Friday 2 December 2016

Godbless Lema Anyimwa Dhamana Kwa Mara Nyingine Tena

Mahakama Kuu Kanda ya Arusha imemnyima dhamana Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA) Godbless Lema. Mahakama hiyo imeeleza kuwa mawakili wamtuhumiwa huyo walipaswa kuonesha kusudio la kukata rufaa ndani ya siku10 kabla ya kukata rufaa.

Hii ni mara ya tano mbunge huyo anakosa dhamana mahakamani tangu alipokamatwa Novemba 3 mwaka huu akiwa mjini Dodoma na kusafirishwa hadi Arusha katika kesi ya uchochezi inayomkabili.

Katika kesi ya msingi lema anatuhumiwa kutoa maneno ya kichochezi dhidi ya Rais Magufuli kwa madai kuwa Mungu ndiye aliyemwambia maneno hayo wakati akiwa anaomba.
Share:

New AUDIO | Madada 6[Mkubwa na Wanawe] - Matobo | Download


Share:

Magazeti ya Leo Ijumaa tarehe 2.12.2016

Share:

HIZI HAPA KURASA ZA NDANI ZA MAGAZETI YA LEO IJUMAA DEC 2 2016

TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE HABARI ZA MICHEZO LEO..


TANO BORA ZA MASWAYETUBLOG KWENYE KATUNI ZA LEO..


KUMI BORA ZA MASWAYETU BLOG KURASA ZA NDANI MAGAZETINI LEO


1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
Share:

Thursday 1 December 2016

Mganga auawa kwa kutaka kubaka mteja

MGANGA wa kienyeji aliyejulikana kwa jina la Kashinje Kashinje (55), mkazi wa kijiji cha Singita kilichopo Kata ya Usanda wilayani hapa ameuawa kwa kupigwa na wananchi ikielezwa alijaribu kutaka kumbaka mteja wake.

Mteja huyo ambaye ni mwanamke mwenye umri wa miaka 20 (jina linahifadhiwa) aliyekwenda kutibiwa kwa lengo la kupata mtoto.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga, Muliro Jumanne, tukio hilo ni la Novemba 29 mwaka huu, akisema lilitokea majira ya saa tano asubuhi.

Alisema Kashinje alifariki dunia alipokuwa anakimbizwa hospitali baada ya kujeruhiwa kwa kitu chenye ncha kali katika jicho la kulia na kupigwa kwa fimbo mgongoni na watu waliojichukulia sheria mkononi.

“Watu hao walijichukulia sheria mkononi baada ya mganga huyo kujaribu kumbaka mwanamke (jina linahifadhiwa), mkazi wa kijiji cha Ishinabulandi wilaya ya Shinyanga ambaye alikuwa akimtibu kwa tiba za asili ili aweze kupata mtoto”, alieleza kamanda Muliro.

Alisema tatizo lililompeleka mwanamke huyo kwa mganga ni kupata tiba ili aweze kupata mtoto.

Kamanda Muliro alibainisha kuwa chanzo cha tukio hilo ni tamaa za kimwili na uongo wa kimatibabu wa kutaka kumuingilia kimwili mgonjwa wake baada ya kumlewesha kwa dawa za kienyeji, lakini alifanikiwa kupiga kelele na ndipo wananchi walipomvamia mganga huyo
Share:

Jiji Arusha lasimamisha wafanyakazi 66

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji La Arusha, Athumani Kihamia ametangaza kusitisha mikataba ya wafanyakazi 66 kati ya 132 wasio na kazi za lazima katika halmashauri hiyo.

Amewasimamisha kazi kwa lengo la kubana matumizi ili fedha zitakazookolewa zitaelekezwa kwenye matumizi ya miradi ya maendeleo na ulipaji wa madeni.
Share:

Scorpion’ akiri kupata mafunzo ya kareti Ifakara


MSHITAKIWA katika kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha, Salum Njwete (34) ‘Scorpion’, amekiri kupata mafunzo ya kareti kutoka chuo cha mafunzo cha Ifakara aliyoyafanya mwaka 1989 hadi 1995.

Aidha, upande wa mashitaka katika kesi hiyo umemuongezea mashitaka ya shambulio kupitia kifungu namba 234 cha Sheria ya Makosa ya Jinai ambacho kinaruhusu kuongeza au kubadilisha mashitaka.

Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga alidai jana mbele ya Hakimu Mkazi, Flora Haule kwamba kesi hiyo imekuja kwa ajili ya mshitakiwa kusomewa maelezo ya awali ambapo katika maelezo ya zaidi ya saa nane, alikiri kuhusu jina lake, sehemu anayoishi ya Machimbo Yombo na mafunzo hayo.

Hata hivyo, alikana kuhusu jina la Scorpion, mashitaka yake na kwamba hakukamatwa wala kuhojiwa na Polisi kuhusu mashitaka hayo.

Katuga alidai kuwa Septemba 6, mwaka huu, mshitakiwa alikuwa maeneo ya Buguruni Sheli na kwamba Septemba 12, alihojiwa na kukamatwa na polisi maelezo ambayo aliyakana.

“Mashahidi watakaotoa ushahidi katika kesi hii wapo sita ambapo upande wetu wa mashitaka utawasilisha vielelezo viwili ikiwemo Fomu namba tatu ya Polisi (PF3) na ripoti ya daktari kwa ajili ya kuthibitisha mashitaka hayo,’’ alidai Katuga.

Hakimu Haule aliahirisha shauri hilo hadi Desemba 14 mwaka huu, kesi hiyo itakapokuja kwa ajili ya kusikilizwa. Katika mashitaka yake, mtuhumiwa inadaiwa alitenda kosa hilo Septemba 6, mwaka huu katika maeneo ya Buguruni Sheli, wilaya ya Ilala.

Inadaiwa, Njwete aliiba mkufu rangi ya fedha wenye uzito wa gramu 34 wenye thamani ya Sh 60,000, bangili ya mkononi na fedha taslimu Sh 331,000, vyote vikiwa na thamani ya Sh 476,000 mali ya Said Mrisho.

Inadaiwa kabla na baada ya wizi huo, alimchoma kisu machoni, tumboni na mabegani mlalamikaji ili ajipatie mali hizo.
Share:

Sheria ya kukata 15% za mkopo wa HESLB yasainiwa


Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli tayari amekwishasaini mabadiliko ya sheria yanayomtaka mwajiri kukata asilimia 15 ya mshahara wa mwajiriwa ambaye ni mnufaika wa mkopo wa elimu ya juu kwa ajili ya kulipa deni lake analodaiwa na Bodi ya Mikopo
Mhandisi Stella Manyanya akiwa
Share:

Sababu za kuanguka ndege ya Brazil zatajwa


Colombia
Visanduku vya mawasiliano ajali ya ndege ya Brazil vyapatikana
Ndege iliyokuwa imewabeba wachezaji wa timu ya mpira kutoka nchini Brazil ambayo ilipata ajali nchini Colombia inasemekana kwa muujibu wa taarifa zilizovuja ndege hiyo iliishiwa mafuta kutoka katika kifaa cha kurekodia mawasiliano.
Katika mnara wa mawasiliano ya ndege , rubani alisikika akirudia mara kadhaa akiomba ruhusa ya kutua kwa dharura kutokana na hitilafu ya umeme iliyokuwamo ndegeni pamoja na kuishiwa mafuta ya ndege.
Kabla hata mawasiliano hayo yaliyorekodiwa kufikia mwisho ,rubani alisikika akisema yuko angani umbali wa futi elfu tisa sawa na mita elfu mbili mia saba na arobaini na tatu.Taarifa za mawasiliano hayo zimekuwa gumzo katika mitandao kadhaa nchini Colombia na hata katika vyombo vya habari nchini humo, na hivyo kumekuwepo fununu za taarifa hizo kuwa huenda zikawa na chembe ya ukweli kwamba kuishiwa kwa mafuta ndiyo chanzo zha ajali ya ndege hiyo.
Wanajeshi wa Colombia waliliambia shirika la habari la AFP, kwamba pamoja na ndege hiyo kuanguka kuna shaka juu ya ajali hiyo kwani pamoja na ndege hiyo kuanguka hakukuwa na mlipuko wowote na kwamba huenda kulitumika nguvu ingine tofauti na nadharia ya kwisha kwa mafuta ndegeni.
Wadadisi wa mambo na wachunguzi bado hawako tayari kufungua mdomo na kuzungumzia juu ya chanzo chochote cha ajali hiyo na kwamba taarifa kamili ya uchunguzi itatolewa baada ya miezi kadhaa.
Wachezaji wa timu ya Chapecoense walikuwa safarini kuelekea nchini Colombian kwenye mji wa Medellin mahali kulikotarajiwa mechi kubwa ya mpira wa miguu ya kihistoria na badala yake wachezaji hao wameacha historia .Kufuatia vifo vya wachezaji wa timu hiyo, ulimwengu mzima umeungana kuomboleza vifo vyao.
Kwa muujibu wa taarifa zilizopatikana kutoka katika shirika la ndege la Lamia watu wanne waliokuwa wasafiri na ndege hiyo wameponea chupuchupu kuwa miongoni mwa waliokufa baada ya kukosa tiketi.
Mmoja wa manusura wa ajali hiyo ambaye ni fundi wa ndege Erwin Tumiri, ameeleza namna alivyokwepa kifo, kwamba yeye alifuata maelekezo yote ya namna ya kujiokoa ,anasema abiria wenzie , walio wengi walisimama na kuanza kupiga kelele nay eye aliamua kuweka sanduku lake la kusafiria kati kati ya miguu yake na kuamua kubaki hivyo.
Visanduku viwili vya mawasiliano vya ndege hiyo vyote vilipatikana na tayari vimeanza kufanyiwa uchunguzi na wataalamu wa masuala ya anga.
Wachunguzi wataalamu kutoka nchini Uingereza wanasaidiana na mamlaka za Amerika Kusini kwasababu ndege iliyopata ajali ilitengenezwa na wana anga wa Uingereza BAE nchini Uingereza.Brazil imeanza siku tatu za maombolezo wakati maelfu ya watu na washabiki wa timu ya Chapecoense wako katika mji yaliko makao makuu ya timu hiyo Chapeco wanaendelea mkesha wa maombolezo wakati maandalizi ya kuchukua mabaki ya wachezaji hao inafanywa na jeshi kurejeshwa Brazil ili kuzikwa kwa pamoja katika uwanja wa Chapeco.
Nchi ya Bolivia tayari imekwisha tuma ndege ya kuchukua mabaki ya raia wake waliokufa katika ajali hiyo nchini Colombia.
Timu hiyo iliandika historia ya mafanikio katika soka kwa kuwa kileleni mwa ligi ya Brazil kwamara ya kwanza mwaka 2014.Kati ya watu 77 waliokuwa wameabiri ndege hiyo miongoni mwao ni watu sita tu ndiyo walionusurika .Abiria walio wengi walikuwa ni wachezaji wa timu ya Chapecoense na waandishi habari wapatao ishirini walikuwa miongoni mwa walipoteza maisha
Share:

FA YAMTANGAZA GARETH SOUTHGATE KUWA KOCHA MKUU WA ENGLAND


gareth-southgate-england-u21s-under-21s-u21-press-conference_3373168
Share:

Magazeti ya Leo Alhamisi december 1 2016

Share:

KURASA ZA NDANI MAGAZETI YA LEO ALHAMISI DECEMBER TAREHE 1.12.2016

TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE HABARI ZA MICHEZO LEO


TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE KATUNI ZA LEO..


KUMI BORA ZA MASWAYETU BLOG KURASA ZA NDANI MAGAZETINI LEO


1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger