Tuesday 30 August 2016

Mtoto wa Shule Alivyofumaniwa na Mwanaume wa zaidi ya Miaka 60 Tanga

August 29 2016 Kupitia Hekaheka ya Clouds FM Geah Habib ametuletea Hekaheka iliyotokea Tanga ambapo mzee mmoja kafumaniwa na mkewe akiwa na mtoto wa shule wa miaka 14.

Mjomba wa mtoto ameeleza kuwa mtoto amekuwa akijiandaa asubuhi na mapema sana na anaaga anaenda shule lakini anapitia kwa huyo mzee na baadaye muda wa saa moja anaena shule……

Mahusiano yameanza tangia January, mpaka sasa hivi ni mwezi wa nane na sisi mpaka tumekuja kugundua ni baada ya kutokea ugomvi, mke wake yule mzee amempiga na kumng’ata mtoto ameumia na sisi ndio tukajua hilo suala.

Mtoto wangu ana miaka kumi nne na mzee huyo ana kama 60 mpaka 70 maana ni babu kabisa, sisi halikuwa hatujui tulikuwa tunajua anaenda shule na alikuwa anamuaga bibi yake maana anakaa na bibi yake kwamba wanatakiwa kuwahi namba kumbe asubuhi anaanza kwanza kwa huyo baba.

Jumatano asubuhi walipokutana na huyo baba kupewa hela mara mke wa huyo baba akatoa akaanza kumshambulia na kumng’ata
Share:

DALADALA LAGONGA MAGARI MATATU MAJI MATITU TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM


Wananchi wakiangalia ajali iliyosababishwa na daladala lenye namba za usajili T 397 BVB linalofanya safari zake kati ya Temeke na Gongo la Mboto kwa kuyagonga magari mengine matatu eneo la Maji Matitu Temeke Dar es Salaam leo asubuhi. Katika ajali hiyo dereva wa gari dogo namba T 628 DFE alijeruhiwa.
Gari dogo namba T 628 DFE lililogongwa na daladala hilo likiwa limeharibika.
Daladala hili likiwa limegonga gari namba T 458 CAN.
Kuku waliokuwa kwenye moja ya gari lililogongwa wakiondolewa kuku kadhaa walipoteza maisha katika ajali hiyo.
Askari wa Usalama barabarani akiangalia ajali hiyo.
Daladala uso kwa uso na gari dogo.

Na Dotto Mwaibale

MKAZI wa Chamazi ambaye ni mwanamke amejeruhiwa baada ya gari lake dogo alilokuwa akiendesha kugongwa na daladala lenye namba T 397 BVB linadodaiwa kuiba njia.

Ajali hiyo imetokea Maji Matitu Temeke jijini Dar es Salaam leo asubuhi ambapo daladala hilo pia liliyagonga magari mengine matatu na kuzua kizaazaa katika barabara ya Charambe kwenda Chamazi.

Mkazi wa eneo hilo Hamisi Juma aliyeshuhudia ajali hiyo amesema ni mungu kasaidia kutokea kwa vifo kwani ajali hiyo ilikuwa ni mbaya sana.

" Saa 12 na dakika 55 nikiwa nasubiri gari kwenda kazini niliona daladala lililokuwa likitoka Charambe kwenda Chamazi lilikuwa likipita upande ambao si wake likiwa katika mwendo wa kasi na ghafla lililigonga gari dogo namba T 628 DFE ambalo ligeuka na kulala katika mtaro" alisema Juma.

Alisema baada ya kuligonga gari hilo liliyaparamia magari mengine madogo mawili likiwepo lililobeba kuku na kuyasukumia kwenye mtaro.

Aliongeza kuwa baada ya kutokea tukio hilo dereva wa daladala hilo alikimbia na kulitelekeza gari lake.

Magari yaliyohusika katika ajali hiyo ni T 628 DFE, T 397 BVB, T 451 CQB na T 458 CAN.

Jitihada za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke ili kuzungumzia suala hilo hazikuzaa matunda baada ya simu yake kuita bila kupokewa alipopigiwa simu mara kadhaa.
Share:

UVCCM Waahirisha Maandamano Yao, Watii Agizo la Jeshi la Polisi


Agosti 22, 2016 Umoja wa Vijana wa CCM tuliutangazia umma na dunia kwamba ifikapo Agosti 31 mwaka huu tutaitisha maandamano ya amani nchi nzima yenye lengo la kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk John Pombe Magufuli kwa utendaji wenye tija, ufanisi na uliorudisha imani na matumaini kwa wananchi.


Msimamo na dhamira ya kufanya maandamano hayo ya amani yenye maudhui na kusudio hilo, bado uko pale pale ingawaje si kwa tarehe tuliopanga na kutangaza awali yaani Agosti 31 mwaka huu.


Jumuiya yetu kama mjuavyo ni ya Vijana wa CCM, (UVCCM) inapata malezi kwa karibu mno na Jumuiya ya Wazazi ya CCM. Wiki ya jana Mwenyekiti wa Wazazi Taifa Nd. Abdallah Bulembo alikutana na waandishi wa habari akitutaka UVCCM tuahirishe maandamano ya Agosti 31 mwaka huu hadi wakati mwingine.


Kwa mujibu wa Katiba ya Chama Cha Mapinduzi, Jumuiya ya Wazazi ndiyo Msimamizi wa Malezi, Maadili na Adabu kwa Vijana wote nchini, sisi UVCCM tunaamini kuwa sikio halishindani na kichwa, mtoto ni mtoto kwa Wazazi wake hakui, hana jeuri wala ubishi.


Mtoto au watoto wanaokaidi amri, ushauri au maelekezo ya Wazazi wao huitwa watukutu, wenye viburi, manunda na wasioambilika. UVCCM si watukutu, hatukufunzwa tuwe wabishi, wakaidi na wenye viburi. Tumezingatia kutii maelekezo, makatazo na maonyo , tumeambiwa tuahirishe maandamano yetu nasi tumekubali na kuheshimu mambo tuliyoaswa.


Sambamba na hilo tumepata majibu ya barua yetu tuliyomwandikia Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP Ernes Mangu) inayotutaka tuache kufanya maandamano yetu kwa sababu Polisi wamezuia mikutano ya hadhara ya Vyama vya Siasa na maandamano nchi nzima.


Jambo jingine ambalo limetufanya pia tuahirishe maandamano yetu ya Amani ni taarifa ya kintelejinsia iliowasilishwa na Kamati yetu ya Usalama na Maadili ya UVCCM mbele ya kikao cha Sekreteriet yetu, nayo ilipendekeza suala hilo liahirishwe kwa wakati huu hadi muda mwingine.


Pia jambo jingine ambalo limefanya maandamano hayo tuyabatilishe ni kulipisha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ ) ambalo litakuwa katika shughuli za maadhimisho miaka 52 tokea kuanzishwa kwake.


Wanajeshi wetu watakuwa katika kazi mbalimbali za kijeshi kwenye kambi zao na mitaani kufanya usafi wa mazingira, hivyo isingependeza na wala si heshima wakati sisi tukiandamana, wao wakifanya kazi muhimu kila mmoja wetu zinazomgusa badala yake ni vyema kuwaunga mkono jambo wanalolifanya la usafi wa mazingira.


UVCCM tumekubali, hatutaki kuingia katika uvunjaji wa sheria hasa baaada ya kutakiwa kuahirisha na mamlaka za Kisheria hadi wakati mwingine muafaka na si wakati huu.


Tunaelewa kwamba uamuzi wetu wa awali wa kutaka kuandamana kwa amani hata kama tungenyimwa kibali ungetugharimu, ungetusababishia madhara na pengine hasara, kwa wakati huu na kuona jambo lenyewe ni la kuipa Ari serikali katika kuhimiza Uwajibikaji, Utendaji na Usimamizi bora wa Uendeshaji wa masuala ya kiutawala.


Tulishusha maagizo kwa Makatibu wetu wote wa Mikoa yote 32 na Wilaya 171 ya Kichama tukiwataka waandike barua katika Ofisi za Ma RPC na OCD, washirikiane ili kuratibu maandamano na kuyafanikisha kama tulivyokusudia.


Watendaji wetu wa ngazi husika wamefuata maelekezo, wametii taratibu zetu za kiutendaji na leo tumewajulisha tena wasitishe maandamano hadi tutakapowapa tena maelekezo mengine. Tunawahimiza na kuwataka ni vyema kutii mamlaka za Kikanuni na Kisheria.

UVCCM kwa wakati huu tumeamua kuachana na maandamano badala yake tunajikita katika matayarisho ya kuwapeleka Vijana wetu wakashiriki katika Mafunzo ya Siasa, Utawala, Uongozi, Ufundi na Ujasiriamali yatakayoanza kufanyika katika Chuo chetu kilichopo huko Ihemi Mkoani Iringa ambapo kitakuwa kielelezo na alama nzuri ya kumuunga mkono Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kwa vitendo.

Tumewataka Makatibu wetu wa Mikoa na Wilaya kuendelea na zoezi la Uratibu na Uhakiki kwa Vijana ambao watateuliwa kushiriki Mafunzo hayo huko Ihemi.

UVCCM tunarejea kusema tena kwamba dhamira ya maandamano yetu ya kusifu Utendaji wa Serikali ya awamu ya tano iko pale pale ila tutapanga tarehe nyingine katika wakati ujao badala ya kufanyika Agosti 31 mwaka huu kama tulivyotangaza hapo awali.

UVCCM tunawataka Vijana wote kuendelea kuheshimu Tunu ya Amani Umoja na Mshikamo wetu kwa Taifa.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Shaka Hamdu Shaka (MNEC)

KAIMU KATIBU MKUU.
Share:

ORODHA YA MAJINA YA WASHINDI WA 2016 MTV VIDEO MUSIC AWARDS (VMAS)

 
mtv-video-music-awards-620x359
Usiku wa jana kwenye Tuza za MTV  VMAS, Mwanadada Beyonce aliibuka mshindi zaidi kwa kuondoka na tuzo saba alizozipata kutoka kwenye vipengele tofauti tofauti alivyokuwa akigombania na wenzie kama kina Adele, Rihanna na wengineo.
Orodha kamili ya vingele na majina ya washindi nimekuwekea hapo chini:-
VIDEO OF THE YEAR
Mshindi: Beyoncé – “Formation”
Adele – “Hello”
Drake – “Hotline Bling”
Justin Bieber – “Sorry”
Kanye West – “Famous”
BEST FEMALE VIDEO
Adele – “Hello”
Mshindi: Beyoncé – “Hold Up”
Sia – “Cheap Thrills”
Ariana Grande – “Into You”
Rihanna ft. Drake – “Work” (short version)
BEST MALE VIDEO
Mshindi: Calvin Harris ft. Rihanna – “This Is What You Came For”
Drake – “Hotline Bling”
Bryson Tiller – “Don’t”
Kanye West – “Famous”
The Weeknd – “Can’t Feel My Face”
BEST COLLABORATION
Mshindi: Fifth Harmony ft. Ty Dolla $ign – “Work From Home”
Beyoncé ft. Kendrick Lamar – “Freedom”
Ariana Grande ft. Lil Wayne – “Let Me Love You”
Calvin Harris ft. Rihanna – “This Is What You Came For”
Rihanna ft. Drake – “Work” (short version)
BEST HIP HOP VIDEO
Mshindi: Drake – “Hotline Bling”
Desiigner – “Panda”
Bryson Tiller – “Don’t”
Chance The Rapper ft. Saba – “Angels”
2 Chainz – “Watch Out”
BEST POP VIDEO
Mshindi: Beyoncé – “Formation”
Adele – “Hello”
Justin Bieber – “Sorry”
Alessia Cara – “Wild Things”
Ariana Grande – “Into You”
SONG OF SUMMER
Mshindi: Fifth Harmony featuring Fetty Wap — “All In My Head”
Drake — “One Dance”
Justin Timberlake — “Can’t Stop The Feeling”
Major Lazer featuring Justin Bieber — “Cold Water”
Calvin Harris featuring Rihanna — “This Is What You Came For”
Sia — “Cheap Thrills”
The Chainsmokers featuring Halsey — “Closer”
Nick Jonas featuring Ty Dolla $ign — “Bacon”
Kent Jones — “Don’t Mind”
Selena Gomez — “Kill ‘Em With Kindness”
BEST ROCK VIDEO
Mshindi: twenty one pilots – “Heathens”
All Time Low – “Missing You”
Coldplay – “Adventure Of A Lifetime”
Fall Out Boy ft. Demi Lovato – “Irresistible”
Panic! At The Disco – “Victorious”
BEST ELECTRONIC VIDEO
Mshindi: Calvin Harris & Disciples – “How Deep Is Your Love”
99 Souls ft. Destiny’s Child & Brandy – “The Girl Is Mine”
Mike Posner – “I Took A Pill In Ibiza”
Afrojack – “SummerThing!”
The Chainsmokers ft. Daya – “Don’t Let Me Down”
BREAKTHROUGH LONG FORM VIDEO
Mshindi: Beyoncé – Lemonade
Florence + The Machine – The Odyssey
Justin Bieber – PURPOSE: The Movement
Chris Brown – Royalty
Troye Sivan – Blue Neighbourhood Trilogy
BEST NEW ARTIST
Mshindi: DNCE
Bryson Tiller
Desiigner
Zara Larsson
Lukas Graham
PROFESSIONAL CATEGORIES
BEST ART DIRECTION
Mshindi: David Bowie – “Blackstar” (Production Designer: Jan Houllevigue)
Beyoncé – “Hold Up” (Production Designer: Jason Hougaard)
Fergie – “M.I.L.F. $” (Production Designer: Alexander Delgado)
Drake – “Hotline Bling” (Production Designer: Jeremy MacFarlane)
Adele – “Hello” (Production Designer: Colombe Raby)
BEST CHOREOGRAPHY
Mshindi: Beyoncé – “Formation” (Choreographer: Chris Grant, JaQuel Knight, Dana Foglia)
Missy Elliott ft. Pharrell – “WTF (Where They From)” (Choreographer: Hi-Hat)
Beyoncé – “Sorry” (Choreographer: Chris Grant, JaQuel Knight, Dana Foglia, Anthony Burrell, Beyoncé Knowles Carter)
FKA Twigs – “M3LL155X” (Choreographers: Aaron Sillis, Benjamin Milan, Kenrick Sandy and FKA twigs)
Florence + The Machine – “Delilah” (Choreographer: Holly Blakey)
BEST DIRECTION
Mshindi: Beyoncé – “Formation” (Director: Melina Matsoukas)
Coldplay – “Up&Up” (Director: Vania Heymann, Gal Muggia)
Adele – “Hello” (Director: Xavier Dolan)
David Bowie – “Lazarus” (Director: Johan Renck)
Tame Impala – “The Less I Know The Better” (Director: Canada)
BEST CINEMATOGRAPHY
Mshindi: Beyoncé – “Formation” (Cinematographer: Malik Sayeed)
Adele – “Hello” (Cinematographer: André Turpin)
David Bowie – “Lazarus” (Cinematographer: Crille Forsberg)
Alesso – “I Wanna Know” (Cinematographer: Corey Jennings)
Ariana Grande – “Into You” (Cinematographer: Paul Laufer)
BEST EDITING
Mshindi: Beyoncé – “Formation” (Editor: Jeff Selis)
Adele – “Hello” (Editor: Xavier Dolan)
Fergie – “M.I.L.F. $” (Editor: Vinnie Hobbs)
David Bowie – “Lazarus” (Editor: Johan Söderberg)
Ariana Grande – “Into You” (Editor: Hannah Lux Davis)
BEST VISUAL EFFECTS
Mshindi: Coldplay – “Up&Up” (VFX Editor: Vania Heymann)
FKA Twigs – “M3LL155X” (VFX Editors: Lewis Saunders and Electric Theatre Collective)
Adele – “Send My Love (To Your New Lover)” (VFX Editor: Jonathan Box, MPC)
The Weeknd – “Can’t Feel My Face” (VFX Editor: Bryan Smaller)
Zayn – “PILLOWTALK” (VFX Editor: David Smith)
Share:

Monday 29 August 2016

Sekta ya Elimu Yaongoza kwa Watumishi Hewa


Image result for Dkt. Ashatu Kijaji
Serikali imeendelea kufanya msako wa kuwabaini watumishi hewa ambapo mpaka kufikia tarehe 20 mwezi huu jumla ya watumishi 16,127 wamebainika kukosa vigezo vya kuajiriwa huku sekta ya elimu ikitajwa kuongoza.
Takwimu hizo zinatolewa na naibu waziri wa fedha na mipango Dkt. Ashatu Kijaji wakati wa zoezi la ugawaji madawati kwenye kata 21 za halmashauri ya wilaya ya Kondoa ambapo amesema tatizo la watumishi hewa limeigharimu serikali fedha nyingi ambazo zingeweza kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
 
Awali katika zoezi hilo mkurugenzi wa halmashauri ya Kondoa Falesy Kibasa amesema licha ya zoezi la madawati kufanyika kwa ufanisi lakini bado wilaya hiyo inakabiliwa na upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa pamoja na waalimu.
 
Katika ugawaji huo mwenyekiti wa kamati ya elimu afya na maji ya halmashauri hiyo Zakaria Balajina amesema halmashauri imejiwekea mkakati wa kuyatunza madawati kwa kuwakabidhi kwa mikataba maalum wakuu wa shule ili waweze kuwajibishwa itakapobainika kumekuwepo na uzembe katika utunzaji wake.
 
Katika zoezi hilo jumla ya madawati 2,260 yamekabidhiwa katika hatua ya awali na linatarajiwa kuwa endelevu ili kukidhi mahitaji katika shule zote za msingi na sekondari.
Share:

VIDEO:ASKOFU GWAJIMA KUMRUDISHA AMINA CHIFUPA

Sina maneno mengi nimekuwekea VIDEO hapo chini;
Image result for gwajima
Share:

Vituo viwili vya Redio vyafungwa kwa muda.





Serikali yafungia vituo viwili vya redio nchini kutokana na kurusha hewani taarifa za kichochezi zinazoweza kuchangia uvunjifu wa amani.

Tamko la kufungwa kwa vituo hivyo vya redio limetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni ,Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Aidha,Waziri Nape alivitaja vituo hivyo kuwa ni Kituo cha Redio Five cha Arusha na Kituo cha Redio Magic FM Dar es Salaam na alisisitiza kuwa utekelezaji wa tamko hilo unaanza leo tarehe Agosti 29, 2016 mara baada ya kutangazwa.

“Uamuzi wa kuvifungia vituo hivyo umefikia baada ya kujiridhisha kuwa kipindi cha MATUKIO kilichorushwa tarehe 25 Agosti ,2016 muda wa 02:00 usiku hadi 03:00 usiku na Kituo cha Utangazaji cha Redio Five Arusha na kipindi cha cha Morning Magic katika kipengele cha KUPAKA RANGI kilichorushwa tarehe 17 Agosti, 2016 kati ya saa 01:00 asubuhi na saa 02:00 asubuhi vilikuwa na maudhui ya uchochezi unaoweza kuleta uvunjifu wa amani na hivyo kukiuka masharti ya kanuni ya 5 (a),(b),(c) na (d) pamoja na Kanuni ya Huduma za Utangazaji (Maudhui) za mwaka 2005”, alisema Waziri Nnauye.

Waziri huyo mwenye dhamana na vyombo vya habari nchini alisema vituo hivyo vimefungiwa kwa muda usiojulikana na ameelekeza Kamati ya Maudhui kuviita vyombo hivyo na kuwasikiliza kwa kina zaidi na kumshauri hatua zaidi za kuchukua kwa mujibu wa Kanuni za Utangazaji za mwaka 2005.

Pamoja na hayo Waziri Nape alivitahadharisha vyombo mbalimbali vya habari ,kutoshawishika kuvunja Sheria na Kanuni zinazoongoza tasnia ya Habari ili kulinda heshima ya tasnia ya habari na kuhakikisha nchi inabaki na Amani.

Hata hivyo Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ya mwaka 2003 Kifungu cha 28 (1) kimempa Mamlaka Waziri wa mwenye dhamana na masuala ya Habari kufungia vyombo vya habari vinavyoweza kurusha hewani habari za uchochezi.
Share:

Lowassa, Mbowe, Mnyika wakamatwa

 
Viongozi wa Chadema wamekamatwa na polisi na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano.
Akizungumzia kukamatwa kwa viongozi hao Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema waliokamatwa na polisi kwa ajili ya mahojiano ni Edward Lowassa, Freeman Mbowe, John Mnyika, Dk Vincent Mashinji na  Said Issah                        
“Tulikuwa kwenye kikao cha Kamati Kuu kilichojumuisha wajumbe na wabunge kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya chama. Jumla ya wajumbe walikuwa 170. Tukiwa kwenye kiako walikuja watu wanasema tunatakiwa polisi kwa sababu tumekiuka agizo la lilitokataza mikutano.”
Share:

ANGELA KAIRUKI: SERIKALI KUAJIRI WATUMISHI ELFU 71 MWAKA HUU WA FEDHA 2016

 


"SERIKALI ITAAJIRI WATUMISHI 71 ELFU MWAKA HUU WA FEDHA"
"ZOEZI LA UHAKIKI WA WATUMISHI HEWA LAKAMILIKA KWA 70%"
"WAAJIRIWA WATARAJIWA WASIHOFU AJIRA ZIPO TU"
Share:

ANGELA KAIRUKI: SERIKALI KUAJIRI WATUMISHI ELFU 71 MWAKA HUU WA FEDHA 2016

 


"SERIKALI ITAAJIRI WATUMISHI 71 ELFU MWAKA HUU WA FEDHA"
"ZOEZI LA UHAKIKI WA WATUMISHI HEWA LAKAMILIKA KWA 70%"
"WAAJIRIWA WATARAJIWA WASIHOFU AJIRA ZIPO TU"
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI TAREHE 29.8.2016





Share:

Sunday 28 August 2016

CHADEMA: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kuhusu picha zinazoashiria shari.
Yanayowakuta Chama cha Chadema Tanganyika Ndio hayo hayo yanayo endelea kuwakuta Chama cha CUF na Wafuasi wao tokea miaka 20 ya Vyama Vingi ianzishwe Zanzibar. CCm wamekuwa wakitumia uniform za CUF kwakufanya shari na mauwaji, uharibifu wa Mali n.k.. Ili wapate Justification yakuwazuia Wazanzibari kudai haki zao.
Ndugu Watanzania kutoka Zanzibar na Tanganyika, lazima tuwe makini sana na kuwajuwa Maadui zetu nini lengo lao la ku.post Picha zinazoashiria SHARI, VITA kwakutumia Bendera na Uniform za Chama cha Democratic na Maendeleo (CHADEMA). Hii ni njia moja yakuonyesha kwamba Watawala hawa Haramu ( Vidiktetor Uchwara) wanajaribu Kutumia UV-CCM na Jeshi la Wananchi kufanya mazoezi ya SHAri ambayo yanaonyesha Watu/ mtu amevaa uniform akiwa na silaha za jadi. Lengo la picha hizi Ni kwamba Serikali haina Ushahidi wowote ule ambao wanawasingizia Vyama vya Upinzani kwamba ni Wachochezi. Sasa wanachokifanya nikujaribu Kujenga Twaasira yakuonyesha kwamba wanaofanya Mazoezi ya kivita ni Wanachama wa Chadema na wanataka kuhatarisha Amani ya Inchi ili Wa-JUSTIFY Kamata kama ya Wananchi wa vyama vya Upinzani vya Siasa na Viongozi wao. Kwataarifa zaidi hebu someni habari hii iliopo hapo chini:
Jioni hii zimeonekana picha za mtu ambaye anadhaniwa kuwa ni mwanamke ameshika silaha za jadi mikononi mwake, panga, upinde na mishale huku akiwa amevalia nguo zenye rangi na nembo za CHADEMA.
Mtu huyo ameonekana pia akifanya mazoezi huku nyuma yake kukiwa na bendera ya CHADEMA ambayo imeshikwa na watu ‘wanaoficha’ sura zao nyuma ya bendera hiyo.
Kwa mtazamo wa haraka picha hizo zinamuonesha mtu huyo akijiandaa kwa ‘shari’ ambayo bila shaka anaijua mwenyewe au na wenzake walioshirikiana naye kupiga hizo picha.
Tungependa kutaarifu umma kuwa picha hizo zisihusishwe kwa namna yoyote ile na Operesheni UKUTA na maandalizi ya Septemba 1 kwa ajili ya mikutano ya hadhara na maandamano ya amani kwa mujibu wa Sheria za Nchi, ambayo inatarajiwa kufanyika katika kutimiza wajibu na haki za kikatiba za Watanzania.
Tumeona ni vyema kuweka sawa jambo hili baada ya watu mbalimbali wapenda haki ambao wangependa kuona Operesheni UKUTA na Septemba 1, zikifanyika na kuendelea kwa amani ili kufikisha ujumbe mzito na muhimu unaokusudiwa kwa maslahi na matakwa ya Watanzania, kuanza kuhoji kuhusu picha hizo.
Lakini pia tumeamua kutozipuuzia picha hizo baada ya kuona dalili za maadui wa demokrasia na watetezi wa uvunjifu wa Katiba na Sheria za Nchi unaoendelea kufanywa na watawala kupitia kauli, matamko na vitendo, wakilenga kuzitumia picha hizo kuwatisha watu na bila shaka kujazia jazia vinyama kwenye vihoja vyao na propaganda nyepesi za kupindisha maudhui na madhumuni ya Septemba 1 na UKUTA kwa ujumla.
Chama kinalaani vikali matumizi ya nembo za chama yaliyofanywa na watu hao kwa namna inayoashiria shari na vurugu huku ikihusishwa na Operesheni UKUTA na Septemba 1. Waliozipiga na kuzisambaza mitandaoni wanajua makusudi yaliyowatuma kufanya hivyo na bila shaka watapaswa kuwajibika kwa walichofanya.
Tunapenda kusisitiza tena, kama ambavyo Chama kupitia kwa viongozi wakuu kimesema mara kadhaa sasa, Operesheni UKUTA na maandalizi ya Septemba 1, vitatekelezwa kwa misingi inayothamini na kuzingatia uwajibikaji kwa maslahi mapana ya Watanzania wote, ikiwa ni pamoja na kudai HAKI na KUPINGA UVUNJAJI WA KATIBA na SHERIA za Nchi kwa njia za AMANI.
Tumaini Makene
Mkuu wa Habari na Mawasiliano CHADEMA
Share:

JESHI LA KUJENGA TAIFA(JKT):TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKANUSHA VIJANA WA KUJITOLEA KURIPOTI KAMBINI



  TAARIFA KWA UMMA

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) linapenda kukanusha taarifa potofu zinazosambazwa kwa njia ya ujumbe mfupi kwenye baadhi ya simu za mkononi na mitandao ya kijamii inayoeleza kuwa” JKT linawataka vijana waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa Kujitolea mwaka 2016, waripoti ofisi za wakuu wa mikoa kati ya terehe 03 – 07 Septemba 2016, tayari kwa kupelekwa kwenye Makambi ya mafunzo ya JKT”.

Taarifa hiyo siyo sahihi na wananchi wanatakiwa kuzipuuza. Utaratibu utakapokamilika wa kuwachukua Vijana hao, JKT itawatangazia kupitia vyombo rasmi vya habari na siyo kwa njia ya simu za mkononi.

Aidha JKT kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Nchini inafuatilia kujua ni mtu gani au kikundi gani kimehusika na upotoshaji huo wa taarifa ili hatua kali za kisheria kuchukuliwa.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya JKT
27 Agosti 2016

Share:

Mwalimu Mbaroni kwa Kuwapa mimba Wanafunzi Watano

 
Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Nyakabungo wilayani Nyamagana mkoani Mwanza, anatuhumiwa kuwapa ujauzito wanafunzi watano wa shule hiyo.
Wanafunzi hao wamebainika kuwa na ujauzito, baada ya uongozi wa shule hiyo kuona mabadiliko kwenye miili yao na kuamua kuwapima afya.
Mkuu wa shule, Boniphace Mjuli amesema baada ya kujiridhisha kuwa wana ujauzito, waliwaandikia barua wazazi wao kuwaita shuleni kwa ajili ya kuwaeleza matokeo ya vipimo na kuchukua hatua stahiki.
Wakizungumzia tukio hilo, baadhi ya wazazi wa watoto waliokutwa na ujauzito wameiomba Serikali ichukue hatua kwa wanaume wote wanaokatisha ndoto za wanafunzi wa kike.
Mzazi Yusuph Yusuph amesema ili kuwajengea mazingira mazuri wanafunzi wa kike, lazima Serikali itekeleze sheria ya kuwakamata wanaume wenye tabia za kutongoza wanafunzi na wahukumiwe kifungo cha maisha jela ili iwe fundisho.
Share:

Wakurugenzi Watano Tpdc Wasimamishwa Kazi Kupisha Uchunguzi

Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI AGOSTI TAREHE 28.8.2016






Share:

Saturday 27 August 2016

Angalia Picha 30: ASKARI WA JESHI LA POLISI SHINYANGA WAKIFANYA MAZOEZI KUJIANDAA KUKABILIANA NA UHALIFU



Leo Jumamosi,Agosti 27,2016 Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limeendelea kufanya ya mazoezi ya utayari wa kukabiliana na vitendo vya kihalifu.
Akiongoza mazoezi hayo,Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro amesema mazoezi hayo aliyoyataja kwa jina la Kiingereza ““Route Match” ni ya kawaida kwa ajili ya kujiweka tayari kukabiliana na uhalifu unaoweza kujitokeza. 
Kamanda Muliro amesema wamekuwa wakifanya mazoezi mara kwa mara lakini kilichofanyikani kubadilisha muda wa kufanya mazoezi na wataendelea kufanya kila siku za Jumamosi. 
“Huu ni mfumo huu ni wa kawaida kwa mujibu wa sheria na kanuni zinazolisimamia jeshi la polisi..tumefanya matembezi yanayohusiana na ukakamavu,yanayojenga ujasiri kwa askari kumsaidia katika utekelezaji wa majukumu yake,kwa hiyo kwa wananchi wanaoishi karibu na kambi ya jeshi siyo wageni wa mambo haya ambayo huwa tunayafanya siku za Jumamosi ”,alieleza Muliro. 
“Kilichofanyika leo tumepita mtaani asubuhi/mchana badala ya usiku/alfajiri (saa 11 hadi saa 1.30) kama vile tumekuwa tukifanya lakini lengo ni moja tu,watambue kuwa jeshi lao la polisi liko imara katika kuwalinda raia na mali zao,kusimamia sheria za nchi na askari mzuri ni yule mkakamavu,mwepesi ana uwezo wa kufikiri haraka kujua kile anachokitekeleza kimesimamia sheria gani”,aliongeza Muliro. 
Alisema mazoezi hayo ni ya kawaida na kusisitiza kuwa kwa wananchi ambao siyo wahalifu na walio wema wamefurahia mazoezi hayo. 
Askari polisi wakiongozwa na kamanda Muliro walipita katika maeneo mbalimbali mjini Shinyanga na maeneo huku wakiwa na vifaa mbalimbali vya jeshi hilo ikiwemo magari,silaha na magari ya maji ya kuwasha. 
Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde alikuwepo maeneo mbalimbali walikopita askari polisi mjini Shinyanga,ametuletea picha 31…Shuhudia hapa chini 
Hapa ni katika kambi ya jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga-Kulia ni Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akitoa maelekezo kwa askari wa jeshi hilo kabla ya kuanza mazoezi mtaani leo majira ya saa tatu asubuhi
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akieleza kuhusu mazoezi ya "Route Match"
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akisisitiza jambo kabla ya kuanza kufanya mazoezi
Askari polisi wakiwa kambini kabla ya kuanza kufanya mazoezi mtaani
Askari polisi wakijiandaa kuanza kufanya mazoezi
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akifanya mazoezi na askari polisi wa jeshi hilo mjini Shinyanga
Askari polisi wakiendelea na mazoezi mtaani
Askari polisi wakiwa katika gari la maji ya kuwasha
Mazoezi yanaendelea katika eneo la Phatom mjini Shinyanga
Gari la maji ya kuwasha likiwa barabarani
Magari ya polisi yakiwa barabarani
Mazoezi yanaendelea
Askari polisi wakiwa ndani ya gari 
Wananchi wakiendelea na shughuli zao huku askari polisi wakiendelea na mazoezi yao
Wananchi wakiendelea na safari zao
Askari polisi wakiendelea na mazoezi yao
Askari wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga wakiwa kambini baada ya kumaliza kufanya mazoezi 
Askari polisi wakiwa kambini baada ya kumaliza kufanya mazoezi mtaani
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akizungumza kambini ambapo aliwaambia askari polisi kuwa watakuwa wanafanya mazoezi ya namna hiyo kila siku za Jumamosi
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akisisitiza jambo
Maafisa wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga wakiwa kambini baada ya kumaliza kufanya mazoezi
Askari polisi wakiwa kambini
Askari polisi wakimsikiliza kamanda Muliro
Kamanda Muliro akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza kufanya mazoezi
Waandishi wa habari wakiwa kambini
Askari polisi wakijiandaa kutawanyika baada ya kumaliza kufanya mazoezi.
Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger