Thursday 31 October 2019

MAVUNDE:SERIKALI KUENDELEA KULIWEZESHA KWA UJUZI KUNDI LA VIJANA

Share:

Wednesday 30 October 2019

Tahadhari Ya Mvua Kubwa Kanda Ya Ziwa

Mamlaka  ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imesema mikoa ya Kanda ya Ziwa itakuwa na mvua nyingi na kuwataka wananchi kuchukua tahadhari.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TMA, mikoa itakayokumbwa na mvua hizo ni Geita, Kagera, Mara na Magharibi mwa Simiyu.

Aidha, kiwango cha athari kinachoweza kutokea ni baadhi ya makazi kuzungukwa na maji, ucheleweshaji wa usafiri, kusimama kwa muda kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi na kijamii.

Wiki kadhaa zilizopita TMA ilitoa tahadhari ya uwapo wa mvua kwenye mikoa mbalimbali nchini ambayo itaanza Novemba hadi Aprili mwakani.

Aidha, siku chache baadaye Mamlaka hiyo ilitoa utabiri wa mvua kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Tanga.

Tangu kuanza kwa mvua hizo, watu 25 wamepoteza maisha katika mikoa ya Morogoro na Tanga, huku madaraja manne yakisombwa na maji na kukatika kwa mawasiliano kwa mikoa ya Kanda ya Kaskazini.



Share:

Makonda awakabidhi Suma JKT ujenzi hospitali Ubungo

Kitengo cha uzalishaji mali cha Jeshi la kujenga Taifa (suma JKT), kimepewa kazi ya kujenga hospitali ya wilaya ya Ubungo.

Kazi hiyo wamepewa na jana Oktoba 29, 2019 na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda ambaye amesema kuwa ujenzi huo unatakiwa kamilika kwa miezi mitatu.

Amebainisha hayo jana alipotembelea eneo itakapojengwa hospitali hiyo Kimara Baruti, ambapo aliambatana na viongozi wengine na kuangalia jinsi maandalizi mbalimbali yalivyoanza kufanyika.

Makonda ametoa shukurani zake kwa mara nyingine tena kwa Rais Dkt. John Magufuli kwa kukubali ombi lake la sh 1.5 bilioni za ujenzi wa hospitali hiyo.

” Wilaya hii ni mpya inahitaji viongozi shupavu wa kuwaletea maendeleo, ni kazi ya viongozi wanaochaguliwa na wananchi.

“Kwa bahati mbaya Ubungo ilipata viongozi wanaojali matumbo yao tu. Hata leo hapa hawapo ila kesho watakuja na maneno matamu ili muwape kura” Alisema Mkuu huyo wa mkoa.

Mkurugenzi mtendaji wa Suma JKT, Kanali Rajabu Mabele amesema kuwa watahakikisha ujenzi huo unakamilika kwa muda uliopangwa.


Share:

Finance Business Partner – Retail Job Opportunity at CRDB Bank

Finance Business Partner – Retail CRDB Bank PLC is looking for suitable person to fill a vacant position of ​Finance Business Partner – Retail​ in the Department of Finance at the Head Office, in Dar es Salaam​. Job Purpose: To be a catalyst that will influence decision making to Retail Business and the bank as a whole. To… Read More »

The post Finance Business Partner – Retail Job Opportunity at CRDB Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Wanaume Wanaonyonya Maziwa Ya Wake Zao Wapewa Onyo

Kaimu Mkurugenzi wa Lishe katika Wizara ya Afya, Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Grace Moshi ametoa onyo kali kwa Wanaume wanaoendeleza tabia ya kupenda kunyonya maziwa ya Wake zao wanaonyonyesha na kuwataka kuacha mara moja kwani kufanya hivyo wanawapunja watoto.

Moshi ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati anazungumza na waandishi wa habari katika semina iliyoandaliwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto ikiwa  ni maandalizi ya mkutano wa mawaziri wa afya wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika(SADC) ambapo amesema  mtoto ili awe na afya njema anahitajika kunyonya maziwa ya mama kwa miezi sita bila kitu chochote.

Amesema kumekuwa na kasumba kwa baadhi ya wanaume kupendelea kunyonya maziwa ya Mama huku wengine wakiwapa masharti kwamba wanyonyeshe Mtoto ziwa moja na lingine wabakishiwe wao.

Amesema Wanaume lazima watambue kuwa maziwa ya Mama ni tiba na kinga kwa Mtoto huku akishangazwa na tabia ya Wanaume wanaopenda kuyanyonya akihoji maana yao hasa ni nini.

Kuhusu lishe nchini ,Moshi amesema kama nchini imepiga hatua kubwa katika eneo la lishe ukilinganisha na huko nyuma.

Ameongeza malengo yaliyowekwa duniani ni kwamba suala la lishe lisiwe zaidi ya asilimia 30 ambapo kwa Tanzania iko katika asilimia 32 ambayo ni juu ya lengo ambalo limewekwa katika eneo hilo la lishe.


Hata hivyo amesema kwa Tanzania katika eneo la lishe ilikuwa na changamoto lakini kupitia mikakati ya Wizara imefanikiwa kupunguza ukubwa wa tatizo la lishe nchini.

Hata hivyo amesema kuna sababu nyingi ambazo zinasababisha ukosefu wa lishe ambao unafanya kuwepo na udumavu na kwamba  kuna mikakati mbalimbali ya kutoa elimu ya kuhamasisha jamii kuzingatia suala la lishe.


Share:

Jobs Opportunities at Save the Children (2 Positions)

2 Jobs Opportunities at Save the Children Deadline 8 November 2019 TEAM/PROGRAM: Programme Operations- Tuwekeze Pamoja LOCATION: Mbozi, Songwe GRADE: TBC POST TYPE: National Child Safeguarding: Level 3 – the responsibilities of the post may require the post holder to have regular contact with or access to children or young people ROLE PURPOSE: The Tuwekeze Pamoja Programme Officer… Read More »

The post Jobs Opportunities at Save the Children (2 Positions) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Education Specialist & Project Coordinator- Job Opportunities at Save the Children Tanzania

Education Specialist &; Project Coordinator- Job Opportunities at Save the Children Tanzania TITLE: Project Coordinator TEAM/PROGRAMME: Programme Operations LOCATION: Full time based in Dodoma Region, Tanzania GRADE: Grade 3 CONTRACT LENGTH: 1 year, renewable CHILD SAFEGUARDING: Level 3: √ the post holder will have contact with children and/or young people either frequently (e.g. once a week or more)… Read More »

The post Education Specialist &; Project Coordinator- Job Opportunities at Save the Children Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

18 Jobs Opportunity at Tanzania Communications Regulatory Authority TCRA

OVERVIEW: The Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) is a quasi-independent Government body responsible for regulating the Communications in Tanzania. It was established under the Tanzania Communications Regulatory Act No. 12 of 2003 to regulate the electronic communications, Postal services and Broadcasting (for Mainland Tanzania only) in the United Republic of Tanzania. The Authority became operational on 1st November… Read More »

The post 18 Jobs Opportunity at Tanzania Communications Regulatory Authority TCRA appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Rais Mstaafu wa Kenya Daniel Arap Moi Alazwa Tena Hospitali Wiki Mbili Baada Ya Kutoka

Rais  wa Zamani wa Kenya, Arap Moi  amelazwa katika Chumba cha Uangalizi Maalum (ICU) katika Hospitali ya Nairobi na madaktari wanasema ni kutokana na maumivu ya kifua na shida katika kupumua

Wiki mbili zilizopita, aliruhusiwa kutoka hospitalini hapo alipokuwa amelazwa huku Katibu wa Chama cha KANU, Nick Salat akisema Moi alienda kwa uchunguzi wa kawaida wa kiafya

Nick Salat amesema, "Alikuwa hospitalini hapo siku kadhaa nyuma na amerudi tu kwa ombi la madaktari wake. Yeye ni mzee na uchunguzi wa mara kwa mara kwa watu wa rika lake ni kawaida tu."

Mwaka jana, Moi aliondoka kwenda Tel Aviv, Israeli kwa uchunguzi wa matibabu akisindikizwa na mwanawe Gideon na Daktari wake, Dkt. David Silverstein


Share:

Marketing And Sales Representative Job Opportunity at Tanyi Tanzania Investment Ltd

ABOUT US Tanyi Tanzania Investment Ltd was incorporated under the companies Act 2002 section 15 of the United Republic of Tanzania on 5 th day of July the year 2017 as a Private limited by Share Company. The company is now engaged in a variety of agricultural and trade activities. In near future, TANYI has the plan to… Read More »

The post Marketing And Sales Representative Job Opportunity at Tanyi Tanzania Investment Ltd appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Administrator :M-PESA Agents Job Opportunity at Vodacom Tanzania

Administrator: M-PESA Agents Dar Es Salaam JOB PURPOSE The M-PESA Agent Administrator will be responsible to assist the M-PESA support Managers deliver against M-PESA revenue targets through effective management of the M-PESA agent network. KEY ACCOUNTABILITIES 1.Daily M-PESA agent network support including agent contract processing, stock management, float monitoring, fraud activity monitoring, PoS allocation, agent communications and training… Read More »

The post Administrator :M-PESA Agents Job Opportunity at Vodacom Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS) Vyapewa ONYO

Na Mwandishi wetu, Mihambwe
Vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS) vimepewa onyo viwe makini zaidi kiutendaji kazi msimu huu  wa Korosho wa mwaka 2019/2020 ili kutokurudia makosa yaliyojitokeza msimu uliopita.

Hayo yamebainishwa na Afisa Tarafa Mihambwe Ndugu Emmanuel Shilatu wakati alipotembelea maghala ya AMCOS yaliyopo Tarafa ya Mihambwe ambapo amesisitiza Serikali kuwa bega kwa bega nao ili tija ionekane pande zote.

"Nimepita kote kuwapongeza kwa kazi nzuri wanazofanya lakini pia nimepita ili kujiridhisha na utaratibu unaotumika wa uuzaji wa Korosho kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani. Serikali inawasisitiza wafanye kazi kiuweledi, kusimamia haki ya Mkulima na kuhakikisha wanakusanya Korosho safi na zilizo na viwango zitakazovutia Wafanyabiashara sokoni. Lengo kuu la Serikali ni kuhakikisha iwe Mkulima ama Amcos wananufaika na jasho lao." Alisisitiza Gavana Shilatu.

Maghala mbalimbali ya Amcos yamefunguliwa tayari kwa msimu 2019/2020 ambapo Wakulima wanapeleka Korosho zao ziuzwe kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.

PICHANI: Afisa Tarafa Mihambwe Emmanuel Shilatu akipata maelezo na kujiridhisha juu ya utaratibu unaotumika kwenye ukusanyaji wa Korosho kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani kwenye msimu wa mwaka 2019/2020 alipotembelea maghala mbalimbali ya vyama vya msingi vilivyopo ndani ya Tarafa ya Mihambwe.


Share:

Wananchi waliovamia Mpaka wa Tanzania na Zambia Watii Agizo la Rais la Kubomoa

Zaidi ya asilimia 80 ya Wananchi waliovamia Mpaka wa Tanzania na Zambia eneo la Tunduma wametii agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na kubomoa majengo na vibanda vyao ili kuacha Mpaka wazi.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela ameyasema hayo mara baada ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa agizo la Rais na kukuta wananchi wametii na wamebomoa.

“Ninawapongeza wananchi wa Tunduma kwakuwa wameitikia agizo la Rais na utekelezaji unakwenda vizuri sana, nyumba na vibanda vingi vimebomolewa na watu wanahamisha bidhaa na vifaa ambavyo watavitumia wakienda sehemu nyingine, hivyo ninawapongeza sana kwa Mwitikio mzuri.”, amesema Brig. Jen. Mwangela.

Ameongeza kuwa kutokana na kuridhishwa na kasi ya kubomoa ameamua kuwaongezea siku tatu ambazo zitatumika kumalizia kuhamisha bidhaa na vifaa kutoka katika eneo la mpaka na baada ya hapo chochote kitakachobaki hapo kitabomolewa na serikali.

Brig. Jen. Mwangela amesema wananchi waliobaki wanapaswa kuondoka na kuacha Mpaka wazi kwakuwa vyombo vya Ulinzi na Usalama kwenye mipaka waweze kutekeleza majukumu yao bila bila kukwamishwa na kituo pia hakutaruhusiwa shughuli za biashara katika eneo la Mpaka.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe George Kyando amesema Jeshi la Polisi limerahisishiwa namna ya kupambana na uhalifu na kuzuia Magendo kutokana na kushafishwa eneo la mpaka.

Kyando amesema anampongeza Rais Magufuli kwa amri ya kusafisha mpaka huo kwani hali ya amani itazidi kuimarika katika eneo hilo na pia ameshuhudia zoezi la kubomoa likifanyika kwa amani.

Afisa Uhamiaji Mkoa wa Songwe Philon Kyetema amesema kabla ya usafishaji wa Mpaka, zoezi la kupambana na wahamiaji haramu lilikuwa gumu kwakuwa walikuwa wanaweza kuingia na kutoka nchi jirani kwa urahisi kupitia vichochoro.

Amesema Wananchi wa Tunduma wategemee hali kuimarika Zaidi kwakuwa sasa wataweza kufanya ukaguzi wakati wote na kwa kutumia njia mbalimbali kama magari pikipiki na hata kwa miguu kwakuwa wamerahisishiwa mazingira ya kufanyia kazi.


Share:

Mwenyekiti Tume Ya Madini Afanya Ziara Dodoma

Na Greyson Mwase, Dodoma
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amefanya ziara Wilayani Dodoma Mjini lengo likiwa ni kukagua shughuli za uchimbaji wa madini  ya ujenzi pamoja na kutatua kero mbalimbali.

Katika ziara yake Profesa Kikula aliambatana pamoja na Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Dodoma, Jonas Mwano na maafisa kutoka Makao Makuu ya Tume ya Madini.

Mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Patrobass Katambi na kupokelewa na Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Michael Maganga, Profesa Kikula alianza ziara yake kwa kutembelea  kituo cha ukaguzi wa madini ujenzi cha Nala kilichopo nje ya jiji la Dodoma na kutembelea baadhi ya machimbo ya mchanga.

Akiwa katika machimbo ya mchanga yanayomilikiwa na kampuni ya Tripple I General Supply Limited yaliyopo katika eneo la Mbalawala, Wilayani Dodoma Mjini mara baada ya kupokea taarifa ya uendeshaji wa shughuli zake, Profesa Kikula aliitaka kampuni hiyo kuhakikisha inaandaa mkataba na kusaini kati yake na wanakijiji wanaozunguka kampuni hiyo kwa ajili ya utoaji wa huduma za jamii (corporate social responsibility) na kuepuka migongano.

“Ni vyema kampuni ikahakikisha kunakuwepo na mkataba au muhtasari unaotambulika kisheria kwa ajili ya makubaliano ya maeneo ambayo kampuni itasaidia kijiji katika kipindi fulani kulingana na vipaumbele vya wananchi,” alisema Profesa Kikula.

Profesa  Kikula alisisitiza kuwa, ni vyema wananchi wakanufaika na rasilimali za madini  kwa kupata huduma za jamii kutoka kwa wawekezaji ikiwa ni pamoja na shule, vituo vya afya, miundombinu, maji na kuendelea kusema kuwa kampuni inatakiwa kuwashirikisha wananchi kwa kuwapa fursa ya kutoa huduma kwenye kampuni kama vile vyakula, ajira.

Awali akitoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula, Mkurugenzi wa Kampuni ya Tripple I General Supply Limited,  Maglan Kipuyo alimpongeza Mwenyekiti kwa ziara yake na kusisitiza kuwa kupitia ziara zake, kero mbalimbali zimekuwa zikitatuliwa pamoja na kupewa elimu bora ya namna ya kuchimba madini ya ujenzi kwa kufuata Sheria ya Madini na kanuni zake.

Akielezea mafanikio ya kampuni yake, Kipuyo alisema tangu kuanzishwa kwa kampuni mapema mwaka huu kampuni imefanikiwa kutoa ajira zaidi ya 200, ununuzi wa mabati kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya kijiji cha Mbalawala na kuboresha miundombinu ya barabara.

Alitaja mafanikio mengine kuwa ni pamoja na malipo ya  wastani wa shilingi milioni 15 kama mrabaha kwa Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Dodoma kwa kila mwezi na kuanza kwa mchakato wa ujenzi wa kisima cha maji kitakachowanufaisha wanakijiji wa Mbalawala.

Aidha, Kipuyo aliongeza kuwa mafanikio mengine ni pamoja na  kuwezesha wenye viwanda vidogo vya kufyatulia matofali mkoani Dodoma kupata mchanga.

Katika hatua nyingine Profesa Kikula alimtaka Afisa Madini wa Mkoa wa Dodoma, Jonas Mwano kuendelea kutoa elimu kwa wachimbaji wa madini ya ujenzi kuhusu umuhimu wa kutoa huduma kwa jamii (corporate social responsibility) kwa wananchi wanaozunguka migodi yao kama Sheria ya Madini na kanuni zake inavyofafanua.

Profesa Kikula pia alitembelea machimbo ya mchanga yanayomilikiwa na  Wema Msuya yaliyopo katika eneo la Mundemu Wilayani Dodoma Mjini na kusisitiza umuhimu wa wachimbaji wa madini ya mchanga kuchimba kwa kufuata Sheria ya Madini na kanuni zake pamoja kuzingatia suala la usalama na utunzaji wa mazingira.

“Mbali na kuchimba mchanga na kulipa mapato Serikalini ni vyema mkahakikisha suala la usalama kwenye shughuli zenu linazingatiwa na kuepusha ajali zinazoweza kujitokeza,”alisema Profesa Kikula.

Naye Meneja wa machimbo hayo, Richard Tairo  mbali na kumpongeza Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula kwa kufanya ziara na kutatua changamoto mbalimbali mara moja alimhakikishia ushirikiano kati ya wachimbaji wa madini ujenzi na Serikali ili Sekta ya Madini  iwe na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi.

Wakati huo huo Profesa Kikula alitembelea viwanda vya kufyatulia matofali vilivyopo katika maeneo ya Vyeyula na Mlimwa C Wilayani Dodoma Mjini ili kujionea namna shughuli zinavyoendeshwa pamoja na ulipaji wa kodi Serikalini.

Profesa Kikula aliitaka Ofisi ya Afisa Madini wa Mkoa wa Dodoma kusimamia kwa karibu zaidi na kuwa wabunifu kwenye zoezi la ukusanyaji wa kodi mbalimbali ili  Serikali iweze kupata mapato yake stahiki.


Share:

Taarifa Kwa Umma: Usitumie Progaramu Za Simu,Whatsap Zilizoghushiwa Kuwa Za NIDA




Share:

Dr Gwajima: Tusimhujumu Rais, Komesheni Ubadhirifu wa Dawa

Na Atley Kuni- TAMISEMI.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dkt. Dorothy Gwajima, amewataka Wafamasia wa Mikoa kote nchini kupambana na kukomesha watu wanaofanya ubadhilifu wa dawa zinazotolewa na serikali kwenda kwenye sehemu za kutolea huduma za afya sambamba na kutafsiri falsafa ya hapa kazi tu kwa vitendo.

Akizungumza katika kikao kazi cha wataalam hao kinachofanyika mjini Dodoma, alisema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametekeleza vema ilani ya Chama cha Mapinduzi kwakuijali na kuipa kipaumbele sekta ya afya na ndio maana katika mwaka wa fedha 2019/20 serikali imepitisha bajeti ya Shilingi bilioni 57.4 ambapo katika mgawanyo eneo la dawa ni miongoni mwa vipaumbele vitatu vilivyo pewa umuhimu.

“Sasa tusimhujumu Mhe. Rais ambaye ameshafanya kazi kubwa na sisi tuliomo ndani ambao tumewekwa kusimamia tunaujuzi na utaalam sehemu ambayo yeye hawezi kuingia, watu wanaiba dawa tunawaangalia, wanaiba vitendanishi tunawaangalia, tutakuwa hatutimizi wajibu wetu kama matazamia yake naya wanachi yanavyotaka” alisema Gwajima.

Gwajima amewataka Wafamasia hao kutumia mfumo wa Ugavi wa dawa wa (elmis) ambao kimsingi taarifa zote za dawa zinaingizwa na kutumika kama muhtadha wa kuombea dawa kwa kila robo. Alisema mfamasia wa Mkoa atakuwa na wajibu wa kuhalalisha maombi ya dawa kwenda MSD kila mara, huku akiitaja mikoa ya kuanzia katika zoezi hilo ni pamoja na Singida, Dodoma, Manyara, Kagera na Geita.

“Tunataka kufanyika kwa Medicine Audit kila robo na taarifa yake kwa kila mkoa iwasilishwe OR-TAMISEMI” alisema Gwajima na kuongeza kuwa “lengo ni kuchakata taarifa za mifumo ya dawa ili kubaini kama kuna hazina ya dawa za kutosha au lah, ili kuweza kusaidia maeneo ambayo yanaupungufu wa dawa.” Alisisitiza Gwajima.

Katika hatua nyingine Gwajima alisema Serikali hivi sasa ipo katika maboresho makubwa ya mfumo wa uendeshaji wa shughuli za Afya (Government of Tanzania Health Management Information System-GoTHOMIS) ambao baada ya kukamilika kwake mfumo utatoa taarifa nyingi za makusanyo ya fedha za dawa mpaka ngazi ya mtumiaji wa mwisho.

Awali kabla yakumkaribisha Mgeni Rasmi, Mkurugenzi wa Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii OR-TAMISEMI, Dkt. Ntuli Kapologwe, alisema Sekta ya Afya imekuwa miongoni mwa sekta zilizo pewa kipaumbele na Mhe. Rais hivyo kama wataalam lazima tuoneshe kwa vitendo kuwa Mhe. Rais hajakosea katika hili.

“Mtakumbuka ziara ya mwanzo kabisa Mhe. Rais, alijielekeza katika sekata hii muhimu kwa mustakabali wa maendeleo nchi hasa wakati huu tunapoelekea katika uchumi wa kati ifikapo 2025. Lakini hakuishia hapo toka ameingia madarakani imeendelea kutenga fedha kwaajili ya kujenga na kukarabati vituo vya kutolea huduma za afya, ambapo katika mwaka wa fedha 2017/18 vituo vya afya 352 zikiwepo Hospitali 9, Vituo vya Afya 304 na Zahanati 39 zilikarabatiwa, lakini hivi sasa vituo vinavyo jengwa na kukarabatiwa vimefikia 470 zikiwemo hospitali 67 mpya za Halmashauri ambazo zitakuwa na idara kamili ya dawa” alisema Kapologwe.

Kikao cha Wafamasia kimetayarishwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo, lengo likiwa nikuweka mipango ya kuhakikisha mianya ya ubadhilifu wa dawa inakomeshwa lakini pia kuweka mikakati endelevu ya upatikanaji wa dawa katika sehemu zote za kutolea huduma za afya.


Share:

Maambukizi Ya Vvu Yapungua Kwa Asilimia 2.3

Na WAMJW- DSM
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa maambukizi ya VVU yamepungua kutoka asilimia 7 mwaka 2003/4 hadi asilimia 4.7 mwaka 2016/17.

Waziri Ummy amesema hayo jana wakati wa mkutano wa kujadili maendeleo ya utekelezaji wa sera ya pamoja ya ushirikiano na Serikali ya Marekani kupitia PEPFAR cop 19 kuhusiana na masuala ya VVU na UKIMWI uliofanyika jijini Dar Es Salaam. “Kuanzia huduma za UKIMWI zianze kutolewa nchini tumeshuhudia mafanikio makubwa kwa upande wa kupunguza maambukizi kutoka asilimia 7 mwaka 2003/4 hadi asilimia 4.7 mwaka 2016/17". Amesema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwemo PEPFAR inaendelea kupanga mikakati mbalimbali ya kudhibiti maambukizi ya UKIMWI, kutoa huduma na matibabu kwa watu wanaoishi na virusi.

Mbali na hayo Waziri Ummy amedai kuwa Serikali imefanikiwa kutoa huduma za utambuzi na matibabu, huku akisisitiza kuwa dhana ya kwamba UKIMWI ni ugonjwa wa kifo imeisha.

Hata hivyo, Waziri  Ummy amesema, kufikia mwezi Septemba mwaka 2019 idadi ya watu waliopima na kujua afya zao imefikia asilimia 77.2 na kati yao asilimia 98 wanaendelea na huduma za VVU pamoja na matumizi ya ARV.

Kwa upande wake Balozi wa Marekani nchini Dr. Inmi Patterson amesema Serikali ya Marekani itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ugonjwa wa UKIMWI na ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa jitihada kubwa inazofanya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika kudhibiti maambukizi na kutoa huduma bora za VVU kwa watu waliogundulika na maambukizi.

Mkutano huo ulijumuisha wadau mbalimbali akiwemo mwakilishi wa Shirika la Afya duniani nchini Tanzania Dkt. Tigest Ketsela pamoja na wataalam kutoka Wizara ya Afya wakiongozwa na Mkurugenzi wa kinga Dkt. Leonard Subi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Tume ya kudhibiti na kupambana na UKIMWI (TACAIDS) pamoja na wadau mbalimbali.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger