Friday 29 November 2019

Credit Officer Job Opportunity at The Guardian Limited (TGL)

Credit Officer Job Opportunity at The Guardian Limited (TGL) OVERVIEW The Guardian Limited (TGL), widely acclaimed as the Home of Great Newspapers, is part of the IPP Group of Companies – one of Tanzania’s leading private sector entities with dignified presence in the print media as well as television and radio broadcasting. TGL currently publishes two upmarket daily… Read More »

The post Credit Officer Job Opportunity at The Guardian Limited (TGL) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Waziri Mhagama Ampa Miezi Miwili Mkandarasi Kukamilisha Hatua Ya Kwanza Kiwanda Cha Bidhaa Za Ngozi Cha Karanga.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mgahama, amempa miezi miwili mkandarasi anayejenga Kiwanda cha bidhaa za ngozi cha Karanga, kilichopo mkoani Kilimanjaro, kukamilisha hatua ya kwanza ya  ujenzi wa kiwanda hicho hadi kufikia tarehe 20 Januari mwaka 2020, ili ujenzi  hatua ya pili ya ujenzi wa kiwanda hicho uweze kuanza mara moja kwa ajili ya kuhakikisha kiwanda kinaanza uzalishaji wa bidhaa za ngozi.

Mkandarasi huyo ambaye ni Kikosi cha ujenzi cha Shirika la Uzalishaji la Magereza ameelekezwa kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha ndani ya kipindi hicho kuhakikisha amejenga majengo manne, ikiwa ni jengo la kuzalisha bidhaa za ngozi na soli za viatu, jengo la mitambo ya umeme pamoja na ghala la vifaa vya ngozi.

Waziri Mhagama ametoa maelekezo hayo mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda hicho leo tarehe 29 Novemba, 2019, mkoani Kilimanjaro, ambapo amefafanua kuwa  kiwanda hicho ni muhimu kujengwa kwa haraka sana kwani kitaiwezesha Tanzania  kuufikia uchumi wa viwanda kwa kuwa bidhaa zitakazozalishwa na kiwanda hicho zina soko kubwa ndani na nje ya nchi hususani katika Jumuiya ya maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
 
“Sisi katika Afrika ni matajiri wa mifugo na bidhaa zinazolishwa na mifugo, lakini hapa nchini  hatuna kiwanda tunachoweza kutegemea katika bidhaa za ngozi, hivyo ni muhimu kuharakisha ujenzi wa kiwanda hiki ili tuweze kutengeneza ajira hapa kati ya elfu tatu hadi elfu nne na ukizingatia nguvu kazi ya nchi yetu asilimia 56 ni vijana.Kiwanda hiki kitakuwa muhimu sana kwa ustawi wa nchi” Amesema Mhagama.

Mhe. Mhagama amewataka watekelezaji wa Mradi huo  kuhakikisha wanakuwa na mpango kazi wa kukamilisha kazi hiyo na kuuwasilisha kwake, lakini pia kuwa  na mpango mkakati wa biashara utakao wezesha kusaidia kupatikana na masoko ya bidhaa hizo. Ameongeza kuwa atakuwa na watu wakufuatilia kwa karibu shughuli za ujenzi huo ili kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati. Huku akisisitiza Changamoto zozote za utekelezaji wa Mradi huo zizingatiwe ili pindi ukikamilika zisije anza kuibuliwa na kuweza kukukosesha mradi kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi,Ajira, vijana na Watu wenye Ulemavu), Andrew Massawe, amemuhakikishia Mhe. Waziri Mhagma kuwa, atafuatilia ushughuli za ujenzi wa mradi huo kwa  karibu ili kuhakikisha maelekezo yake yanatekelezwa kwa  kila hatua za ujenzi ili kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa muda uliopangwa.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma, Hosea Kashimba amemhakikishia Mhe.Waziri Mhagama kuwa atahakiksha kuwa ujenzi huo unakuwa na ubora na unakamilika ndani ya muda aliouelekeza ili watanzania waweze kunufaika na  bidhaa za kiwanda hicho lakini pia waweze  kupata ajira za uhakika kutoka katika kiwanda hicho.

Utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Viwanda vya ngozi Karanga unatekelezwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF),na Magereza kupitia wataalamu wake wa ndani na timu ya washauri elekezi wa viwanda TRIDO.

Mradi wa ujenzi wa Kiwanda cha bidhaa za ngozi cha Karanga unatokana na Kampuni ijulikanayo kwa jina la “Karanga leather Industries Co Ltd” iliyoanzishwa mwaka 2017  kwa lengo la kutekeleza mradi wa viwanda vya bidhaa za ngozi katika eneo la gereza la Karanga , kampuni hiyo iliingia ubia kati  ya uliokuwa mfuko wa Pensheni PPF ambapo kwa sasa majukumu yake yamechukuliwa na PSSSF pamoja na Jeshi la Magereza kupitia Shirika la Uzalishaji. Malengo ya ubia huo nikuongeza wigowa uzalishaji wa bidhaa za ngozi na kuongeza thamani ya ngozi nchini.

MWISHO.


Share:

Waziri Mkuu: Madhehebu Ya Dini Yameisaidia Serikali Kupata Viongozi Wazuri

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema madhehebu ya dini yametoa mchango mkubwa katika kuwapata viongozi wa Serikali wanaofuata maadili mema na miiko ya uongozi.

Akizungumza  wakati alipofungua Msikiti wa Haq – Kionga ulioko Magomeni, jijini Dar es Salaam leo mchana (Ijumaa, Novemba 29, 2019), Mheshimiwa Majaliwa amesema imedhihirika kwamba waumini wazuri wa dini mbalimbali wamebainika kuwa ni viongozi wazuri na waadilifu ndani ya Serikali.

Amewasihi viongozi wa dini waendelee kuwafundisha maadili mema waumini wao ili Taifa liendelee kuwa na raia wema ambao baadhi yao ndiyo watakakuwa viongozi katika ngazi mbalimbali hapo baadaye.

“Nyumba za ibada ndiyo mahali sahihi panapojengwa maadili mema kwa watu wa rika zote, hivyo nawaomba Watanzania wawe waumini wazuri wa dini zao kwani kwa kufanya hivyo watakuwa pia ni raia wema,” amesema Mheshimiwa Majaliwa.

Amesema wazazi na walezi wanawajibika kuwarithisha watoto wao imani za dini vizuri kwani anaamini kwa kufanya hivyo watoto watajengewa misingi mizuri ya imani ya dini na maadili mema na watakapokuwa watu wazima watakuwa ni raia wema.

Mheshimiwa Majaliwa aliwasilisha mchango wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli wa sh. milioni 10 na yeye pia alichangia sh. milioni tano ili zisaidie katika awamu ya pili ujenzi wa msikiti huo.

Naye Sheikh Masoud Jongo ambaye alimwakilisha Sheikh Mkuu wa Tanzania katika ufunguzi wa msikiti huo, alisema uhuru mkubwa wa kuabudu uliopo nchini ndiyo sababu kubwa inayoifanya Tanzania iwe ni nchi ya amani na utulivu.

Sheikh Jongo amewaomba Watanzania wautumie vizuri uhuru mkubwa wa kuabudu uliopo nchini kwani ni nchi chache duniani zinazotoa uhuru mkubwa wa kuabudu kwa wananchi wake kama ilivyo hapa Tanzania.

Baadhi ya viongozi walioshiriki katika ufunguzi wa msikiti huo ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, mbunge wa Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia na mbunge wa Kibaha Vijijini, Abuu Juma.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, NOVEMBA 29, 2019.


Share:

Picha : ABIRIA WANUSURIKA KIFO HIACE IKITEKETEA KWA MOTO STENDI YA MABASI SOKO KUU MJINI SHINYANGA


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Abiria ambao idadi yao haijajulikana wamenusurika kuungua baada ya gari aina ya Hiace yenye namba za usajili T998 AAP linalofanya safari zake Shinyanga kwenda Maswa kuteketea kwa moto.

Tukio hilo limetokeo leo Ijumaa Novemba 29,2019 majira ya saa nane na nusu wakati abiria wakiwa wamepanda kwenye Hiace hiyo wakijiandaa kuanza safari kuelekea Maswa mkoani Simiyu.

Dereva wa Hiace hiyo aliyejulikana kwa jina Basu Gereja amesema chanzo ni kupasuka kwa Betri na kusababisha gari hilo kuwaka moto.

"Chanzo ni Betri kulipuka,tumefanya utaratibu wa kuwatoa abiria kwenye gari kisha kupiga simu Zimamoto kwa ajili ya msaada ambao wamefika na kusaidia kuzima moto huu,gari ilikuwa inatoka Shinyanga kwenda Maswa",amesema Basu.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wameiambia Malunde1 blog kuwa dereva alikuwa amewasha gari akijiandaa na safari ndipo ghafla walipoona gari linawaka moto ndipo utaratibu wa kuwatoa abiria ukaanza kufanyika huku abiria wengine wakitokea madirishani kwa sababu mlango uligoma kufunguka.

Mratibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Shinyanga Edward Lukuba (Afisa Oparesheni Mkoa wa Shinyanga) amesema wamepata taarifa za kuteketea gari kwa kuchelewa na kukuta gari hilo linaungua na kufanikiwa kuzima moto huo huku akiwasisitiza wananchi kujitahidi kuwa wanatoa taarifa mapema pindi majanga yanapotokea.
Maafisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakiendelea kuzima moto uliokuwa unateketeza Hiace katika Stendi ya Mabasi Soko Kuu Mjini Shinyanga - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mratibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Shinyanga Edward Lukuba (Afisa Oparesheni Mkoa wa Shinyanga) akiwa eneo la tukio


Share:

Arsenal yamfuta kazi Kocha Mkuu Unai Emery

UNAI Emery aliyekuwa kocha mkuu wa Arsenal amepigwa chini ndani ya kikosi hicho baada ya kudumu nacho kwa muda wa miezi 18 akiwa kazini.

Arsenal imefikia uamuzi huo baada ya jana kupigwa na Frankfurt bao 2-1, kwa mchezo wa saba mfululizo bila ushindi (sare 5 na  vipigo 2).
 

Arsenal imemtangaza Freddie Ljungberg kuwa kocha wa muda na kurithi mikoba ya Emery.


Share:

Viwanja Bei nafuu: Bunju na Mapinga (Kimele)

Kwa Mapinga vipo viwanja vya 20/25 bei milion 5, 20/30 bei milion 6, 20/40 bei milion 8, nusu eka milion 25 na eka milion 50

Kwa Bunju vipo viwanja vya sqm 1000 kwa milion 30.

Ukipata ujumbe huu mjulishe ndugu/jamaa/rafiki, na biashara hii haina dalali/udalali.

Mpigie mhusika: 0758603077


Share:

Harmonize Kumkabili Ali Kiba Disemba 8

Wasanii wa Tanzania, Alikiba na Harmonize watakutana katika jukwaa moja la tamasha la Fiesta litakalofanyika katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam Desemba 8, 2019.

Waandaaji wa tamasha hilo Jumanne Novemba 26, 2019 wametangaza baadhi ya wasanii nchini watakaoshiriki Fiesta, wakiwemo wawili hao.

Kukutana jukwaani kwa wasanii hao kunasubiriwa kwa hamu kutokana na Harmonize kuachana na lebo ya Wasafi, hivyo mashabiki wengi kutaka kumshuhudia akitoa burudani nje ya lebo hiyo.

Alhamisi ya Oktoba 24, 2019, Harmonize alieleza jinsi alivyouza nyumba zake tatu na baadhi ya mali ili kuilipa lebo ya Wasafi Sh500 milioni kwa ajili ya kupata hakimiliki ya kutumia nyimbo zake na jina.

Alibainisha kuwa mkataba alioingia na lebo ya Wasafi inayomilikiwa na msanii Diamond Platnumz ilikuwa na kipengele cha kulipa kiasi hicho cha fedha ikiwa atavunja mkataba ili aweze kuendelea kutumia nyimbo pamoja na jina lake la kisanii.

Wakati akiwa Wasafi, Harmonize hakuwahi kushiriki tamasha la Fiesta tofauti na Ali Kiba aliyewahi kushiriki mara kadhaa.


Share:

Diamond Platnumz Ambwaga Ali Kiba

Shirika la Utangazaji CNN limetaja wanamuziki bora 10 barani Afrika, akiwemo msanii wa Tanzania, Diamond Platnumz.

Orodha hiyo inamfanya Diamond kuwa msanii pekee kutoka Afrika Mashariki kuingia katika orodha hiyo ya wasanii wanaofanya vizuri katika muziki.

Wengine waliotajwa ni Burna Boy wa Nigeria ambaye pia ameteuliwa katika tuzo za Grammy zitakazofanyika Januari 2020 pamoja na Yemi Alade, Tiwa Savage na Wizkid wote wa nchi hiyo.

Mtunzi, mwanaharakati na mshindi wa tuzo ya Grammy kutoka nchini Benin, Angelique Kidjo pia amejumuishwa katika orodha hiyo.

Pia wapo waimbaji wa Afrika Kusini, Sho Madjozi, Busiswa Gqulu ambaye pia ni mwandishi wa nyimbo na mshairi, rapa wa Zambia, Mwila Musonda maarufu Slapdee.

Diamond ambaye ameingia katika tasnia ya muziki miaka 10 iliyopita amekuwa na mafanikio makubwa.


Share:

Mfumo wa vifurushi vya Bima ya Afya Wazinduliwa Rasmi...Elimu Kutolewa Nyumba Kwa Nyumba

Mfumo wa vifurushi vya Bima ya Afya umezinduliwa rasmi jana jijini Dar es Salaam, huku Mwenyekiti wa Bodi ya Mfumo wa Bima ya Taifa (NHIF) Anna Makinda, akisema watu watafuatwa mpaka majumbani kupewa elimu ili wajiunge.

Makinda ambaye ni Spika Mstaafu wa Bunge, aliwataka pia watumishi wa vituo vya afya na hospitali, kuwa na lugha nzuri kwa watu wanaotumia bima hizo.

Alisema kuna baadhi ya wahudumu wa afya wamekuwa hawatoi kipaumbelea kwa watu wanaotumia bima ya afya na kuwataka waache tabia hizo.

“Utoaji wa huduma za afya sasa unaenda kwa ushindani, hospitali yenye wahudumu wa afya wanaotoa huduma nzuri ndio watakaopata fedha nyingi, mtu akiumwa atatamani kwenda kwenye hospitali inayotoa huduma nzuri.

“Wahuduma waendelee kuwa na bidii, kuna baadhi ya wahudumu wa afya wamekuwa na lugha chafu kwa wagonjwa hasa wanaotumia bima, hawa nawaambia waache tabia hiyo wagonjwa, wanahitaji lugha zenye faraja.

“Uzinduzi huu unaenda na ile azima ya Tanzania ya viwanda, utakuwa na msaada katika kuleta  afya njema kwajamii kwani bila afya njema hakuna uchumi wa viwanda, hivyo ni msaada mkubwa kwa wananchi wote, watumishi watapita majumbani kutoa elimu ya vifurushi hivi ili watu wengi wajiunge,”alieleza Makinda.

Kutokana na baadhi ya watu kuamini kuwa kukata bima ni kupoteza fedha, Makinda aliwaomba Watanzania waweke kipaumbele katika kupata bima ya afya kwa hiyari ili kuepuka gharama kubwa wanapougua.


Share:

Tanzania Communication Officer at Frankfurt zoological Society – Tanzania

Job Summary The Frankfurt Zoological Society (FZS) is an international conservation NGO based in Germany. FZS is active in biodiversity-rich areas on four continents. The Africa Program includes projects in five focal countries: Ethiopia, Tanzania, Zambia, Zimbabwe and the DR Congo. It is coordinated from the Africa Regional Office (ARO) based in Arusha, Tanzania. FZS seeks to improve… Read More »

The post Tanzania Communication Officer at Frankfurt zoological Society – Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Marketing Manager Tanzania at SPENN TANZANIA LTD

Job Summary We at SPENN are looking for a Marketing Manager with a rock-solid vision to join our team! As a Marketing Manager you will be overseeing the marketing activities in Tanzania and implement our global strategy to the Tanzanian market.   You will be a part of the department located in Dar es Salam. You may also… Read More »

The post Marketing Manager Tanzania at SPENN TANZANIA LTD appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Humphrey Polepole Ampiga KIJEMBE Sumaye Baada ya Kupigwa Chini Uchaguzi CHADEMA

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole, amempiga  kijembe  Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye baada ya kubwagwa kwenye Uchaguzi wa Kikanda ndani ya CHADEMA

“Nimesikia Mzee Sumaye hata Uenyekiti sijui wa “Kitongoji” wamembwaga huko Pwani, alipokuwa CCM @ccm_tanzania tulimpa kwa upendeleo Uwaziri Mkuu Miaka 10. Mzee, nadhani muda umefika huko hakuna watu, mimi na wewe tunajua imetosha. Mwenzio amepumzika na muda wa kulea wajukuu anao!” ameandika ujumbe huo katika akaunti yake ya Twitter.
 
Uchaguzi huo ulifanyija jana jioni Kibaha Pwani wa kumpata mwenyekiti wa Kanda ya pwani

Kwa nafasi ya Mwenyekiti, Mgombea alikuwa Mzee Sumaye peke yake ndipo zikapigwa kura za ndio au hapana

Matokeo ya kura za ndio kwa Mzee Sumaye ni 28, na kura za Hapana ni 48 .Hivyo, nafasi ya Mwenyekiti bado iko wazi.


Share:

Sales & Marketing Officer at Europlast LTD

Job Summary Europlast LTD is one of top,well-established Manufacturing company. We are seeking to higher highly distinguished and innovative Sales & Marketing Officers. Minimum Qualification: Diploma Experience Level: Mid level Experience Length: 3 years Job Description Attributes Fluent in English and Kiswahili proficiency. Must have a Skype Account(necessary for interviews) Education & Qualification Diploma or Bachelor Degree in Sales, Marketing or Business Administration… Read More »

The post Sales & Marketing Officer at Europlast LTD appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Country Transformation Manager Job at Plan International

Country Transformation Manager Job Opportunity at Plan International, Career Opportunities: Country Transformation Manager (36994) Req ID 36994 – Posted 18/11/2019 – Country (2) – Programme Strategy Job Description Print Preview The Organisation Plan International is an independent development and humanitarian organisation that advances children’s rights and equality for girls. We believe in the power and potential of every… Read More »

The post Country Transformation Manager Job at Plan International appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Jumia Yafunga Biashara zake Tanzania

Mtandao wa biashara Barani Afrika umefunga biashara yake nchini Tanzani ikiwa ni siku chache tu baada ya kusitisha shughuli zake nchini Cameroon

Kulingana na taarifa iliyopatikana imeeleza kuwa Jumia imefunga shughuli zake nchini Tanzania ili kuwekeza rasilimali katika masoko mengine

Taarifa hiyo inasomeka:
"Kwa kuzingatia tathmini yetu ya kuelekea mafanikio, tumefanya maamuzi magumu ya kusitisha shughuli zetu  Tanzania kuanzia Novemba 27, 2019.

"Tanzania kuna fursa kubwa lakini tumeona ni vyema kutumia rasilimali zetu katika masoko mengine, uamuzi huo sio rahisi lakini unatusaidia kuweka mkazo na rasilimali zetu mahali ambapo tunaweza  kuleta matunda na kusaidia ustawi wa Jumia"

Aidha, imesema itaendelea kutumia mtandao wake wa ''Jumia Deals'' katika kuendelea kuwasaidia maelfu ya wafanyabiashara ambao wanautumia kukutana na wanunuzi

Novemba 18, 2019 kampuni hiyo ambayo makao makuu yake yapo nchini Nigeria ilifunga biashara zake  nchini Cameroon kwa sababu kama hizo.


Share:

Geographic Information Systems Expert & Health Management Information Systems Specialist, Jobs at ICAP Tanzania

Geographic Information Systems Expert & Health Management Information Systems Specialist, Jobs Opportunities at ICAP Tanzania, Deadline 15 December 2019 Health Management Information Systems (HMIS) Specialist, Tanzania Job no: 492297 Work type: Regular Full-Time Location: Tanzania – Dar es Salam, Tanzania – Kagera, Tanzania – Kigoma, Tanzania – Mara, Tanzania – Mwanza, Tanzania – Pwani, Tanzania – Tanga Categories:… Read More »

The post Geographic Information Systems Expert & Health Management Information Systems Specialist, Jobs at ICAP Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Product Development and Evaluation Specialist at One Acre Fund in Iringa, Tanzania

Tanzania – Product Development and Evaluation Specialist at One Acre Fund in Iringa, Tanzania Position: Tanzania Product Development and Evaluation Specialist Seeking an exceptional qualitative research professional with 3-5 years of experience who can drive actionable trial and scale recommendations for trial products About One Acre Fund Founded in 2006, One Acre Fund supplies smallholder farmers with the… Read More »

The post Product Development and Evaluation Specialist at One Acre Fund in Iringa, Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger