Monday 1 July 2019

ESRF YAANDAA WARSHA KUBORESHA MRADI WA PSDS 2006


Mkuu wa Idara ya Utafiti na Machapisho wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Profesa Fortunata Makene akitoa neno la ukaribisho kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida wakati wa warsha ya kitaifa ya utekelezaji wa mkakati wa maendeleo kwa nchi za Afrika Mashariki unaozingatia mchango wa sekta binafsi (EAC- PSDS) iliyoandaliwa na ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. (EAC- PSDS) iliyoandaliwa na ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Ofisa wa kitengo cha maendeleo ya sekta binafsi Ofisi ya Waziri Mkuu, Diana Makule akiwasilisha mada ya mtazamo wa jumla wa PSDS 2006 na matokeo ya utekelezaji wake wakati wa warsha iliyoandaliwa na ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Mtaalamu wa masuala ya tabia nchi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Martha Ngalowera akiwasilisha mada kuhusu uchakataji wa mazao ya kilimo katika mradi wa PSDS 2006 kwa kuangalia vifungu vinavyohusiana na tabia nchi kwenye warsha iliyoandaliwa na ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa warsha, Meneja Ufuatiliaji na Tathmini , Kituo cha Taasisi ya Maendeleo Endelevu (CSDI), Dk Isaack Nguliki akizungumzia biashara kuchagiza uchakataji wa mazao ya kilimo kwa kuangalia vifungu vinavyohusiana na tabia nchi katika PSDS kwenye warsha iliyoandaliwa na ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Bi. Rehema Mbugu kutoka Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF)akiongoza majadiliano ya mtazamo wa jumla wa PSDS 2006 na matokeo ya utekelezaji wake wakati wa warsha iliyoandaliwa na ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Washiriki wakishiriki majadiliano wakati wa warsha ya kitaifa ya utekelezaji wa mkakati wa maendeleo kwa nchi za Afrika Mashariki unaozingatia mchango wa sekta binafsi (EAC- PSDS) iliyoandaliwa na ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Mshehereshaji ambaye pia ni Mkuu wa kitengo cha Uwezeshaji na Utawala Bora wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Danford Sango akisisitiza jambo wakati wa warsha ya kitaifa ya utekelezaji wa mkakati wa maendeleo kwa nchi za Afrika Mashariki unaozingatia mchango wa sekta binafsi (EAC- PSDS) iliyoandaliwa na ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Idara ya Utafiti na Machapisho wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Profesa Fortunata Makene akifafanua jambo wakati wa warsha ya kitaifa ya utekelezaji wa mkakati wa maendeleo kwa nchi za Afrika Mashariki unaozingatia mchango wa sekta binafsi (EAC- PSDS) iliyoandaliwa na ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
**
Wakati Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imejikita katika kutaka kuendeleza mkakati wa sekta binafsi (PSDS) 2018-2022, wenye lengo la kuweka mazingira mazuri ya biashara yatakayochochea ushindani ndani ya sekta binafsi kwa kuongeza uwekezaji, tija na biashara, Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) imekutanisha wadau kuangalia namna ya kuboresha mkakati huo.

Katika warsha hiyo wadau walizungumzia na kuainisha mambo mbalimbali yenye lengo la kuuwezesha Mkakati huo kutoa mchango wenye uelewa wa mabadiliko ya tabia nchi, uzalishaji wenye msukumo wa kibiashara na uchakataji wa bidhaa za kilimo.

Dk. Tausi Kida Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), akifungua warsha hiyo mwishoni mwa wiki alitaka washiriki kuwa makini ili kuweza kuona namna gani wanaweza kuimarisha mkakati huo.

Akishawishi umakini katika warsha hiyo ya kitaifa ya utekelezaji wa mkakati wa maendeleo kwa nchi za Afrika Mashariki unaozingatia mchango wa sekta binafsi (EAC- PSDS), alisema bila umakini mchango wa mkakati huo hautaonekana.

Katika warsha hiyo wadau walizungumzia upenyo wa maendeleo endelevu katika uchakataji wa bidhaa za kilimo.

Warsha hiyo ikiwa ni sehemu ya awamu ya pili ya mradi wa kuendeleza kilimo katika nchi za Afrika mashariki unaoangalia mabadiliko ya tabia nchi na mahusiano ya kibiashara katika nchi hizo- (PACT EAC2). Mradi huo umekuwa ukiendeshwa na ESRF kwa kushirikiana na CUTS International yenye makao makuu yake mjini Geneva Uswisi.

Mkurugenzi huyo wa ESRF alisema kwamba toka mwaka 2015 mradi umekuwa ukifanya majadiliano ya kina kwa sekta mbalimbali ambazo nyingi ni mtambuka ili wadau wengi wawe wanajua kwa pamoja mabadiliko ya tabia nchi, mahusiano yao na uzalishaji, biashara, usalama wa chakula na viwanda vya kuchakata bidhaa za kilimo.

Kwa mujibu wa Dk Tausi warsha hiyo ilikuwa na lengo la kuwapa nafasi wadau wote kuangalia njia bora zaidi ya kuwezesha uchakataji endelevu wa viwanda vya bidhaa za kilimo ili kuvipa thamani kupitia sekta binafsi.

Mkurugenzi huyo aliwataka washiriki kujadili kwa kina mchango wa sekta binafsi katika kuchagiza uelewa wa mabadiliko ya tabia nchi, na uendelezaji wa kilimo biashara na usalama wa chakula katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.

“Kutokana na ukweli huo napenda mazungumzo yetu ya leo yajikite zaidi katika kufanikisha mkakati wa sekta binafsi kuhusu maendeleo (PSDS) 2018-2022 kuhusu wajibu wake kuendeleza uchakataji wa bidhaa za kilimo endelevu utakaozingatia mabadiliko ya tabia nchi biashara na usalama wa chakula.” alisema Dk Tausi.

Katika warsha hiyo ambapo mada mbili ziliwasilishwa moja ikizingatia mabadiliko ya siasa na sheria nchini na mazingira ya sasa kuhusiana na mkakati huo wa kuwezesha ukuaji wa sekta binafsi na dhana ya uendelezaji wa kilimo biashara katika uhusiano na mabadiliko ya tabia nchi na nyingine.

Mada hizo zimetolewa na wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na Ofisi ya Waziri Mkuu,wakiangalia PSDS ilivyowezeshwa kusaidia sekta binafsi kuchochea uelewa wa mabadiliko ya tabia nchi, kilimo biashara na uchakataji wa bidhaa za kilimo na usalama wa chakula.

Mada hizo ziliwasilishwa na Diana Makule wa Ofisi ya Waziri Mkuu na Martha Ngalowera wa Ofisi ya Makamu wa Rais.
Share:

Heslb Online Application system now open 2019/20

HESLB  Online Application system now open 2019/20, heslb application, olams heslb go tz, maombi ya mkopo heslb 2019

HESLB has officially started to receive electronic Loan applications for Academic year 2019/2020

Welcome to Online Loan Application and Management System (OLAMS). ONLY Tanzanian Nationals are eligible to apply for higher education student loans. Kindly provide TRUE information about yourself and follow all the instructions to fill and submit your application package.
Applications for 2019/2020 Academic Year will be accepted from 01st-July-2019 and the deadline will strictly be 15th-August-2019 at 23:59 Hours.


  1. Kindly read carefully the Guidelines and Criteria for Issuance of Loans for 2019/2020 before applying; Download
  2. Click Apply for Loan for registration using your Form IV Index Number and year of completion;
  3. After Providing and confirming your Form Four Index number, you will receive your Control Number (99111xxxxxxx),
  4. Use the generated Control Number to Pay a Non-Refundable Application Fee of TZS 30,000.00 (Pay in-full, NOT by Instalments) through:

MPesa, Tigo Pesa, HaloPesa, Airtel Money, T-Pesa or EzyPesa

  • through Control Number

“generated by the system”

    • as reference number and thereafter you will receive a confirmation message (receipt);

    You can use your Control Number from OLAMS to pay application fee at any NMB, TPB or CRDB Bank Branch or respective Agents. Should you need any assistance, kindly refer to provided instructions or call HESLB Helpdesk through

+255 550 7910

  • ,

0736 665 533

  • or

0739 665 533

 

Apply Now

The post Heslb Online Application system now open 2019/20 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Katibu Mkuu Wizara Ya Kilimo (SMT) Mhandisi Mtigumwe Na Naibu Katibu Mkuu Wizara Ya Kilimo (SMZ) Bi Mansura Waongoza Kikao Cha Mashirikiano

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo (SMT) Mhandisi Mathew Mtigumwe na Naibu Katibu Mkuu (SMZ) Bi Mansura Mosi Kassim wameongoza kikao cha mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania katika sekta ya Kilimo.

Kikao hicho kimefanyika ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya ofisi ya Makamu wa Rais Muungano kwa wizara zote za SMT na SMZ kukutana na kuzungumzia Mashirikiano baina yao.

Vikao kama hivyo hutuama kujadili kwa pamoja namna ya kutatua changamoto za Muungano zilizopo katika sekta ya Kilimo.

Katika kikao hicho kumejadiliwa kuhusu utekelezaji wa maazimio mbalimbali yaliyowekwa katika kikao cha makatibu wakuu wa sekta ya Kilimo kilichofanyika mwezi Machi, 2018.

Kadhalika, maeneo mengine ya mashirikiano yaliyojadiliwa ni pamoja na Maendeleo ya mazao, utafiti na mafunzo, huduma za umwagiliaji na Zana za Kilimo na Sera, na Mipango na uimarishaji wa takwimu.

Kikao kazi hicho kilifanyika tarehe 24 Juni, 2019 katika ofisi za wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar.



Share:

Watoroshaji dhahabu katavi kukiona

Mkuu wa mkoa wa Katavi  Juma Homera ameapa kupambana na wanaotorosha dhahabu huku mpaka sasa watu wawili wakishikiliwa na jeshi la polisi kwa kununua dhahabu kinyume cha sheria mkoani humo

RC Homera akiwa ziarani katika migodi mbalimbali ikiwemo Dilifu ambao ni mgodi wa wachimbaji wadogo na mgodi mkubwa wa Katavi na Kapufi mining  alieleza anachotaka wachimbaji wadogo wakauuze madini yao katika soko la madini la mkoa huo.

Homera alianza majukumu ya ukuu wa mkoa ikiwa soko limeshafanya biashara kwa kununua dhahabu gram 238, May 23/2019 jambo ambalo lilimfanya aanze kufatilia na kubaini dhahabu nyingi inayopatikana Mkoani Katavi inauzwa nje ya mkoa wa  Katavi nakupelekea soko hilo kusua sua.

Kufuatia jambo hilo limemfanya  Homera kuyafanyia kazi mapungufu ya soko hilo, mpaka sasa ununuzi na uuzaji wa madini ni Grams 6317.2 sawa na Kg 6 na Grams 317.2 yenye thamani ya Tshs.Million 519,155,127.56 zimenunuliwa kwa kipindi cha Mei na June 30/2019 na serikali kupata mrahaba (Royality7%) Tsh Milioni 36,340,858.92 na Service levy  0.3% Tsh.milioni 1,401,718.85.

Aidha ameimarisha mifumo ya Benk mbili katika soko hilo na ameendelea kuwa bana mablokers na wanunuzi wenye leseni na wachimbaji mbalimbali  kuhakikisha pia wanauza madini yao kwenye soko la mkoa ili tujenge uchumi wa Tanzania na kumuunga mkono Rais wetu Dkt.John Joseph Pombe Magufuli katika kuinua uchumi na miundombinu ya nchi hii kwa kulipa kodi


Share:

Ujangili Wapunguza Idadi Ya Faru Kutoka Zaidi Ya Elfu 10 Hadi 161 Pekee

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Imeelezwa kuwa  idadi ya wanyamapori aina ya  Faru weusi[Black Rhino]   imepungua kutoka faru   zaidi ya elfu  kumi kwa miaka 1970 mpaka 1980 na  kubaki faru   161 pekee  hadi sasa hapa nchini  kutokana na Ujangili.
 
Hayo yamesemwa jijini Dodoma na Waziri wa Maliasili na Utalii Dokta  Hamis Kigwangalla wakati akizindua mpango kazi  wa kulinda na kutunza Faru weusi uliofanyika katika ukumbi wa chuo cha Mipango jijini Dodoma.
 
Dokta Kigwangalla amesema kutokana na tishio kubwa la faru kutoweka hapa nchini kwa sababu ya   ujangili, serikali imeandaa mikakati kabambe ya kudhibiti ujangili hali ambayo imeanza kuzaa matunda na kuanza kusababisha faru kuongezeka  ambapo  serikali imetenga Dola milioni 61 sawa na zaidi ya Tsh.Bilioni 120 za kitanzania  kwa ajili ya utekelezaji wa mipango hiyo.
 
Aidha,Dokta Kigwangalla amesema sekta ya  utalii hapa nchini  huzalisha zaidi ya Dola za Marekani bilioni 2  ambazo huchangia asilimia 25%  ya fedha za kigeni  na kuchangia asilimia 17% ya mapato ya ndani ya nchi [GDP ]  na imetoa ajira rasmi laki sita[600,000]  na zisizo rasmi milioni mbili[2000,000] hivyo ulinzi wa wanyamapori  walio katika hatari ya kutoweka wakiwemo faru utaendelea kuimarishwa  na mpango wa serikali ni kuhakikisha  uzalishaji wa faru unaongezeka kwa kasi kwa miaka mitano ijayo.
 
Katika hatua nyingine ,Dokta Kigwangalla ameitaka jamii kuachana na mila potofu za kutumia pembe za faru kama  dawa za kuongeza nguvu za kiume kwani imani hizo hazina ukweli wowote na zinapaswa kupuuzwa.
 
Mtafiti kutoka   taasisi ya utafiti ya wanyamapori nchini,TAWIRI Dokta Edward Kohi  amesema kunahitaji teknolojia zaidi ili kuhakikisha faru anatunzwa   ambapo miaka ya 1998 waliingia kwenye tatizo la kutoweka hadi sasa kuna faru 161 wanaoweza kuhesabiwa na kuonekana.
 
Pia  ,Dokta Kohi ametaja malengo madhubuti ya  Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania,[TAWIRI ] ni Pamoja   kuongeza idadi ya faru si chini ya 5%  kwa mwaka,kuwa na uwezo wa kuhamisha faru kutoka eneo  moja hadi jingine,kuhakikisha ujangili wa faru uwe chini ya 1%     pamoja na kuwa na mfumo wa mawasiliano na mipaka mingine.
 
Naye mwakilishi kutoka  mfuko wa wanyamapori ulimwenguni[WWF] Dokta  Simon Lugandu amesema mradi wa kuhifadhi na kutunza  faru Tanzania unaendelea   katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya uhifadhi wa mazingira ‘
 
Ikumbukwe kuwa Tanzania ilishaanza   kutumia teknolojia ya kufuatilia faru ambapo mradi wa teknolojia hiyo ya kifaa chenye uwezo  wa kutoa  maelezo mwenendo wa faru  ,unagharimu dola za kimarekani 111,320  na unatekelezwa kwa ushirikiano na maafisa wa TANAPA ,Maafisa wa Shirika  la Wanyama la Frankfurt[FZS]na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania[TAWIRI]


Share:

Spika Mstaafu wa Bunge Pius Msekwa Aunga Mkono Tundu Lissu Kuvuliwa Ubunge

Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Pius Msekwa amedai uamuzi uliofanywa  na Spika wa Bunge Job Ndugai wa kumvua Ubunge aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu uko sawa, kwani yeye alishawahi kuwavua Wabunge zaidi ya 50 katika kipindi chake, kwa kosa la utoro ndani ya Bunge.

"Uzoefu wangu mimi katika hili Spika yuko sawa kabisa, kwa sababu hata mimi mwenyewe nilishawavua Wabunge wengi kipindi cha uongozi wangu nawashangaa sana wanaohoji hatua hiyo, ni jambo la Kikatiba lililofanywa na Spika Ndugai" amesema Msekwa

"Mimi mwenyewe niliwavua wengi tu na wala sio mmoja, Wabunge wa Zanzibar walikiuka kifungu cha Katiba alichokinukuu Spika Ndugai, tena walikuwa kama 50 hivi wote nikawavua Ubunge na uchaguzi ulifanyikla tena." ameongeza Msekwa

"Inawezekana watu wakasema Tundu Lissu nchi nzima inajua kuwa anaumwa, lakini katiba haisemi kuwa lazima usikilize kutoka magazetini au mitandaoni inatakiwa Mbunge aandike barua." amesema Pius Msekwa

June 28 katika vikao vya kujadili miswada mbalimbali ya kisheria kwa ajili ya mwaka mpya wa fedha Spika Job Ndugai alitangaza kuwa jimbo la Singida Mashariki liko wazi kufuatia Mbunge wake kutotoa taarifa kuwa yuko wapi.


Share:

Afisa Mtendaji Mkuu wa Safaricom,Bob Collymore Afariki Dunia

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya simu ya Safaricom, Bob Collymore amefariki dunia. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Safaricom, matuti yamekuta Collymore asubuhi ya leo Jumatatu Juni 1, 2019 akiwa nyumbani kwake jijini Nairobi.

Vyombo vvya habari vya Kenya vimesema mwenyekiti wa kampuni hiyo Nicholas Ng'ang'a amesema afya ya Collymore ilikuwa mbaya kwa majuma ya hivi karibuni.

Collymore, alichukua likizo ya matibabu ya miezi tisa mwishoni mwa mwaka 2017 na kwenda Uingereza kwa ajili ya matibabu ya saratani na alirejea  Kenya Juni mwaka jana.

Collymore alianza kuongoza Safaricom mwaka 2010 kutoka kwa Michael Joseph ambaye kwa sasa ni mmoja wa wajumbe wa bodi ya kampuni hiyo.

Mwaka 2017 wanahisa walipiga kura kuongeza mkataba wa Bob Collymore kwa miaka miwili baada ya mkataba wake kuisha. Mkataba aliokuwa akiufanyia kazi ulikuwa unatarajiwa kufikia tamati mwaka 2020 na kumfanya kuwa Mkurugenzi aliyekalia kiti hicho kwa muda mrefu zaidi.

Viongozi kadhaa wakiwemo Rais Uhuru Kenyatta wametuma salamu za rambirambi kwa familia kutokana na kifo hicho.



Share:

MTENDAJI MKUU WA SAFARICOM AFARIKI DUNIA

Aliyekuwa ofisa mtendaji mkuu wa kampuni ya Safaricom nchini Kenya, Bob Collymore amefariki dunia leo asubuhi, Julai Mosi, 2019.

Taarifa iliyotolewa na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Safaricom, Nicholas Nganga imesema Collymore alikuwa anasumbuliwa na saratani kwa muda mrefu.

“Oktoba 2017 alienda Uingereza kwa matibabu na akarejea Julai 2018 kuendelea na majukumu yake huku akihudhuria hospitali kila ilipobidi. Mara ya mwisho alikuwa anatibiwa katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Aga Khan hapa Nairobi kabla hali yake haijawa mbaya zaidi,” amesema Nganga.

Raia huyo wa Uingereza ambaye hivi karibuni aliteuliwa kuwa mjumbe wa bodi ya taasisi ya saratani nchini Kenya, ameacha mke, Wambui Kamiru, na watoto wanne.

Kifo cha Collymore (61), kimetokea mwezi mmoja kabla hajastaafu kwani alipanga kuachia wadhifa huo Agosti mwaka huu.

Katika kipindi cha uongozi wake katika kampuni hiyo kubwa ya mawasiliano Afrika Mashariki,  imeweza kuisogeza mbele huduma ya M-Pesa iliyozinduliwa mwaka 2007, hivyo kuleta mageuzi katika sekta ya fedha Afrika.

Wakati Afrika ikisifika duniani kwa ubunifu huo, Collymore ni miongoni mwa watu muhimu katika maendeleo hayo ambayo sasa yanawanufaisha mamilioni ya wananchi huku ikirahisisha huduma za benki za biashara pia.

Tangu alipoanza kuiongoza kampuni hiyo mwaka 2010, Collymore amaeifanya Safaricom kuwa kampuni kubwa nchini Kenya inakohudumia wateja wawili katika kila watu watano wanaotumia simu ya mkononi.
Chanzo - Mwananchi
Share:

Picha : BODI YA USAJILI WA WABUNIFU MAJENGO (AQRB) YAWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WA HABARI


Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Arch. Dkt Ludigija Bulamile akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishishi wa habari Jijini Dar es Salaam yaliyoandaliwa na bodi hiyo kuhusu kuacha kuichanganya taaluma yao na ile ya wahandisi badala yake iuelimishe umma tofauti iliyopo baina ya taaluma hizo mbili na umuhimu wa kuwatumia wataalamu
hao wanapofanya ujenzi. Picha zote na Philemon Solomon
Kaimu Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Arch.Albert Munuo, akisoma taarifa kuhusu majukumu ya bodi hiyo (kulia) Mwenyekiti wa Bodi hiyo Dkt. Ludigija Bulamile.
Afisa Mkuu wa Sheria Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Ibrahim Mohamed akielezea makosa mbali mbali ya kisheria yanayofanywa yakiwemo yale ya uuzwaji wa ramani hadharani pasipo kufuata taratibu. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Arch . Dkt Ludigija Bulamile akipitia taarifa mbali mbali za bodi hiyo.
Watumishi wa bodi hiyo wakiwa katika mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishishi wa habari yaliyoandaliwa na bodi hiyo kuhusu kuacha kuichanganya taaluma yao na ile ya wahandisi badala yake iuelimishe umma tofauti iliyopo baina ya taaluma hizo mbili na umuhimu wa kuwatumia wataalamu hao wanapofanya ujenzi.
Afisa Mdhibiti Mwandamizi wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Mlezi Makuka (kushoto aliyesimama) akichangia mada yake wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishishi wa habari yaliyoandaliwa na bodi hiyo kuhusu kuacha kuichanganya taaluma yao na ile ya wahandisi badala yake iuelimishe umma tofauti iliyopo baina ya taaluma hizo mbili na umuhimu wa kuwatumia wataalamu hao wanapofanya ujenzi.
Arch. Mbaraka Igangula akichangia mada.
QS.Mashaka Bundara akisisitiza jambo.
Arch.Joseph Ringo akichangia mada wakati wa mafunzo hayo.
Waandishi wa Habari wakichangia mada mbali mbali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yaliyoandaliwa na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) kuacha kuichanganya taaluma yao na ile ya wahandisi badala yake iuelimishe umma tofauti iliyopo baina ya taaluma hizo mbili na umuhimu wa kuwatumia wataalamu hao wanapofanya ujenzi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Dkt. Ludigija Bulamile akijibu maswali.
Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Dkt. Ludigija Bulamile, Kaimu Msajili Albert Munuo pamoja na waandishi wa habari na wajumbe wa bodi hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) 

 ****
BODI ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) imewataka wanahabari nchini kuacha kuichanganya taaluma yao na ile ya wahandisi badala yake iuelimishe umma tofauti iliyopo baina ya taaluma hizo mbili na umuhimu wa kuwatumia wataalamu hao wanapofanya ujenzi.

Akizungumza wakati akifungua mafunzo ya
kuwajengea uwezo waandishishi wa habari yaliyoandaliwa na menejimenti ya bodi hiyo mwishoni mwa wiki Jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa AQRB Dkt. Ludigija Bulamile alisema lengo ni kuwaelimisha waandishi shughuli na majukumu yake katika sekta ya ujenzi ili waweze kuuelimisha umma wa
watanzania faida na hasara za kutowatumia wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi wanapofanya ujenzi wowote. 

Alisema kumekuwa na mkanganyiko wa utoaji taarifa
unaofanywa na waandishi wakati wanaripoti masuala yanayohusu taaluma hizo hivyo ili kuondoa mkanganyiko huo wanahabari wana kila sababu ya kuyatumia mafunzo haya kwa kuwaelimisha wengine kuzitumia kalamu zao
kuuelimisha umma tofauti za taaluma hizo.

'Elilimisheni jamii umuhimu wa kuwatumia wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi katika ujenzi ili waweze kupata makazi bora, ambayo pia yatawapa nafuu kwenye gharama za ujenzi kulingana na matakwa,'alisema Bulamile. 

Aliongeza kufafanua zaidi sababu za wahandisi kufahamika zaidi na umma kuliko wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi pamoja na kufanya kazi zinazoshabihiana kuwa ni pamoja na taaluma hiyo kuchelewa kuingia  nchini. 

"Mpaka sasa nchi nzima ina wataalamu wa taaluma hii wasiozidi 1,500 hili bado ni tatizo kulingana na idadi ya
watu na mahitaji yake," alisema Dkt. Bulamile na kuongeza bodi imeendelea kuongea na baadhi ya vyuo vikuu vilivyopo nchini vione umuhimu wa kufundisha taaluma hii ili kuongeza idadi ya wataalamu watakaowezesha kuibadili
sura ya nchi hapo baadae katika sekta ya ujenzi kwa kubuni majengo ya kisasa yanayoendana na wakati.

Kwa upande wake Kaimu Msajili wa bodi Mkadiriaji Majenzi
Albert Munuo alisema kuwa,pamoja na kusajili wataalamu wa fani hiyo na makampuni pia wanamajukumu ya kukagua miradi ya ujenzi inayoendelea ili kuona kama wataalamu wamehusika.

" Tumekuwa tukikagua ujenzi wa miradi mbalimbali 
mikubwa inayoendelea na kwamba kwa sasa tunajipanga kuutembelea mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa SGR ili kujionea ni kwa namna gani Wabunifu Majengo na
Wakadiriaji Majenzi wameshiriki ,'alisema Munuo

Aliongeza kuwa AQRB ni taasisi ya serikali iliyopo chini ya
Wizara ya Ujenzi na kwamba mpaka sasa ina ofisi katika kanda tano ikiwepo Kanda ya Mashariki, kanda ya ziwa, kanda ya kaskazini ,nyanda za juu kusini na kanda
ya kati. 

Mafunzo hayo pamoja na kuhudhuriwa na baadhi ya waandishi kutoka vyombo mbalimbali zikiwepo televisheni, redio na magazeti pia wataalamu wengine wa ujenzi kutoka AQRB akiwepo mwanasheria wao alishiriki na kusema yapo makosa mbali mbali ya kisheria yamekuwa yakifanywa ikiwepo lile la uuzwaji wa ramani hadharani pasipo kufuata taratibu. 

Hata hivyo wataalamu hao waliongeza kutolea mfano kwa kusema asilimia 90 ya nyumba zilizojengwa Dar es salaam zimejengwa bila vibali na kusababisha hasara kwa jamii pale ambapo eneo hilo linapokuja kubainika kuwa si mahali sahihi kwa ujenzi wa makazi na kulazimika kubomolewa. 

Share:

Maelfu ya Wananchi waandamana Tena nchini Sudan .....7 Waripotiwa Kufariki dunia

Watu wasiopungua saba wanaripotiwa kuuawa nchini Sudan baada ya vikosi vya usalama vya nchi hiyo kutumia mkono wa chuma kuyatawanya maandamano ya wananchi ya kutaka utawala wa kiraia.

Taarifa zaidi zinasema kuwa, maandamano makubwa ya jana ya wananchi wa Sudan katika miji mbalimbali ya nchi hiyo ukiwemo mji mkuu Khartoum yaligeuka kuwa umwagaji damu baada ya vikosi vya usalama kuwavamia waandamanaji na kuwafyatulia risasi.

Wananchi hao walikuwa wakishiriki katika maandamano ya kutoa wito kwa Baraza la Kijeshi la Mpito la nchi hiyo kukabidhi madaraka ya nchi kwa utawala wa kiraia.

Duru za hospitali zinasema kuwa, watu karibu mia mbili wamejeruhiwa.

Baraza la Kijeshi la Sudan lilichukua madaraka tarehe 11 Aprili mwaka huu baada ya jeshi la nchi hiyo kumpindua Omar Hassan al-Bashir.  

Tangu Hapo, wananchi walianza kuandamana tena wakilitaka Jeshi likabidhi Madaraka ya nchi kwa utawala wa kiraia.


Share:

Waziri wa Viwanda na Biashara Akerwa na Watanzania Wanaobeza Ubora wa Korosho ya Tanzania

Waziri wa Viwanda na Biashara ,Innocent Bashungwa amekemea baadhi ya Watanzania wanaopotosha  na kukandia kuwa korosho ya Tanzania iliyopo kwenye maghala ,haina ubora ambapo amewapasha kuacha propaganda zisizo na tija kwa Taifa.

Ameyasema hayo mjini Kibaha alipotembelea kiwanda cha Kubangua Korosho cha Terra Cashew na kiwanda cha sabuni ya unga cha Keda vilivyopo wilayani Kibaha mkoani Pwani.

Bashungwa alisema kuwa korosho ya Tanzania ni bora na iko kwenye daraja la kwanza na la pili huku daraja la tatu likiwa ni kidogo sana.

“Tunaitangazia dunia kuwa korosho ya Tanzania ina ubora na viwango vinavyotakiwa na katika kuhakikisha ubora huo nimepita kwenye maghala yote 37 ambayo yanahifadhi korosho nikiwa na wataalamu tumehakiki na kujionea hali halisi,” alisema Bashungwa.

Alisema kuwa wameandaa taarifa za kila ghala na aina na ubora wa korosho hivyo wanunuzi wanaweza kupata taarifa zote juu ya korosho na aina wanayoitaka.


Share:

Maamuzi ya IGP Sirro na IGP wa Msumbiji kuhusu mauaji ya Watanzania 10

Mkuu  wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro amekutana na kufanya mazungumzo ya kina na Mkuu wa Jeshi la Polisi wa nchi ya Msumbiji, Bernardino Rafael kuhusu mauaji ya Watanzania 10 yaliyotokea Juni 26, mwaka huu, katika kijiji cha Mtole nchini Msumbiji.

Watanzania hao waliuawa kwa kupigwa risasi na wengine kushambuliwa kwa mapanga katika kijiji hicho kilichopo mpakani mwa Tanzania na Msumbiji pembezoni mwa mto Ruvuma, ambapo mkuu huyo wa jeshi la Msumbiji amekiri kuwepo kwa wahalifu nchini mwake.

Baada ya kikao hicho, IGP Sirro aliwaambia waandishi wa habari mjini Mtwara kuwa kwa pamoja wameweka mikakati ili kuhakikisha kuwa matukio kama hayo hayatokei tena, kwa lengo la kuendelea kukuza uhusiano na ujirani mwema baina ya mataifa hayo mawili.

Kikao hicho kilikuwa na lengo la kuweka mikakati ya pamoja kati ya nchi hizi mbili na kuweza kupambana na wahalifu, wanaofanya vitendo vya kuwatia hofu wananchi wa nchi zetu hizi mbili.

“Kama nilivyowaambia jana kuwa IGP wa Msumbiji atakuja tukae pamoja na tupange mikakati ya kuweza kupambana na hawa wahalifu wanaotusumbua Watanzania, lakini pia wanawasumbua watu wa Msumbiji,” alisema IGP Sirro.

Alisema katika kikao hicho wamekubaliana mambo yanayoweza kufanyika katika kukabiliana na wahalifu, ambao siku zote huwa hawana mipaka kwa hiyo isiwe sababu ya kuzifanya nchini hizi mbili kushindwa kupambana nao.

“Ili kukabiliana na uhalifu wa kuvuka mipaka ni lazima kuwe na ushirikiano wa nchi hizi mbili na kikubwa ni kubadilishana taarifa na kufanya doria za pamoja ili kundi hili la watu wachache ambao wamekuwa wakisumbua na kufanya uhalifu kwa watanzania watiwe mbaroni na sheria ziweze kuchukua mkondo wake na kuleta majibu yaliyokuwa sahihi.

“Hivyo tumeweka mikakati ya kuhakikisha wale wote waliohusika na mauaji ya Watanzania na watu wa Msumbiji wanakamatwa haraka sana na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.”


Share:

Uturuki yamuonya vikali mbabe wa kivita wa Libya Jeneral Khalifa Haftar

Uturuki imesema kuwa vikosi vya kiongozi wa Libya Khalifa Haftar ”vitalengwa” ikiwa hawatawaachia huru haraka raia sita wa Uturuki. 

Vikosi vya Jenerali Haftar vilisema siku ya Ijumaa kuwa vitashambulia maslahi ya Uturuki kwa kuwa taifa hilo linaunga mkono serikali ya Libya inayoungwa mkono na jumuia ya kimataifa.

Pia walidai kuwa waliharibu ndege isiyo na rubani ya Uturuki kwenye anga la Tripoli.

Libya imekumbwa na machafuko na mgawanyiko tangu kuondolewa madarakani na kuuawa kwa aliyekuwa kiongozi wa taifa hilo, Muammar Gaddafi mwaka 2011.

Jenerali Haftar alianza mashambulizi dhidi ya serikali inayotambuliwa na jumuia ya kimataifa,(GNA) inayoongozwa na waziri mkuu Fayez al-Sarraj, mwezi Aprili.

Uturuki inaunga mkono GNA, inapeleka ndege zisizo na rubani, silaha na magari kwa ajili ya kusaidia juhudi za serikali kupambana na vikosi vya Jenerali Haftar, ambavyo vinadhibiti sehemu kubwa ya mashariki na kusini mwa Libya.

Jenerali Haftar kutoka jeshi la taifa la Libya (LNA) amesema atashambulia meli za Uturuki kwenye maji ya Libya na maeneo muhimu ya kibiashara ya Uturuki.

Pia amezuia ndege za kibiashara kutoka Libya kwenda Uturuki.

Mapema siku ya Jumapili, Uturuki ilisema ”italipa kisasi kwa kuchukua hatua kali zaidi” kwa vitisho vyovyote kutoka kwa vikosi vya Jenerali Haftar.

Waziri wa ulinzi wa Uturuki, Huluski Akar ameonya kuwa vikosi vya LNA vya Libya vitalipa mashambulizi yoyote watakayofanya dhidi ya maslahi ya Uturuki.

Uturuki imesema inataka kupunguza mapigano dhidi ya Jenerali Haftar, ambaye anaungwa mkono na Umoja wa falme za kiarabu na Misri.

Siku ya Alhamisi, GNA ilichukua mji muhimu wa Gharyan, mji ambao ni ngome ya vikosi vya bwana Haftar.

Credit:BBC


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu 1 July





















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger