Sunday 27 November 2016

SERIKALI KUNUNUA NDEGE ZA KISASA KUIMARISHA ULINZI HIFADHI ZA TAIFA



SERIKALI imepanga kununua ndege za kisasa ili kuimarisha ulinzi katika Hifadhi za Taifa nchini.
Hayo yamesemwa jana na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi wakati akihojiwa na kipindi maalumu cha TUNATEKELEZA kinachorushwa hewani na kituo cha Televisheni ya Taifa (TBC1).
Meja Jenerali Milanzi anasema Serikali imeweka mfumo maalumkatika  kulinda hifadhi zilizopo na ili kuweza kukabiliana na ujangili unaojitokeza katika hifadhi mbalimbali nchini.
“Sekta ya Utalii nchini inachangia pato la taifa kwa takribani asilimia 17.5 na kutoa ajira kwa zaidi ya watumishi milioni 3 katika sekta mbali mbali ya utalii nchini, hivyo ni vyema tukaweka mikakati madhubuti katika kulinda vyanzo vilivyopo” alisema Meja Milanzi.
Aidha, alisema kuwa Serikali itaendelea kuwachukulia hatua kali za kisheria watu wote watakaobainika kujihusisha na ujangili pamoja na biashara ya magogo ili kulinda hifadhi za Taifa na kuweza kuvutia watalii nchini.
Aidha Meja Jenerali Milanzi aliitaka jamii kwa ujumla kuona umuhimu wa kutumia nishati mbadala ili kulinda misitu iliyopo kwa kutunza mazingira na hifadhi za taifa.
Mbali na hayo Meja Jenerali Milanzi alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazovutia watalii wengi kutoka Marekani na Uingereza hivyo kuwataka wananchi kuzingatia sheria na kanuni zinazosimamimia Hifadhi za Taifa ili kuzudi kuvutia watalii nchini.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOV 27 2016

Share:

MADEREVA WA SERIKALI NA TAASISI ZA UMMA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI



KAMANDA wa Polisi wa kikosi cha usalama Barabarani Mohammed Mpinga ametoa wito kwa madereva wote ikiwemo madereva wa Serikali na Mashirika ya Umma kuzingatia sheria za Usalama Barabarani.
Kamanda Mpinga ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya “Abiria paza sauti” inayotarajiwa kuzinduliwa tarehe 28 Novemba, mwaka huu.
Kamanda Mpinga alisema kumekuwa tabia ya baadhi ya madereva hususani wa Serikali na mashirika ya umma ya kutofuata sheria za usalama barabarani kwa kuendesha magari kwa mwendokasi, na kuwaonya kuwa sheria ni msumeno na inapaswa kufuatwa na kila mtu.
“Kumekuwa na madereva hasa wa magari madogo kusafiri kwenda maeneo mbalimbali ya nchi huku wakiwa hawana uzoefu wa kuendesha umbali mrefu na hivyo kupelekea uvunjifu wa sheria za barabarani kwa kuendesha kwa mwendokasi na kusababisha ajali” alifafanua Kamanda Mpinga.
Akifafanua zaidi Kamanda alisema uzoefu unaonyesha kuwa katika kipindi hiki cha kuelekea mwisho wa mwaka kumekuwa na ongezeko kubwa la magari barabarani, na hivyo kuwataka wananchi kuzingatia sheria za barabarani ili kuweza kupunguza ajali za barabarani.
Kwa upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Mabalozi wa Usalama Barabarani, Jackson Kalikumtima alisema lengo la kampeni ya Paza Sauti ni kuhamasisha ushiriki kamilifu wa wananchi katika kukabiliana na ajali kwa kuchukua hatua stahiki bila ya uwepo wa askari.
Pia alisema kuwa kampeni hiyo imelenga kubadili tabia na mtazamo wa madereva kuhusu usalama barabarani ili waendeshe kwa kuzingatia sheria bila shuruti na kubadili mtazamo wa wananchi kuhusu usalama barabarani ili watambue kuwa usalama barabarani ni jukumu la kila mmoja.
Naye Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, (ASP), Deus Sokoni alisema mkakati wa kupunguza ajali barabarani katika kampeni hiyo  umelenga katika kutoa elimu kwa jamii ili kuona suala la usalama barabarani ni jukumu la kila mmoja na si jukumu la Polisi pekee.
“hakuna asiyetumia barabara duniani, hatutaki ajali tunataka kuishi salama, hivyo kila abiria anawajibu wa kutunza na kutii sheria za barabarani “ aliongeza Mwanasheria huyo.
Mwenyekiti wa Chama cha Kutetea Abiria Taifa (CHAKUA), Hassan Mhanjama aliwataka abiria wote nchini hususani wanaotajaria kusafiri mwishoni mwa mwaka kuwasiliana na Mamlaka ya Usafirishaji SUMATRA pindi watakapopandishiwa nauli mbali na taratibu zilizopo
Share:

HIZI HAPA KURASA ZA NDANI MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBER TAREHE 27.11.2016

TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE HABARI ZA MICHEZO LEO


TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE KATUNI ZA LEO..


KUMI BORA ZA MASWAYETU BLOG KURASA ZA NDANI MAGAZETINI LEO


1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
Share:

Saturday 26 November 2016

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA VYUO VYA VETA 2017

Image result for VETA.GO.TZ
Share:

MH.UMMY MWALIMU :TAHADHARI KUHUSU UTAPELI HUU

 MoHCDGEC
Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOFANIKIWA KUHAMIA CHUO KIKUU UDOM 2016/2017

 Image result for UDOM.AC.TZ
Share:

Muuguzi anayedaiwa kumwambia mama wa mgonjwa ‘ataisoma namba kumchagua Magufuli’ atambuliwa

Mbeya. Muuguzi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya anayedaiwa kumkamshifu Junes Elias, mkazi wa Mbozi mkoani Songwe na Rais John Magufuli ametambuliwa.

Mganga mkuu wa hospitali hiyo, Dk Gloria Mbwille alisema muuguzi huyo ametambuliwa na kwamba tume imeundwa kuchunguza tuhuma zinazomkabili.

Hata hivyo, alikataa kuzungumzia zaidi kuhusu muuguzi huyo wala kumtaja jina akisema taarifa zaidi zitatolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla baada ya tume kukamilisha uchunguzi huo. Juzi mchana, Junes alimueleza Makalla kwamba alifika hospitalini hapo Novemba 22 asubuhi akitokea wilayani Mbozi.

Alisema baada alifuata taratibu za kufungua kadi kwa gharama ya Sh5,000 kwa ajili ya kutaka matibabu ya mtoto wake, Joyce Asifiwe (9), lakini alikashfiwa kwenye dirisha la dawa akiambiwa ataisoma namba kwa kumchagua Rais Magufuli.

Alisema baada ya kumuona daktari aliandikiwa dawa za kwenda kuchukua kwenye dirisha ambako ndiko alikotolewa maneno ya kashfa.

“Kwenye dirisha hilo nilimkuta muuguzi mmoja ambaye aliniambia kwamba dawa zote zinauzwa. Hapa hakuna dawa za bure, si mlimchagua Magufuli, sasa mtaisoma namba,’’ alisema akidai kumnukuu aliyemtaja kuwa ni muuguzi.


Baada ya kumsikiliza malalamiko hayo, Makalla aliagiza mganga mkuu aitwe, lakini ilielezwa alikuwa safarini, hivyo kaimu wake, Dk Ismail Macha alifika.

Makalla alimueleza Dk Macha kwa kifupi yaliyojiri kutoka kwa mlalamikaji huyo na kumtaka waongozane hadi hospitalini na kuwaita wauguzi waliokuwa zamu Novemba 22 dirisha la dawa ili amtambue mhusika na achukuliwe hatua jambo ambalo limefanyika.
Share:

Rais wa Zamani wa Cuba, Fidel Castro Afariki Dunia

CUBA: Rais wa zamani wa Cuba, na kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha nchini humo, Fidel Alejandro Castro Ruz amefariki dunia leo akiwa na umri wa miaka 90.
Share:

Magazeti ya Leo Jumamosi november tarehe 26.11.2016

Share:

Friday 25 November 2016

official VIDEO | MwanaFA Ft. Vanessa Mdee – Dume Suruali | Watch/Download


dume
Share:

Rais Magufuli amualika Rais wa Zambia kwa ziara ya siku 3

Share:

Ripoti ya uchunguzi wa mali za BAKWATA yakabidhiwa

Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari Zuber  jana amekabidhiwa ripoti ya awali iliyoandaliwa na tume ambayo ameiunda  kwa ajili ya kufanya uchunguzi  na kuzibainisha  mali zote za  Baraza kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).

Akizungumza wakati wa kumkabidhi ripoti hiyo, Mwenyekiti wa tume hiyo Sheikh Abubakari Khalid Hajj alisema kuwa  ripoti hiyo imefanyika kwa muda wa miezi mitatu licha ya kukumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ufinyu wa muda.

Aidha aliwambia wanahabari kuwa uchunguzi huo umehusisha ufuatiliaji wa mali za Bakwata katika Mkoa wa Dar es salaam pekee,ikiwemo majengo,viwanja, pamoja na kupitia mikataba mbalimbali ili  kujiridhisha kama imefuata taratibu za kisheria.

Akizungumza mbele ya wanahabari mara baadi ya kupokea ripoti hiyo Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari Zuber alisema kuwa ataipitia ripoti hiyo  ili kujua yale yaliyobainishwa na tume yake, na kuahidi kuyafanyia kazi mapema iwezekanavyo.

Hata hivyo Mufti huyo ameiongezea muda wa miezi mitatu tume hiyo ambayo ina jumla ya  wajumbe wanane kwa ajili ya kukamilisha kuandaa ripoti ya mkoa wa Dar es salaam kabla ya kuhamia mikoa mingine kwani zoezi hilo litafanyika nchi nzima.
Share:

Magazeti ya Leo Ijumaa Ya Novemba 25 2016

Share:

Thursday 24 November 2016

RC Makonda Aamuru Mwenyekiti wa Mtuu Akamtwe na Kuwekwa Rumande Hadi Upelelezi Utapokamilika

Share:

Wataalam wa afya kuanza kusajiliwa na kupewa leseni

Wataalamu mbalimbali wa sekta ya afya, sasa wataanza kusajiliwa na kupewa leseni zitakazowatambulisha na zitakuwa na masharti maalumu.

Hayo yamesema na Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Muhammad Kambi  jana Jumatano  jijini Dar es salaam, wakati akifungua mkutano wa mwaka wa Chama cha Wafiziotherapia (APTA).

Alisema serikali imeanza mchakato wa kuipitia upya Sheria ya Madaktari wa Tanganyika, ambayo itaongezwa sharti hilo pamoja na kuundwa kwa bodi maalumu itakayosimamia maadili ya watumishi hao.

“Lakini hivi sasa kuna taaluma nyingi ndani ya hii fani, kwa mfano ninyi wataalamu wa fiziotherapia. Mpo lakini sheria haiwatambui, kwa maana hiyo inakuwa vigumu hata kuwafuatilia. Ndiyo msingi wa kuipitia upya sheria hii,” alisema.

“Katika sheria mpya itakayoboreshwa, kila mtumishi atatakiwa kukata leseni. Kila mtumishi atatakiwa kujiendeleza kielimu, kuongeza ujuzi ili aendane na wakati uliopo kwa sababu mambo yanabadilika, kile ulichosoma jana unahitaji kujifunza zaidi,” alisema.

Aidha Kambi alisema tayari maboresho ya sheria hiyo yameshawasilishwa katika Kamati ya Baraza la Mawaziri ya Katiba na Sheria na imeshapitiwa.
Share:

Mwanafunzi Apigwa Risasi na Polisi Dar,Askari Wawili Watiwa Mbaroni

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger