Thursday 3 March 2016

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MARCH 03 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

RATIBA YA USAILI WA MITIHANI YA MCHUJO WA KADA ZA MJNUAT UTAKAOFANYIKA CHUO KISHIRIKISHI CHA ELIMU DAR ES SALAAM (DUCE) TAREHE 05/03/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

TANGAZO LA KAZI DEC 29, 2015 AWAMU YA KWANZA: SAA MOJA KAMILI ASUBUHI 
UKUMBI
KADA
LECTURE THEATRE  “A”
Ø  HUMAN RESOURCE OFFICER AND ADMNISTRATIVE
Ø  SENIOR ACCOUNTANT   
LECTURE THEATRE  “B”
Ø  SYSTEM AND NETWORK ADMINISTRATION  
Ø  WARDEN II                          
Ø  RECORDS MANAGEMENT ASSISTANT I 
LECTURE THEATRE  “C”
Ø  PLANNING OFFICER II     
Ø  ACCOUNTANT II    
Ø  ESTATE OFFICER II           
  AWAMU YA PILI: SAA TATU NA NUSU ASUBUHI
UKUMBI
KADA
LECTURE THEATRE  “A”
Ø  PROCUREMENT AND SUPPLIES OFFICER II             
LECTURE THEATRE  “B”
Ø  ASS.  PROCUREMENT AND SUPPLIES OFFICER II 
Ø  PUBLIC RELATION OFFICER II       
LECTURE THEATRE  “C”
Ø  INTERNAL AUDITOR II      
Ø  OFFICE ASSISTANT          
Share:

Wednesday 2 March 2016

MPYA:HAYA HAPA MAJINA SECOND SELECTION YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2016-DAR ES SALAAM

Share:

CHADEMA Kususia ziara na Vikao vya Maendeleo Dar es Salaam

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesusia ziara ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika manispaa za Temeke, Kinondoni na Ilala na kuthibitisha kutoshiriki katika kikao cha bodi ya barabara kinachotarajiwa kufanyika leo kwa kile wanachodai kushinikiza kuachiwa kwa madiwani na mbunge ambao wanaeshikiliwa na jeshi la polisi.

Akielezsea hatua hiyo jana, Meya wa Manispaa ya Kinondoni Boniface Jacob alisema kuwa hawaoni sababu ya kuendelea na vikao mbalimbali vya jiji wakati hawajui hatma ya wenzao ambao mpaka sasa wanashikiliwa na polisi na wengine wanaitwa kufika kituoni hapo kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kusababisha fujo katika zoezi la uchaguzi wa meya wa Jiji la Dar es Salaam.

Kikao kikubwa cha kujadili mipango ya maendeleo ya jiji la Dar es Salaam kinatarajiwa kufanyika leo  ambapo mada kuu itakuwa ni ujenzi wa barabara katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.
Share:

Polisi Wafanya Upekuzi Nyumbani Kwa Halima Mdee

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam jana lilifanya upekuzi mkubwa katika nyumba ya Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema) baada ya kumtilia shaka kuwa na nyaraka muhimu za vikao vya uchaguzi wa Meya wa Jiji hilo.

Kikosi cha jeshi hilo kilifika katika nyumba ya mbunge huyo majira ya saa tisa alasiri na kufanya mazungumzo na Mwanasheria wake, John Mallya ambapo baada ya kukamilisha taratibu za kisheria walianza zoezi la upekuzi uliochukua zaidi ya saa moja.

Kiongozi wa kikosi hicho cha Polisi, aliwaambia waandishi wa habari kuwa walilazimika kufanya upekuzi katika nyumba hiyo baada ya kusadikika kuwa wakati wa vurugu zilizotokea katika ukumbi wa Karimjee jijini humo wikendi iliyopita kufuatia kuahirishwa kwa uchaguzi wa Meya wa Jiji, Mdee aliondoka na faili muhimu lenye madokezo yanayohusu uchaguzi huo.

Hata hivyo, baada ya kukamilisha upekuzi huo, Polisi walijiridhisha kuwa hakukuwa na nyaraka hizo ndani ya nyumba hiyo wala kitu chochote ambacho wangekitilia shaka licha ya kukuta nyaraka nyingi za mbunge huyo. Hivyo, walitoa cheti maalum cha kuthibitisha kuwa hakuwa na nyaraka zozote kinyume cha sheria.

“Wamekagua nyaraka zote. Madai yao ni kuwa Halima alimpora au alichukua nyaraka za kiongozi wa Jiji, lakini wamekuta hakuna jambo lolote ambalo linatiliwa shaka. Na wametoa Certificate inayoonesha kwamba hakuna chochote ambacho kimechukuliwa,” alisema Mwanasheria wa Mbunge huyo, John Mallya.

Mdee alishikiliwa na Polisi na kulala rumande juzi kutokana na tuhuma za kushiriki katika vurugu zilizotokea katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, Jumamosi, Februari 27.

Wengine wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi ni Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara.
Share:

Seleiman Jafo Amemvua Madaraka Meneja wa Mamlaka ya Maji Mji Mdogo wa Kisarawe

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Seleiman Jafo amemvua madaraka Meneja wa Mamlaka ya Maji Mji Mdogo wa Kisarawe mkoani Pwani, Listen Materu kwa kile alichodai ameshindwa kusimamia majukumu yake kikamilifu.

Pia, Jafo ameuagiza uongozi wa halmashauri hiyo kuondoa kero zinazolalamikiwa na wananchi hasa idara za ardhi, afya na elimu.

Akisikiliza kero za wapigakura wake juzi, Jafo alisema uchunguzi alioufanya ameubaini kwa miaka mitano iliyopita kuwa baadhi ya watendaji wa vitengo na idara wa halmashauri hiyo walikuwa hawawajibiki kwa makusudi, lengo lao lilikiwa ni kujenga chuki baina ya mbunge na wananchi jambo ambalo limefikia kikomo.

“Kuna watu waligeuza wilaya hii kama shamba la bibi, walikuwa wanatumia mali za umma kwa kufanya ubadhirifu sasa wasiseme kuwa wamesalimika, kama wamehama au wamehamishwa tutawafuata kokote walipo na watawajibishwa kwa mujibu wa sheria,” alisema.

Naibu waziri huyo alisema, kuwavua madaraka na kuwawajibisha watendaji wabovu hakutaishia kwa watumishi waliopo wilayani hapa, bali hata waliofanya ubadhirifu na kuhama au kuhamishiwa maeneo mengine.

Katika kuboresha wilaya hiyo na kuharakisha maendeleo, Jafo alisema ni wajibu wa halmashauri kuhakikisha inatenga maeneo ya ujenzi wa stendi, machinjio na utekelezaji wake ufanyike haraka na kuwataka iwapo watakabiliwa na changamoto za kukwamishwa mpango huo wasisite kuwasiliana naye.
Share:

Wauguzi sita Temeke wasimamishwa Kazi kwa kuuza gloves

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Naibu Waziri wa Afya, Dk Hamis Kigwangalla amewasimamishwa kazi wauguzi sita katika hospitali  ya  Temeke kwa kosa la kuomba rushwa.

Wauguzi waliosimamishwa ni Hadija Salum, Beatrice Temba, Agnes Mwampashe, Elizabeth Mwilawa, Mariam Mohamed na Marion Said, ambao walikuwa zamu katika wodi ya wajawazito wakati wa tukio hilo.

“Nimewasimamisha kazi wauguzi wote waliokuwa zamu jana (juzi) asubuhi, nakuagiza Msajili wa Baraza la Wauguzi uwasimamishe hadi utakapowasafisha kupitia kamati ya msajili,” alisema Dk Kigwangalla.

Mmoja wa wajawazito, Loshan Seif alisema alipowasili juzi asubuhi kwa ajili ya kujifungua, muuguzi mmoja wa zamu alimtaka kulipia Sh5,000 za gloves.

“Siku zote huwa natumia bima lakini jana (juzi) wakaniambia hawatumii, nitoe Sh5,000 za gloves, baadaye niliambiwa natakiwa kuwa na uzi wa mshono, sindano na vingine hivyo kama sina nitoe fedha,” Seif.

Dk Kigwangalla alifanya ziara ya ghafla hospitalini hapo jana saa 9.00 alasiri.

Akizungumza jana alasiri baada ya kufanya ziara ya ghafla Hospitalini hapo na kupata malalamiko hayo kutoka kwa wanawake waliojifungua.

“Mama anaambiwa atoe fedha ya gloves Sh5,000 wakati dukani zinauzwa Sh1,000, nataka liwe fundisho kwa wote wanaotuongezea vifo vya wajawazito kwa tamaa ndogondogo,” alisema Kigwangalla.

Katika ziara hiyo, Dk Kigwangalla alishuhudia ubovu wa vyumba viwili vya upasuaji na kutoa maelekezo kwamba, virekebishwe ndani ya miezi sita.

“Hali ni mbaya ndani ya hizi ‘theater’ zote mbili zifanyiwe ukarabati iwapo itashindikana nitazifunga, lazima ziwe na hadhi yake na nitakuja kukagua,” alisema.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO MARCH 02 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Tuesday 1 March 2016

HII NDIO BEI MPYA YA PETROLI,DISELI NA MAFUTA YA TAA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Felix Ngamlagosi amesema ‘kuanzia tarehe 2 Machi bei za mafuta zimebadilika ikilinganishwa na toleo lililopita la Februari 2016.
Kwa Machi 2016 bei ya rejareja za petroli imepungua Tsh 31 kwa lita sawa na 1.70%, Diesel imepungua Tsh 114 kwa lita sawa na 7.10% na mafuta ya taa yamepungua kwa Tsh 234 kwa lita sawa na 13.75%’
‘kwa kiasi kikubwa, kupungua huku kwa bei za mafuta kwenye soko la ndani kumetokana na kuendelea kushuka kwa bei za mafuta katika soko la dunia
Share:

MPYA:TAARIFA KWA WANAFUNZI WALIOHAMISHWA TOKA ST.JOSEPH ARUSHA TO MWENGE UNIVERSITY(MWECAU) 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Announcement to all Transfer Students from St. Joseph - Arusha Campus to MWECAU


You are informed to report to the University on Monday 7th March 2016 at 9:00 am for registrations and orientations. Remember to come with all credentials as directed by TCU.
Those from distant regions and who can not go home from Arusha and back to MWECAU on 7th March may report direct to MWECAU from thursady 3rd March 2016 . That will give them time to settle for accommodation as shown in the timetable below.
NB:
  • There are no directives for any payments yet.
  • Do not make any payment trough M-pesa, Tigo Pesa or Artel Money to the University
Issued by
Athanas Sing’ambi,
Public Relations Officer
                                          Orientation Timetable
Date Time Event Participant Venue
Thu 3 – Sun 6/03/2016 09:00am – 16:00pm Arrival and accommodation setting PRO & Admission Officer At the gate
Mon 7/3/2016 09:00am -12:00pm Campus Tour PRO & Admission Officer New Hall
14:00pm -16:30Pm General Meeting and Introduction Remarks VC, DVCAA, DVCAF, Deans & Directors and All staff Present New Hall
Tue 8/3/2016 08:00am- 16:30pm Issuing registration numbers, Temporary IDs and Agreement form to the Students Admission officer, PRO, Dean of Students, Bursar ICT
Wed 9/3/2016 08:30am- 12:00pm Introduction to UMS course Registration procedures ICT team ICT
12:00pm- 16:30pm Online updating Details, Courses Registration and printing document to be submitted to Dean faculty of Science Students  
Thu 10/3/2016 08:00am- 09:30am Orientation- Dean of Students Fr. Deo, Ms Nacy New Hall
09:30am- 10:30am Orientation- Counseling Unit Chaplain & Counselor New Hall
11:00am-13:00pm Orientation- University Laws & Regulations Corporate Counsel New hall
14:00pm-16:00pm University examinations Examinations officer New Hall
Fri 11/3/2016 08:30am- 09:30am Orientation- Financial Matters DVCAF & Bursar New Hall
  10:00am- 12:30am Orientation- Academic Matters; Special Arrangement for the group DVCAA, Dean Faculty of Science, HODS & Academic Staff Science Departments New Hall
  14:00pm- 16:30pm Loan Issues Loans Officer New Hall
14/3/2016 08:00am- Classes begin without exception Timetable Lecturer room
Share:

Applications for Postgraduate 2016-17-UDOM

Share:

USAJILI WA WATAHINIWA WA KUJITEGEMEA WA CSEE NA QT 2016 UNAENDELEA KWA ADA YA KAWAIDA HADI TAREHE 31 MACHI 2016.

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
USAJILI WA WATAHINIWA WA KUJITEGEMEA WA CSEE NA QT 2016 UNAENDELEA KWA ADA YA KAWAIDA HADI TAREHE 31 MACHI 2016.
Share:

Dk. Kigwangalla aagiza kufungwa chumba cha upasuaji cha Hospitali ya Sanitas ya Mikocheni

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
[​IMG]
Naibu wa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla ameagiza kufungwa mara moja Chumba cha upasuaji cha hospitali ya Sanitas ya Mikocheni Jijini Dar es Salaam baada ya kubaini kuwa na kasoro mbalimbali ikiwemo mfumo na ramani yake kimefungwa kwa kutokidhi vigezo vya kimataifa vya namna chumba hicho kinavyotakiwa kuwa.
Dk. Kigwangalla ametoa agizo hilo mapema jana Februari 29.2016, alipofanya ziara ya kushtukiza kwenye hospitali hiyo majira ya saa nane na nusu mchana ambapo baada ya kutembelea hospitali nzima na kushuhudia namna ya utolewaji wa huduma, hakuridhishwa na hali aliyokutana nayo kwenye chumba hicho na kutoa maagizo kwa Msajili wa Hospitali Binafsi, Dkt. Pamela Sawa kufunga chumba hicho mpaka uongozi wa hospitali hiyo utakapofanya marekebisho ya mapungufu yaliyopo.

“Chumba cha upasuaji hakiko sawa, siwezi kuvumilia kuacha chumba hiki kiko chini ya kiwango cha kimataifa. Rekebisheni chumba hiki kwa kutumia mfumo wa ramani wa wizara,” alieleza Dkt. Kigwangalla wakati wa kutoa maagizo kwa mmoja wa Ofisa wa Hospitali hiyo.

Aidha uongozi wa hospitali hiyo umepewa siku saba wawe wamewasilisha maelezo ya kutowalipa mishahara kwa kipindi cha miezi minne watumishi wake pamoja na jinsi wanavyoteketeza taka hatarishi za hospitali hiyo.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri huyo alipata malalamiko kutoka kwa watumishi hao ambao wamelalamikia kukatwa kwa makato ya mafao pasipo kupelekwa mahali husika kwa zaidi ya miaka mitatu na nusu.

Dkt. Kigwangalla alivitaja viwango vya chumba cha upasuaji kuwa kinatakiwa chumba cha kubadilishia mavazi,kunawa mikono,sehemu ya alama maalum zenye rangi nyekundu, meza ya upasuaji, ukanda wa usafi, chumba cha mapunziko baada ya kutoka kwenye upasuaji na chumba cha kusafishia vifaa vya upasuaji na kuna mashine maalum kwa kuwa kila upasuaji una idadi ya vifaa vinavyotumika.

Aliongeza kuwa viwango hivi vinawekwa ili kuepuka maambukizi.

Kwa upande wake Meneja Uendeshaji wa hospitali hiyo, Bi. Gean Cabral alisema watarekebisha mapungufu yaliyobainika pamoja na kufanya yale yote waliyoagiziwa baada ya tukio hilo.


Share:

Halima Mdee Atupwa Rumande,Mahakama yakana kuzuia uchaguzi wa Meya Dar

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Wakati mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee akilala rumande akihusishwa na vurugu zilizotokea Jumapili wakati uchaguzi wa meya wa Jiji la Dar es Salaam ulipokwama, Mahakama ya Kisutu imelikana zuio lililotumika kuzuia shughuli hizo. 
Uchaguzi huo ulipangwa kufanyika Januari 23, mwaka huu, lakini uliahirishwa ili kuandaa mfumo bora wa upatikanaji wajumbe kutokana na CCM kutaka kuingiza wapigakura nje ya waliotakiwa.

Ulikwama tena Februari 8, baada ya Halmashauri ya Jiji la Dar kubaini kasoro ya nyongeza ya majina 14 ya wajumbe kutoka manispaa za Ilala na Kinondoni.

Jumapili iliyopita ilikuwa ni mara ya tatu, kukwama tena kutokana na zuio lililosababishwa na kesi iliyofungiliwa na Saad Kimji na Suzan Masawe.

Hata hivyo, zuio hilo la muda la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu lililotumika kuahirisha uchaguzi wa meya na naibu meya wa Jiji, uliopaswa kufanyika Februari 27, 2016 limebainika kuwa ni batili.

Jana, Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Waliarwande Lema alisema Saad Kimji na Suzan Massawe walifungua kesi Februari 5, 2016 wakizuia uchaguzi wa meya na naibu wake ambao ulipaswa kufanyika Februari 8,2016.

Hakimu Lema alibainisha baada ya kufungua shauri hilo, Mahakama ya Kisutu iliweka zuio la muda ili kesi hiyo ianze kusikilizwa Februari 15, 2016 lakini walalamikaji hawakutokea mahakamani hivyo mahakama ikapanga kusikiliza kesi hiyo Februari 23, lakini hawakutokea pia.

Alisema kutokana na hali hiyo, aliliondoa shauri hilo mahakamani hapo na hivyo zuio hilo likawa limekufa. 
Aliongeza kuwa aliyesema Mahakama ya Kisutu imetoa zuio ni muongo na kwamba zuio halali ni lazima liwe na jina la Hakimu pamoja na sahihi.

Kukamatwa kwa Mdee 
Katika sakata la jana, Mdee na madiwani wengine watatu walilazwa rumande kutokana na kutuhumiwa kumshambulia Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando 
Wanatuhumiwa kufanya kosa hilo baada ya vuta nikuvute kutokea Jumapili iliyopita wakati shughuli ya kuwasaka viongozi hao wa jiji zilipokwaa kisiki kwa mara ya tatu, na CCM kuamua kukimbilia mahakamani.

Hali hiyo, ilizua tafrani kati ya madiwani na wananchama wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) baada ya uchaguzi huo kuahirishwa kwa zuio la muda la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. 
Tafrani hiyo ndiyo iliyosababisha vurugu ambazo inadaiwa kuwa katika purukushani hizo Mdee alimshambulia Mmbando mara baada ya kutangaza kuahirisha uchaguzi huo.

Polisi waliokuwa wanalinda usalama kwenye ukumbi wa Karimjee ambako uchaguzi huo ulitakiwa kufanyika, walimtoa nje Mmbando.

Akitoa maelezo mafupi kwa waandishi wa habari jana baada ya Mdee kuhojiwa kwa takriban saa sita, wakili wake , Profesa Abdalah Safari alisema mbunge huyo anashikiliwa kwa kosa hilo na atalala rumande.

“Kimsingi nilikuja kumsikiliza akitoa maelezo yake, ameshatoa lakini hakuna ushahidi wowote wa kosa analodaiwa kufanya la kushambulia Theresia,” alisema. 
Hata hiyo, Profesa Safari alisema kutokana na kosa hilo Mdee alikuwa na haki ya kuwekewa dhamana lakini polisi wamekataa.

“Mdee angeweza kujidhamini hata mwenyewe lakini wamekataa na kutokana na kosa hili anatakiwa kulala rumande kwa saa 48, zikizidi ina maana atapelekwa mahakamani,” alisema.

Profesa Safari, ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa Chadema Bara, alisema mbali na Mdee pia madiwani watatu wanashikiliwa na polisi kwa kosa hilo.

Madiwani hao ni Humphrey Sambo wa kata ya Mbezi, Ephraim Kinyafu (Saranga), wakati hakumtaja jina diwani wa tatu.

Awali wakati mahojiano hayo yalipoanza saa 7:00 mchana, taarifa kutoka kwa mmoja wa makada wa chama hicho zilieleza kuwa Mbunge wa Ukonga (Chadema), Mwita Waitara pia alitakiwa kufika kituoni hapo kutoa maelezo na anatarajiwa kuwasili leo.

Wakati wa polisi wakimhoji Mdee, wanachama wa Chadema walifika kituoni hapo, akiwapo Ester Bulaya, ambaye ni mbunge wa Bunda Mjini, Esther Matiko (Bunga Vijijini) na Henry Kilewo ambaye ni kanda wa Chadema.

Mapema jana mchana kabla ya Mdee kufikishwa kituoni hapo, ilielezwa kuwa polisi walizingira nyumba yake na kumtaka aende kituoni. 
Hata hivyo, mbunge huyo hakutoka hadi alipowasiliana na wakili wake ambaye alienda naye kituoni kwa ajili ya mahojiano.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMANNE MARCH 1 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger