Saturday 25 February 2017

Rais Magufuli Ateua Mwenyekiti Wa Bodi Mamlaka Ya Masoko Ya Mitaji Na Dhamana

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli,  amemteua Dkt. John Kedi Mduma kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dkt. John Kedi Mduma umeanza tarehe 23 Februari, 2017.

Dkt. John Kedi Mduma ni Mhadhiri Mwandamizi, Idara ya Uchumi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Dkt. John Kedi Mduma anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bi. Grace Rubambey ambaye amemaliza muda wake.
***

Share:

mpya:Taarifa Kuhusu UTAPELI Ajira za JWTZ

Share:

Friday 24 February 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEB 24 2017

Share:

Mahakama Yamzuia RPC Kujibu Swali la Tundu Lissu

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imemzuia shahidi wa kwanza katika kesi inayomkabili Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na wenzake watatu, kujibu swali linalohusu mamlaka ya kikatiba ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC),  kufuta uchaguzi uliofanyika Oktoba 25,2015. Kwa mujibu wa Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba , swali hilo la Lissu halina mashiko.

Lissu alimuuliza shahidi ambaye ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Ilala, Salum Hamduni kwamba, Jecha Salim Jecha ana mamlaka gani kikatiba kufuta uchaguzi uliofanyika Oktoba 25, 2015.

Lissu alimuuliza Kamanda Hamduni kama anafahamu mamlaka yapi ya kikatiba ambayo Mwenyekiti wa ZEC, Jecha aliyatumia kufuta uchaguzi mkuu wa madiwani, wabunge na Rais.

Wakili wa Serikali, Paul Kadushi amedai kuwa shahidi huyo amekwenda mahakamani kutoa ushahidi kuhusu maelezo na kwamba si kutoa tafsiri ya kisheria kuhusu Katiba ya Zanzibar.

Kadushi amedai anapinga shahidi wake kujibu swali hilo kwamba Mwenyekiti wa ZEC ana mamlaka ya kufuta uchaguzi ama la na kueleza kuwa shahidi huyo hana ufahamu wa sheria na si mtaalamu wa Katiba na sheria.

''Napinga shahidi kujibu swali hili ambalo kimsingi linamtaka atafsiri sheria, jambo ambalo silo lililomleta na wala hana utaalamu wa kisheria. Hata hivyo, mahakama hii haina mamlaka ya kutafsiri Katiba isipokuwa ni mahakama ya kikatiba na mahakama kuu ndio yenye uwezo huo,'' alidai Kadushi.

Lissu alipinga hoja hizo kwa maelezo kwamba, pingamizi la wakili wa serikali halina maana kwa sababu suala la mamlaka halali au si halali ya Zanzibar limeletwa na upande wa mashitaka wenyewe, kama ambavyo mashitaka ya pili katika kesi hiyo wameeleza kuwa habari iliyochapishwa ingeweze kuleta chuki kwa Wazanzibar kuichukia nchi yao.

Alidai kuwa, masuala ya mamlaka wameyaleta wenyewe wanapaswa kukabiliana nayo, kwa kuwa Sheria ya Ushahidi namba 147, kifungu kidogo cha pili na Sheria namba 157 ya sheria hiyo, vinaweka wazi kwamba shahidi anaweza kuulizwa swali lolote na kwamba si lazima liwe ndani ya kile anachokitolea ushahidi.

Hakimu Simba amesema, mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kuzungumzia Katiba ya Zanzibar.

Amesema mahakama katika kesi hiyo haitazungumzia uhalali au kutokuwa halali kwa Mwenyekiti wa ZEC, Salim Jecha kufuta au kutofuta uchaguzi mkuu Zanzibar.

"Pingamizi la upande wa mashitaka ambao ulipinga masuala ya kikatiba ambayo mbunge huyo alikuwa akimuuliza shahidi kuhusu Jecha ana mamlaka gani kikatiba kufuta uchaguzi uliofanyika Oktoba 25, 2015, ni sahihi na shahidi hatakiwi kujibu swali hilo," amesema Hakimu Simba.

Lissu amedai uamuzi huo hautamuathiri na kwamba anakubaliana nao kwamba haruhusiwi kuuliza swali hilo kwa shahidi hivyo waendelee na ushahidi.

Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Machi 8 na 9, mwaka huu na kuutaka upande wa mashitaka kupeleka mashahidi ili kesi iishe kwa kuwa watu wengi wanaifuatilia hivyo iishe waendelee na shughuli za maendeleo.

Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Mhariri wa gazeti la Mawio, Simon Mkina, mwandishi wa gazeti hilo, Jabir Idrisa na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehboob.

Wanadaiwa kati ya Januari 12 na 14, mwaka huu, Dar es Salaam, kwa lengo la kuleta chuki kwa wananchi wa Zanzibar, Jabir, Mkina na Lissu, kwa pamoja waliandika na kuchapisha taarifa‎ za uchochezi zenye kichwa cha habari kisemacho, 'Machafuko yaja Zanzibar'.

Katika mashitaka yanayomkabili Mehboob, anadaiwa kuwa, Januari 13 katika jengo la Jamana, Dar es Salaam, alichapisha gazeti la Mawio lililokuwa na taarifa za uchochezi, pia alichapisha gazeti hilo bila ya kuwasilisha hati ya kiapo kwa Msajili wa Magazeti.
Share:

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Chaipinga TCU.,Chasema Hakijawahi Dahili Wanafunzi Vilaza

Share:

Wednesday 22 February 2017

Tcu: Orodha ya Vyuo na Majina ya wanafunzi waliokosa sifa za kupewa nafasi za vyuo Tanzania 2016/2017


 Image result for tcu tz
Share:

Mahakama Yamkingia Kifua Mbowe,Yaamuru Asikamatwe

Mahakama  Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetoa zuio la muda kuzuia Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe asikamatwe na Polisi hadi maombi yake, aliyoyaomba ya kutaka asikamatwe, yatakaposikilizwa kesho.

Katika kesi hiyo ya kikatiba namba 1 ya mwaka 2017, Mbowe anapinga mamlaka ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, Simon Sirro na Mkuu wa Upelelezi wa kanda hiyo (ZCO), Camilius Wambura, ya kutaka kumkamata hadi maombi hayo yatakaposikilizwa.

Maombi ya kesi hiyo yataanza kusikilizwa Februari 23, mwaka huu saa 7:30 mchana katika chumba cha wazi cha mahakama ili kuruhusu watu mbalimbali kusikiliza kesi hiyo.

Jopo la majaji watatu likiongozwa na Sekieti Kihiyo akisaidiana na Jaji Lugano Mwandambo na Jaji Pellagia Kaday lilitoa zuio hilo, hata hivyo walisema Polisi wanaweza kumuita Mbowe kwa mahojiano pindi watakapomhitaji.

Kesi hiyo ambayo ilisikilizwa kwa vipindi vitatu kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana, mahakama iliamuru upande wa wadai ambao uliongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu, kurekebisha maombi yao kwa kuwa hawakumuingiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) licha ya kuishitaki serikali.

Hali hiyo ilitokana na mawakili wa upande wa wadai, Lissu ambaye alipinga kitendo cha Mwanasheria wa Serikali, Gabriel Malata kuwatetea wadaiwa hao ambao ni RC, RPC na ZCO katika kesi hiyo kwa kuwa hawajaitaja serikali.

Akijibu hoja hiyo, Malata alidai kuwa waliofunguliwa madai hayo sio Makonda, Sirro wala Wambura, bali ni serikali hivyo ana mamlaka yote ya kuwawakilisha.

Baada ya pande zote kuwasilisha hoja zake, mahakama ilimruhusu Malata kuendelea kusikiliza kesi hiyo ambapo pia iliagiza upande wa wadai kufanya marekebisho ya maombi hayo na kumuongeza AG kama mdaiwa.

Hata hivyo, Lissu aliomba waruhusiwe kufanya marekebisho hayo kwa kumuongeza AG, ombi ambalo halikuwa na pingamizi.

‘’Tutafanya marekebisho ya maombi yetu na marekebisho mengine madogo madogo kwa namna tutakavyoona inafaa siku ya Jumatatu na tutawapa wajibu maombi Machi 6 mwaka huu na Machi 8 mwaka huu itatajwa kwa ajili ya kusikiliza maombi hayo,’’ alidai Lissu.

Mbowe aliwasili mahakamani hapo akiwa na gari lenye usajili namba T 830 aina ya Land Cruiser, saa chache kabla ya kesi yake kuitwa katika chumba namba 64 kwa ajili ya kusikilizwa.

Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai mkoani Kilimanjaro, alifika mahakamani hapo baada ya kutoka Kituo Kikuu cha Polisi saa 7 usiku, alikokuwa anahojiwa na kupekuliwa kuhusu sakata la dawa za kulevya.

Aidha, viongozi mbalimbali wa chama hicho wakiwemo Mbunge wa Kibamba, John Mnyika, Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, madiwani na wafuasi wao walijitokeza kwa wingi, kusikiliza kesi hiyo huku wakifurahia amri ya mahakama ya kuzuia kutokamatwa kwa mwenyekiti huyo.

Katika kesi ya msingi, Mbowe anaomba mahakama iwazuie wadaiwa kutekeleza azma yake ya kumtia mbaroni, pia itoe amri ya kuwazuia kumkamata hadi hapo kesi hiyo ya kikatiba, itakapomalizika na kwamba polisi wasiendelee na mchakato wowote dhidi yake hadi hapo kesi hiyo itakapomalizika.

Anadai kuwa sheria inayompa Mkuu wa Mkoa mamlaka ya kutoa amri ya kumkamata na kumweka ndani mtu, iko kinyume cha katiba, kwa madai kuwa ilitungwa katika mazingira ambayo hapakuwa na vituo vya polisi vya kutosha.

Pia anadai kuwa kwa mazingira ya sasa, sheria hiyo imeshapitwa na wakati na anaiomba mahakama itamke kuwa ni kinyume cha katiba.

Mbowe pia anadai kuwa hata kama Mkuu wa Mkoa alikuwa anatekeleza mamlaka yake kwa mujibu wa sheria hiyo, basi hakutimiza matakwa ya kisheria, ambayo ni pamoja na kutoa taarifa kwa Hakimu wa Mahakama ya Wilaya au ya Hakimu Mkazi.

Vile vile, anaiomba mahakama kama itaona kuwa Mkuu wa Mkoa alikuwa sawa kutoa amri hiyo, basi imwamuru afuate matakwa ya kisheria, ikiwa ni pamoja na kulinda haki za binadamu katika kutekeleza madaraka yake hayo.
Share:

TCU: ORODHA YA WANAFUNZI WASIO NA SIFA KATIKA VYUO VYA ELIMU YA JUU 2016/2017

TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA
Image result for tcu tz
TAARIFA KWA UMMA
WANAFUNZI WASIO NA SIFA KATIKA VYUO VYA ELIMU YA JUU
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inautangazia Umma kuwa zoezi la uhakiki wa sifa za wanafunzi wanaondelea na masomo kwenye Vyuo vya Elimu ya Juu nchini kwa mwaka 2016/2017 limekamilika katika baadhi ya vyuo. Katika kutekeleza zoezi hilo Tume imebaini kuwa kuna wanafunzi ambao wamedahiliwa katika programu ambazo hawana sifa.
Orodha ya wanafunzi wasio na sifa imeshawasilishwa kwenye vyuo husika. Hivyo, wanafunzi wote wanaondelea na masomo kwenye Vyuo vya Elimu ya Juu nchini wanaweza kutazama matokeo ya uhakiki wao kupitia kiunganisho (link) (Bonyeza Uhakiki wa Sifa za Udahili).
Tume inawaarifu wanafunzi wote ambao majina yao yameorodheshwa wawasiliane na vyuo vyao ili kuthibitisha sifa zao kabla ya tarehe 28 Februari 2017. Wanafunzi ambao hawatafanya hivyo hawatatambuliwa na Tume na hivyo kukosa sifa za uanafunzi.
TCU inatoa rai kwa wanafunzi wote kutembelea tovuti ya Tume (www.tcu.go.tz) mara kwa mara ili kupata taarifa mpya kuhusu uhakiki wa sifa za wanafunzi.
Imetolewa na
Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania

20/02/2017
Share:

Ridhiwani Kikwete ajibu shutuma ya kutajwa kwenye orodha ya watuhumiwa wa dawa za kulevya

Mbunge wa jimbo la Chalinze mkoani Pwani kwa tiketi
Share:

WANAWAKE 13 WAHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA 2 KWA KOSA LA KUJIUZA HUKO MOROGORO

 Dada poa hao wakitoka  ser
o ya Mahakama ya Nunge wakipanda Difenda  kuelekea Magereza.
Share:

WANAOSOMA CHINA KUISOMA NAMBA,SERIKALI YASISITIZA KUSITISHA FEDHA ZA MIKOPO KWA WANAFUNZI WANAOSOMA NCHINI CHINA

Serikali kupitia wizara ya elimu,sayansi na teknolojia imesisitiza kusitisha pesa za mikopo ya nauli za kwenda masomoni na malipo mengine yote yaliyokuwa yanatolewa kwa wanafunzi wanapata ufadhili wa masomo kutoka kwa nchi rafiki ikiwemo nchi ya China.
Kauli hiyo imetolewa kupitia barua(ya tarehe 7,February,2017) iliyoandikwa na wizara ya elimu ,sayansi na teknolojia kwenda ubalozi wa Tanzania chini China wakati wakijibu barua iliyoandikwa na wanafunzi wanaosoma nchini china kuomba serikali kuangalia vizuri maamuzi hayo.
Takribani miezi miwili iliyopita,Bodi ya mikopo (HESLB) iliauandikia barua ubalozi wa Tanzania nchini china kuueleza maamuzi ya serikali kusitisha utoaji wa fedha za nauli kwa wanafunzi hao.Lakini wanafunzi hao hawakuridhika na maamuzi hayo hivo kuamua kuiandikia barua wizara ya elimu kuangalia vizuri maamuzi hayo.
 
Kwa mujibu wa barua hii ,wanafunzi watatakiwa kujigharamia wenyewe gharama za kwenda na kurudi masomoni kitu ambapo awali walikuwa wanapatiwa na serikali ya Tanzania.
Hii hapa barua mpya uliyosisitiza kutotoa pesa hizo na nauli kwa wanafuni hao
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO FEBRUARY 22,2017

Share:

Tuesday 21 February 2017

 HIZI HAPA HABARI KALI SIKU YA LEO JUMANNE FEB 21 2017

 

MBOWE APEKULIWA USIKU ARUDISHWA POLISI,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>https://goo.gl/T5jbX8 

 

MAGAZETI YA LEO JUMANNE FEB TAREHE 21.2.2017,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>https://goo.gl/PHqMKK


SHAMSA FORD AMLILIA MUMEWE ALIEKAMATWA KWA KESI YA MADAWA YA KULEVYA,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>https://goo.gl/6s58nV


NECTA YAWATAKA WANANCHI KUPUUZA TAARIFA ZILIZOTOLEWA KUHUSU MCHUJO KIDATO CHA KWANZA,SOMA ZAIDI HAPO>>>>https://goo.gl/gmq5ds


AUDIO | Shamba Darasa(Mkubwa na Wanawe) - Mwanamke | Download,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>https://goo.gl/Ce1kdr 

 

Mahaba Niue!! MZEE WA MIAKA 98 AFUNGA NDOA NA BIBI WA MIAKA 88,SOMA ZAIDI HAPO>>>https://goo.gl/pU13e0

 

 

Share:

Mahaba Niue!! MZEE WA MIAKA 98 AFUNGA NDOA NA BIBI WA MIAKA 88



Mzee Willy Kinyua (98) amefunga ndoa na Joyce Nyambura (88) baada ya wenza hao kuishi pamoja kwa zaidi ya miaka 60.
Share:

AUDIO | Shamba Darasa(Mkubwa na Wanawe) - Mwanamke | Download


Share:

NECTA YAWATAKA WANANCHI KUPUUZA TAARIFA ZILIZOTOLEWA KUHUSU MCHUJO KIDATO CHA KWANZA

Share:

SHAMSA FORD AMLILIA MUMEWE ALIEKAMATWA KWA KESI YA MADAWA YA KULEVYA

Mwigizaji Shamsa Ford ambaye ni mke wa Mfanyabiashara Chidi Mapenzi aliyeitwa Polisi kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya, ameandika yafuatayo ikiwa ni mara ya kwanza toka aitwe Polisi kuhojiwa.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger