Thursday, 12 October 2023

WATALAKA NA WATALAKIWA WAPEWA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI ILI KUJIKWAMUA KIUCHUMI

 



MKUU wa Idara ya Rasilimali Watu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Mkoa wa Tanga Sharifa Coshuma akizungumza wakati akifungua mafunzo ya watalaka na watalakiwa yaliandaliwa na Shirika lisilo la kiserikali la Msamaria Mwema (Good Samaritan Charitable and Pain Relief-GSCPR)yaliyolenga kutoa elimu kwa kundi hilo la watalaka na watalakiwa ya ujasiriamali kwa lengo ka kuwawezesha kujikwamua kiuchumi kushoto ni Katibu Mkuu wa Shirika hilo Lulu George na kulia ni Mkurugenzi wa Shirika hilo Rodgers Chamani


MKUU wa Idara ya Rasilimali Watu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Mkoa wa Tanga Sharifa Coshuma akizungumza wakati akifungua mafunzo ya watalaka na watalakiwa yaliandaliwa na Shirika lisilo la kiserikali la Msamaria Mwema (Good Samaritan Charitable and Pain Relief-GSCPR)yaliyolenga kutoa elimu kwa kundi hilo la watalaka na watalakiwa ya ujasiriamali kwa lengo ka kuwawezesha kujikwamua kiuchumi kushoto


Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Msamaria Mwema (Good Samaritan Charitable and Pain Relief-GSCPR) Rodgers Chamani akizungumza wakati wa mafunzo hayo kulia ni Katibu wa shirika hilo Lulu George

Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Msamaria Mwema (Good Samaritan Charitable and Pain Relief-GSCPR) Rodgers Chamani  akizungumza wakati wa mafunzo 

Katibu Mkuu wa Shirika hilo Lulu George akisisitiza jambo wakati akitoa mada katika mafunzo hayo



Afisa Miradi wa Shirika hilo Sadick Shembilu akisisitiza jambo wakati wa mafunzo hayo

Washiriki wakiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi




Na Oscar Assenga, TANGA

MKUU wa Idara ya Rasilimali Watu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Mkoa wa Tanga Sharifa Coshuma  amefungua mafunzo ya watalaka na watalakiwa huku akifichua siri ya wanawake wengi kuishi marefu kuliko wanaume kwamba ni uvumilifu na kutoishi na viny’ongo moyoni.

Mafunzo yaliandaliwa na Shirika lisilo la kiserikali la Msamaria Mwema (Good Samaritan Charitable and Pain Relief-GSCPR)yaliyolenga kutoa elimu kwa kundi hilo la watalaka na watalakiwa ya ujasiriamali kwa lengo ka kuwawezesha kujikwamua kiuchumi.

Sharifa alisema Wanawake wengi ni wepesi kuzungumzia matatizo yao tofauti na wanaume hatua inayowasaidia kuepukana na magonjwa ya moyo na kuweza kuishi kwa muda mrefu bila chuki wala vikwazo.

“Kwa kweli kuzungumza na kuwa wawazi ndio tiba sahihi katika jambo lolote katika kumuweka mtu huru lakini viny’ongo havisaidii na vinakuwa vibaya sana katika jamii na hatarishi kwa afya“,Alisema Afisa huyo.

Aliwataka wanawake hao kuzingatia mafunzo wanayopewa kwa mustakabali wa maisha yao na familia hasa kwa kuzungitia kuwa jukumu la malezi ya watoto bado lipo mikononi mwao


Awali akizungumza katika mafunzo hayo Katibu Mkuu wa Shirika hilo Lulu George alianza kuwashukuru TPA kwa kuwapa nafasi ya kushirikiana na wakina mama hao ili kuwawezesha kupata mafunzo ya kujikomboa kiuchumi.

Lulu alisema wanaamini kama taassi mbalimbali zilizopo Mkoani Tanga zikiendelea kuwashikia mkono itawezesha Shirika hilo kusambaza elimu ya ujasiriamali,kujitambua,maisha baada ya talaka sambamba na changamoto ya ukomo wa hedhi kwenye makundi mbalimbali kwa jamii.

“Tunaamini wakina mama hao wakiwa na akili iliyotulia wanaweza kufanya mabadiliko mazuri ya kiuchumi,kupitia wamama hawa hawa wataweza kuitumia Bandari yetu ya Tanga kufungua fursa mbalimbali za kibiashara ndani na nje ya nchi na hatimaye kuongeza pato la mtu mmoja mmoja,mkoa na Taifa kwa ujumla”,alifafanua.

Katibu Mkuu huyo alisema baada ya mafunzo hayo wanatarajia kuunda vikundi vitakavyowezesha wamama hao kufanya shughuli zao kwa pamoja na hatimaye kufikia malengo waliyokuwa wamejiwekea katika kukidhi mahitaji yao.

“Yapo mambo mengi wanaweza kufanya kwani Mkonge peke yake wakitumia fursa iliyopo katika kuongeza thamani kwa bidhaa zinazotokana na zao hilo watafika mbali kwa sababu uhitaji wa bidhaa za zao la Mkonge ndani na nje ya nchi bado ni mkubwa sana ,tunatarajia wamama hawa wafike kwenye soko la dunia”,alisema.

Hata hivyo aliisihi jamii kuondoa dhana kwamba mtu aliyetalakiwa ni mtu mwenye laana au aibu kwani unyanyapaa huo husababisha watu waliotalikiana kuishi katika maumivu makubwa na kushindwa kujisamehe.

“Lakini tuwashukuru Bandari ya Tanga kwa kuwaezesha kuendelea kuwapa matumaini kundi hili ambalo kwenye jamii lilionekana kwamba mtu akipewa talaka amelaaniwa au hafai lakini mara baada ya kuwapa mafunzo kuna maisha baada ya talaka wakina mama hawa wamekuwa watulivu na wameweza kurudisha tabasamu la matumaini”alisema.

Lulu alisema Shirika la Msamaria Mwema linaendelea kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan za kumkomboa mwanamke kwenye nyanja zote ikiwa ni pamoja na kulinda afya ya akili changamoto inayowakabili wanawake wengi kwa sasa.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI OKTOBA 12, 2023

 






















Share:

Wednesday, 11 October 2023

KAMATI YA SIASA KATA YA KILIMANI YAKAGUA UJENZI WA SHULE



Na Barnabas Kisengi, Dodoma

Mapema leo Oktoba 11  2023 viongozi wa kamati ya siasa ya chama cha Mapinduzi  kata ya kilimani  pamoja na wajumbe wa secretariat  ya kata ya kilimani    Wamefanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa shule  ya msingi  unatekelezwa katika mtaa wa Chinyoyo kata ya Kilimani 

Pamoja na kuona kasi  ya ujenzi huo  unavyokwenda  viongozi hao  wamesisitiza ujenzi huo  uongeze kasi  kulingana na mkataba unavyoelekeza  licha ya kuwa na changamoto ndogo ndogo  ambazo  hazizuii mradi huo  kusimama.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi kata ya Kilimani Nathani Chibeye amesema ujenzi huo wa shule ya msingi hiyo utakuwa mkombozi kwa kata ya Kilimani kwa kuwa kata hiyo tangu ipate Uhuru haijawahi kuwa na shule ya msingi jambo ambalo hupelekea watoto wa mitaa minne ya Kilimani kusoma katika shule za kata nyingine na kusababisha kutembea umbali mrefu kuitafuta elimu.

"Hata hivi Sasa sisi kama viongozi wa Chama Cha Mapinduzi kata ya Kilimani tunaishukuru SERIKALI YA AWAMU YA SITA INAYOONGOZWA NA RAIS SAMIA SULUHU  HASSAN kwa kuweza kutupatia fedha za ujenzi wa shule hii ambayo itakuwa mkombozi kwa wananchi wa kata ya kilimani"amesema Chibeye.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Mapinduzi kata ya Kilimani Rotta Ndimbo ameitaka kamati ya ujenzi na mkandarasi kuhakikisha wanatanguliza uzalendo katika ujenzi wa shule hiyo ili thamani ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi huo zinatumika kama zilivyo kusudiwa.

Ziara hiyo ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi kata ya Kilimani ni mwendelezo wa kugagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na serikali katika kata ya Kilimani ili kuhakikisha utekelezaji wa ilani ya chama unafanikiwa.


Share:

RAIS MWINYI AKABIDHI CHETI CHA SHUKURANI YA UDHAMINI e-GA



Na Mwandishi Maalum. 

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, akimkabidhi cheti cha shukrani ya udhamini Mkurugenzi wa Huduma za TEHAMA wa  Mamlaka ya Serikali Mtandao ( e-GA) Ricco Boma, kwenye Mkutano Mkuu wa 7 wa Mashirika ya Utangazaji ya Umma Kusini mwa Afrika (SABA). 

Mkutano huo unafanyika kwa siku tatu kuanzia  Oktoba 10 hadi 12 katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Kisiwani Unguja ambapo  e-GA ni miongoni mwa wadhamini wa mkutano huo.

Share:

MKANDARASI WA MAJI, UJENZI HOSPITALI SUMBAWANGA DC 'WAMCHEFUA' CHONGOLO, AWATULIZA WALIOMSIMAMISHA NA NDOO ZA MAJI


Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Komredi Daniel Godfrey Chongolo ameonekana kutoridhishwa na hatua ya Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Sumbawanga Vijijini, ambapo ameagiza Serikali mkoani Rukwa pamoja na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kutuma timu ya uchunguzi ili kubaini kinachokwamisha mradi huo kukamilika, huku ukionekana kutekelezwa chini ya kiwango cha ubora na thamani ya fedha kilichopelekewa hadi sasa.

Mbali na kutoridhishwa na ujenzi huo wa hospitali unavyotekelezwa, Komredi Chongolo pia alionekana kukerwa na mkandarasi wa Mradi wa Maji wa Ilemba, Jimbo la Kwela, ambaye pamoja na RUWASA Mkoa wa Rukwa kumwekea msukumo ili ajenge kwa kasi ya kukamilisha ndani ya muda wa mkataba, bado ameendelea kusuasua huku akitoa visingizio vingi vya kutomaliza kazi hiyo kwa wakati ili wananchi wa Kata ya Ilemba, Vijiji vya Ilemba A na B na Kata ya Kaswepa, wapate maji safi na salama ya kutumia.

“Mkuu wa Wilaya, hakuna kucheka na waliopewa kazi hizi. Tukiacha hali hii, mambo hayataenda na hiyo sio sawa hata kidogo. Hatuwezi kuacha mambo yaende namna hii. Tutakuwa hatutendi haki na tutakuwa hatujitendei haki wenyewe na nafasi zetu za kuwatumikia wananchi. Wananchi wanachotaka ni huduma. Huko aliko anakosema anauguliwa, kuna Mkuu wa Wilaya mwenzako, wasiliana nae upate uhakika na akija aje na Ushahidi wa kuwa alikuwa anauguliwa.

“Vinginevyo ikifika tarehe 30 mwezi huu ambao mkataba wake ulikuwa unakamilika, asiongezewe mkataba. Tusitengeneze mazingira ya watu kucheza na miradi ya maendeleo na fedha za umma kama zao binafsi. Wekeni utaratibu, mwezi mmoja hajamaliza kazi mnavunja mkataba na mtengeneze mbadala kwa kutumia Force Account. Tunataka watu wapate maji, sio vinginevyo,” amesema Chongolo.

Komredi Chongolo ametoa maelekezo hayo Oktoba 10, 2023 akiwa katika Kata ya Mtowisa na Ilemba, mara baada ya kukagua mradi huo wa Maji wa Ilembo wa Tsh. 1.9 bilioni ambao bado uko asilimia 27 na hospitali ya wilaya iliyoanza kujengwa tangu Disemba 2021 na mkandarasi aitwae Kuyella Enterprises, huku ukitakiwa kukamilika Machi 2022, lakini hadi alipofika mahali hapo kuutembelea na kuukagua, ulikuwa haujakamilika.

Katika hatua nyingine msafara wa Katibu Mkuu huyo wa Chama cha Mapinduzi, umesimamishwa maeneo ya Mwela, Mtowisa, Msia, Talanda, Milepa na Kinambo, Milepa akelekea Kioze na Ilemba, ambapo wananchi walitaka awasikilize changamoto zao na kuzitolea maelekezo ya kuzitafutia ufumbuzi.

Katika eneo la Kijiji cha Mwela, Kata ya Mtowisa, watu mbalimbali wakiwemo akina mama na vijana kijiji hicho, kilichopo Halmashauri ya Sumbawanga Vijijini walisimamisha msafara wakiwa na ndoo za maji, wakitaka awaondolee kero ya uhaba wa maji na namba ya utambulisho wa kijiji hicho.

"Huduma za afya tunazo...umeme tunao...barabara inapitika...hata pembejeo za kilimo tunapata. Hatuna tatizo na huduma zingine Katibu Mkuu wa CCM. Changamoto zetu hapa ni mbili tu, maji haya unavyoyaona si salama wala si safi. Lakini pia tuna changamoto ya namba ya kijiji chetu hiki kutotambuliwa huko wilayani," alisema mwananchi aliyejitambulisha kuwa ni Mwenyekiti wa Wananchi hao.

Kufuatia hali hiyo Komredi Chongolo aliwatuliza wananchi hao kwa kutoa maelekezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Mhe. Nyakia Ally kuhakikisha changamoto za wanakijiji hao zinatatuliwa ndani ya muda mfupi, ikiwa ni pamoja na kukutana nao kwenye kikao akiwa na timu yake ya wataalam kutoka wilayani, siku ya Ijumaa, wiki hii ili wajadiliane nao namna ya kutatua kero hizo kwa njia shirikishi. Ndugu Chongolo aliahidi kufuatilia suala hilo kwa ukaribu.

Ndugu Chongolo alimwagiza Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, kwa kutumia RUWASA, wapeleke gari la kuchimba kisiama katika kijiji hicho kwa haraka, wakati wakiendelea kutafuta vyanzo vingine vya uhakika, baada ya Meneja wa RUWASA kutoa taarifa kuwa katika mipango yao kijiji hicho kiko ndani ya maeneo ambayo yamepangiwa mradi wa maji utakaogharimu Tsh. 1.3, utakaokuwa mwarobaini wa kero hiyo.

Mbali ya kutembelea miradi hiyo ya Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya, mradi wa Maji Ilemba na kuzungumza na wananchi katika maeneo hayo, pamoja na kwingine alikosimamishwa, Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Chongolo pia alitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Kaoze na kuzungumza na wananchi wa kata hiyo, kabla ya hitimisha ziara yake Jimbo la Kwela, kwa kuzungumza na wananchi wa Kata ya Kilyematundu, Sumbawanga Vijijini.

Share:

UHASIBU ARUSHA YAIMARISHA MASOMO YA UJASIRIAMALI ILI VIJANA WAJIAJIRI


Chuo cha Uhasibu Arusha [IAA] Kimeanza kutoa Masomo ya Ujasiriamali Kwa Vijana wanaojiunga na chuo hicho kwa lengo la kuwajengea uwezo ili kuweza kujiajiri pindi wanapo hitimu masomo katika chuo hicho.

Akizungumza katika Wiki ya vijana inayoadhimishwa kitaifa mkoani Manyara Mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha [INSTITUTE OF ACCOUNCY ARUSHA -IAA] Prof.Eliamani Sedoyeka amesema kwasasa chuo hicho kimeweka nguvu katika kuwawezesha vijana kwa kuwaelimisha hususani katika maswala ya ujasiriamali ili kuongeza wigo mpana kwa vijana hao kujiajiri na kuacha dhana ya kuajiriwa.

Aidha Prof.Sedoyekaa ameongeza Kuwa pamoja na kuwepo kwa wingo mpana wa kuajiriwa hasa kwa wanafunzi wanaohitimu katika chuo cha uhasibu Arusha [IAA] lakini masomo ya ujasiriamali yameongeza fursa zaidi kwa vijana hao katika kujiongezea kipato katika kujiajiri ili kuongeza uchumi wao na kujikwamua na wimbi la umaskini.

Baadhi ya Wanafunzi wa chuo cha Uhasibu Arusha [IAA] Bwa.Ruben Abeli na Bi Spensiaodha Mongo Wamepongeza uongozi wa chuo hicho kwa kuweka msisitizo katika maswala ya Ujasiriamali kwani mpaka sasa wamefanikiwa kuzalisha bidhaa mbalimbali na kushiriki na vijana wengine katika Wiki ya vijana ambayo imefanyika kitaifa katika mkoa wa Manyara ambayo imehudhuriwa na vijana kutoka Mikoa mbalimbali hapa nchni.

Hata hivyo Masomo ya ujasiriamali yanayotolewa na chuo cha Uhasibu Arusha -IAA yameonekana Kuwa na toka kwa vijana wanaojiunga na chuo hicho kwani yamekuwa yakiwaandaa katika kujiajiri wenyewe pindi wanapo hitimu Masomo yao.




Share:

Tuesday, 10 October 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 11,2023

Share:

KAMISHNA WAKULYAMBA: HONGERENI TANAPA KWA UHIFADHI ULIOTUKUKA NA USIO NA MAWAA.


Na. Jacob Kasiri- Kitulo.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Mhe. Benedict Wakulyamba amelipongeza Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa uhifadhi uliotukuka na usio na mashaka kwa taifa.

Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo tarehe 10.10. 2023 alipotembelea Hifadhi ya Taifa Kitulo iliyopo wilayani Makete katika mkoa wa Njombe.

Ndani ya hifadhi hiyo Kamishna Wakulyamba alitembelea Lango la Mwakipembo, Uwanda wa Maua, Maporomoko ya maji ya Mwakilema na Mwakipembo.

Baada ya kuviona vivutio hivyo na baadhi ya mamalia wachache walioonekana kwa muda huo, hakusita kuonesha furaha yake alipotazama upande wa Mashariki na kuona mandhari nzuri iliyonakshiwa kwa safu za milima  ya Livingstone na tambarare iliyotaradadi kwa maua yenye rangi tofauti mithili ya zulia.

"Nimeridhishwa na kazi nzuri za uhifadhi mnazozifanya maafisa na askari wa TANAPA. Hongereni  kwa kuendelea kuhifadhi rasilimali zetu, serikali na wizara inatambua kazi nzuri mnayoifanya ya uhifadhi kwani mnajituma usiku na mchana.”

Kwa tafsiri isiyo rasmi mwanamapinduzi kutoka nchini India Mahatma Gandhi aliwahi kusema, Utajiri wa taifa lolote lile duniani unategemeana na jinsi taifa hilo linavyoheshimu na kulinda wanyamapori wake. Hivyo wanachokifanya TANAPA ni kuendeleza falsafa hiyo.

Aidha, Kamishna Wakulyamba alisisitiza  maelekezo ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angela Kairuki (Mb) kutekelezwa, kutafuta eneo kwa ajili ya ujenzi wa uwanja mdogo wa ndege karibu na Hifadhi ya Taifa Kitulo ambao utakuwa chachu ya kukuza utalii na kufungua fursa za uwekezaji kwa wananchi wa maeneo jirani.

" Kufanya kazi kwa uadilifu ndio msisitizo namba moja, msijihusishe na vitendo vinavyokinzana na maadili ya kazi kama vile rushwa na ujangili," aliongeza Kamishna Wakulyamba.

Kamishna Wakulyamba pia, aliwataka maafisa na askari kujiendeleza kielimu alisema, "mnapopata nafasi msisite kujiendeleza katika fani ya uhifadhi au fani nyingine kulingana na matakwa ya taasisi, mnaposoma hakikisheni hamuathiri utendaji kazi wa shirika."

Aidha, Kamishna Wakulyamba alifanikiwa kutembelea Ofisi za Makao Makuu ya Kanda ya Kusini yaliyopo Rujewa Wilayani Mbarali, na kuwapongeza TANAPA  kwa ujenzi wa ofisi kubwa na yenye hadhi ya Kanda.

Kamanda wa Uhifadhi Kanda ya Kusini Steria Ndaga, akimkaribisha Naibu Katibu Mkuu huyo alisema, "Kanda ya kusini ina jumla ya maafisa na askari 17, kati yao wawili ni wa kike na 15 ni jinsia ya kiume".

"Lengo la uanzishwaji wa kanda hii ni kuratibu na kusimamia shughuli za Uhifadhi, Utalii na mwenendo mzima wa Ikolojia katika Hifadhi za Taifa Ruaha, Kitulo na Katavi" alisema Kamishna Ndaga.

Kanda ya Kusini - TANAPA ilianzishwa mwezi mei, 2019 baada ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania lenye makao makuu yake jijini Arusha kufanya ughatuzi wa madaraka uliopelekea  kuanzishwa kwa kanda nne.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger