Friday 20 January 2017

KACHUMBARI YAUA MKE MJINI SHINYANGA

MKAZI wa mtaa wa Mageuzi, kata ya Ngokolo, manispaa ya Shinyanga, Ibrahimu Daniel (42) amemuua mke wake, kwa kushindwa kuhifadhi vizuri kachumbari na kupika mboga isiyo na kiwango.
Share:

RATIBA YA KUHAMIA DODOMA IPO PALEPALE

 
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama amesema ratiba ya kuhamia Dodoma kwa mawaziri, manaibu, makatibu wakuu na manaibu iko palepale.

Amesema watakaoshindwa kufanya hivyo, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa atatoa mwongozo. Jenista alisema jana kuwa baada ya Februari 28, mwaka huu kutafanyika tathimini na kuangalia utekelezaji wake umefikia wapi, na kwamba kwa wale ambao hawatatekeleza agizo hilo, Waziri Mkuu Majaliwa atatoa mwongozo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Jenista alisema uamuzi ulitolewa na Rais John Magufuli uko palepale.

Alisema hata Waziri Mkuu amekuwa akisisitiza ratiba ya kuhamia Dodoma kwa awamu ya kwanza Februari mwaka huu ambayo itahusisha mawaziri, manaibu mawaziri, makatibu wakuu na manaibu wao na baadhi ya watumishi wa wizara.

"Kazi yetu itakuwa ni kuangalia utekelezaji utakuwa umefikia wapi na asiyetekeleza Waziri Mkuu atatoa mwongozo,” alisema Jenista.

Pia alisema amekuwa akikagua nyumba ambazo zinafanyiwa ukarabati kwa ajili ya watumishi watakaohamia Dodoma ikiwemo nyumba za Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) eneo la Kikuyu, ambapo ukarabati wake unaendelea vizuri.

Alisema nyumba hizo za ghorofa, zitawezesha baadhi ya watumishi kupata nyumba za makazi, ambapo pia taasisi nyingine zinaendelea na ujenzi wa nyumba za watumishi.
Julai mwaka jana, Rais Magufuli alitangaza kuhusu serikali yake kuhamia Dodoma kabla ya kumalizika kwa muhula wake wa kwanza wa miaka mitano, na tayari Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alikwisha kuhamia katika makao makuu hayo ya nchi yaliyotangazwa mwaka 1973.

Akiahirisha Mkutano wa Nne wa Bunge la 11 mwishoni mwaka jana, Waziri Mkuu Majaliwa alisema serikali itahamia Dodoma kwa awali, na kueleza kuwa awamu ya kwanza itakuwa kati ya Septemba 2016 hadi Februari, 2017 ikiwahusisha Waziri Mkuu, mawaziri, makatibu wakuu, manaibu makatibu wakuu na walau idara mbili za kila wizara.

Alisema awamu ya pili itakuwa Machi 2017 hadi Agosti 2017, ya tatu Septemba 2017- Feb 2018, ya nne Machi 2018- Agosti 2018, na ya tano Septemba 2018-Februari 2019; na kwamba awamu hizo zitatumika kwa ajili ya kuendeleza mchakato wa kuhamisha watumishi hadi wote wawe wamehamia Dodoma.

Share:

VIDEO | Isha Mashauzi & Mashauzi Classic - Kismet | Watch/Download

Share:

WANAFUNZI WANAOSOMEA DIPLOMA KUANZA KUPEWA MIKOPO KUTOKA BODI YA MIKOPO

http://www.habarileo.co.tz/images/resized/images/frequent/joyce-ndalichako2_210_120.jpg
SERIKALI imewasilisha pendekezo la mabadiliko ya Sheria ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ili kuwezesha wanafunzi wanaochukua Stashahada katika vipaumbele vya kitaifa, kupewa mikopo ya kuwawezesha kuchukua elimu husika.
Share:

MAGAZETI YA LEO IJUMAA TAREHE 20.1.2017

Share:

Thursday 19 January 2017

Maiti iliyozikwa na Kisha Baadae Kukutwa Iko Nyumbani Kitandani Yazikwa Tena Chini Ya Ulinzi Mkali wa Polisi

Share:

PICHA: Rais Magufuli Alivyomuapisha Profesa Ibrahim Hamisi Juma Kuwa Kaimu Jaji Mkuu Wa Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Profesa Ibrahim Hamisi Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam  Jumatano Januari 18, 2018.  Anayeshuhudia kushoto ni Jaji Mkuu mstaafu Mohamed Chande Othman. 

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimkabidhi nyenzo za kazi baada ya kumuapisha Profesa  Ibrahim Hamisi Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam  Jumatano Januari 18, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimpongeza baada ya kumuapisha Profesa  Ibrahim Hamisi Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Januari 18, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan  na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Katibu Mkuu Wizara ya Sheria na Katiba Profesa Sifuni Mchome na Naibu wake Mhe. Amon Mpanju wakiwa katika picha ya pamoja na majaji wa mahakama ya Rufaa, Majaji wa Mahakama kuu baada ya kumuapisha Profesa  Ibrahim Hamisi Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam  Jumatano Januari 18, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, katika picha ya pamoja na majaji wa mahakama ya Rufaa na Majaji wa Mahakama kuu baada ya kumuapisha Profesa  Ibrahim Hamisi Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam  Jumatano Januari 18, 2018. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, katika picha ya pamoja na watendaji wa Mahakama baada ya kumuapisha Profesa  Ibrahim Hamisi Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam  Jumatano Januari 18, 2018.
Share:

Waziri Mkuu Amaliza Mgogoro Wa Mpaka Kilindi Na Kiteto,Awaonya viongozi wa siasa wasiwavuruge wananchi

Share:

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARY TAREHE 19.1.2017

Share:

JESHI LA SENEGAL KUIVAMIA GAMBIA USIKU WA KUAMKIA LEO ILI KUMNG'OA RAIS YAHYA JAMMEH ALIEOGOMA KUACHIA MADARAKA

Jeshi la Senegal limesema kuwa majeshi ya Afrika Magharibi yataingilia suala la Gambia usiku wa kuamkia tarehe ya mwisho wa madaraka ya Rais Yayha Jammeh ambayo ni leo  ili akabidhi madaraka kwa mshindi wa uchaguzi mkuu uliofanywa mwezi uliopita.

Vikosi kutoka Senegal vimesogea katika mipaka ya Gambia, Nigeria pia imetuma vikosi vya anga katika eneo hilo.

Rais wa Mauritania Mohamed Ould Abdel Aziz yuko nchini Gambia kwa kile kilichotajwa kuwa ni juhudi za mwisho za kumshauri bwana Jammeh kuachia madaraka kwa Rais mteule wa Gambia Adama Barrow ambaye kwa sasa yuko nchini Senegal.

Senegali imeomba Jumuiya ya Usalama ya Umoja wa Mataifa kushinikiza Umoja wa nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) kuchukua hatua za msingi katika kuhakikisha Rais mteule wa Gambia anakabidhiwa madaraka.
Chanzo: BBC
Share:

Wednesday 18 January 2017

AUDIO | Bill Nass Ft. Mwana FA - Mazoea | Download

Share:

Tuesday 17 January 2017

Nogesha Upendo Ya Vodacom Yaja Na Tsh Bilioni 32 Za M-pesa

Wakati wateja na wananchi mbalimbali wakiendelea kunufaika na promosheni ya Nogesha Upendo ya Vodacom katika kujishindia mamilioni ya fedha kila siku pindi wanunuapo vifurushi kwenye simu zao, sasa malipo ya faida ya kutumia M-Pesa ambayo yameanza wiki hii yanaufanya mwanzo wa mwaka mpya kuwa mzuri zaidi kwa mamilioni ya wateja na mawakala wa M-Pesa.

Awamu hii ya malipo ya faida ya utumiaji wa M-Pesa inafikia jumla ya Tsh Bilioni 32/- na itawawezesha watumiaji wa M-Pesa kuuanza mwaka vizuri ambapo kila mtumiaji atapata sehemu ya gawio kulingana na matumizi ya akaunti yake ya M-Pesa. Malipo haya yanafanyika kwa awamu na yatawanufaisha wateja na mawakala wa M-Pesa waliopo kila kona ya Tanzania. Ikiwa ni mwendelezo wa mtandao huo kuwarudishia faida ya gawio hilo kampuni hiyo  imekwishagawa zaidi ya Tsh Bilioni 39 katika awamu zilizopita. Hii inamaanisha kwamba awamu hii itakapokamilika, ni zaidi ya Tsh Bilioni 70 zitakuwa zimewekwa moja kwa moja kwenye mifuko ya wateja wetu.

“Ugawaji huu wa faida ya kutumia M-Pesa kwa wateja na mawakala wetu ni muendelezo wa dhana kuu ya promosheni yetu ya”Nogesha Upendo”. Kila mtumiaji wa M-Pesa atapata pesa ya ziada kwenye akaunti yake, ambayo atakuwa na uhuru wa kuitumia vyovyote anavyopenda kama kununua vifurushi, kulipia huduma na bidhaa au kuwatumia ndugu na jamaa zake. Mteja mwenye matumizi makubwa kwenye M-Pesa, anapata gawio kubwa “zaidi la faida” Alisema Ian Ferrao, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania.
Kuona kiasi cha gawio lako, tuma SMS yenye neno KIASI kwenda 15300. Utapokea SMS inayoonesha kiasi cha pesa kitakachotumwa kwenye akaunti yako. Vifurushi vya Cheka, Intaneti na YaKwakoTu vinaweza kununuliwa kwa kutumia gawio hili la faida. Kununua vifurushi kwa kutumia pesa uliyopokea, Piga *150*00# chagua NUNUA MUDA WA MAONGEZI/VIFURUSHI kisha chagua kifurushi unachohitaji.

Promosheni ya Nogesha Upendo ipo kwenye wiki ya 7 sasa ambapo zaidi ya wateja 200 washajishindia Tsh Milioni 1 pesa taslimu na 600 wengine wameshashinda Tsh 100,000/- za kila siku. Kuendelea kuongeza nafasi za kushinda zawadi za siku na wiki za hadi Tsh Milioni 1/- mteja anatakiwa kununua kifurushi chochote cha Vodacom ambapo ataingia kwenye droo moja kwa moja.
Share:

Magazeti Ya Leo Jumanne ya January 17 2017


Share:

Monday 16 January 2017

HII HAPA TAARIFA KAMILI KUHUSU MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2016


Share:

Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya January 16 2017




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger