lililopo Ilala Jijini Dar es Salaam, Eng. Stellah Manyanya amesema kuwa kutokuwepo kwa mipango kina ya muda mrefu na utafiti duni ndio chanzo kikubwa hadi leo hii jengo hilo kushindwa kufikia lengo walilojiwekea la kuwa saidia wafanyabiashara wadogowadogo kuwa na sehemu yao ya kufanyia shughuri zao.


Share:

Elimu Ya Umeme Kwa Wasioona Yaipa Tanesco Taswira Mpya

SHIRIKA la Umeme Nchini TANESCO limeendesha semina maalum inayohusu masuala ya Umeme kwa wanachama wa chama cha wasioona  Tanzania (TLB)  mkoani Morogoro.

Akizungumza wakati wa uzinduzi  wa warsha hiyo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  Loata Ole Sanare amesema kuwa Tanesco  imeonyesha mfano mzuri wa kuigwa kwa kutoa elimu hiyo kwa watu wa kundi  maalum katika jamii.

Alisema pia kupitia hili shirika limetoa taswira kuwa mashirika ya Umma yanafuata muelekeo wa Raisi John Pombe Magufuli ambae ni  Raisi wa wanyonge na kwa kujali wateja wake hata wa Makundi maalum kwa kutoa elimuYa Umeme itakayowasaidia katika maisha yao ya kila  siku.

Mkuu huyo wa Mkoa  amewataka wasioona kutokuwa wanyonge kwakudhani kuwa  Serikali haiwatambui na kusema kuwa Serikali ipo pamoja nao na kuwakaribisha katika ofisi za Mkoa, muda wowote watakapokua na changamoto zozote.

Naye Kaimu meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoa wa Morogoro William Masome amesema Kuwa TANESCO chini ya Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Tito Mwinuka imetambua umuhimu wa watu wenye Ulemavu wa kutoona kupatiwa elimu ya Umeme ili waweze kutambua fursa  zitokanazo na umeme zitakazoweza kuwainua kiuchumi lakin pia kuwafundisha jinsi ya kutumia umeme vizuri (matumizi Bora ya umeme)ili wasilipe gharama kubwa
Kwenye kununua Umeme.

Naye kwa upande wake Mratibu wa idara ya maendeleo, Vijana na Chipkizi toka TLB , Bw.Kiongo Itambu ameishukuru TANESCO kwa kuwapatia elimu hiyo Maalum ambayo itawasaidia hasa katika kujiepusha na matukio ambayo yanaweza kuathiri usalama wao.

Alisema kwani wameshajua athari za kukaa karibu na miundombinu ya umeme  na  kuahidi kushirikiana na TANESCO katika kuwafichua wanaolihujumu Shirika kwa kuiba umeme na kuharibu miundombinu ya Shirika.

Aidha Bw. Kiongo alimuhakikishia Mkuu wa mkoa kuwa wao kama watu wenye ulemavu ni kama watu wengine, ni mara chache kusikika wasioona ikiwa na sifa ya kuliibia shirika la umeme na watakuwa mabalozi wa kuhakikisha Tanesco haiujumiwi ili kukuza kipato chake kwa maendeleo ya Shirika na Taifa kwa ujumla

Mwisho.


Share:

Chama cha Walimu Tanzania Kujenga Kiwanda Cha Mikate Lishe Simiyu

Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kinatarajia kujenga kiwanda cha mikate lishe kupitia kampuni yao inayosimamia Maendeleo ya Walimu ya biashara (TDCL), katika eneo la Ng’hami wilayani Maswa mkoani Simiyu.

Akimkabidhi  Katibu wa Chama cha Walimu Nchini, Mwl. Deus Seif hati ya kiwanja chenye ukubwa wa hekari mbili (2), Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe amesema wilaya imetoa kiwanja hicho bure, ikiwa ni moja ya njia ya kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya viwanda ambapo kumhakikishia upatikanaji wa malighafi ya kiwanda hicho (viazi lishe)

“Tumejipanga kuzalisha viazi lishe vya kutosha vitavyotumika kama malighafi ya kiwanda hiki na tayari wakulima wamepewa mbegu za viazi hivyo, niendelee kuwakaribisha CWT wilayani Maswa, kama kuna uwekezaji mwingine mnahitaji kufanya karibuni, hata kama ni tawi la benki yenu ile ya walimu tunawakaribisha sana,” alisema Dkt. Shekalaghe.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Simiyu amesema kukamilika kwa kiwanda hicho kutasaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa lishe ambalo limekuwa ni changamoto kwa  Mkoa wa Simiyu.

Aidha, Mtaka amesisitiza Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashautri na wataalam wa kilimo wahakikishe mbegu ya viazi lishe inapatikana kwa wingi ili wananchi wanapohitaji waipate

 Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania(CWT) Taifa, Mwl. Deus Seif amesema chama hicho kinaunga mkono sera ya Tanzania ya Viwanda huku akibainisha kuwa ujenzi wa kiwanda hicho utaenda haraka kwa kuwa tayari kampuni ya CWT inayosimamia miradi imeshaanza kulifanyia kazi suala hilo.

Ameongeza kuwa pamoja na kujenga kiwanda cha mikate lishe, chama hicho pia kinatarajia kuchukua uwakala katika Kiwanda cha Chaki cha Maswa ili kusambaza chaki zinazozalishwa wilayani humo katika shule zote nchini.


Share:

Kampeni Ya Elimu Kwa Mlipakodi Kuanza Kesho Dar

Na Veronica Kazimoto, Dar es Salaam
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), inatarajia kuanzisha Kampeni ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi katika Mkoa wa Dar es Salaam itakayodumu kwa siku 13 kuanzia kesho tarehe 2 hadi 14 Desemba, 2019.

Akizungumzia kampeni hiyo leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo amesema kuwa lengo ni kutoa elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kodi pamoja na kusikiliza malalamiko, changamoto na kupokea maoni kutoka kwa wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla.

"Kampeni hii ni mwendelezo wa kampeni ambayo imemalizika katika Mikoa ya Morogoro na Pwani na sasa tunaingia katika Mkoa wa Dar es Salaam tukiwa na lengo la kuwaelimisha walipakodi na wananchi masuala yanayohusu kodi, kupokea maoni yao, kusikiliza changamoto na malalamiko ili tuweze kuyatafutia ufumbuzi", alisema Kayombo.

Kayombo ameongeza kuwa kampeni hiyo itaambatana na huduma ya usajili wa wafanyabiashara wapya wasiokuwa na Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi yaani TIN.

"Pamoja na kutoa elimu ya kodi, kupokea maoni na kusikiliza changamoto za walipakodi pia tutatoa huduma ya usajili wa walipakodi wapya ambapo tutawapatia cheti cha Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi tukiwa na dhumuni la kupanua wigo wa walipakodi hapa nchini", aliongeza Kayombo.

Mkurugenzi Kayombo amebainisha maeneo ambayo yatafikiwa katika kampeni hiyo kuwa ni Ilala, Kinondoni, Temeke na Kariakoo na itafanyika kwa njia ya semina katika vituo vilivyopangwa kwenye maeneo hayo pamoja na kuwatembelea walipakodi katika biashara zao yaani duka kwa duka.

MWISHO.


Share:

WENYEVITI WAPYA WA VIJIJI NA VITONGOJI JIMBO LA KISESA MKOA WA SIMIYU WAAPISHWA, MBUNGE MH. LUHAGA MPINA AWATAKA WAKATAMBUE MAHITAJI YA WANANCHI, KUTANGAZA MAFANIKIO YA RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI

 Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na wajumbe wao kutoka Jimbo la Kisesa wilayani Meatu Mkoa wa Simiyu wakila kiapo cha utii  kwenye hafla iliyofanyika Mwandoya Makao Makuu ya Jimbo la Kisesa.
 Wenyeviti wote wa Vijiji vya Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya kuapishwa.
 Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Ikigijo Kata ya Mwabusalu Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo
 Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Itinje Kata ya Itinje Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo

  Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Lingeka  Kata ya Lingeka Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo
 Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha  Matale Kata ya Tindabuligi Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo
 Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha  Mbugayabahnya Kata ya  Mbugayabahnya Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo

 Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Mwashata  Kata ya  Mwabuma Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo
 Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Ntobo  Kata ya Kisesa  Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo
  Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Nyanza  Kata ya Mwakisandu  Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo
Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Semu  Kata ya Isengwa  Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo

Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha  Ming’ongwa Kata ya Sakasaka  Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili December 1















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger