Thursday 30 May 2019

KAMPUNI YA JATU KUFANYA MKUTANO MKUU WA WANAHISA WAKE JUMAMOSI,JUNI MOSI JIJINI DAR


Mkurugenzi  Mtendaji wa JATU  PLC  Peter Isare
***
Mkutano mkuu wa Kampuni ya Umma ya Jenga Afya, Teketeza Umaskini (Jatu TLC) umepangwa kufanyika Jumamosi June Mosi, katika Ukumbi wa Mgulani jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, wanachama wa Kampuni hiyo watachagua viongozi wapya wa bodi ambao watakua na jukumu la kuingiza kampuni hiyo kwenye soko la hisa ( DSE)

Mkurugenzi  Mtendaji wa JATU  PLC  Peter Isare alisema kuwa kampuni hiyo itaingia rasmi kwenye soko la hisa mapema mwezi August kwa mtaji wa Shilingi Bilion 7.5

Akizungumzia kampuni hiyo alisema ilianzishwa na vijana 2015 kuhusiana na masuala ya afya na lishe na haki za binadamu, watu wengi wanapata changamoto kwenye masuala mbali mbali, "Wengi ni maskini wanashindwa kumudu gharama za maisha na kusababisha migogoro kwenye jamii,"alisema na kuongeza

"Tuwe na afya lakini tuweze kujitegemea na kuwa na afya nzuri, tumejikita kwenye kilimo, masoko na bima ya afya, watu wengi wanahitaji kuwekeza katika biashara na kuhitaji mikopo.

Alisema kampuni hiyo ya umma imesajiliwa mwaka 2016 na imefanikiwa katika Kilimo cha Mpunga Kilombero, Manyara kilimo cha Alizeti na Mahindi, Tanga kulimo cha Maharage.

"Tunawawezesha wakulima kulima kilimo cha kisasa, na kuwapatia wataalamu ambao watawapa elimu, na kilimo ni cha muda wote kisichotegemea hali ya hewa.

"Igima kiwanda cha kukoboa mchele, Kibaigwa kiwanda cha mahindi na alizeti, tunaunganisha kilimo na viwanda, na soko tumelitengeneza wenyewe."

Alisema Jatu unaponunua chochote kama chakula, ni rahisi kukuza faida Kwani kuna mfumo rasmi wa kugawa faida, mteja akinunua bidhaa anapata bonasi ambapo gawio analipata mwisho wa mwezi.

Alisema kampuni hiyo imekuwa inawawezesha wakulima kulima kilimo cha kisasa, na kuwapatia wataalamu ambao wanawapa elimu, na kilimo ni cha muda wote kisichotegemea hali ya hewa.

“Kilimo kinalipa ukikitilia manani, Jatu tuna watu zaidi ya 13,000 ambao wanafanya kilimo na biashara, kama kampuni tunanufaika pia na kupata mazao moja kwa moja kutoka kwa mkulima bila kupitia kwa madalali wa kati.” alisema 


Alisemaunaweza kujiunga kwa kuuza bidhaa upata mgao kila mwezi au ujiunge kwenye kilimo, au kununua hisa kupata gawiwo ukapata faida kutokana na faida ya kampuni.
Share:

Picha : WOMEN FUND TANZANIA YATAMBULISHA MRADI WA KUWEZESHA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA KITAIFA WA KUZUIA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO SHINYANGA

Shirika lisilo la kiserikali la Women Fund Tanzania linalofanya shugghuli za utetezi wa haki za wanawake na ujenzi wa tapo ya wanawake Tanzania lenye makao yake jijini Dar es salaam limetambulisha rasmi Mradi wa Kuwezesha Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Mradi huo wa “Support for the implementation Fund for National Plan of Action to End Violence Against Women and Children” umezinduliwa na kutambulishwa rasmi leo Alhamis Mei 30,2019 wakati wa Kikao cha Wadau wa Haki za Wanawake na Watoto na upingaji wa ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto wilaya ya Shinyanga kilichofanyika katika Ukumbi wa Karena Hoteli Mjini Shinyanga.

Akizindua Mradi huo,Katibu Tawala Wilaya ya Shinyanga,Boniface Chambi kwa niaba ya Mkuu wa wilaya hiyo,alisema mradi huo utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

“Tunawashukuru sana Women Fund Tanzania kwa kutuletea mradi huu katika halmashauri yetu,ninachoweza kusema huu ni mfuko wezeshi kwa jamii,sisi kama serikali tutatoa ushirikiano,kinachotakiwa sasa ni kuwa na mawasiliano kati ya Women Fund Tanzania na wadau watakaowezeshwa/ watakaopata ruzuku,toeni taarifa serikalini”,alisema Chambi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania, Carol Francis Mango alisema mradi huo utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu kama majaribio katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

“Tumeichagua halmashauri hii iwe ya mfano kwa sababu kuna matukio mengi ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto,ili kufanikisha mradi huu tutatoa ruzuku kwa mashirika ya wanawake na wasichana kwa ajili ya utekelezaji wa mikakati mbalimbali ya ukombozi wa mwanamke na msichana”,alieleza Mango.

“Miongoni mwa Watekelezaji wa mpango wa kitaifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto na ambao ndio walengwa wa mradi huo ni Halmashauri,Mashirika,taasisi na asasi zisizo za kiserikali ‘NGOs’,mabaraza ya watoto na jamii kwa ujumla”,aliongeza.

Aidha alisema lengo la WFT ni kuchangia harakati za kutetea haki za wanawake,kuwawezesha na kuendeleza mikakati ya ujenzi wa vuguvugu la utetezi wa nguvu za pamoja ili kukuza haki na usawa wa wanawake kimapinduzi nchini.

“Sisi ni mfuko wa kwanza na pekee unaolenga kutoa ruzuku kwa ajili ya kuendeza shughuli za utetezi wa haki za wanawake hususani waliopo kwenye ngazi ya jamii.Tunataka kuchangia katika kujenga tapo la wanawake imara nchini Tanzania kwa kufadhili na kuimarisha uwezo wa wanawake kwa njia ya kuendeleza mikakati ya kuunganisha nguvu za pamoja na kutafuta rasilimali”,aliongeza.

Aidha alisema shirika hilo liko mbioni kufungua ofisi mkoani Shinyanga ili kurahisisha uratibu wa shughuli za mradi huo mkoani Shinyanga.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Katibu Tawala Wilaya ya Shinyanga, Boniface Chambi akitambulisha na kuzindua Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na Shirika la Kijamii la Women Fund Tanzania. Kushoto ni Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania,Carol Francis Mango,kulia ni Kaimu Mkurugenzi halmashauri ya wilaya ya Shinyanga,Deus Mhoja . Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Sehemu ya Wadau wa Haki za Wanawake na Watoto wilaya ya Shinyanga wakiwa katika Ukumbi wa Karena Hoteli Mjini Shinyanga.
Katibu Tawala Wilaya ya Shinyanga,Boniface Chambi akitambulisha na kuzindua Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini.
Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania,Carol Francis Mango akitoa wasilisho la Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania,Carol Francis Mango akielezea kuhusu Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Wadau wakimsikiliza Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania,Carol Francis Mango.
Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania,Carol Francis Mango akiendelea kufafanua kuhusu mradi huo.
Mratibu wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia akielezea malengo ya kikao cha wadau wa haki za wanawake na watoto.
Mratibu wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia  akizungumza ukumbini.
Wadau wakiwa ukumbini.
Afisa kutoka Women Fund Tanzania,Neema Msangi akifafanua jambo ukumbini.
Mdau, Kassabrankahr Herman kutoka shirika la AGPAHI akiuliza swali wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Afisa Mabadiliko ya tabia,mawasiliano na jinsia - Mradi wa Sauti shirika la Engender Health Tanzania,Matilda Nombo akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto.
Mkurugenzi wa shirika la TVMC,Musa Jonas Ngangala akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto.
Mkurugenzi wa shirika la Agape ACP, John Myola akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto.
Wadau wakifuatilia matukio ukumbini.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga,Ngasa Mboje akilishukuru shirika la Women Fund Tanzania kupeleka mradi katika halmashauri yao na kuahidi kutoa ushirikiano wakati wa utekelezaji wa mradi.
Mganga Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Dkt. Rashid Mfaume akitoa neno la shukrani kwa Women Fund Tanzania na kueleza kuwa uongozi wa mkoa wa Shinyanga umepokea mradi huo na wapo tayari kutoa ushirikiano wote kufanikisha malengo ya mradi huo unaolenga kuwakomboa wanawake na watoto.
Kaimu Mkurugenzi halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Deus Mhoja akiwahamasisha wadau wa haki za wanawake na watoto kuchangamkia fursa ili kuhakikisha jamii inaondokana na mambo maovu.
Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania,Carol Francis Mango akiwaomba wadau wa haki za wanawake na watoto kushirikiana na WFT kutetea haki za wanawake na watoto.
MC wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto, Elizabeth Mweyo akitoa maelekezo ukumbini,
Picha ya pamoja baada ya uzinduzi wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto.
Picha ya pamoja.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Share:

Naibu Waziri Nditiye Awataka Watanzania Kusoma Kwanza Maelekezo Ya Tiketi Kabla Ya Kukata Tiketi Ili Kuondoa Migogoro.

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Atashasta Nditiye amewataka watanzania  Kuwa na desturi ya kusoma kwanza maelekezo yaliyopo kwenye tiketi  ya kusafiria  pindi wanapotaka kusafiri ili kuondoa migongano na migogoro baina yao na Wamiliki wa Vyombo vya Usafiri. 

Mhe.Nditiye ameyasema hayo Mei 30,2019 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa ShauriMoyo  Mhe.Mattar Ali Salum  aliyehoji juu ya  baadhi ya kampuni za usafiri hususan Usafiri wa Majini kwa njia ya Boti  kuuza tiketi kwa abiria  kwa ajili ya Safari  lakini abiria anapochelewa safari tiketi hiyo  huwa haitumiki  na hivyo kusababisha hasara na usumbufu kwa abiria . 

Katika Majibu yake Mhe.Nditiye amesema tiketi ni moja ya mkataba kati ya abiria na mmiliki wa chombo cha usafiri hivyo abiria  anatakiwa kusoma kwanza maelekezo yaliyo kwenye tiketi na kama hatoridhika na maelekezo hayo ana ruksa ya kusitisha kukata tiketi ili kuondoa usumbufu.

Hata hivyo,Mhe.Nditiye amesema ufuatiliaji wa Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano  kupitia TASAC Umebaini kuhusu changamoto hizo na serikali inalifanyia uchunguzi.


Share:

Msemaji wa Serikali: Maono Na Mtazamo Wa Rais Magufuli Yazidi Kupaisha Makusanyo Ya Mapato Ya Madini

Na Mwandishi Wetu,MAELEZO
SERIKALI imesema maono na mtazamo yakinifu wa Rais Dkt. John Magufuli katika usimamizi na ufuatiliaji wa sekta ya madini, umewezesha ongezeko maradufu la makusanyo ya mapato ya sekta hiyo kutoka Tsh Bilioni 210 mwaka 2015/16 hadi kufikia Tsh Bilioni 302 kwa mwaka 2018/19 na kuifanya Tanzania kuzidi kujijenga Kiuchumi.

Akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari leo Alhamisi (Mei 30, 2019) Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, alisema Serikali ya Awamu ya Tano inafanya kazi kisayansi na itahakikisha rasilimali za nchi zinaendelea kulindwa ili ziweze kuleta manufaa kwa Watanzania wote.

Dkt. Abbasi alisema mara baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuingia madarakani Novemba 2015, ilifanya mageuzi mbalmbali katika usimamizi na ufuatiliaji wa rasilimali za madini, kwani huko nyuma Serikali ilikuwa ikipoteza kiasi kikubwa cha fedha na kuamua kuchukua hatua stahiki ikiwemo kufanya mabadiliko katika Sheria ya Madini ya mwaka 2010.

“Tulipofanya marekebisho katika sheria yetu ya madini mwaka 2017, matokeo tumeanza kuyaona kwani tumedhibiti mianya yote ya upotevu wa mapato yetu na kuanza kusimamia kwa umakini mkubwa utoroshaji mkubwa wa madini ambapo ilisababisha Serikali kupoteza kiasi kikubwa cha mapato” alisema Dkt. Abbasi.

Akitolea mfano Dkt. Abbasi alisema kufuatia agizo la Rais Dkt. John Magufuli la kuanzishwa kwa masoko ya madini ambayo ni utekelezaji wa sheria ya madini ya mwaka 2017, hadi sasa kuna jumla ya masoko 24 ambayo yamekuwa yakithibiti ubora, thamani na takwimu za madini nchini, ambapo soko la kwanza lilianzishwa Mkoani Geita, mwezi Machi mwaka huu.

Aidha Dkt. Abbasi alisema Takwimu za jumla za uzalishaji wa dhahabu katika kipindi cha miezi miwili , mkoani Geita kuanzia mwezi Machi hadi Mei, mwaka huu zinaonyesha kuwa uzalishaji umeongezeka kwa kiasi kikubwa na kufikia kilo 312.65 za dhahabu ukilinganisha na uzalishaji wa dhahabu  kilo 259.12 zilizokuwa zikizalishwa kabla ya masoko hayo.

“Mwezi April, pekee uliweka rekodi ya Geita kwa kuzalisha kilo 200 ambazo hazijapata kufikiwa mkoani humo kwa wachimbaji wadogo na wa kati na kwa Takwimu za Mei mwezi mwaka huu zinazidi kuthibitisha kuwa Watanzania wanapaswa kuendelea kumuombea na kumuunga mkono Rais Magufuli” alisema Dkt Abbasi.

Kwa mujibu wa Dkt. Abbasi alisema eneo lingine la mageuzi yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika sekta ya madini ni pamoja na maamuzi iliyochukua ya kujenga ukuta kuzunguka eneo la wachimbaji wa Madini ya Tanzanite Mkoani Manyara ambao Serikali iliweka mifumo ya masoko na ukaguzi, na hivyo kuchangia ongezeko la mapato ya wachimbaji wadogo na Serikali kwa ujumla.

Akifafanua zaidi Dkt. Abbasi alisema uzalishaji wa madini ya Tanzanite kutoka kwa wachimbaji wadogo ulioripotiwa kwa mwaka 2016 ulikuwa kilo 164.6 na kilo 147 kwa mwaka 2017, ambapo Serikali iliweka kukusanya kiasi cha Tsh Milioni 71 (2016) na Tsh Milioni 166 (2017), lakini uzalishaji huo uliongezeka maradufu mara baada ya Serikali kujenga ukuta huo.

“Uzalishaji uliongeza sana mara baada ya ujenzi wa ukuta kwani Kilo 781.2 zilizalishwa mwaka 2018 na kuiingizia Serikali mapato ya Tsh Bilioni 1.43 na uzalishaji kwa mwaka 2019 katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Mei ulikuwa kilo 1086.05 zenye thamani ya Tsh Bilioni 1.422” alisema Dkt. Abbasi.

Aliongeza kuwa mabadiliko hayo yameanza kuleta faida kwa nchi ambapo kwa sasa nchi nyingi za Afrika zimeanza kuiga mageuzi yanayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano ikiwemo kupitia upya mikataba na wawekezaji na pia watafiti mbalimbali wanairejea Tanzania inayogeuza “laana” ya madini kuwa “Baraka” ya Madini.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521


Share:

Serikali yakanusha kuwalazimisha wafanyakazi wake kuwa na laini ya TTCL

Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbas amesema hakuna agizo la Serikali linalolazimisha mfanyakazi wa Serikali kuwa na laini ya TTCL isipokuwa viongozi wanaowekewa vocha za Serikali kwamba ni muhimu kuwa na laini hizo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo amesema taarifa inayosambaa kwenye mitandao kuhusu hilo ni ya upotoshaji na kuwataka wananchi kuipuuza.


Share:

Rais Magufuli arejea nchini akitokea Zimbabwe

Rais John Magufuli amerejea nchini kutoka Zimbabwe ambapo amepokelewa na viongozi mbalimbali wakiwemo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jen.  Venance Mabeyo.

Rais  Magufuli kwa takribani wiki moja sasa amekuwa ziarani katika nchi kadhaa za Afrika, ziara hizi za wanachama wa SADC zilikuwa muhimu kwa sababu ya uhusiano wa kipekee na kihistoria wa Tanzania na nchi hizo 


Share:

ATCL yamvuruga Nape, ahoji kucheleweshwa kwa ndege

ATCL yamvuruga Nape, ahoji kucheleweshwa kwa ndege


Share:

ACHAPWA VIBOKO 40 KISA KULA EMBE OVYO OVYO HADHARANI MWEZI WA RAMADHAN

 Ibrahim Ismail, jamaa mwenye umri wa miaka 20 amepatikana na hatia ya kula embe wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhan na kupokea mijeledi 40 kwa kosa hilo.

 Ismail ambaye alituhumiwa kula wakati Waislamu wengine wakifunga, amepatikana na hatia hiyo na mahakama inayoongozwa na sheria za Shariah katika eneo la Ringim, mjini Jigawa, nchini Nigeria. 

Ibrahim Ismail alipokea mijeledi 40 kwa kula embe wakati wa mfungo wa Ramadhan   katika soko la Ringim baada ya afisa wa mahakama kumsomea mashtaka

Jaji Safiyanu Ya’u, alitoa amri kwamba jamaa huyo acharazwe mijeledi 40 hadharani ili iwe funzo kwake na kwa wengine ambao walikaidi sheria za mwezi mtukufu. 

Kushiriki mlo kwa wakati usiofaa inakinzana na sheria za kifungu cha 370 za mji wa Jigawa, Nigeria. 

 Awali, Nabahani Usman ambaye ni kamanda wa polisi wa Kano Hisbah, alionya kwamba yeyote atakayepatikana akila ovyo ovyo hadharani atachukuliwa hatua kali kwa kukaidi sheria za mfungo wa Ramadhan. 

Aliongeza kuwa, wale watakaonaswa wataachiliwa huru iwapo watatoa ushahidi wa ripoti ya daktari kwamba walikuwa wanaruhusiwa kula kwa sababu za kiafya. 
Chanzo - Tuko
Share:

Video Mpya: Rich Mavoko - Usizuge

Video Mpya: Rich Mavoko - Usizuge


Share:

ANUSURIKA KUFA BAADA YA KUJIKATA UUME KWA WEMBE

Jamaa kutoka kijiji cha Bula, kaunti ya Isiolo  nchini Kenya aliripotiwa Jumatano kujikata uume wake, akitumia wembe baada ya kuzidiwa na dawa za kulevya. 

Kwa mujibu wa ripoti ya eDaily, mamake jamaa huyo alifichua kwamba kisa hicho kilitokea wakati mwanawe huyo wa miaka 27, Abshiro Abdi, alikuwa akizikata kucha zake. 

 Kwa sasa, abdi anapokea matibabu katika hospitali ya rufaa ya Isiolo. 

Msimamizi wa hospitali hiyo Daktari Hussain Abdi Mohamud adokeza kwamba, mwathiriwa alikuwa amepoteza fahamu alipowasilishwa katika kituo hicho cha afya na kuwa alikuwa ametumia dawa za kulevya kupita kiasi.

 "Alivuja damu nyingi...lakini atakapopata nafuu bado atakuwa na uwezo wa kujisaidia kama kawaida. Nguvu zake za kiume hazitaathirika lakini iwapo kutakuwepo na uwezekano basi madaktari wa upasuaji watamshughulikia kwa njia nyingine ile," Daktari Mahamud alisema. 

Wakati uo huo, alitoa wito kwa vijana kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya akisema kuwa wanahatarisha maisha yao. 

"Vijana wanapaswa kujiepusha na dawa za kulevya za aina yoyote ile, la si hivyo, watazidi kuhatarisha maisha yao, afya yao na mawazo yao pia yataathirika," aliongeza.

Chanzo - Tuko
Share:

MKE,HAWARA MTOTO WAUA MUME MOROGORO

Boniface Agustino (46) mkazi wa Chamwino Manispaa ya Morogoro, anadaiwa kuuawa na mke, mpenzi wake na mtoto wake kwa kupigwa kwa kitu kizito kichwani kwa kile kinachodaiwa kuwa wivu wa kimapenzi.


Majirani walioshuhudia tukio hilo, akiwamo Mariam Mohamed, walidai kuwa juzi majira ya saa 8:00 mchana, walisikia vishindo na kelele kutoka kwa mwanamume huyo akiomba msaada na kudai kuwa mke wake anataka kumuua huku wakiwa chumbani kwao.

Mohamed alisema, awali mwanaume huyo alikuwa na ugomvi na mke wake, jambo ambalo lilisababisha ndugu kulisuluhisha, lakini wanashangazwa kuona mwanamke huyo akishirikiana na mtoto wake, wamefikia hatua ya kufanya mauaji hayo.

Alidai kuwa mwanamke huyo, Neema Godfrey, alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamume aliyefahamika kwa jina moja la Salum ambaye alikuwa mpangaji wake katika nyumba waliyokuwa wakiishi na mume wake, huku pia mwanamume huyo akiwa na uhusiano wa kimapenzi na binti yake, Alphonsina Boniface.

Pia Nipashe ilizungumza na ndugu wa marehemu, Revina Makundi, ambaye alisema kaka yake huyo na mkewe walikuwa na ugomvi kila mara ambao yeye alikuwa akiusuluhisha kuhusu Boniface kumbaka binti yake wakati akiwa mdogo kwa imani za kishirikina.

Aidha, Makundi alisema wanandoa hao walikuwa na ugomvi wa kimapenzi baada ya mpangaji wao kutembea na Godfrey na binti yake, hatua iliyosababisha mpangaji huyo kufukuzwa, lakini baadaye alirudi.

Mtendaji wa Kata ya Chamwino, Bright Sospeter, alisema majira ya 10:00 jioni alisikia watu wakieleza tukio hilo huku wakiwa na hisia za kutokea mauaji ndipo walijumuika na viongozi wengine.

Alisema walipofika eneo la tukio walimhoji mwanamke ambaye ni mke wa marehemu na kusema mumewe alirukwa na akili mchana na ndiyo maana alisema anauawa na muda huo wakati anaulizwa hakuwapo.

Sospeter alisema walipoingia ndani, walimkuta na kumkuta binti na kumuuliza ndipo akasema baba yake alienda kwa Ustaadhi kuombewa, hivyo hayupo jambo lililowafanya walazimike kupekua nyumba nzima na ndipo walipokuta akiwa tayari amefariki dunia akiwa chooni, huku pembeni yake kukiwa na mchi na damu sakafuni.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa, alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo na kusema wanawashikilia watu watatu kwa mahojiano zaidi.

Aliwataja watu hao kuwa ni Neema Godfrey (41) mkazi wa Chamwino, Alponcina Boniface (19) na mtu mwingine ambaye hakumtaja kwa sababu za kiuchunguzi.

Mutafungwa alisema inadaiwa kuwa mpangaji aliyekuwa amehamishwa alihusika baada ya kuingia ndani akiwa amevaa vazi aina ya dela hadi usoni na baadaye kutoroka. Aliwataka wananchi wa mkoa wa Morogoro hususan wakazi wa Chamwino, kushirikiana na polisi kufanikisha mtuhumiwa mwingine wa mauaji kupatikana.
Share:

BABA AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUBAKA MTOTO WAKE

Said Rashid (36), mkazi wa Mbezi Juu jijini Dar es Salaam amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni akikabiliwa na shtaka la kumbaka mwanaye mwenye umri wa miaka 13.

Akisoma hati ya mashtaka jana Jumatano Mei 29, 2019 mbele ya hakimu, Anifa Mwingira, wakili wa Serikali, Matarasa Hamisi amedai kati ya mwaka 2016 na 2019 mshtakiwa alimbaka mtoto wake huku akijua kufanya hivyo ni kosa la kisheria.

Matarasa amedai upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kuomba mahakama kupanga tarehe nyingine ya kutajwa.

Wakati mshtakiwa huyo akikana kufanya kitendo hicho Hakimu Mwingira alieleza kuwa dhamana ipo wazi, akimtaka kuwa na wadhamini wawili wanaotambulika kisheria watakaosaini bondi ya Sh1 milioni kila mmoja.

Hata hivyo, mshtakiwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kupelekwa rumande hadi Juni 10, 2019.

Na  Pamela Chilongola, Mwananchi 
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 30,2019


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger