Wednesday 4 November 2015

Tume ya taifa ya uchaguzi yaombwa kutoa tarehe ya kupiga kura jimbo la Lulindi.

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Tume ya taifa ya uchaguzi imeombwa kuweka wazi mapema iwezekanavyo tarehe ya kupiga kura ya ubunge jimbo la Lulindi vinginevyo ucheleweshaji huo unaathari kwa wapiga kura na vyama vyenye wagombea.
Tume ya taifa ya uchaguzi ililazimika kusitisha upigaji kura ya ubunge katika jimbo la Lulindi baada ya jina la mgombea wa chama cha wananchi CUF Amina Thomas Msham kukosewa katika karatasi za kupigiwa kura na kusomeka Msham Thomas Mcham.
 
Akizungumzia hilo mdhamini wa chama cha NLD ambaye pia ni mgombea wa jimbo la Lulindi Modesta Makaidi na uongozi wa chama cha mapinduzi mkoa wa Mtwara wameonyesha wasiwasi wao na kuzungumza haya.
 
Akizungumza kwa njia ya simu msimamizi wa uchaguzi jimbo hilo Beatres Maiko amesema analitambua hilo na kwa sasa yuko jijini Dar es Salaam kufuatilia suala hilo.
 
Jimbo la Lulindi limefanikiwa kufanya uchaguzi wa rais na madiwani, wagombea ubunge wanaotarajiwa kupigiwa kura ni Jerome Bwanausi wa CCM, Modesta Makaidi wa NLD na Amina Thomas Msham wa CUF, jimbo lingine linalotarajiwa kufanyiwa uchaguzi mkoani Mtwara ni la Masasi mjini kutokana na mgombea wake Emmanuel Makaidi kufariki dunia.
Share:

Marais 8 Kushuhudia Magufuli Akiapishwa

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

MARAIS wanane wa Afrika ni miongoni mwa viongozi mbalimbali kutoka nje ya nchi, watakaohudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya Tano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli. 

Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Magufuli ataapishwa rasmi kuwa Rais wa Awamu ya Tano kesho kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Dk Magufuli (56) alitangazwa mshindi wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu, baada ya kupata kura 8,882,935, sawa na asilimia 58.46 ya kura halali zilizopigwa, hivyo kumrithi Rais Jakaya Kikwete katika Ikulu ya Magogoni, ambayo tayari imeshakaliwa na marais wengine wanne. 

Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa iliyotolewa jana Dar es Salaam, sherehe za uapisho zitahudhuriwa na Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka mataifa mbalimbali, Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa na Kikanda na Wawakilishi mbalimbali kutoka nje ya nchi. Iliwataja miongoni mwa marais watakaohudhuria sherehe hizo ni Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini. 

Wengine ni Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Rais Filipe Nyusi wa Msumbiji na Rais Edgar Lungu wa Zambia. Taarifa ya Mambo ya Nje ilieleza kuwa Malawi itawakilishwa na Makamu wa Rais, Saulos Chilima wakati Namibia itawakilishwa na Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje, Netumbo Nandi-Ndaitwah. Aidha, Serikali ya China itawakilishwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala. 

“Vilevile nchi nyingine ambazo zimethibitisha kushiriki na zitawakilishwa na kati ya Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika au Balozi ni pamoja na Burundi, Comoro, Angola, Botswana, Lesotho, Madagascar na Mauritius. “Nyingine ni Norway, Oman, Sudan Kusini, Sweden, Umoja wa Falme za Kiarabu, Marekani, Uingereza, Shelisheli, Swaziland, Algeria, Misri, Benin, Denmark, Ethiopia, Finland, Ufaransa, Ghana, India, Japan, Kuwait, Uholanzi na Nigeria,” ilifafanua taarifa hiyo. 

Ilieleza kuwa Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa na Kikanda, waliothibitisha kushiriki au kutuma wawakilishi wao ni Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Afrika (AU), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Umoja wa Ulaya (EU) na Jumuiya ya Ukanda wa Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR). 

Wabunge wapya kuwasili Dar Katika hatua nyingine, wabunge wapya waliochaguliwa katika Uchaguzi Mkuu wanatarajiwa kuwasili Dar es Salaam leo kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk John Magufuli zitakazofanyika kesho. 

Akizungumzia kuwasili kwa wabunge hao, Ofisa Habari Mwandamizi wa Bunge, Prosper Minja alisema wabunge hao wanatarajiwa kuwasili leo Dar es Salaam wakiwa na vyeti vyao vya kuteuliwa kuwa wabunge vinavyotolewa na Msimamizi wa Uchaguzi wa eneo husika. 

“Tunategemea kesho (leo), wabunge wapya watawasili kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwa rais mteule na tunategemea waje na cheti hicho pamoja na kitambulisho kingine kinachomtambulisha,” alisema Minja. 

Alisema mara baada ya wabunge hao kuwasili, wanatakiwa kwenda Ukumbi wa Karimjee kwa ajili ya kutambuliwa na kupewa kitambulisho cha siku ya sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk Magufuli. 

Tamko la Jeshi la Polisi Wakati huo huo, Jeshi la Polisi nchini limejipanga kuhakikisha usalama na ulinzi unaimarishwa wakati wa kuelekea sherehe za kumwapisha Rais Mteule, Dk John Magufuli. 

Akizungumza jana Dar es Salaam, Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo, Makao Mkauu ya Polisi, Paul Chagonja alisema jeshi lake kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama, litahakikisha kunakuwa na usalama wa raia na mali zao katika kuelekea sherehe za kumuapisha Rais Mteule. 

“Niwaombe wananchi kutupa ushirikiano kwa kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi pindi waonapo vishawishi ama vitendo vyovyote vya uvunjifu wa sheria,” alisema Kamishna Chagonja. Aidha, Chagonja aliwataka wananchi kuendelea kuheshimu sheria za nchi na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa raia na mali zao. 

“Jeshi la Polisi linawataka wananchi kote nchini kuendelea kuheshimu sheria za nchi na kujiepusha na vitendo vya aina yoyote ile ambavyo vinaweza kuhatarisha usalama wa raia na mali ikiwemo maandamano yanayopangwa bila kufuata taratibu,” alisema Chagonja na kuongeza: “Jeshi la Polisi halitasita kuchukua hatua kali kwa mtu au kikundi chochote kitakachoonesha viashiria vya uvunjifu wa sheria ama kutaka kuvuruga amani ya nchi yetu.” 

Mbali ya kuwashukuru wananchi na wadau waliotoa ushirikiano kuhakikisha amani ya Watanzania inadumu katika kipindi cha uchaguzi na wakati huu wa kuelekea kuapishwa kwa Rais Mteule, alikiri jeshi hilo kuwashikilia watu kadhaa na baadhi yao kufikishwa mahakamani kutokana na kufanya makosa wakati wa uchaguzi. 

Bila kutaja idadi, Chagonja alisema, “Ni kweli kuna watu kadhaa tumewakamata kwa makosa mbalimbali wakati wa uchaguzi, kuna wengine wamefikishwa mahakamani, na kuna wengine bado wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi na wengine wamewekewa dhamana.” Imeandikwa na Ikunda Eric na Anastazia Anyimike.
Share:

TEMCO: Uchaguzi Ulikuwa HURU na wa HAKI

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

TIMU ya Waangalizi wa Ndani wa Uchaguzi Mkuu (TEMCO), imesema kwamba tathmini yao kwa Uchaguzi Mkuu uliofanyika hivi karibuni, unastahili hati ya uchaguzi safi, huru na wa haki ambao umeangukia alama A. 

Aidha, Temco imesema kwamba hata hivyo ikizingatiwa hisia za kutoridhishwa na baadhi ya wadau wa uchaguzi kuhusu uhuru wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), sheria na kanuni pamoja na upungufu kadhaa, imeshindwa kuupa uchaguzi huo alama A na hivyo kutoa alama B kwamba ingawa uchaguzi ulikuwa wa huru na haki. 

Akitoa taarifa ya awali ya TEMCO kuhusu Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu mbele ya waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kiongozi wa timu hiyo, Dk Benson Bana alisema upungufu mdogo hauepukiki hivyo timu yao kutoa alama 60-69 ambayo inaangukia kwenye alama B. 

“Waangalizi wa ndani tulipoangalia kutoka kwenye taarifa za waangalizi wetu waliokuwa wamesambaa nchi nzima, toka mwanzo wa uchaguzi huu yaani katika utengaji majimbo, uteuzi ndani ya vyama, kampeni na siku yenyewe ya kupiga kura uchaguzi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania unaangukia alama A, lakini kutokana na dosari hizo tunatoa alama B,” alisema Dk Bana. 

Alizitaja baadhi ya sababu hizo kuwa ni pamoja na kutoruhusu Watanzania walioko nje ya nchi kupiga kura, kuwepo na mgombea binafsi na watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa kwamba sio waajiriwa wa Tume. 

Aidha, Dk Bana aliyataja mapungufu mengine kuwa ni katika kampeni hizo wagombea walijinadi wao badala ya vyama vyao vilivyowasimamisha, jambo ambalo lilijitokeza hasa kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Chama Cha Mapinduzi (CCM). 

“Hili halikutufurahisha kabisa, mgombea kuwa mtu binafsi kuliko kunadi taasisi zao hilo halikuwa jambo jema katika kukuza demokrasia na hii imejitokeza hasa kwa CCM na Chadema,” alisema Dk Bana. Alisema kwa mujibu wao, kampeni za vyama kuna ambazo hazikuzingatia muda na pia maneno yasiyofaa kujitokeza katika kampeni hizo. 

Hata hivyo, alisema tathmini za Temco zilionesha siku ya kupiga kura, hakukuwa na mambo yoyote ya kusababisha uchaguzi usiwe wa huru na wa haki watu walipiga kura katika hali ya amani na pia kura zilihesabiwa katika hali hiyo bila kuwapo vurugu pamoja na matokeo kutangazwa. 

Dk Bana alisema tathmini yao inaonesha pia kuwa vyama vya CCM, Chadema na CUF vilitumia demokrasia vizuri katika kuwapata wagombea wa nafasi mbalimbali ndani ya vyama na kwamba vyama vingine havikuwa na demokrasia hiyo na kwamba kulikuwa na matumizi makubwa ya fedha kwa CCM na Chadema. 

Kuhusu uchaguzi wa Zanzibar, Dk Bana alisema Temco imepokea kwa mshituko uamuzi wa kufutwa matokeo ya uchaguzi uliotangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha wa kufuta uchaguzi wa Zanzibar kwa madai kuwa haukuwa wa huru na haki. 

“Tulikuwa na watazamaji 22 wa muda mrefu na 704 wa muda mfupi wa Temco Zanzibar, ambao waliangalia mchakato mzima wa uchaguzi na taarifa zao za awali zinaonesha kuwa shughuli zote za kabla ya uchaguzi zilifanyika kwa amani na utulivu, inashangaza uamuzi wa kusitisha kura zikiendelea kuhesabiwa,” alisema Dk Bana. 

Alisema Temco inaishauri ZEC kufikiria upya uamuzi huo kwa lengo la kufikia uchaguzi huru na wa haki kuimarisha amani, huku ikiitaka Serikali kuingilia kati kuleta amani kwa Zanzibar ikishirikiana na wadau wengine wa amani.
Share:

Sitta atangaza Kuwania Nafasi ya Kuwa Spika Bunge la 11

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

WAZIRI wa Uchukuzi, Samuel Sitta ametangaza kuwa atawania nafasi ya Spika ili kuliongoza Bunge la 11. Sitta aliyewahi kuwa Spika wa Bunge la Tisa amekuwa kada wa kwanza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kujitosa katika mchuano wa kuwania nafasi hiyo nyeti wakati huu ambao Bunge limevitaka vyama vya siasa viwe tayari kwa ajili ya kupeleka majina ya wateule wao wa nafasi hiyo mara itakapotangazwa kuwa wazi. 

Msemaji wa Spika huyo mstaafu, John Dotto alisema jana Dar es Salaam kuwa Sitta amemua kuwania nafasi hiyo kutokana na uwezo na uzoefu alionao wa kuendesha Bunge. Alisema Sitta anaamini kuwa uwezo wake aliouonesha katika kuendesha Bunge la Tisa akitumia kaulimbiu yake ya ‘Spika wa Kasi na Viwango’ itamfanya aendane na kasi ya utendaji wa Rais Mteule, Dk John Magufuli. 

Sitta alijizolea sifa wakati akiwa Spika wa Bunge la Tisa kuanzia mwaka 2005 hadi 2010, ikiwamo Bunge hilo kufanyia marekebisho ya kanuni mbalimbali zilizolifanya liwe na makali na kuibua kashfa nzito ikiwamo ya Richmond ambayo ilisababisha Waziri Mkuu, Edward Lowassa kujiuzulu na alilirejeshea makali Bunge. 

Tayari Bunge la Jamhuri ya Muungano limetangaza kuanza kwa mchakato wa kumpata Spika mpya wa Bunge, atakayerithi mikoba ya Spika Anne Makinda. Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel akizungumza na vyombo vya habari Dar es Salaam mapema wiki hii alisema kuwa mgombea wa nafasi ya Spika, anaweza kuwa Mbunge au mwanachama yeyote wa chama kwa masharti kwamba kama si Mbunge, jina lake lazima liwasilishwe kwanza Tume ya Taifa ya Uchaguzi siku tano kabla ya uchaguzi kujiridhisha kuwa mgombea huyo ana sifa za kuwa Mbunge. 

Bunge hilo la Tisa lilipata ufanisi na mafanikio kadhaa kutokana na ubunifu na ujasiri wa baadhi ya wabunge wakiongozwa na utayari wa Sitta ambaye wakati akishika nafasi hiyo aliahidi kuwa ‘spika wa kasi na viwango.’ 

Mafanikio yaliyopatikana katika Bunge hilo ni pamoja na kutungwa kwa Kanuni mpya za Bunge za mwaka 2007, ambazo zimeelezwa kuwa zilisaidia kwa kiasi kikubwa kuliwezesha lifanye kazi kwa ufanisi kama vile kuondoa ukiritimba wa serikali kuwa ndiyo pekee inayoweza kupeleka muswada bungeni. 

Kanuni hizo mpya za mwaka 2007 ambazo zilitokana na kufanyia marekebisho makubwa kanuni za Bunge za mwaka 2004, zilitoa mamlaka kwa kamati za kudumu za Bunge kuwa na uwezo wa kupeleka mswada kwa ajili ya kujadiliwa bungeni na hatimaye kuwa sheria.
Share:

RC Dar aonya wanaoamsha hisia za uvunjifu wa amani

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


VIONGOZI wa vyama vya siasa wametakiwa kuheshimu Katiba ya nchi kwa kuacha kuendeleza mgogoro na kuamsha viashiria vya uvunjifu wa amani ya nchi kwa madai ya kutokukubaliana na matokeo ya Urais yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). 

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki aliyasema hayo jana wakati akizungumza kwenye mkutano wa Kamati ya Amani ya viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Dar es Salaam uliofanyika jana Dar es Salaam. 

Alisema kwa mujibu wa Katiba ya nchi NEC pekee ndiyo yenye mamlaka ya kutangaza matokeo na ikishafanya hivyo hakuna mahali pa kwenda kupinga. Alisema wanasiasa hao kwa kusambaza taarifa za kufanya maandamano ya kupinga matokeo hayo ni uchochezi na kukiuka sheria za nchi ambapo kunaweza kusababisha uvunjifu wa amani. 

“Wapo watu ambao hawataki kuheshimu hilo, wanasambaza meseji za uchochezi ambazo zinaweza kuvuruga amani yetu …” alisema Sadiki. Aliwaomba viongozi hao wa dini kuendelea kuhubiri amani kwani kamati hiyo imefanya kazi kubwa katika kuhakikisha nchi inapita salama katika uchaguzi licha ya kuwepo kwa matukio madogo ya uvunjivu wa amani. 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Shehe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum alisema katika kipindi cha kuanzia kampeni, upigaji kura na baada ya uchaguzi, mambo yameenda vizuri kwa kuwa amani imetawala. 

Alisema kutokana na amani kutawala hata baadhi ya mataifa mengine ambayo yalikuwa yakitamani kuona Tanzania ikiingia katika machafuko yamepata mshangao kuona bado amani inaendelea kuwepo. 

Hata hivyo, alitaka wagombea ambao hawakuridhika na matokeo yaliyotolewa wafuate taratibu badala ya kuwashawishi na kuwatumia wananchi kuingia barabarani na kufanya vurugu na maandamano. “Walioshindwa wasiwatumie Watanzania kuingia barabarani kufanya vurugu, tuheshimu damu za Watanzania,” alisema Sheikh Alhad.
Share:

HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO MUHIMBILI UNIVERSITY-MUHAS 2015/2016

Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBER 04 2015

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Share:

Tuesday 3 November 2015

HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA MUST 3RD BATCH 2015/2016

Share:

TAARIFA MUHIMU KUHUSU "MALIPO" KWA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SPECIAL DIPLOMA UDOM 2015/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
slide1
IMPORTANT NOTICE TO SPECIAL DIPLOMA STUDENTS
ALL STUDENTS ARE REQUIRED TO PAY UNIVERSITY DIRECT COSTS FOR ACADEMIC YEAR 2015/2016 BEFORE REPORTING TO THE UNIVERSITY.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBER 03 2015

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY











Share:

Monday 2 November 2015

NAFASI ZA KAZI 640 UHAMIAJI KWA KIDATO CHA NNE NA SITA ,MWISHO WA KUTUMA MAOMBI NOVEMBER 6 2015-SIFA UWE UMEPITA JKT

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Habari yako,
Uhamiaji wametangaza nafasi za kazi zipatazo 640 kwa wahitimu wa kidato cha SITA na NNE ,Tafadhali tuma Waweza fanikiwa mpe taarifa na mwenzako,

KUSOMA TANGAZO HILO BONYEZA HAPO CHINI,
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji anatangaza nafasi za kazi katika Idara ya Uhamiaji. Nafasi hizo ni za Koplo wa Uhamiaji na Konstebo wa Uhamiaji. fuata ukurasa huu kwa maelezo zaidi.
Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO CHUO KIKUU IFM 2015/2016-FIRST LOT

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Habari yako,
Kama kawaida yetu MASWAYETU BLOG tunanedelea kukuletea kitu roho inapenda,Hatimae IFM imetoa majina ya waliopata mkopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016.

Tunaendelea kutoa huduma yetu ya kuangalizia watu majina yao,endapo utahitaji kuangaliziwa jina fanya yafuatayo;


1.TUMA JINA LAKO MFANO JUMA JUMA S4050/0018/2012-HELSB 2015/2016-ifm

2.HUDUMA HII UTATOZWA TSHS 1000 AMBAYO UTAITUMA KWA MPESA KWENDA
   NAMBA 0768260834 AU TIGO PESA 
0652740927


3.TAFADHALI MAJINA YOTE YATUMWE KWENYE NAMBA YA VODA 0768260834
4.UTAJIBIWA MDA MFUPI TU BAADA YA KUTUMA PESA

5.TUMA PESA KWANZA NDIO UTUME JINA NA EXAM NAMBA YAKO.

NOTE:PIA TUNAYO MAJINA YA VYUO VYOTE YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO 2015/2016
BONYEZA HAPA KUONA MAJINA HAYO
Share:

HAYA HAPA MAJINA YA NYONGEZA YA WANAFUNZI WA;IOCHAGULIWA MUHIMBILI 2015/2016

Share:

MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO 2015/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Habari yako,
Kama kawaida yetu MASWAYETU BLOG tunanedelea kukuleteam kitu roho inapenda,Hatimae Bodi imetoa amjina ya wanafunzi waliopata mkopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016.

Tunaendelea kutoa huduma yetu ya kuangalizia watu majina yao,endapo utahitaji kuangaliziwa jina fanya yafuatayo;

Share:

HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MIKOPO YA ELIMU YA JUU VYUO MBALIMBALI KWA MWAKA WA MASOMO 2015/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Habari yako,
Kama kawaida yetu MASWAYETU BLOG tunanedelea kukuleteam kitu roho inapenda,Hatimae Bodi imetoa amjina ya wanafunzi waliopata mkopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016.

Tunaendelea kutoa huduma yetu ya kuangalizia watu majina yao,endapo utahitaji kuangaliziwa jina fanya yafuatayo;
1.TUMA JINA LAKO MFANO JUMA JUMA S4050/0018/2012-HELSB 2015/2016

2.HUDUMA HII UTATOZWA TSHS 1000 AMBAYO UTAITUMA KWA MPESA KWENDA
   NAMBA 0768260834 AU TIGO PESA 
0652740927

3.TAFADHALI MAJINA YOTE YATUMWE KWENYE NAMBA YA VODA 0768260834
4.UTAJIBIWA NDANI YA DK MOJA TU.
5.TUMA PESA KWANZA NDIO UTUME JINA NA EXAM NAMBA YAKO.
HESLB Officially welcomes Local Undergraduate loan applicants for Academic Year 2015/2016 to view their loan allocation status ( FIRST LOT )
To view your Loan Allocation, kindly type your Form IV Index number in the space provided and Type in the security code shown . 
TO FIND YOUR NAME
Share:

Sunday 1 November 2015

SUA: Fourth Batch of Selected Students to join Undegraduate Degree Programmes For Academic Year 2015/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

The following applicants have been selected to join various undergraduate degree programmes for the 2015/2016 academic year which starts on the 2nd November, 2015
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OCTOBER 31 2015

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
DSC01922 DSC01923
.
.
DSC01921
.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger