Saturday 2 April 2016

New AUDIO | Baghdad Ft. Profesa J Don Koli & Nikki Mbishi - Mtazamo (Remix) | Download

Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WATANZANIA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA JESHI LA MAGEREZA 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
(Jeshi la Magereza)

TANGAZO LA KUITWA CHUONI
Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania Bara anawatangazia wafuatao kuwa wamechaguliwa kujiunga na Jeshi la Magereza baada ya Usaili kufanyika katika kambi mbalimbali za JKT.  Usaili huu ulihusu vijana waliohitimu Shahada ya Kwanza, Stashahada, Astashahada, Kidato cha Sita na Kidato cha Nne.
 
Wahusika wote wanatakiwa kuripoti katika Ofisi za Wakuu wa Magereza Mikoa mara wapatapo taarifa hii tayari kwa safari ya kwenda Chuo cha Mafunzo ya Awali kilichopo Kiwira Tukuyu Mkoani Mbeya.
 
Mafunzo yanategemewa kuanza tarehe 12 Machi, 2016 hivyo mwisho wa kuripoti chuoni ni tarehe 14 Machi, 2016.  Yeyote atakayeshindwa kuripoti kwa tarehe iliyotamkwa kwenye tangazo hili hatapokelewa.
 
Wahusika wanatakiwa kuzingatia mambo yafuatayo:-
1.Walete vyeti halisi vya masomo na vya kuzaliwa, vikiwa na pamoja na nakala 5 za kila cheti.
2.Picha (Passport size) za rangi 5 za hivi karibuni.
3.Chandarua cheupe cha duara ft 31/2, shuka nyeupe mbili, mto wenye foronya nyeupe zisizo na maua/maandishi.
4.Fedha taslimu Tshs.90,000/=.
5.Kalamu za wino,  za risasi na madaftari ya kutosha.
6.Cheti cha afya kutoka kwa hospitali ya Serikali.
7.Nguo za kiraia za kutosha sweta, raba (Brown au nyeusi) na soksi
8.Kwa wale wenye kadi za Bima waje nazo na
9.Kila mwanafunzi atajitegemea kwa nauli ya kwenda.

Tangazo hili linapatikana kwenye mbao za matangazo zilizopo Ofisi za Magereza, tovuti ya Magereza kwa anwani ya www.magereza.go.tz sanjari na blog ya Magereza kwa anwani ya www.magereza.blogspot.com
 
Imetolewa na Kamishna Jenerali wa Magereza.
 
SIGNED
Dr. J. A. Malewa  -  CP
Kny:  KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA
 
 
<<<<<<<<BONYEZA HAPA KUONA MAJINA YOTE>>>>>>

<<<<<<BONYEZA HAPA KWA MAJINA YA NYONGEZA>>>>
Share:

Official VIDEO | Mh Temba x Jokate Mwegelo​ - Fundi

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

https://youtu.be/FmNBsdof0io
Share:

NAFASI ZA KUJIUNGA NA NGAZI YA CHETI NA DIPLOMA CHUO CHA MARIAN(MARUCO) 2016/17

Share:

SERIKALI KUPITIA WIZARA YA AFYA KUAJIRI WATUMISHI WA AFYA (AJIRA ZA AFYA 2015/16) 10000

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Serikali kuajiri watumishi wa afya 10,000

Serikali inatarajia kuajiri watumishi 10,000 wa sekta ya afya katika mwaka ujao wa fedha ili kukabiliana na upungufu wa wataalamu wa fani hiyo nchini.

Hayo yalisema jana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamis Kigwangalla wakati akizindua majengo yatakayotumika kufundishia wakunga na wauguzi yaliyokarabatiwa na Chuo Kikuu cha Aga Khan (AKU).

Dk Kigwangalla alisema Serikali ina upungufu wa asilimia 51 ya wakunga na wauguzi na ili kukabiliana nao, imeamua kuongeza idadi ya wanafunzi katika vyuo vya afya.

“Nakipongeza Chuo Kikuu Cha Aga Khan kwa kuzalisha wataalamu wa fani ya ukunga na uuguzi kwa ngazi ya shahada na bado Serikali inahitaji kuwa na vyuo vingi vya afya ili kupunguza tatizo la uhaba wa wataalamu wa afya,” alisema.

Awali, Makamu wa Rais na Ofisa Mkuu wa Fedha wa AKU, Al-Karim Haji alisema chuo hicho kimepatiwa Sh2.9 bilioni na Benki ya Ujerumani (KFW) kwa ajili ya kukarabati vyumba na majengo ya kufundishia watalaamu hao.

“Lengo letu ni kuongeza ubora wa watumishi wa fani ya ukunga na uuguzi kwa sababu hapa nchini tumebaini kuwa kuna upungufu mkubwa wa vifaa na vyuo vya kisasa vyenye ubora wa kufundisha,” alisema Haji.

Alisema kupitia uboreshaji huo, AKU itachukua wauguzi na wakunga ambao wako kazini na kuwafundisha mara mbili kwa wiki ili waongeze ujuzi na kuwawezesha kupata shahada kwa wale wenye stashahada.

“Katika kipindi cha miaka 10, Chuo Kikuu Cha Aga Khan kimefanikiwa kuwafundisha manesi zaidi ya 600 katika ngazi ya stashahada na shahada,” alisema Haji.

Waziri wa Uchumi na Maendeleo wa Ujerumani, Dk Gerd Muller alisema walitoa kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kuboresha sekta ya afya nchini.

Katibu Mkuu mstaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Dk Richard Sezibera alikipongeza chuo hicho kwa kuboresha sekta hiyo na mchango wake unaonyesha namna wataalamu wa afya watakavyopata elimu bora ambayo inakidhi viwango vya kimataifa.
Share:

Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa Naye Afikishwa Mahakamani Leo Kwa Tuhuma Za Rushwa

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa amepandishwa kizimbani mahakama ya Kisutu leo akituhumiwa kuomba rushwa ya Shilingi  milioni 30  akiwa kwenye Kamati za Bunge.
Ndasaa  anakuwa  mbunge  wa  nne  wa  CCM kupandishwa  mahakamani  kwa  tuhuma  za  rushwa  baada  Mbunge wa Mwibala, Mh.Kangi Lugola,Mbunge wa Mvomero Mh.Sadiq Murad pamoja na Mbunge wa jimbo la Lupa Mh.Victor Mwambalaswa  kupandishwa  mahakamani jana kwa tuhuma za kuomba rushwa ya milioni 30 toka kwa mkurugenzi wa Gairo  ili taarifa yake ipitishwe bila kujadiliwa.
Share:

Bosi wa Zamani wa TRA na Wafanyakazi wa StanBic Benki Wafikishwa Mahakamani

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Aliyekuwa Kamishna Mkuu wa TRA Dkt. Harry Kitilya na wenzake Shose Sinare na Sioi Solomoni wamefikishwa mahakamani (Kisutu DSM) leo kwa mashitaka 8 ikiwemo tuhuma za kujipatia fedha kiasi cha Dola za Marekani milioni 6, mwezi Machi mwaka 2013, ili kufanikisha mkopo kutoka Benki ya Stanbic kwenda serikalini.

Watuhumiwa hao wamekana makosa na kurudishwa rumande hadi April 8, 2016

Share:

TAKUKURU Kuwafikisha Mahakamani Kamishna Mkuu wa Zamani wa TRA na Wafanyakazi Wawili wa Stanibic Benki

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) leo tarehe 1/4/2016 imewafikisha Mahakamani aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania na Mwenyekiti wa ‘Enterprise Growth Market Advisors Ltd’ (EGMA), Bw. Harry Msamire Kitilya; aliyekuwa Mkuu wa Idara ya Ushirikiano na Uwekezaji wa Benki ya Stanbic Tanzania, Shose Mori Sinare pamoja na Aliyekuwa Mwanasheria wa Benki ya Stanbic Tanzania, Bw. Sioi Graham Solomon.

Washtakiwa wote wanashtakiwa kwa makosa ya:- Kula njama na kujipatia kwa udanganyifu kinyume na kifungu Na. 384 cha  Kanuni ya Adhabu (Cap 16 R.E. 2002) ; Kughushi kinyume na kifungu Na. 333,335 (a) na 337 cha Kanuni ya Adhabu (Cap 16 R.E 2002) ; Utakatishaji wa fedha haramu kinyume na kifungu Na. 12 (a) 13 (a) cha Sheria ya ya Utakatishaji fedha Na. 12 ya Mwaka 2006 ‘Anti- Money Laundering Act’.

Mashtaka hayo yalisomwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Mhe. Hakimu Emirius Mchauro. Kwa upande wa Jamhuri kesi hii inasimamiwa na Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Serikali Herman Tibabyekomia, Christopher Msigwa na  Mwendesha Mastaka wa TAKUKURU Stanley Luoga. Washtakiwa wanatetewa na Wakili wa Kujitegemea Ringo Tenga, Rosai Mbwambo, Semo na Nyaisa.

Washitakiwa wote watatu wamepelekwa rumande, wamekosa dhamana kwani  Kifungu Na. 148 (5) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) Kinazuia utoaji wa dhamana kwa washtakiwa wa Utakatishaji wa fedha haramu. Kesi hii itatajwa tena tarehe 8/4/2016.

IMETOLEWA NA
OFISI YA AFISA UHUSIANO
TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA, MAKAO MAKUU
1 APRIL, 2016.
Share:

Bakwata Wakabidhi Msaada wa Madawati 500 kwa Serikali

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

BARAZA Kuu la Waislaam nchini (Bakwata) kwa kushirikiana na Shia wamekabidhi msaada wa madawati 500 kwa serikali ili kusaidia upungufu wa madawati katika shule za msingi na sekondari.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi madawati, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Bin Zuberi amesema kuwa katika msaada hawaangalii suala la dini kinachoangaliwa ni watakaolia madawati hayo ni watanzania.

Mufti Zuberi amesema kuwa wamechangia katika kusaidia serikali kauli mbiu ya elimu bure katika kuweza kusaidia watanzania wapate elimu.

Amesema kuwa wataendelea kushawishi waislaam katika kuendelea kuchangia elimu ili watoto wapate elimu iliyo bora kwa kuwa  serikali pekee yake haiwezi kutatua changamoto zote za elimu.
 
Mwenyekiti wa SHIA, Azim Dewj amesema kuwa amepeleka msaada huo katika bakwata ikiwa ni kuonyesha umoja na jinsi ya kusaidia serikali katika upande wa elimu.

Amesema kuwa ataendelea kushawishi matajiri wenzake kuangalia namna watakavyosaidia katika sekta ya elimu upande wa madawati kuwa kila mwaka kuweza kuchangia madawati 1000.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi akizungumza kwa niaba ya Waziri Mkuu amesema kuwa msaada wa madawati hayo ni mkubwa kutokana na changamoto iliyopo mbele yao.
 
Amesema kuwa idadi ya wanafunzi wa darasa la kwanza kuandikishwa umeongezeka  kutokana na mpango wa elimu bure  hivyo serikali kupata madawati ni jambo la furaha na kuwataka wadau wengine kujitokeza kuchangia madawati kutokana na mahitaji kuwa makubwa.
Share:

Rais Magufuli Amteua Hilda Nkanda Kuwa Kamishna Wa Kazi

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bi. Hilda Nkanda Kabisa kuwa Kamishna wa kazi.

Kabla ya Uteuzi huo, Bi. Hilda Nkanda Kabisa alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Bi. Hilda Nkanda Kabisa, anachukua nafasi iliyoachwa na Bw. Sauli Kinemela ambaye amestaafu kwa mujibu wa Sheria.

Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Siza D. Tumbo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC).

Kabla ya Uteuzi huo, Prof. Siza Tumbo alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) aliyebobea katika masuala ya Uhandisi Mitambo ya Kilimo.

Prof. Siza Tumbo anachukuwa nafasi iliyoachwa wazi na Evarist Ng'wandu ambaye alistaafu kwa mujibu wa sheria.

Uteuzi huu wa watendaji wakuu wa taasisi za serikali umeanza tarehe 26 Machi, 2016.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Chato

01 April, 2016
Share:

MSHAHARA WA RAIS MAGUFULI NI MILION 9,500,000/=

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli jana alimpigia simu mtangazaji wa kipindi cha ‪Clouds360‬ cha ‪‎CloudsTv‬, Hudson Kamoga baada ya kusikia watu wanazungumzia kuhusu mshahara wa Rais.

Rais alisema mshahara alioukuta na ambao analipwa  ni milioni 9 na laki 5 (9,500,000)   na  wala  sio milioni 30  kama  wanavyodai wapinzani. Amelazimika kuyasema hayo wakati wa uchambuzi wa magazeti kupitia Clouds360.

Aliahidi akirudi kutoka likizo yupo tayari kuonyesha nyaraka za malipo ya mshahara wake.

Gazeti  la  Nipashe toleo  la jana  lilikuwa na habari  iliyowanukuu Tundu Lissu  na  Zitto Kabwe wakitaka Rais Magufuli ataje Mshahara wake na aweke wazi kama anakatwa kodi ili kuondoa sintofahamu iliyopo .
 
Hivi karibuni, Dk. Magufuli ameahidi kupunguza mishahara ya baadhi ya vigogo inayozidi shilingi milioni 15 ili mtumishi anayepata mshahara mkubwa zaidi usizidi kiasi hicho.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL 02 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
 MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL TAREHE 02/04/2016






Share:

Friday 1 April 2016

EWURA-TANESCO YASHUSHA BEI YA UMEME 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Mamlaka ya Usimamizi wa Huduma za Nishati na Maji EWURA imetangaza kushusha bei za umeme kuanzia leo kwa watumiaji wote wa viwango tofauti.

Kushuka huko kwa bei ya umeme ni kutokana na ombi la Shirika la Umeme Tanzania TANESCO kutaka bei za umeme zipunguzwe sambamba na hilo gharama za huduma kwa baadhi ya wateja zimeondolewa.

Bei mpya kwa watumiaji wadogo ni sh.100 kwa uniti, watumiaji wa kati ni sh.292 toka 298 ya zamani.Wafanyabiashara wadogo ni sh. 195 toka sh. 200 ya hapo awali.

Bei mpya kwa wafanyabiashara wa kati ni sh.157 toka sh. 159. Wanaonunua kwa wingi (bulk) ni sh. 152 toka sh. 156 ya hapo awali
Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA NYONGEZA YA WANAFUNZI WA ST.JOSEPH WALIOHAMISHIWA SUA APRIL 2016

Share:

TAARIFA MUHIMU KWA WANAFUNZI WALIOHAMISHIWA UDOM KUTOKA ST.JOSEPH 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Logo

Transferred Students from St. Joseph University to The University of Dodoma


IMPORTANT ANNOUNCEMENT
TRANSFERRED STUDENTS FROM ST. JOSEPH UNIVERSITY TO THE
UNIVERSITY OF DODOMA

This is to inform all students transferred from St. Joseph University in Tanzania to The University of Dodoma that, they are required to report to their respective Colleges (College of Education and College of Natural and Mathematical Sciences) at the University of Dodoma on Saturday 9th April 2016. effectively from 8.00am to 6.00pm.
All students are required to pay tuition fees and direct costs for academic year 2015/2016. Students who will fail to comply with this notice will not be allowed to join the university. Payment must be made before students reporting to the University as follows:
Share:

Mkazi wa Mwananyamala Apandishwa Mahakamani Kwa Kutishia Kumuua Rais Magufuli Kwa Kujitoa Mhanga

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Kondakta wa daladala, Hamim Seif (42) mkazi wa Mwananyamala Ujiji, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shtaka la kutishia kumuua Rais John Magufuli kwa maneno.

Seif alipandishwa kizimbani mahakamani hapo jana mchana na kusomewa shtaka hilo na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kenneth Sekwao.

Mshtakiwa huyo alikana shtaka hilo na Hakimu Mkazi, Hellen Liwa alisema kuwa dhamana ya mshtakiwa huyo iko wazi na alitakiwa kuwa na wadhamini wawili, kutoka taasisi ya Serikali inayotambulika, ambaye atasaini hati ya dhamana ya Sh2 milioni.

Licha ya dhamana yake hiyo kuwa wazi, mshtakiwa huyo alishindwa kukamilisha masharti hayo kwani baada ya kusomewa mashtaka alipoulizwa kama alikuwa na wadhamini alishindwa kuwapata.

Akimsomea shtaka linalomkabili, Wakili Sekwao alisema kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Machi 10 mwaka huu katika baa ya Soweto, Makumbusho wilayani Kinondoni kinyume cha kifungu cha 89 (2) (a) na kifungu cha 35 cha Sheria ya Kanuni za Adhabu.

Wakili Sekwao alisema akiwa katika baa hiyo, mshtakiwa alitishia kumuua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Magufuli kwa maneno kwa njia ya kujitoa mhanga.

Kwa haya mambo anayoyafanya Rais Magufuli, mimi nimo tayari kujilipua kwa kujitoa mhanga ili kumuangamiza,” alisema Wakili Sekwao akimnukuu mshtakiwa huyo.

Hata hivyo, Wakili Sekwao alisema upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na akaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kesi hiyo kutajwa.
Share:

MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRIL TAREHE 1/4/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Magazeti ya Leo April 1, 2016


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger