Friday 1 February 2019

SERIKALI YAONGEZA USALAMA WA TAARIFA ZAKE

Naibu waziri wa nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dokta Marry Mwanjelwa amezitaka taasisi za umma kuhakikisha suala la usalama wa taarifa za serikali linakuwa la lazima wakati wa kubuni,kusanifu,kujenga,kusimika na kuendesha mifumo ya TEHAMA. Dokta Mwanjelwa alitoa agizo hilo jiji Dodoma wakati akifungua kikao kazi cha pili cha serikali mtandao. Amesema njia moja wapo ya kujihakikishia usalama ni kuhakikisha utengenezaji wa mifumo unazingatia programu ambazo wataalamu wao wanaweza kutambua kinachofanyika badala ya kuwa na mifumo ambayo hawajui kinachofanyika nyuma ya pazi. “kwa namna ya kipekee kabisa…

Source

Share:

MSAIDIZI WA ASKOFU KKKT AREKODIWA VIDEO AKIFANYA MAPENZI NA MTOTO WA MCHUNGAJI MWENZAKE KWENYE GARI


Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Richard Kasesela

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Richard Kasesela amelishauri Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT Dayosisi ya Iringa kumuondoa /kutomfumbia macho aliyekuwa Msaidizi wa Askofu wa Dayosisi hiyo mchungaji Yusto Kinyori kwa tuhuma ya kufanya mapenzi na mtoto wa mchungaji mwenzake kwenye gari.

Kasesela amesema hayo kwenye Mkutano Mkuu wa kumchagua Msaidizi wa Askofu wa kanisa hilo uliofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT usharika wa Ipogolo ambapo amesema kuwa anayo video clip ikionesha mchungaji huyo akifanya mapenzi kwenye gari na mtoto wa mchungaji mwenzake.

Kasesela amesema kuwa kinachomuuma zaidi viongozi wa dini ndiyo wanaotumwa kwenda serikali kuwawakilisha baadhi ya viongozi au kutoa matamko mbalimbali kwa niaba ya kanisa lakini kiongozi huyo amekengeuka kwa sababu ya kitendo alichokifanya na kushauri kanisa limuondoe haraka kwa sababu analiaibisha kanisa.

Kwa upande wake Askofu wa Kanisa hilo Dayosisi ya Iringa Mchungaji Blastone Gavile amesema mkutano huo maalumu umefanyika kutokana na vikao vilivyofanyika mwishoni mwa mwakajana kujadili ofisi ya msaidizi wa askofu kutokana na tuhuma zilizokuwa zikimkabili.

Mara baada ya kufanya uchaguzi huo walimpata msaidizi wa askofu Askari Mgeyekwa ambaye alikuwa mkuu wa KKKT usharika wa Kihesa na ameibuka kidedea kwa kupata kura 480, kura za hapana 17 na zilizoharibika 10 na jumla ya wapiga kura walikuwa 457.
Chanzo - EATV
Share:

ALIYEMLA MWENZAKE AKAMATWA AKIJIFANYA DAKTARI


Raia mmoja nchini Urusi, Boris Kondrashin mwenye umri wa miaka 35, amekamatwa na polisi akijifanya daktari, baada ya kubainika kufanya tukio la mauji miaka 20 iliyopita, na kunywa damu ya mtu aliyemuua.

Boris alikamatwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa wakazi wa mji wa Chelyabinsk nchini humo, mara tu walipomkumbuka na kukumbuka yale aliyoyafanya miaka ya nyuma.

Boris ambaye ni mtoto kutoka familia yenye heshima nchini humo huku baba yake akiwa ni mtaalamu wa masuala ya saikolojia, alitumia pesa zake kupata vyeti feki na kujifanya daktari wa saikolojia na daktari wa matatizo ya uraibu (adiction), ambapo alifanikiwa kupata kazi katika hospitali mbali mbali katika mji wa Chelyabinsk.

Mwaka 1998 kijana huyo alipokuwa mwanafunzi, alimuua mwanafunzi mwenzake na kumkatakata, kisha kula sehemu za mwili wake ikiwemo ini, na kunywa damu yake.

Polisi walipomkamata alikiri kufanya kosa hilo akijifananisha na 'vampire', na kwamba alitumwa na shetani kukamilisha kazi hiyo.

Hata hivyo mahakama ilimkuta kijana huyo na matatizo ya akili, hivyo alipelekwa kwenye kituo cha magonjwa ya akili, na alipopata unafuu aliachiwa huru.

Wakazi wa maeneo hayo wamesema kwamba walimtambua baada ya mwanamke mmoja kwenda hospitali hapo kupata matibabu.

 Mwanaume huyo amesema alimkumbuka daktari huyo kuwa ndiye aliyemwambia kuwa yuko kwenye orodha ya wanafunzi wengine ambao alipanga kuwaua na kuwanywa damu zao.
Boris Kondrashin
Share:

AKAMATWA AKISAFIRISHA MAITI YA MTOTO


Mwanaume mmoja anashikiliwa na vyombo vya usalama nchini Malawi baada ya kukutwa akisafiri na maiti ya mtoto kwenye treni.

Akithibitisha kukamatwa kwa mtu huyo, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini humo, Joseph Sauka, amesema kwamba mwanaume huyo aliyejulikana kwa jina la James Majawa, 28, wa kijiji cha Chimphamba alikuwa akisafiri kutoka Limbe kwenda Nayuchi.

Kamanda Sauka ameeleza kwamba maiti ya Mtoto huyo ilibainika baada ya harufu ya kitu kilichoharibika kuenea kwenye Treni hiyo iliyokuwa na abiria wengine.

Amefafanua kwamba baada ya upekuzi ndipo maiti hiyo ikabainika huku ikiwa imetolewa sehemu za siri.

Hata hivyo Kamanda Sauka ameeleza kwamba bado wanaendelea na uchunguzi zaidi huku wakisisitiza kwamba maiti hiyo siyo ya mtoto mwenye ualbino.
Share:

MWANAMUZIKI BOBI WINE ATANGAZA KUGOMBEA URAIS UGANDA KUMNG'OA MUSEVENI

Mwanamuziki Bobi Wine ambaye ni mbunge amesema atawania urais nchini Uganda katika uchaguzi mkuu ujao akidhamiria kumwondosha madarakani, Rais Yoweri Museveni.

Bobi Wine ambaye jina lake halisi ni Robert Kyagulanyi, amekiambia kituo cha televisheni cha Marekani cha CNN kuwa amejiandaa kumkabili Rais Museveni.

“Tuna Waganda wengi waliojiandikisha kama wapiga kura wapya, na hii ndiyo njia pekee ya kumwondosha Museveni,” amesema Bob Wine ambaye yuko ziarani nchini Marekani.

Alipoulizwa kama ana uwezo wa kukabiliana na Rais aliyekaa madarakani kwa muda mrefu, mwanasiasa huyo anayewavutia vijana wengi alijibu: “ Sawa, jambo hili limekuwa likijitokeza mara kwa mara na watu wengi wamekuja kwangu wakitaka niwanie nafasi hii.

“Tumekuwa tukijadiliana na timu yangu na lazima niseme tumeamua (yeye na timu yake) kwa dhati kabisa kukabiliana na Rais Museveni katika uchaguzi ujao wa Rais.

Museveni alishinda katika uchaguzi uliofanyika 2016 na kulingana na matakwa ya katiba hakuruhusiwa kuwania tena madaraka kutokana na umri wake lakini marekebisho yaliyofanyika baadaye yalimwondolea kizingiti hicho.

Pia, Bunge la nchi hiyo lilipitisha marekebisho ya sheria kwa kurefusha muhula wa Rais kuwa madarakani kutoka miaka mitano hadi kufikia saba. 







Share:

SERIKALI KUONGEZA NGUVU YA SEKTA BINAFSI KUWAINUA WAJASIRIAMALI ILALA

Na Heri Shaban Serikali imesema itashirikiana na Kampuni ya Guru Planet kuwainua Wajasiriamali wa Wilaya ya Ilala. Hayo yalisemwa na Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto wakati wa ufunguzi wa tamasha la Wajasiriamali lililoandaliwa na Kampuni ya Guru Planet kwa kushirikiana na Manispaa ya Ilala Dar es Salam jana ambapo zaidi ya vikundi 300 vimeshiriki. Akizunguza katika tamasha hilo Naibu Meya Ilala Kumbilamoto alisema dhumuni la manispaa ya Ilala kufanya tamasha Kwa kushirikiana na Kampuni ya Guru Planet ulitokana na Guru Planet imekuwa ikiendesha shughuli zake za kuwajengea…

Source

Share:

Uchawi Bariadi : BINTI AKUTWA CHINI YA UVUNGU WA KITANDA CHA BIBI YAKE HAJITAMBUI


Tukio la Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Ikinabushu (jina limehifadhiwa) kukutwa chini ya uvungu wa kitanda cha bibi yake, limetikisa viunga vya mji wa Bariadi, Simiyu. 

Taarifa zaidi zinaripoti kwamba, mwanafunzi huo alitoweka katika mazingira ya kutatanisha tangu tarehe 25 Januari mwaka huu hapo kijijini kwao Ikinabushu na baada ya siku tano alikutwa chumbani kwa bibi yake akiwa hajitambui.

Binti huyo inaeleza kwamba, alikuwa akiishi kwenye nyumba aliyokuwa akiishi bibi yake (Kwandu Kiuluma) na ndugu zake wengine akiwemo mama yake wa kambo na ndugu zake.

Kaka wa binti huo Samson Lambo amesema kuwa, aliambiwa na baba yake mdogo anayeishi Kigoma kwamba, amepokea taarifa za kupotea kwa mdogo wake na kwamba, yeye hakua akijua kuhusu ndugu mkasa huo.

Samson anasema, alipoanza kufuatilia na kuuliza, baadhi ya watu walimweleza kwamba, walikutana na mdogo wake huyo kwenye ghala maeneo ya nyumbani kwao na walipomwita alikataa na kuingia kwenye ghala hilo.

“Nilipopata taarifa hizo niliongeza wasiwasi kuhusu kupotea kwake. Kama familia tulikaa na kuamua kumtafuta kwa njia mbadala ili kujua alipo,” amesema Samson na kuongeza;

“Kwenye kikao chetu cha familia baada ya kuamini kuna mambo ya nguvu za giza, tulikubaliana kumwita mganga. Baada ya mganga kufanya dawa zake, akatuambia kuwa mtoto yupo ndani.”

Samsoni anasema, walimuuliza mganga huyo kwamba humo ndani anapatikana wapi?, ndipo walipoambiwa wakamwangalie chini ya uvungu wa kitanda cha bibi yake na kumkuta akiwa amelala hapo.

“Tulichofanya ni kumtoa kwani alikuwa na madaftari yake ya shule na alituomba maji na chakula,” amesema.

Mwanafunzi huo alisema kuwa, hana kumbukumbu yoyote kama alitoweka lakini siku moja akiwa kitandani, aliwaona watu wengi wanaume kwa wanawake wamemzunguka akiwemo bibi yake huyo.

Binti huyo amesema kuwa, alikuwa akienda shule kama kawaida na anashangaa kuambiwa kwamba hakuwa akienda shule, “mimi nashangaa kuwa eti siendi shule, najiona nilikuwa naenda shule kila siku.”

Hata hivyo, bibi huo (Kwandu) licha ya kukiri binti huyo kukutwa chini ya uvubgu wa kitanda chake, alisema hahusiki na kuongeza;

“Labda kuna watu wamefanya hivyo kupitia mimi lakini sihusiki kwa kupotea kwa mjukuu wangu.”

Deusdedit Nsimeki, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu ameeleza kuwa, wanamshikilia bibi huo kwa mahojiano zaidi.

Chanzo - Mwanahalisionline
Kuwa wa Kwanza kupata habari na matukio yanayojiri Tanzania na dunia kwa ujumla kwa kupakua/ kudownload App ya Malunde 1 blog tukuhabarishe masaa 24.

Tembea na dunia kiganjani mwako sasa.

Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. Hii ndiyo mpya kabisa,ina alama hii ↡↡
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.malunde.blog
Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install

https://bit.ly/2Qb7qyF

NB: App uliyokuwa unatumia mwanzo tumeifuta na kuleta mpya ya kisasa zaidi..Tafadhali fuata maelekezo hapo juu... Usikubali kukosa habari kizembe..Pakua app yetu Mpya ya Malunde1 blog Sasa

Share:

MASHETANI WEKUNDU WAMPATIA MKATABA MNONO ANTHONY MARTIAL

Mshambuliaji machachari wa Manchester United Anthony Martial amesaini kandarasi mpya na Manchester United itakayombakisha katika uga wa Old Trafford mpaka Juni 2024.

Anthony Martial amefunga magoli 46  katika mechi 162 alizoichezea Manchester United.

Martial mwenye miaka 23, alijiunga na United kutoka Monaco Septemba 2015 kwa pauni milioni 36, lakini hakuwa na furaha klabuni hapo mwaka 2018 na kocha aliyepita Jose Mourinho alikuwa radhi kumuuza.

Mkataba wake mpya utamfanya asalie na Mashetani Wekundu mpaka atakapotimu miaka 29, na kuna kipengele kinachoruhusu mkataba huo kuongezwa kwa mwaka mmoja.

 "Kwa umri wake, ana ubongo mzuri wa mpira, ambao, ukijumuishwa na kipaji chake cha kipekee kinamfanya awe mchezaji mwenye mustakabali mzuri kabisa,"
alisema kocha wa muda wa United Ole Gunnar Solskjaer.

Mwezi Juni, ajenti wa Martial alisema mteja wake alikuwa anataka kuhama, na Mourinho alikuwa radhi, lakini uongozi wa United ulizima jaribio hilo na wakafungua ukurasa mpya wa majadiliano.

Chanzo:Bbc
Share:

MAMA AVUA NGUO MAHAKAMANI ... ASHINDA KESI

Jepkosgei alikuwa akitarajia uamuzi wa kesi iliyojikokota kortini kwa muda wa miaka 10, Mama huyo aliamua kuvua nguo zote mahakamani baada ya jaji kuahirisha uamuzi wa kese hio tena kwa kudai alihitaji muda zaidi kupitia ushahidi.

Alikasirishwa na jaji na kuanza kupiga kelele kortini huku akivua nguo mbele ya umma.

Jepkosgei alishikwa na hamaki na kuvua nguo zote mbele ya Jaji Anthony Ndung’u kwa kuahirisha kesi hiyo, kwa mara nyingine.

Ndung’u alipotazamiwa kutoa uamuzi wake Alhamisi, Januari 17 kuhusu kesi hiyo iliyojikokota kortini tangu 2009, aliiahirisha kwa kudai alihitaji muda zaidi kupitia ushahidi uliowasilishwa kabla ya hatimaye kusoma uamuzi huo na hatua hiyo ikamkera sana Jepkosgei.

Jumatano, Januari 30 Katika Mahakama ya Nakuru, Jaji aliusoma uamuzi wake na kumfanya Jepkosgei kuridhika mno.

 “Kwa kufuata utaratibu naondoa amri inayomzuia Jepkemoi, msimamizi wa ardhi ya Chemerus kugawanya ardhi nambari Nakuru/Municipality Block 13/312. Msimamizi ana uhuru wa kuitumia ardhi atakavyo," Ndung'u aliamrisha.

Chanzo:Tuko
Share:

MKENYA CLIFTON MIHESO ATUA ULAYA


Aliyekuwa winga wa Afc Leopards Mkenya Clifton Miheso amejiunga na klabu ya Ureno Clube Olimpico de Montijo.

Klabu hiyo ya Ureno imethibitisha kwamba imesajili mchezaji huyo wa Harambee stars ambaye alikuwa akiipigia Buildcon ya Zambia.

Klabu hiyo inasema Miheso ataongeza nguvu kwenye kikosi chao.

Ikumbukwe kuwa hii itakuwa mara ya kwanza kwa Miheso mwenye umri wa miaka ishirini na tano kupigia klabu ya Ulaya.

Klabu hiyo ya Olympic imetakia Miheso kila la heri klabuni hapo ambayo inapatikana mjini Montijo.

Montijo inacheza katika ligi ya daraja la tatu huko Ureno.
Share:

AFARIKI TENA BAADA YA KUFUFUKA

Hirpha Negero aliamka katika jeneza lake mwezi Novemba muda mfupi kabla ya kuzikwa.

Mawanamume wa Ethiopia aliyefufuka wakati wa mazishi yake miezi mwili iliyopita amefariki dunia.

Hirpha Negero alithibitishwa kufa mwezi Novemba ambapo aliwekwa ndani ya jeneza kwa saa tano, lakini wakati wa mazishi yake wanavijiji walisikia akigonga jeneza.

''Nilisikia mtu akilia, nilijihisi kuishiwa na pumzi ndipo nikajaribu kujitoa katika hali hiyo, nilikua mnyonge , hata sikuweza kuzungumza," alisema Hirpha

Baadae alisema alifanikiwa kuwaita watu, hapakua na mtu yeyote karibu.

Mchimba kaburi Etana Kena anasema watu waligutushwa na tukio hilo na wote walikimbia na kuliacha jeneza, ilibidi ajifungulie mwenyewe.

Baada kisa hicho hafla ya mazishi iligeuka kuwa sherehe.

 "Nimezika zaidi ya miili 50 au 60. Sijawahi kushuhudia maajabu kama haya. Alionekana kama amefariki," Kena ambaye ni mjomba wa Hirpha alisema

Bw.Hirpha alisema kuwa aliona mahali pazuri sana wakati alipokua amepoteza fahamu, ambapo mwanamume aliyekua amevalia nguo nyeupe alimwambia rudi nyumbani.

Dkt Birra Leggese amesema huenda Hirpha alipoteza fahamu vibaya sana "deep coma".

Mchimba kaburi wa awali alimzika tena Hirpha kwa mara ya pili siku ya Alhamisi, siku moja baada ya kifo chake.

 ''mara hii nilikua na hakika amefariki kwasababu, alishuhudia jinsi alivyougua kwa muda mrefu." alisema
Share:

NANI HUDANGANYA ZAIDI KATI YA WANAUME NA WANAWAKE?

Ndiyo, wanaume huongopa zaidi ya wanawake, hayo ni matokeo ya utafiti mkubwa uliofanyika kuhusu udanganyifu.

Taarifa za tafiti  565 zikihusisha watu 44,000 zilichakatwa na taasisi ya Max Planck na Technion za Ujerumani na Israel.


Lakini,wanawake si wakweli kihivyo. 42% ya wanaume waligundulika ni waongo,ikilinganishwa na 38% ya wanawake.

Utafiti huo pia umebaini kuwa vijana ni waongo zaidi ya wazee.

 kila mwaka kiwango cha ukweli hupanda kwa 0.28%.

Habari ndio hio.
Share:

WANNE WASHIKILIWA NA POLISI KWA MAUAJI,MWINGINE KWA KUMDHALALISHA RAIS MAGUFULI

Na Dinna Maningo, Tarime. Jeshi la Polisi mkoa wa Polisi Tarime / Rorya linamshikilia mtu mmoja kwa kosa la kumdhalilisha Rais John Magufuli kupitia mtandao wa Whatssap na  linawashikilia watuhumiwa wanne kwa kosa la mauaji. Kamanda wa Polisi mkoa wa Polisi Tarime/Rorya Henry Mwaibambe alisema kuwa januari,24, 2019 majira ya saa nne  polisi walifanikiwa kumkamata  Sabato Marwa kwa kosa la kutuma picha kwenye mtandao wa kijamii wa whatssap liitwalo Tarime Ishi na Mimi. “Picha hiyo ilikuwa na maandishi yaliyoandikwa MAGUFULI  2015 na alama ya dole gumba,picha hiyo ilikuwa ikimdhalalisha Rais…

Source

Share:

NYOKA WA AJABU AUA WATU WATANO SUMBAWANGA..HUUA SIKU ZA JUMAPILI

Na Gurian Adolf -Sumbawanga

Maofisa Maliasili wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa, wameamua kushirikiana na mtaalamu wa tiba za jadi wa kijiji cha Kinambo, Tarafa ya Milepa, kumsaka nyoka wa ajabu anayedaiwa kuua watu watano kwa nyakati tofauti kijijini hapo. 

Diwani wa Kata ya Milepa wilayani Sumbawanga, Aporinali Macheta, alisema jana kwamba, nyoka huyo aina ya koboko anadaiwa kugonga na kusababisha vifo vya watu watano katika kipindi cha miaka minne tofauti.

Alisema jambo la kushangaza ni kwamba nyoka huyo amekuwa na kawaida ya kugonga watu kila mwaka katika moja ya siku ya Jumapili. 

Alisema siku kama hiyo ya Jumapili mwaka 2016 nyoka huyo aliwagonga watu wawili ambao walifariki dunia muda mfupi baadaye.

Alisema kuwa msako dhidi ya nyoka huyo umeanza baada ya juzi kumgonga na kumsababishia kifo Ndoti (60), mkazi wa Kijiji cha Kinambo, ambaye alifariki muda mfupi baada ya kugongwa na nyoka huyo.

Alisema nyoka huyo anapatikana katika mti mmoja wa mwembe ambapo baada ya kumgonga mtu hutokomea porini.

Macheta aliongeza kuwa baada ya tukio hilo wanakijiji walimwandikia barua Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kuomba wataalamu wa Maliasili ambao walifika kijijini hapo jana. 

Alisema walifika na kuanza kuendesha msako dhidi ya nyoka huyo kwa kumtumia kijana aitwaye Seif Sikanda, ambaye ni mtaalamu wa tiba za asili.

“Msako wa nyoka huyo unaendelea, lakini leo (jana) tulifanikiwa kumuua kwa risasi nyoka mdogo mwenye urefu wa futi saba aina ya koboko... tunaendelea kumsaka yule mkubwa ambaye ndio tishio la maisha ya wananchi wa kijiji hiki,” alisema. 

Ofisa Mtendaji wa kijiji hiko, Richard Sungura, alisema pamoja na nyoka huyo kumgonga na kusababisha kifo cha Ndoti, pia amesababisha vifo vya Elezina Kasele (68), Saise Shigela (21), John Mboganzuri (63) na Benedicto Kasele (14). 

Alisema nyoka huyo pamoja na kuua watu hao kwa nyakati fofauti, pia amekuwa aking’ata mifugo kama ng’ombe, mbuzi na mbwa. 


CHANZO- NIPASHE

Share:

MBUNGE ATUPWA JELA KWA KUCHAPISHA UONGO TWITTER

Mbunge na aliyekuwa waziri wa zamani wa michezo Ivory Coast, amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela, baada ya kusambaza taarifa za uongo kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Alain Lobognan aliandika katika ukurasa wake wa Twitter tarehe 9 Januari kuwa mkuu wa upelelezi ametoa tamko la kukamatwa kwa mbunge mwenzake, taarifa hiyo ilizua gumzo na fujo kwa miongoni wa wafuasi wa mbunge huyo.

Lakini mkuu wa upelelezi alikanusha kutoa tamko hilo kama alivyoandika Lobognan katika ukurasa wake wa Twitter.

Mbunge huyo ambaye yupo katika mgomo wa kula siku zaidi ya kumi sasa anasema kuwa kesi yake imeingiliwa kisiasa.

Mwanasheria wake bi Affoussiata Bamba Lamine, amesema kuwa wana mpango wa kukata rufaa.

Ameongeza pia kuwa kesi ya mteja wake imeingiliwa kisiasa, na kusema kuwa analengwa kwasababu ya ukaribu wake waziri mkuu wa zamani na alikua pia kiongozi wa zamani wa waasi Guillaume Soro.

Kwasasa ni spika wa bunge, mwezi uliopita kiongozi huyo alitangaza kuachia madaraka kama spika.

Wachambuzi wanasema kuwa huenda ameanza kujiandaa na kugombea urais mwaka 2020.
Chanzo - BBC
Share:

Picha : WATAFITI WATAKIWA KUONGEZA NGUVU KATIKA UTAFITI WA UGONJWA WA MALARIA


Mtaalamu wa magonjwa ya Damu, Vinasaba na Saratani Professa Lucio Luzatto wa Chuo cha MUHAS akiwasiliasha mada katika kongamano la Kisanyansi la Kitafiti ambalo Mada ilikuwa ni Mchango wa Chuo Kikuu MUHAS katika mapambano dhidi ya Malaria Tanzania lililofanyika leo jijini Dar es Salaam. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Wageni waalikwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu MUHAS wakifuatilia.
Wageni waalikwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu MUHAS wakifuatilia.
Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Prof. Appolinary Kamuhabwa akiwasiliasha mada ya 'Malaria kwa akinamama wajawazito na Watoto' katika kongamano la Kisanyansi la Kitafiti ambalo Mada ilikuwa ni Mchango wa Chuo Kikuu MUHAS katika mapambano dhidi ya Malaria Tanzania lililofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Mtaalam wa Masuala ya Dawa wa Chuo cha MUHAS, Prof. Omary Minzi akiwasiliasha mada katika kongamano la Kisanyansi la Kitafiti ambalo Mada ilikuwa ni Mchango wa Chuo Kikuu MUHAS katika mapambano dhidi ya Malaria Tanzania lililofanyika leo jijini Dar es Salaam.


Wageni waalikwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu MUHAS wakifuatilia.

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Prof Andrew Barnabas Pembe akifuatilia kwa makini mada.
Mkufunzi Mwandamizi wa Chuo cha MUHAS, Dkt Bill Ngasala akiwasiliasha mada katika kongamano la Kisanyansi la Kitafiti ambalo Mada ilikuwa ni Mchango wa Chuo Kikuu MUHAS katika mapambano dhidi ya Malaria Tanzania lililofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Wageni waalikwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu MUHAS wakifuatilia.
Mhadhiri Mwandamizi katika Idara ya Damu ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Julie Makani (kwanza kushoto) akitoa ufafanuzi juu ya ugonjwa wa Siko Seli unavyoendana na ugonjwa wa Malaria.
Mtafiti wa Malaria wa Taasisi ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu kilichopo Bombo Hospitali, Tanga, Deus Ishengoma akizungumzia ukata wa fedha unavyonyongonyesha tafiti bunifu.
Mmoja ya mdau wa masuala ya afya akiuliza swali.
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma MUHAS na Mloganzila, Hellen Mtui akitoa shukrani zake za pekee kwa wote walioweza kushiriki katika kongamano la Kisanyansi la Kitafiti ambalo Mada ilikuwa ni Mchango wa Chuo Kikuu MUHAS katika mapambano dhidi ya Malaria Tanzania lililofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Muhadhara huo, Prof. Lyamuya akihitimisha kongamano la Kisanyansi la Kitafiti ambalo Mada ilikuwa ni Mchango wa Chuo Kikuu MUHAS katika mapambano dhidi ya Malaria Tanzania lililofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.

Utafiti umeonyesha ugonjwa wa Malaria kwa akinamama wajawazito na watoto umepungua kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na awali.

Kwa upande wa Zanzibar ugonjwa wa Malaria umepungua kwa kiwango kikubwa hivyo ni vyema Tanzania Bara kuendelea kupambana ili ifikapo 2030  tatizo la ugonjwa wa Malaria kwa jamii umalizike.

Hayo ameyabainisha Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Prof. Appolinary Kamuhabwa anayesimamia Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaaluma  wakati akiwasiliasha mada katika kongamano la Kisanyansi la Kitafiti ambalo Mada ilikuwa ni 'Mchango wa Chuo Kikuu MUHAS katika mapambano dhidi ya malaria Tanzania' lililofanyika jijini leo Dar es Salaam.

Amesema kuwa kadili mama mjamzito anavyotumia vizuri dawa za kujikinga na ugonjwa wa  Malaria wakati akiwa amepata ujauzito ndivyo anavyoweza kuepukana na ugonjwa huo.

"Kawaida mama mjamzito anapofika wiki ya 13 huwa anapewa dawa za kuzuia Ugonjwa wa Malaria kwa ajili ya yeye na kumkimkinga mtoto, hivyo akizitumia sawa sawa kwa kufuata maelekezo ya dokta pindi anapojifungua huwa salama," amesema.

Prof Kamuhabwa amesema kuwa mujibu wa matokeo ya awali yaliyofanyika katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam imeonyesha Maambukizi ya Ugonjwa wa Malaria yamepungua chini ya asilimia moja jambo linaloletea faraja kubwa.

"Tafiti ni jukumu letu kubwa na tunaangalia magonjwa ya kipaumbele katika nchi na Malaria ni ugonjwa wa kipaumbe maana unaathiri akinamama wajawazito na watoto walio chini ya miaka 5 hivyo hatuna budi kupambana zaidi" amesema.

Amesema kwa sasa MUHAS wanaendesha tafiti nyingine ya dawa mbadala ya Malaria kwa akinamama wajawazito na watoto maana dawa ile ya awali SP imeonyesha kuwaletea sugu akina mama.

"Tunafanya tafiti huko Rufiji ya dawa mbadala ya kuzuia maambukizi ya Ugonjwa wa Malaria ambapo Shirika la Afya Duniani limetutaka tufanyie utafiki katika nchi mbali mbali dunia japo wenzetu Kenya na Uganda matokeo yameonyesha dawa hiyo inafanya vizuri lakini kabla hapa kwetu hatujaanza kuitumia lazima nasi tufanye utafiki ila matokeo ya awali yanaonyesha dawa hii inafanya vyema.

Dawa wanayoifanyia utafiti inamchanganyiko wa mseto na dawa nyingine ili kupata mbadala na kuachana na SP kwa ajili ya kinga ya akina mama wajawazito na watoto ila tunamalizia utafiti ili tuje tutoe matokeo ifikapo machi mwaka huu.

Kwa upade wake Mtafiti wa Malaria wa Taasisi ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu Kilichopo Bombo Hospitali, Tanga, Deus Ishengoma ameiomba serikali kuwasaidia watafiti ili waweze kuibua tafiti zinazotoa majibu tofauti kwa jamii ambapo ka sasa ambapo tafiti nyingi zimekuwa zikigharimiwa na mashirika ya nje jambo linalowanyima uhuru kwa kufanya tafiti za kigunduzi.

"Serikali iliahidi kutoa asilimia moja ya pato la Taifa ili kuwawezesha watafiti nchi nzima ili waibue tafiti za kigunduzi, lakini mpaka leo kimya... tambueni fedha tunazopewa na mashirika ya nje zinakuwa zimelenga kile wanachokitaka wao na tufanye tofauti na tungewezeshwa kufanya tafiti za kigunduzi zingeleta tija kwa jamii, mfano kubuni mbinu mpya za kukabili Ugonjwa wa Malaria katika maeneo yenye Malaria kubwa kule Kanda ya Ziwa, Kigoma na Kusini mbinu ziwe tofauti, vile vile maeneo yenye maambukizi kidogo kama Dodoma, Kilimanjaro, Arusha na  Manyara na kuelekea ukanda wa nyanda za juu kusini mwa Tanzania napo kukawa na mbinu tofauti," Amesema Ishengoma.

Pia ameomba jamii kutumia vema vyandarua wanavyopewa ili kuzuia wasiumwe na mbu na kuachana na mila potofu zinazoweza kudhoofisha mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria ikiwemo kusema kuwa vyandarua vinazalisha kunguni, vinapoteza hamu ya unyumba kwa wapenzi na wengine wanafugua kuku.

Awali akifungua kongamano la Kisanyansi la Kitafiti ambapo Mada ilikuwa ni Mchango wa Chuo Kikuu MUHAS katika mapambano dhidi ya Malaria Tanzania lililofanyika jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Chuo Kikuu MUHAS, Prof Andrew Barnabas Pembe amewaomba watafiti kujitokeza kwa wingi kufanya tafiti zitakazoleta matokeo Chanya katika jamii yetu.

"Niwaombe watafiti wote kujitokeza kwa wingi kuungana na Chuo chetu Cha MUHAS ili tufanye  tafiti zenye tija ili kuweza kutatua matatizo mbali mbali kwa jamii," amesema.

Kongamano hilo la pili limehudhuriwa na watalaamu kutoka Wizara ya Afya, Shirika la Afya Duniani (WHO), SIDA Tanzania, Kituo cha Utafiti Ifakara, Mradi wa Taifa wa kuzuia Malaria pamoja na Vyuo mbali mbali na wadau wa Afya.
Share:

CHADEMA WAMJIBU NDUGAI,WADAI ANAONGOPEA BUNGE NA UMMA WA WATANZANIA


Ndugu wanahabari na watanzania wote, bila shaka mmemsikia Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Job Ndugai tarehe 31 /01/2019 akitoa taarifa bungeni au kile alichakuwa akikiita kuwa ni ufafanuzi juu ya malalamika ya malipo ya matibabu ya Mh Tundu Lissu (MB) wa Singida Mashariki na Mnadhimu mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni.


CHADEMA tunalazimika kumjibu Spika Ndugai kwa kuwa bila haya na kwa makusudi ameamua kuliongopea Bunge na umma wa Watanzania. Mh Tundu Lissu ametibiwa na Chama chake CHADEMA, wanachama mmoja mmoja,mashirika mbalimbali ya ndani na nje ya nchi, watanzania waishio ndani na nje na sambamba na hilo wabunge mmoja mmoja walichangia takribani Tsh 43 millioni kutoka katika posha zao kama walivyofanya watanzinia wengine.

Mh Lissu ni Mbunge halali wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa mujibu wa sheria ya bunge anastahili kulipwa mshahara wake wa kibunge na posha mbalimbali na pia kutibiwa na Bunge. 

Takribani Tsh. 207 million alizopatiwa Mh Lissu ni stahikl zake halali za kibunge na si pesa ya Matibabu kama Spika alivyoliongopea bunge na umma wa Watanzania. 

Spika amedai kuwa anazo nyaraka za uthibitisho wa malipo ya matibabu tunamtaka atoe hizo nyaraka hadharani .

Sisi Chama,Familia na Mh Lissu mwenyewe wote tuna nyaraka zote za Matibabu kwa kila hatua. Tunalitaka Bunge kulipia Matibabu ya Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa ni haki yake kisheria na si huruma kama anavyojaribu kuonyesha

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger