Monday 2 January 2017

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARY TAREHE 2.1.2017

Share:

LOWASA APONGEZA USHINDI WA TRUMP

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, amewapongeza raia wa Marekani kwa kumchagua Donald Trump kuwa rais mpya wa nchi hiyo.

Kwa mujibu wa Lowassa, Trump atakuwa rais mwenye kufanya uamuzi mgumu kwa kuwa ni shupavu na ana uwezo.

Trump ambaye ni Rais Mteule wa Marekani, alichaguliwa kuwa Rais mpya wa Marekani baada ya kumshinda mpinzani wake, Hillary Clinton, mwishoni mwa mwaka jana.

Lowassa aliyasema hayo jana katika misa maalumu ya shukrani ya mwaka mpya 2017 iliyoshirikisha madhehebu mawili ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Monduli na Kanisa Katoliki, wilayani Monduli, Mkoa wa Arusha.

Ibada hiyo, ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo wa Serikali na wa vyama vya siasa, wakiwamo Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro ambaye pia ni Katibu wa Chadema, Mkoa wa Arusha.

“Wamarekani hawakufanya makosa kumchagua Trump kwani anaonekana kuwa na uwezo mkubwa wa kuongoza Taifa hilo tajiri duniani ambalo linategemewa na mataifa mengine.

“Dunia imebadilika, amechaguliwa rais mmoja huko Marekani ambaye ni mwamba kweli kweli.

“Hatuwezi kumtabiri mambo yake yatakavyokuwa, lakini inabidi kila mtu afanye kazi kwa bidii na kwa maarifa kwa sababu huyo hakubali upuuzi wowote,”alisema Lowassa.

Lowassa ambaye pia aliwahi kuwa Mbunge wa Monduli kwa miaka 20, aliwataka wananchi kufanya kazi kwa bidii na kuacha kulalamika kwani hiyo ndiyo njia iliyo sahihi ya kuweza kuondokana na umasikini.

“Mwaka jana, tarehe kama hii, tulimuaga Mbunge Julius Kalanga na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Monduli, Isack Joseph, nikawaambia nawatakia heri wachape kazi vizuri, naona wamefanya vizuri au siyo?alihoji Lowassa.

Akizungumzia upande wake, Lowassa alisema hivi sasa anafanya siasa za kimataifa tofauti na siasa alizokuwa akifanya kipindi kilichopita.

“Mimi sitaki kusema sana maana watasema napiga siasa. Siku hizi napiga siasa za kimataifa, naomba niwatakie heri ya mwaka mpya na kila mtakachoshika, Mungu akibariki kiwe dhahabu,”alisema
Share:

Tulia: Tanzania mpya inawezekana

Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson amesema kuwa Tanzania mpya yenye matokeo chanya kwa mwaka 2017 iwapo inawezekana  iwapo kila mmoja wetu atafanya kazi kwa bidii ili kuliletea taifa maendeleo.

Ameyasema hayo wakati wa ibaada maalum  ya mkesha wa kitaifa wa mwaka mpya uliofanyika katika uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam, Dk. Tulia amewataka watanzania kuwa na ushirikiano wa pamoja ili kufikia maendeleo.

“Tanzania mpya na nchi mpya yenye matokeo chanya kwa mwaka 2017 inawezekana hivyo tushirikiane kwa pamoja na kila mmoja akifanya kazi kwa bidii, lazima maendeleo yatapatikana tu”amesema Dk. Tulia.

Aidha, amewataka watanzania kuendelea kutoa ushirikiano kwa viongozi wa serikali ili waweze kupata maendeleo kwa haraka zaidi.
Share:

Sunday 1 January 2017

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARY TAREHE 1.1.2017

Share:

MWANAFUNZI AUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA MFANYABIASHARA TARIME



MFANYABIASHARA Robert Mwikwabe, maarufu kama Ndugu, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumpiga risasi ya kichwani na kusababishia kifo papo hapo mwanafunzi wa kidato cha tatu wa shule ya sekondari Sirari, Masaite Mrimi(17).
Kutokana na tukio hilo, Mwikwabe ambaye pia ni mmliki Hoteli katika mji mdogo wa Sirari wilayani Tarime mkoani Mara, alinusurika kuteketezwa yeye na familia yake Hali hiyo ilitokea baada ya wananchi kuamua kuchoma moto lori la mfanyabiashara huyo na kwenda nyumbani kutaka kuchoma hoteli.
Mashuhuda walisema tukio hilo ni la juzi mchana, jirani na nyumba anayoishi mwanafunzi huyo, eneo la stendi mpya ya mabasi na malori ya Ngerengere.
Walisema mfanyabiashara huyo alifika akiwa na lori lake likiwa na mawe na alisimama na kutaka kuchukua pumba za mchele, zilizomwagwa na malori yanayosafirisha ng’ombe kwenda nchini Kenya.
Eneo hilo ni jirani na nyumbani kwao marehemu, ambako kulitokea mzozo kati ya Robert na wazazi wa mwanafunzi huyo. Kufuatia mzozo huo, mwanafunzi huyo aliyekuwa na panga mkononi, alimtishia kumkata Robert, ambaye alichomoa silaha yake aina ya bastola na kumpiga risasi kichwani na kumsababisha kifo.
Baada ya tukio hilo, familia ya marehemu na wananchi walianza kumfukuza Robert aliyeacha lori lake likiwa na mawe na kukimbilia lori lake lingine la jirani. Kisha alikimbilia Kituo cha Polisi Sirari, kuokoa maisha yake.
Umati mkubwa wa watu kutoka vijiji vya Ngerengere na Sirari, walikwenda nyumbani kwa mfanyabiashara huyo kwa lengo la kutaka kuchoma moto hoteli na nyumba.
Lakini, polisi na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorius Luoga walifanya juhudi kubwa kuwazuia wananchi hasa vijana, kuacha kuteketeza mali za mfanyabiashara huyo yakiwemo magari, ambayo sasa yamehifadhiwa kituo cha polisi kwa ajili ya usalama.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Tarime-Rorya, Andrew Satta alithibitisha kutokea kwa kifo cha mwanafunzi huyo na kwamba maiti imehifadhiwa katika hospitali ya wilaya Tarime.
Share:

ATUMBUKIA GHAFLA KWENYE CHEMBA YA MAJI TAKA YENYE UREFU WA FUTI 12 DAR


Mkazi wa Temeke Mikoroshoni, Miradji Sanyero, jana alipatwa na mkasa wa kutumbukia katika ‘chemba’ ya kupitishia maji taka yenye urefu zaidi ya futi 12, iliyopo eneo la Bakhresa, Tazara, Barabara ya Mandela jijini Dar es Salaam.
Alipatwa na mkasa huo akiwa katika harakati ya kujitafutia maisha, ambapo ghafla alitumbukia katika chemba hiyo iliyokaa vibaya katika mlango mkuu unaotumiwa na magari makubwa wa ofisi za Bakhresa.
Akijojiwa, akiwa mahututi, alisema “Nilikuwa napita jirani huku nikichukua tahadhari nisigongwe na magari yanayoingia na kutoka katika ofisi hizo, ndipo nikajikuta ghafla nimetumbukia ndani ya chemba hii na kuumia kidole cha mkono wa kulia, miguuni na mbavu ambazo sasa zinauma sasa”.
Wafanyabiashara wadogo (machinga) wa eneo hilo, walisema chemba hiyo ni hatari na watu kadhaa wametumbukia katika kipindi cha hivi karibuni. Walidai huyo alikuwa mtu wa tatu.
“Tunaomba Tanroads wafike eneo hili, waone kisha wazibe chemba hii. Kama hawatafanya hivyo, kuna hatari ya kupoteza maisha hasa watoto wadogo ambao uwezo wao wa kuhimili vishindo ni mdogo sana” alisema machinga mmoja, Ali Tematema.
Gazeti hili lilishuhudia baadaye trafiki wakishirikiana na wananchi, wakimsaidia Sanyero kwenda kupanda bajaji kwenda Polisi kuchukua Fomu Namba 3 ili aende hospitali kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.
Chanzo-Habarileo
Share:

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MWANDISHI WA HABARI KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA AGIZO LA DC KAHAMA


 


TAARIFA KWA UMMA

UONGOZI wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Shinyanga (SPC),na baadhi ya waandishi wa habari wilayani Kahama,wamekutana na mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu ili kupata muafaka wa tatizo la kukamatwa na kufikishwa mahakamani mwandishi wa habari wa kujitegemea Paul Kayanda.

Kikao hicho cha usuluhishi kilichofanyika leo Jumamosi Desemba 31,2016 katika ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo,kimehudhuriwa pia na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya ya Kahama. 


Kayanda alikamatwa jana Desemba 30,2016 na kufikishwa mahakamani kwa agizo la Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu akimtuhumu kuandika habari za kumdhalilisha na kuzisambaza kwenye barua pepe mbalimbali za vyombo vya habari.


Katika kikao ,Uongozi wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga ,ulimuomba mkuu wa wilaya Nkurlu kutaka kufahamu kilichomsukuma kuchukua maamuzi hayo,na nini ushauri wake juu ya suala hilo lakini pia kumsikiliza mwandishi Paul Kayanda.


Baada ya kusikiliza pande zote mbili,kikao kilibaini kuwepo kwa mapungufu katika habari iliyoandikwa na Kayanda kuhusu habari ya laptop mbili zilizoibiwa nyumbani kwa mkuu huyo wa wilaya.

Mkuu huyo wa wilaya alikiri kuwepo kwa tukio la wizi nyumbani kwake lakini mwandishi huyo aliandika habari kwa kuingilia uhuru binafsi wa kiongozi huyo akielezea watu wanaoingia na kutoka nyumbani kwake lakini maisha anayoishi na kijana wake.


Kwa kuangalia maslahi mapana ya umma kutokana na kutegemeana katika kusukuma maendeleo ya jamii baina ya uongozi wa serikali na waandishi wa habari ,kikao kimemtaka Kayanda kumwomba radhi mkuu huyo wa wilaya kwa kuingilia uhuru wake binafsi na kuuhusisha na habari ya wizi wa laptop badala ya kujikita kwenye tukio la wizi wa laptop pekee.


Kikao pia kimebaini kuwa pamoja na mapungufu ya mwandishi, ni ukweli ulio wazi kuwa mkuu huyo wa wilaya aliibiwa kompyuta mpakato (lap top) mbili nyumbani kwake na kuagiza vijana watatu wakamatwe kwa mahojiano polisi akiwemo mmoja anayeishi nyumbani kwake japo ameelezea kuwa hakujua walishikiliwa kwa siku ngapi.


Mkuu huyo wa wilaya pia alieleza kukerwa na ujumbe mfupi wa maandishi kwa njia simu ya mkononi (sms) alizodai kutumiwa na Kayanda kwa kutumia simu nyingine (tofauti na anayotumia) zenye lugha ya kumtuhumu na kumdhalilisha.

Hata hivyo kikao hakikuona kuwepo kwa ushahidi wa moja kwa moja kuthibitisha kama ni za mwandishi huyo kweli au la huku kikao kikiomba sms hizo zifuatiliwe ili wamiliki wa namba hizo wajulikane .


Baada ya kujadiliana kwa kina katika kikao hicho kilichodumu kwa muda wa saa mbili,Kayanda amemwomba mkuu wa wilaya msamaha kwa mapungufu yaliyojitokeza katika habari hiyo aliyoiandika, na mkuu wa wilaya ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Kahama amekubali kumsamehe mwandishi huyo akiahidi kufuata taratibu zingine kuondoa kesi mahakamani na kutaka kusafishwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ilikoandikwa habari hiyo.


Nkurlu amesema anatambua kazi nzuri inayofanywa na waandishi wa habari wilaya ya Kahama na mkoa wa Shinyanga kwa ujumla katika kuandika habari zinazohusu serikali na akaomba kudumishwa kwa ushirikiano uliopo baina ya viongozi wa serikali na waandishi wa habari ili kusaidia kuharakisha maendeleo ya wananchi huku akiwasisitiza waandishi wa habari kuzingatia weledi katika kazi zao.

Aidha Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga imewasisitiza waandishi wa habari kuzingatia weledi na kufuata maadili katika kutekeleza majukumu yao ili kuepuka migongano isiyokuwa na tija kwa umma.

Pia tunawashauri wadau wote wa habari pindi inapotokea kuingia katika mgogoro wowote ama na waandishi wa habari au chombo cha habari si vyema kwenda mahakamani moja kwa moja bali wawasiliane na viongozi wa klabu za waandishi wa habari katika mkoa husika ili kusuluhishana na kuwekana sawa.

Imetolewa na 

Kadama Malunde

MWENYEKITI –SPC

Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu,waandishi wa habari na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Kahama wakiwa katika kikao cha usuluhishi
Waandishi wa habari wakiwa katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kahama
Kikao kinaendelea
Waandishi wa habari wakiondoka katika ofisi ya mkuu wa wilaya baada ya kikao kumalizika

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0757478 553 ,0625 918 527

Malunde1 blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari kwa urahisi zaidi
 Bofya Hapa
Share:

Soma habari hizi pia:

TAFUTA HABARI HAPA

Harusi- Itendele Mchenya

HABARI KALI ZAIDI 2016

Kali ya Mwaka: NYOKA WA MAAJABU AFA NA MTU WAKE,ALIKUWA AMEMBEBA KWENYE NGUO YAKE

NB-Siyo nyoka aliyeuawa DUNIANI kuna mambo, ndivyo unaweza kusema kutokana na mkazi wa Mtaa wa Mateka, Manispaa ya Songea, Denis K...

Tazama Video Hapa

 Bofya Hapa

Ngoma ya Asili:MANJU MATEMBA IGOMWASHU -BENI

HABARI KALI MWEZI HUU

UNGANA NASI HAPA

MAKTABA YETU

Instal Malunde1 blog kwenye simu yako

 Bofya Hapa

Translate This Blog

Powered by Google TranslateTranslate
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger