Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Sunday 8 December 2019

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Jingu Aipeleka Kampeni Ya Makazi Bora Monduli

Na Mwandishi Wetu Arusha
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto anayeshughulikia Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu amewataka wananchi kuhakikisha wanaboresha makazi yao kutoka makazi ya nyumba za nyasi na tembe kwenda nyumba za tofali na bati.

Aliyasema hayo leo Wilayani Monduli mkoani Arusha alipokuwa akitembelea miradi mbalimbali ya maendeleo iliyoamasishwa na wataalam kutoka Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli kwa kuamsha ari ya wananchi kushiriki katika miradi ya Maendeleo.

Dkt. Jingu aliwataka wataalam wa Maendeleo ya Jamii nchini kuhakikisha wanakuwa chachu ya mabadiliko na wanawezesha jamii kuwa na mawazo chanya ya kujiletea maendeleo na kubadili changamoto kuwa fursa za kimaendeleo.

"Wataalam wa Maendeleo ya Jamii tuweke nguvu katika kuhakikisha tunabadili jamii zetu kuwa na mawazo chanja hasa ya kujitegemea na kujiletea maendeleo" alisema Dkt. Jingu.

Dkt. Jingu aliongeza kuwa Sekta ya Maendeleo ya Jamii inapaswa kuwa chachu ya maendeleo katika taifa letu hivyo Vyuo vya Maendeleo ya Jamii vinatakiwa kutoa wataalam wenye weledi na stadi za kubwa za kuleta mabadiliko katika jamii.

"Vyuo vya Maendeleo ya Jamii tutoe wataalam wenye weledi  wa kuhakikisha tunatumia fursa zilizopo katika jamii kutatua changamoto zilizopo" alisema Dkt. Jingu.

Wakati huohuo akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli Dkt. Jingu amewataka wanafunzi hao kusoma kwa bidii na kuhakikisha wanatumia stadi watakazopata kubadilisha maisha yao na jamii kwa ujumla.

Dkt. Jingu aliwataka wanafunzi hao kuitumia bahati ya kuwa mmoja ya wanafunzi katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli kwa kuhakikisha wanafanikisha ndoto zao walizozilenga kuzitimiza katika maisha yao kwa kuzingatia masomo na nidhamu.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli Bw. Elibariki Ulomi alimuhakikishia Katibu Mkuu kuwa Chuo hiyo kitahakikisha kinashirikiana na wananchi wa Wilaya ya Monduli katika kutekeleza Kampeni ya Makazi Bora ili kuwawezesha wananchi kuboresha makazi yao na kuhakikisha kinatoa Wataalam wa Maendeelo ya Jamii watakosaidia kuleta mabadiliko katika taifa.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Monduli Bi. Rose Mhina alisema kuwa Halmashauri hiyo imeshaanza kutekeleza kampeni ya Makazi bora kwa kuipeleke ajenda hiyo kwa madiwani na kutoa michoro maalum kwaajili ya ujenzi wa nyumba bora za gharama nafuu.

Aliongeza kuwa Kampeni hiyo ya kuhamaisha ujenzi wamakazi bora itahamasishwa na katika jamii na maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka wilayani maoaka kwemye kata ili kuhakikisha wananchi wanajitoa na kuboresha makazi yao.

Kampeni ya Kuboresha makazi inalenga kuiwezesha jamii ambayo inaishi katika makazi yasiyo bora kuweza kuboresha makazi yao kwa kutumia ramani ziliziotolewa na Halmashauri walizopo zikiwa ni nyumba za gharama nafuu.

MWISHO.


Share:

TRA Yang’ara Tuzo Za NBAA , Yapata Ushindi Wa Jumla

Na Veronica Kazimoto-Dar es Salaam
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeshinda tuzo mbili ikiwemo mshindi wa jumla katika uandaaji bora wa taarifa za hesabu mwaka 2018 kwa kufuata viwango vya Kimataifa vya Uandaaji wa Hesabu katika Taasisi za Umma yaani mfumo wa IPSASs.

Katika hafla ya utoaji wa tuzo hizo iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha NBAA Bunju jijini Dar es Salaam, TRA imeibuka mshindi wa kwanza katika uandaaji bora wa taarifa za hesabu kwenye kipengele cha Wakala wa Serikali na mshindi wa jumla kwa taasisi, wakala, kampuni na mashirika mbalimbali ambayo yamefanya vizuri katika kuandaa taarifa za fedha katika shughuli zao za kila siku.

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hizo, Kamishna Mkuu wa TRA Dkt. Edwin Mhede, ameipongeza Idara ya Fedha na idara nyingine ndani ya mamlaka hiyo kwa kufanikisha upatikanaji wa tuzo hizo.

“Nachukua nafasi hii kumshukuru mkuu wa idara anayehusika na Idara ya Fedha pamoja na wakuu wa idara nyingine ndani ya mamlaka maana zote zinatoa mchango mkubwa kuhakikisha idara hii inatoa taarifa sahihi na zenye kuleta mipango sahihi kwa mamlaka na serikali kwa ujumla,” alisema Dkt. Mhede.

Dkt. Mhede alieleza kuwa, taarifa sahihi ni msingi wa mipango kwa kuwa taasisi isiyopanga kushinda ni sawa na taasisi inayopanga kushindwa hivyo suala la uandaaji bora wa taarifa za hesabu ni moja ya ufanisi wa ofisi yoyote hapa ulimwenguni.

Bodi ya Uhasibu na Ukaguzi wa Hesabu (NBAA) ndio hutoa tuzo hizo kila mwaka ambapo mwaka 2017 TRA iliibuka mshindi wa kwanza tena katika uandaaji bora wa taarifa za hesabu katika kipengele cha Wakala wa Serikali.

Mwisho.



Share:

Jafo Akerwa Na Utendaji Kazi Wa Watumishi Manispaa Ya Shinyanga

SALVATORY NTANDU
Waziri wa nchi ofisi ya Rais,Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo amemwagiza katibu Mkuu wake TAMISEMI kuwahamisha vituo vya kazi Maafisa wawili wa Manispaa ya Shinyanga baada ya kubainika kufanya kazi kwa makundi hali ambayo inaweza kukwamisha shughuli za Umma.

Waziri Jafo amewataja maafisa hao kuwa ni pamoja na Ofisa utumishi wa manispaa ya Shinyanga, Magedi Magezi pamoja na Mweka hazina Paschal Makoye, wahamishwe na  kuwapelekwa katika katika vituo vingine vya kazi.

Jafo ametoa agizo hilo jana baada ya kupokea taarifa ya mkoa wa Shinyanga, kutoka kwa  mkuu wa mkoa wa shinyanga,  Zainab Telack, katika ziara yake ya kikazi ya siku moja iliyoenda sambamba  na ukaguzi wa  ujenzi wa hospitali halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

“Kuna tabia ya watumishi katika manispaa hii wanafanya kazi kwa  makundi na hakuna umoja hasa wakuu wa idara kila mtu ni  mtawala na kusababisha utendaji kazi mbovu nimeamua kuwaondoa ili wakafanya kazi katika sehemu nyingine kuliko kuliko kuwaacha wakiendelea kuwagawa watumishi”alisema Jafo.

Waziri Jafo amesema TAMISEMI itaendelea kufuatilia nyendo za watumisho wote  wa Halmshauri nchini ambao wanafanya kazi kwa mazoea ambao hawaendi na kasi ya Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dk John Pombe Magufuli kwa kuwachukilia hatua za kidhamu ikiwanipamoja ka kuwahamisha katika vituo vya kazi.

“Mimi niko hapa kumsaidia Mh,Rais na siwezi kukubali kuona watumishi wanafanya kazi kwa makundi,nimeshatoa maelekezo kwa wakuu wote wa idara kufanya kazi kwa kushirikiana ili ufanisi wa shughuli za serikali ziweze kufanikiwa na wananchi wapate huduma bora”alisema Jafo.

Katika hatua nyingine Waziri Jafo, amepongeza ujenzi wa hospitali halmashauri ya wilaya ya Shinyanga baada ya kuyakagua na kuridhika na ujenzi wake na kusema kuwa  Rais Dk John Magufuli amekubali kutoa  Shilingi Milioni 500 ziwezekutumika kuongeza majengo mengine.

Nae  mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, alibainisha kuwa  kuwa  Serikali ilitoa Shilingi, Bilioni 3 kwaajili ya kujengwa hospitali mbili za wilaya katika mkoani huo, katika Halmashauri za Ushetu na Shinyanga  ambazo ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 90.

Mwisho.


Share:

Rais Magufuli Pamoja Na Mkewe Mama Janeth Magufuli Wasali Misa Takatifu Dominika Ya Pili Ya Majilio Katika Kanisa Kuu La Epifania Parokia Ya Bugando Jijini Mwanza

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli wamejumuika pamoja na waumini wengine wa Kanisa Kuu la Epifania Parokia ya Bugando jijini Mwanza  katika Misa Takatifu ya Dominika ya pili ya Majilio iliyoongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza Mhashamu Renatus Nkwande leo tarehe 8/12/2019.



Share:

Kijana Wa Kazi Amuibia Bosi Wake Hati Na Kuikopea

Na. Hassan Mabuye, WIZARA YA ARDHI-Iringa
Mkazi wa Iringa mjini Bi. Lugano Mwadini amejikuta katika deni linalopelekea karibu nyumba yake kupigwa mnada baada kijana wake wa kazi kukopa pesa kiasi cha shilingi 1,000,000 kwa kutumia hati yake ya umiliki wa ardhi ambayo amemuibia.

kadhia hiyo imetokea wakati wa mkutano wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi kupitia programu yake ya 'Funguka kwa Waziri' mkoani Iringa alipokuwa akisikiliza na kutatua kero za ardhi kwa wananchi wa mkoa wa Iringa katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo katika Manispaa ya Iringa.

katika mkutano huo Bi. Lugano alimtuhumu Kijana wake wa kazi kwa kumuibia hati na kuenda kukopa kwa Bw. Laurence Panklas ambaye ni askari wa jeshi la polisi mkoani Iringa anayekopesha kwa riba ya 400,000 kila mwezi ambazo kijana huyo hakuweza kuzirudisha kwa wakati jambo lililopelekea kutaka kuuzwa kwa nyumba yake ili kufidia deni hilo.

Bi. Lugano Mwadini aligundua hayo baada ya kupigiwa simu na mkopeshaji huyo kumtaka kwenda kubalisha umiliki wa hati hiyo ili apewe mtu mwingine kwa kuwa hati yake imekopewa na inadaiwa shilingi 1,400,000.

"Mi nilikuwa sipo lakini nikaja kupata taarifa kwa kupigiwa simu kwamba kijana wangu wa kazi ameniibia hati yangu wakati nikiwa katika kazi zangu na amekopea kwa askari mmoja ambaye anakopesha kwa riba ya laki nne kila mwezi, kwa hiyo kijana wangu anadaiwa 1,400,000 na hajalipa hadi sasa" Alisema Bi. Lugano Mwadini.

Waziri Lukuvi alimuagiza Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Iringa Juma Bwire kushughulikia suala hilo, kwanza kwa askali wa jeshi la polisi ambaye anafanya biashara ya pesa na kama ana kibali cha biashara hiyo na analipa kodi, kama halipi basi alipe kodi kwa miamala yote aliyowahi kufanya.

Aidha Waziri Lukuvi aliagiza kukamatwa kwa kijana huyo wa kazi ili alipe deni hilo kwa Bosi wake na kueleza kwanini amefanya uhalifu huo wa kuiba hati ya mtu mwingine.

Katika mkutano huo Waziri Lukuvi aliweza kusikiliza na kutatua migogoro ya wakazi wa mkoani Iringa takribani 200 kwa siku moja ambapo baadhi ya wananchi walieleza kuridhishwa kwa juhudi za waziri lukuvi kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi ya wakazi wa maeneo mbali mbalibila nchini bila kubagua.


Share:

Form One Selection 2020 katavi region

Form One Selection Katavi Region 2020 The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office, Check it here http://Katavi.go.tz/ Form one selection for the academic year 2020 The following students have been selected to join form one for Katavi Secondary schools for the… Read More »

The post Form One Selection 2020 katavi region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Majina ya wanafunzi waliochaguliwa kidato cha kwanza 2020

Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo ametangaza wanafunzi waliochaguliwa kujiunga  na Kidato cha Kwanza  mwaka 2020  kuwa ni  701,038 sawa na asilimia 92.27 ya wanafunzi 759,000 waliofaulu.

Jafo ameeleza kuwa wavulana waliochaguliwa ni 335,513 sawa na asilimia 47.86 na wasichana 365,525 sawa na asilimia 52.14.

Mhe. Jafo alifafanua kuwa kwa mwaka 2019 jumla ya wanafunzi 759,737 walifaulu sawa na asilimia 81.3 ya waliofanya mtihani, wakiwemo wavulana 363,999 sawa na asilimia 47.9 na wasichana 395,738 sawa na asilimia 52.08.

Kati ya waliofaulu wamo wanafunzi wenye Ulemavu 1,461 sawa na asilimia 0.19 wakiwemo wavulana 777 na wasichana 684 aliongeza Jafo.

==>>Tazama Majina Hapo chini











Dar es Salaam
Tabora

Pwani
Lindi
Mtwara
Rukwa
Geita

Katav
Iringa

Kagera

Ruvuma
Mara

Tanga
Kigoma
Shinyanga
Manyara


Share:

LIVE: Hafla Ya Uwekaji Jiwe La Msingi Ujenzi Wa Meli Mpya , Chelezo Na Ukarabati Wa Mv Victoria Na Butiama

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli anaweka Jiwe la Msingi miradi ya Ujenzi wa Meli Mpya , Chelezo na Ukarabati wa M.V  Victoria  na M.V Butiama katika Ziwa Victoria Jijini Mwanza. Sherehe zinazofanyika Katika Bandari ya Igogo Jijini Mwanza.


Share:

Form One Selection Simiyu Region for 2020

Form One Selection 2020 Simiyu Region The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office, Check it here http://Simiyu.go.tz/ Form one selection for the academic year 2020  The following students have been selected to join form one for Simiyu Secondary schools for the… Read More »

The post Form One Selection Simiyu Region for 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form one selection 2020 academic year (Public Notice)

Form one selection>>701,038 students equivalent to 92.27 percent who passed the standard seven exam in 2019 have been selected to continue with Form One in 2020.>> When they had the opportunity, 58,699 of their classmates did not get a chance because of the shortage of classrooms while the construction of classrooms should be done early so that they… Read More »

The post Form one selection 2020 academic year (Public Notice) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili December 8















Share:

Bodi Ya Mikopo Yatangaza orodha mpya ya wanafunzi 698 waliofanikiwa kupata mikopo katika dirisha la rufaa

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza orodha ya majina 698 ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliofanikiwa kupata mikopo katika dirisha la rufaa kufuatia kukosa au kupata kiwango kidogo cha mkopo katika awamu nne zilizopita.

Wanafunzi hao 698 wamepangiwa mikopo yenye thamani ya TZS 2.46 bilioni na hivyo kufanya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopata mikopo hadi sasa kufikia 49,485. Taarifa ya kina kuhusu utoaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2019/2020 itatolewa wiki ijayo baada ya uchambuzi wa mwisho kukamilika.

Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru amesema leo (Jumamosi, Desemba 7, 2019) jijini Dar es salaam kuwa taarifa zaidi kuhusu viwango walivopangiwa zinapatikana katika akaunti zao binafsi walizotumia kuomba mkopo – Student’s Individual Permanent Account (SIPA) kupitia https://olas.heslb.go.tz 

“Tumeshaweka taarifa za hawa wanafunzi katika mfumo na hivyo kila mmoja anatakiwa aingie katika akaunti yake ya SIPA ambapo ataona taarifa zake ambazo pia zinatumwa vyuoni,” amesema Badru.

Kwa mujibu wa Badru, HESLB imeboresha mifumo yake na hivyo wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza walioomba mikopo wanaweza kuona taarifa zao kutoka popote walipo kwa kutumia simu zenye mtandao wa intaneti (simu janja).

Taarifa hii pia inapatikana kwenye mitandao ya kijamii na tovuti ya HESLB ambayo ni www.heslb.go.tz

Imetolewa na:
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU



Share:

CHADEMA Kushiriki maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru Jijini Mwanza

Kamati kuu Chadema imeazimia kushiriki maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika.

Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa chama hicho kushiriki maadhimisho hayo yanayofanyika kila Desemba 9 tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu mwaka 2015.

Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Chadema, Tumain Makene imesema hatua hiyo inalenga kukuza na kuendeleza uraia mwema, uzalendo na mapenzi ya nchi yetu.

“Kamati kuu ya Chadema imeazimia kwa kauli moja kuwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aongoze ujumbe wa baadhi ya viongozi wakuu na waandamizi wa chama watakaokiwakilisha chama kushiriki katika maadhimisho hayo.”

“Chama kinawaelekeza wanachama na wapenzi wake jijini Mwanza na maeneo ya jirani kujumuika na Watanzania wengine kushiriki na kuadhimisha siku hii muhimu kwa Taifa letu,” amesema Makene


Share:

Saturday 7 December 2019

MKUU WA MKOA WA KAGERA AMESEMA HATAKI KUSIKIA SUALA LA UPUNGUFU WA MADARASA

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali  Marco Gaguti
Na Ashura Jumapili - Malunde 1 blog
MKUU wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali  Marco Gaguti,amesema  hataki kusikia suala la upungufu  wa madarasa na kuzitaka halmashauri zote za Wilaya mkoani humo kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu wanapokelewa na kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2020.

Brigedia Jen.Gaguti,alitoa agizo hilo katika kikao cha wadau wa elimu mkoani humo kilichofanyika katika Manispaa ya Bukoba.
“Wanafunzi wote waliofaulu wapokelewe kwenye shule walizopangiwa  kwa wakati kwaajili ya kuanza masomo yao ya kidato cha kwanza”alisema BrigediaJen.Gaguti.
Awali Ofisa elimu mkoa wa Kagera Juma Mhina,alisema kuwa mkoa wa Kagera una kabiliwa na upungu wa vyumba vya madarasa 283.
Mhina ,alisema halmashauri zinahimizwa kushirikisha jamii na wadau mbalimbali wa elimu katika ujenzi wa vyumba vya madarasa na utengenezaji wa madawati ili ifikapo mwezi Machi ,2020 wanafunzi waliofaulu waweze kujiunga na kidato cha kwanza.
Alisema Wilaya inayoongoza kwa upungufu wa vyumba vya madarasa ni Wilaya ya Muleba vyumba 66,Karagwe vyumba 56,Biharamulo vyumba 37,Kyerwa 32,Bukoba Manispaa 32,halmashauri ya Bukoba 32,Missenyi 31 na Ngara vyumba 8.

Mwalimu Aidan Bahama,ni mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Ngara ,alisema jitihada za kupunguza  uhaba  wa vyumba vya  madarasa zilizotokana na  kikao cha wadau wa elimu cha mwaka 2018 wilayani humo.
Bahama,alisema Wilaya ya Ngara mwaka jana ilikuwa na upungufu  wa vyumba saba vya madarasa .
“Tuliona kuna upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa  kwa shule za sekondari na msingi ,Wilaya ilifanya tathimin  kuona shule zenye upungufu  na idadi ya madarasa yanayohitajika kwa shule husika”alisema mkurugenzi.
Alisema baada ya tathimini  mkurugenzi na mkuu wa Wilaya ya Ngara walishirikiana  wakaamua  kujenga vyumba  Zaidi ya vilivyokuwa vinahitajika hivyo walijenga vyumba 22 badala ya vyumba 7.

Alisema Rais kupitia kwa Wazairi wa Tamisemi alitoa kiasi cha shilingi milioni 25 kwa kila shule ambazo zilisaidia kukamilisha maboma  yaliyokuwa hayajakamilika na kuongeza vyumba vingine na kuwa na jumla ya vyumba 48 vya madarasa.

Alisema hata huo upungufu wa vyumba vya madarasa 8 mwaka huu vipo katika hatua mbalimbali za ukamilishaji  hadi kufika mwezi Januari 2020 hakutakuwa na upungufu wa chumba hata kimoja.
Alisema mafanikio hayo ni nguvu ya pamoja kati ya mkurugenzi,mkuu wa wilaya,wananchi na wadau wa elimu wilayani ngara.
Mwisho.
Share:

WALENGWA WA TASAF WAASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII ILI KUONDOKANA NA UMASKINI


Mwenyekiti wa bodi ya TASAF, Dr. Moses Kusiluka (aliyevaa shati nyeupe) akikagua baadhi ya bidhaa zinazouzwa na baadhi ya walengwa wa TASAF katika kijiji cha Khusumay
wilayani Karatu kama njia mojawapo ya kujiongezea kipato.
Mwenyekiti wa Bodi ya TASAF Dr.Moses Kusiluka ambaye pia ndiye Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Ikulu ( aliyevaa koti ) akikagua moja ya majengo ya Shule ya Sekondari yaliyojengwa na TASAF katika kijiji cha Khusumay wilaya ya Karatu. 
Nyumba za Walimu na hosteli ya wanafunzi ( picha ya juu na chini ) yaliyojengwa na TASAF katika Shule ya Sekondari ya Khusumay yanaelezwa kuhamasisha wanafunzi kuhudhuria masomo na kupunguza tatizo la mimba kwa watoto wa kike.
Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Bw. Ladisilaus Mwamanga akifungua bomba la maji kwenye moja ya nyumba zilizojengwa na TASAF katika Shule ya Sekondari Khusumay wilaya ya Karatu Mkoani Arusha. 
Baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya TASAF,Wadau wa Maendeleo na Menejimenti ya TASAF akiangalia ujenzi wa daraja linalojengwa na walengwa wa TASAF katika kijiji cha
Nala wilaya ya Karatu mkoani Arusha kwa utaratibu wa Ajira ya muda.
Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Uongozi ya TASAF, Maafisa wa Serikali na Wadau wa Maendeleo wakiangalia ng’ombe wa mmoja ya Walengwa ambao amewapata baada ya kujumuishwa kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika kijiji cha Nala wilaya ya Karatu mkoani Arusha.

Na Estom Sanga- Karatu 

Katibu Mkuu ofisi ya Rais-Ikulu -Dr. Moses Kusiluka ametoa wito kwa Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF kufanya kazi kwa bidii ili waweze kuondokana na umaskini uliokithiri. 

Dr. Kusiluka ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Bodi ya taifa ya Uongozi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF ameyasema hayo kwa nyakati tofauti alipotembelea na kukutana na baadhi ya walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini na kukagua miradi inayotekelezwa na TASAF katika wilaya ya Karatu mkoani Arusha ambako aliambatana pia na baadhi ya Wajumbe wa bodi . 

Amesema Serikali inatambua changamoto ya Umaskini unaowakabili wananchi ,lakini akasisitiza kuwa ili kuitokomeza changamoto hiyo wananchi wanapaswa
kujituma kwa kufanyakazi kwa bidii na maarifa na kutumia vizuri mazingira wezeshi yaliyowekwa na Serikali kuinua mapato yao. 

Aidha Dr. Kusiluka amehimiza wazazi kutilia mkazo suala la elimu kwa watoto wao ambao amesema Hiyo ndiyo njia ya uhakika ya kujenga jamii bora ya baadaye itakayoleta ukombozi wa kweli wa ujenzi wa uchumi thabiti wa
kaya husika na taifa kwa ujumla huku ikikemea vikali vitendo vyovyote vinavyoathiri maendeleo ya wanafunzi hususani watoto wa kike. 

‘’tumieni vizuri fursa mliyoipata ya kuwa shuleni ili mtimize ndoto zenu za kuwa wataalamu wa fani mnazozitaka katika utumishi wa taifa hapo baadaye’’ alisisitiza Dr. Kusiluka baada ya kukagua nyumba na hosteli ya wanafunzi wa kike katika shule ya sekondari ya Khusumay ambayo
yamejengwa na TASAF. 

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo wa
Bodi ya taifa ya Uongozi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii- TASAF amesema licha ya mafanikio makubwa yaliyopatikana katika utekelezaji wa Shughuli za Mfuko huo , Serikali imeanza kuchukua hatua madhubuti za kuhakikisha
kuwa Mfuko huo unaendelea kuwa nyenzo muhimu katika kusaidia jitihada za kupunguza umaskini nchini. 

Wakiwa katika kijiji cha Khusumay,Wajumbe hao wa bodi ya taifa ya Uongozi ya TASAF ,walitembelea kaya za baadhi ya walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini na
kujionea namna walengwa hao walivyofanikiwa kuboresha makazi yao, kununua mifugo hususani mbuzi, ng’ombe ,kuku na nguruwe kwa kutumia ruzuku waliyoipata kutoka TASAF kama njia mojawapo ya kukuza uchumi wa
kaya za Walengwa hao. 

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa
Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF- Bw. Ladislaus Mwamanga ameishukuru serikali kwa kuendelea kuuthamini Mfuko huo na kuridhia utekelezaji wake kuendelea katika sehemu ya pili ambayo amesema imeagizwa kutekelezwa
katika maeneo yote nchini.
Share:

WAZEE 2271 WAPATIWA KADI ZA CHF KAHAMA


Na Salvatory Ntandu - Kahama 
Wazee 2271 katika Halamshauri ya Mji wa Kahama mkoani Shinyanga wamepatiwa kadi za bima ya afya iliyoboreshwa (CHF) ambazo zitawasaidia kupata matibabu bure kwa mwaka mzima na kuondokana kwenda kwa waganga wa kienyeji kutafuta tiba.

Wazee wasiojiweza waliosajiliwa na baraza la wazee la Halmashauri ya mji wa Kahama mkoani Shinyanga ni 6247 na waliopatiwa kadi za CHF ni 2271.

Hayo yalibainishwa jana Mwenyekiti wa Baraza la wazee wa Halmshauri ya Mji kahama, Willfred Bilago wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini kahama alisema hapo awali wazee walikuwa wanahangaika kupata matibabu kutokana na kukosa kadi za CHF iliyoboreshwa.

“Wazee tulikuwa tunaona ni bora kwenda kwa waganga wa kienyeji kutafuta tiba mbadala kuliko kwenda katika hospitali ambapo tulikuwa hatuthamini na wengi wetu walipoteza maisha kutokana huduma hizo zisizokuwa za kitaalamu”alisema Bilago.

Alisema kadi za CHF zimesaidia wazee wasiojiweza kupata huduma za matibabu ambapo kwa unafuu na haraka kwani katika hospitali ya Halmashauri ya Mji wa kahama kunadirisha la kuhudumia wazee na madaktari maalum kwa ajili wao.

“Tunawaomba wadau,wafanyabiashara,viongozi wadini kusaidia upatikanaji wa kadi za CHF kwa wazee wasiokuwa na waangalizi ili waweze kupata matibabu bure kwani suala hili tukiiachia serikali pekee kwani nasi tunawajibu wa kuwatuza wazee wetu” alisema Bilago.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Abel Shija alisema kuwapatia kadi za CHF wazee katika halmashauri hiyo ni takwa la kisheria hivyo hawana budi kulitekeleza agizo hilo.

Kwa mujibu wa sera ya taifa ya wazee ya mwaka 2003 inazielekeza halmashauri kuhakikisha haki za wazee waliofikia miaka 60 zinalindwa pamoja na kuwapatia huduma bure za matibabu.
Share:

Picha : BODI YA WAKURUGENZI AGPAHI YATUA SIMIYU...RC MTAKA AWAPONGEZA KUSAIDIA WANANCHI...'KAZI ZENU SIYO ZA KUMULIKA KWA TOCHI'


Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka ameipongeza Asasi ya kitaifa isiyo ya kiserikali ya Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) kwa kutekeleza kikamilifu miradi ya UKIMWI na kuwagusa wananchi moja kwa moja. 

Mhe. Mtaka ametoa pongezi hizo Desemba 6,2019 kwenye kikao cha Bodi ya Wakurugenzi wa AGPAHI na wadau wa UKIMWI mkoani Simiyu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu. 

Mtaka alisema AGPAHI ni taasisi maarufu mkoani Simiyu kutokana na kwamba imekuwa ikifanya vitu vinavyoonekana katik sekta ya afya mkoani humo kwa kusaidia wananchi. 

“Nawapongeza sana AGPAHI kazi yenu inaonekana,kazi yenu haihitaji tochi ili kuona mnachofanya. Huwezi kuzungumzia mafanikio ya mkoa wa Simiyu kwenye sekta ya afya bila kuwataja AGPAHI”,alisema Mhe. Mtaka. 

“Tunazo taasisi 14 zinazojishughulisha na masuala ya afya mkoani Simiyu. Hawa wadau 13 wangefanya walau robo tu ya kilichofanywa na AGPAHI,tungekuwa na maendeleo makubwa sana katika mkoa wetu na nchi kwa ujumla”,aliongeza Mtaka. 

Mkuu huyo wa mkoa aliipongeza Bodi ya Wakurugenzi wa AGPAHI inayoongozwa na Watanzania kwa kutekeleza miradi inayogusa maisha ya wananchi huku akizitaka taasisi zingine kuiga mfano wa AGPAHI. 

“Wajumbe wa bodi ya AGPAHI mna ujasiri wa kutembelea miradi yenu kwenye mikoa kwa sababu miradi ipo.Nyinyi mna vitu,magari yenu pia yamekuwa yakitusaidia sana.Kuna baadhi ya taasisi hazina ujasiri wa kutembelea miradi kwa sababu hawana miradi,wengine kazi yao ni kugonga semina tu mwaka mzima.Hebu tufanye kazi zinazogusa wananchi tubadilishe mkoa huu”,alieleza Mtaka. 

Katika hatua nyingine Mtaka alisema serikali itaendelea kushirikiana na wadau wote wa maendeleo mkoani humo ili katika kuwaletea maendeleo wananchi. 

Mtaka alitumia fursa hiyo kuwakumbusha wananchi kutumia kondomu ili kupunguza maambukizi ya VVU huku akibainisha kuwa kuwa upo umuhimu wa kuvunja ukimya,vijana waelezwe ukweli kuhusu UKIMWI kwamba upo na unaua hivyo wachukue tahadhari. 

Kwa upande wake,Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu alisema AGPAHI inatekeleza miradi yake ya UKIMWI kwa kushirikiana na serikali lengo likiwa ni kuhakikisha fedha zinazotolewa na wafadhili zinawanufaisha watanzania. 

“Tunaushukuru mkoa wa Simiyu kwa ushirikiano mnaotupatia,tunajitahidi kufanya kazi kuwafikia wananchi,AGPAHI tunataka mtoto asizaliwe na maambukizi ya VVU,hivyo tutaendelea kushirikiana na serikali katika kutoa huduma za VVU na UKIMWI kwa wananchi”,alisema Dkt. Ngirwamungu. 

Alisema AGPAHI inaendelea kuongeza ubora na upatikanaji wa huduma za matunzo na tiba za VVU kwa watoto wachanga,vijana na watu wazima katika mikoa ya Simiyu,Mwanza,Mara na Shinyanga. 

Meneja Miradi AGPAHI mkoa wa Simiyu Dkt. Julius Sipemba alisema AGPAHI inatoa huduma za VVU na UKIMWI kwa mkoa mzima wa Simiyu ambapo Mkoa wa simiyu una vituo 233 vya kutolea huduma za afya na 73 kati ya hivyo hupata usimamizi wa moja kwa moja kutoka AGPAHI.

Alisema wagonjwa wanaopata huduma kwenye vituo 73 ni sawa na 95% ya wagonjwa wote walioko kwenye vituo 233.

"AGPAHI inaboresha miundombinu kwa kujenga na kukarabati majengo, huduma za maabara kwa kununua madawa na vifaa 'iliwezesha maabara za wilaya kutoka nyota moja mpaka tatu', imetoa magari mapya kwa halmashauri 4 kati ya 6, imetoa pikipiki, msaada wa kuchunguza kifua kikuu, Saratani ya mlango wa kizazi",alieleza Dkt. Sipemba.

Aliongeza kuwa AGPAHI pia inaajiri watoa huduma wa afya kwenye maeneo yenye uhitaji na inatoa mafunzo kwa watoa huduma kulingana na miongozo ya wizara ya afya.

Wakiwa mkoani Simiyu,Wajumbe wa bodi ya AGPAHI wametembelea Kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi,kukutana na Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu na Mkuu wa mkoa wa Simiyu pamoja na wadau wa VVU na UKIMWI mkoani Simiyu.

 ANGALIA PICHA ZA MATUKIO HAPA CHINI
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akizungumza katika kikao cha Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa AGPAHI na wadau wa afya mkoani Simiyu Desemba 6,2019. Kushoto ni Mkurugenzi wa AGPAHI, Dkt. Sekela Mwakyusa,kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akiipongeza AGPAHI kwa huduma za VVU na UKIMWI inazotoa mkoani Simiyu.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akielezea namna serikali inavyoshirikiana na wadau kuwaletea maendeleo wananchi.
Katibu Tawala mkoa wa Simiyu mhe. Jumanne Sagini akiipongeza AGPAHI kwa kutekeleza miradi inayogusa wananchi mkoani Simiyu.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu akizungumza katika kikao cha wadau wa afya mkoa wa Simiyu. Alisema lengo la AGPAHI ni kuhakikisha hakuna mtoto anazaliwa na maambukizi ya VVU.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu akizungumza katika kikao cha wadau wa afya na kueleza kuwa AGPAHI itaendelea kushirikiana na serikali katika kutoa huduma za VVU na UKIMWI.
Mkurugenzi wa AGPAHI, Dkt. Sekela Mwakyusa akielezea shughuli zinazofanywa na AGPAHI mkoani Simiyu.
Awali Mkurugenzi wa AGPAHI, Dkt. Sekela Mwakyusa akiwashukuru viongozi wa mkoa wa Simiyu kwa kuendelea kushirikiana na AGPAHI katika kutekeleza miradi ya VVU na UKIMWI. Kulia ni Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Simiyu Dkt. Gamitwe Mahazo.
Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Simiyu Dkt. Gamitwe Mahazo akizungumza katika kikao hicho.
Meneja Miradi AGPAHI mkoa wa Simiyu Dkt. Julius Sipemba  akiwasilisha mada kuhusu shughuli zinazofanywa na asasi ya AGPAHI mkoani Simiyu.
Meneja Miradi AGPAHI mkoa wa Simiyu Dkt. Julius Sipemba akielezea maeneo ambayo AGPAHI inahudumia mkoani Simiyu.
Mkuu wa wilaya ya Bariadi Mhe. Festo Kaswaga akichangia hoja wakati wa kikao cha wadau wa afya mkoani Simiyu.
Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Festo Dugange akichangia hoja wakati wa kikao cha wadau wa afya mkoani Simiyu.
Mganga Mkuu Halmashauri ya wilaya ya Busega Dkt. Godfrey Mbagali akichangia hoja wakati wa kikao cha wadau wa afya mkoani Simiyu.
Kikao kinaendelea.
Mnufaika wa miradi inayotekelezwa na AGPAHI mkoa wa Simiyu Pendo Gidion akielezea namna huduma ya baba,mama na mtoto ilivyomsaidia ambapo aliwataka wanawake wajawazito kujitokeza kupima VVU ili kuepuka kuzaa watoto wenye maambukizi ya VVU.
Kijana James Leonard akielezea jinsi alivyonufaika na Klabu za watoto na vijana zinazohudumiwa na AGPAHI. Aliwataka vijana wajitokeze kupima afya zao na pale wanapobainika kuwa na maambukizi ya VVU basi watumie dawa za kufubaza makali ya VVU kwani kuwa na maambukizi ya VVU siyo mwisho wa maisha.
Kijana Duhye Masunga akiwashauri wazazi kuwa wawazi kwa watoto wao kama wamezaliwa na maambukizi ya VVU
Minza Manyama akiwahamasisha wazazi na walezi kuwa wawazi kwa watoto waliozaliwa na maambukizi ya VVU. Alitumia fursa hiyo kuipongeza AGPAHI kwa huduma za VVU na UKIMWI inazoendelea kutoa kwa wananchi.
Kikao cha wadau wa afya kikiendelea.
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI wakiwa kwenye kikao cha wadau wa afya mkoani Simiyu.
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI wakiwa kwenye kikao cha wadau wa afya mkoani Simiyu.
Kikao kinaendelea.
Awali Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu (kulia) akimwelezea Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka huduma zinazotolewa na AGPAHI katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI wakati wajumbe wa bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI ilipotembelea ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akielezea namna mkoa wa Simiyu unavyonufaika na huduma zinazotolewa na AGPAHI mkoani Simiyu. Kushoto ni Mkurugenzi wa AGPAHI, Dkt. Sekela Mwakyusa,kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akiwapongeza wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI kwa kusimamia vizuri asasi ya AGPAHI ambapo asasi hiyo imekuwa maarufu sana mkoani Simiyu kutokana na kugusa maisha ya wananchi.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akiipongeza AGPAHI kwa kutekeleza miradi inayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja ..alisema 'Tunahitaji local contents zaidi kutoka kwa wadau wanaotekeleza miradi katika mkoa wa Simiyu.
Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Festo Dugange akiwashukuru AGPAHI kwa kusaidia sekta ya afya mkoani Simiyu.
Awali Mkurugenzi wa AGPAHI, Dkt. Sekela Mwakyusa akitambulisha wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI baada ya kuwasili katika ofisi ya Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Festo Dugange (wa kwanza kulia),katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu.
Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Festo Dugange akiwakaribisha wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu akielezea lengo ziara ya wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI mkoani Simiyu. 
Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Festo Dugange akiwakaribisha wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI mkoani Simiyu. 
Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Festo Dugange  akiteta jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu wakati wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI wakielekea katika kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi ili kuangalia namna huduma zinavyotolewa.
Kushoto ni Meneja Miradi AGPAHI mkoa wa Simiyu Dkt. Julius Sipemba  akielezea huduma zinazotolewa na AGPAHI katika Kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu (katikati) akiuliza jambo katika Kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi.

Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI wakiwa katika chumba cha kutunzia mafaili ya wateja katika Kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi. Wa kwanza kulia ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya wilaya ya Bariadi,Dkt. Mwanaidi Churu akitoa maelezo kwa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya wilaya ya Bariadi,Dkt. Mwanaidi Churu akionesha kitabu cha kumbukumbu za wateja katika Kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi. 
Wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI wakiwa kwenye chumba cha dawa katika kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi. 
Wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI wakiwa nje ya kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi. 
Picha ya pamoja uongozi wa mkoa wa Simiyu,AGPAHI na wadau wa afya mkoani Simiyu.
Picha ya pamoja uongozi wa mkoa wa Simiyu,AGPAHI na  wanufaika wa miradi inayotekelezwa na AGPAHI mkoani Simiyu.
Picha ya pamoja uongozi wa mkoa wa Simiyu na AGPAHI.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger